Kutolewa kwenye mashindano Biashara united ni uzembe wa TFF na Waziri mwenye dhamana

Timu moja ya nchini Mali inaitwa Binga fc wametembea kwa miguu km 15 kufika liberia ilipokuwa timu pinzani waliyopangiwa nayo na wamepiga game nzito na kufanikiwa kusonga mbele.

Sisi hatujafikia hatua ya kutembea kwa mguu uwezo tunao wa kujichanga hata biashara wapumbafu walushindwa kuomba msaada wachangiwe hadi inakuwa hivi.

Nimeumia sana.
 
Simba inaonekana ndio mmeihujumu biashara

Kwa kauli zenu inaonyesha mna bifu na Hawa watu.

Kwamba up ushaidi umeshindwa kupeleka takukuru waufanyie kazi?

Kwamba nyie mtashinda kila mechi na litimu libovu ?
Tuliwabeba sisi wenyewe halafu tuwahujumu tena? Ushenzi wao na huyo Hapi wao.

Mashindano ya kimataifa yanahitaji intelijensia na maandalizi ya kimkakati nje na ndani ya uwanja, Simba inahusikaje?
 
Waziri anahusikaje hapo? Kwani Biashara ni timu ya Taifa? Kwahiyo na Harmonize akishindwa kwenda kwenye Tuzo za Africa Music Awards, Waziri atumbuliwe sio? Na Shilole akishindwa kwenda kwenye Mashindano ya Kusasambua, Waziri atumbuliwe sio?
[emoji1787][emoji1787][emoji1787][emoji1787][emoji1787]
 
Well said[emoji122][emoji122][emoji122]
 
Biashara hata kwenye semina elekezi iliyoendeshwa kwa vilabu vi 4 vilivyoshiriki kimataifa iliyoendeshwa na TFF hawakutuma muwakilishi wakidai hawana nauli.

We unaona hii timu iko serious?
Duhhhh
 
Nawashangaa sana mnailaumu serikali kwa hili ilhali hiyo tff inajiendesha kwa misingi yake na sheria zake kadri ilivyopangiwa na wakubwa zake Africa na duniani kiujumla. Hamkumbuki kipindi yanga inapitisha bakuli kwani serikali ilitoa fungu lolote??

Sio biashara tu timu nyingi nchini zina ukata, huyo waziri sio kosa lake biashara kukosa fungu wakuu, huo ni uzembe wa biashara wenyewe.
 
Taasisi haziendi hivyo mkuu, biashara kama club wanabeba asilimia 95 ya lawama.....wasijifariji.

Sent from my SM-M205F using JamiiForums mobile app
Yes huu mzigo wataubeba wao wenyewe...kuna mwaka kati ya Ruvu shooting au JKT Ruvu mmoja wao aliqualify kuwakilisha nchi kimataifa lakini akajitoa mashindanoni wakidai wana ukata...sasa biashara kwanini hawakuchukua maamuzi kama haya mapema!?.Hii inaonyesha hii timu haipo serious hata kidogo
 
Sidhani kama TFF na Wizara zinahusika hapa.

Ni uzembe wa viongozi wa Biashara kutokuwa wawazi na kuwashirikisha wahusika niliowataja hapo juu.

Ni jambo la aibu na fedheha kwetu Watanzania.
 
haya ndio madhara ya kutizama usimba na uyanga tu na kusahau timu zingine zinazokua, ningekuwa Rais ningekula vichwa vingi sana kwa hili...yaani haiwezekani miwaziri ipoipo tu inakenua meno ofisini haishiriki kusaidia timu kufika mchezoni..hovyo sana. CCM YA MAGUFURI isingeweza kubali na kuvumilia ujinga huu, nI CCM YA SASA TU NDIO INAWEZA KULEA MAUJINGA KAMA HAYA
 
Hata kama hakuna ambaye angelaumu kuhusu Biashara FC kushindwa kusafiri, wananchi tunapaswa kuombwa radhi.

Ndiyo.

Vinginevyo tujue tu tunafanya mambo yetu bila malengo.

Hao viongozi wa timu kwanini hawakuomba fedha kwa serikali au hata sisi wananchi tuwachangie?

Hivi morale ya wachezaji wa Biashara FC itabaki kuwa ileile kwa mwenendo kama huo?

Morale ya mashabiki na wapenda soka au wanayoipenda Biashara FC itabaki vilevile?

Hili tusilichukulie kama jambo dogo. Huenda ni mfano tu katika uendeshaji wa mambo yetu mengi kiuchumi, kisiasa na kijamii.

Ni aibu, aibu, aibu kubwa sana.

Wanaosema TFF haihusiki wamechagua kuangalia mambo kwa jicho moja na ndiyo maana yakatokea yaliyotokea.

Tukumbuke timu huwa zinawakilisha nchi ndiyo maana hata wimbo wa Taifa hupigwa kabla mechi kuanza. Na hata mabalozi makini huhakikisha na kufuatilia timu zinakuwa salama na kutoa kila aina ya msaada.

Sidhani kama TFF jukumu lao ni kuripoti tu timu A ilicheza michezo yote waliyo pangiwa na timu B haikwenda mechi ya marudiano sababu haikuwa na fedha nk.

Tunahitaji ukombozi mkubwa wa kifikra na hata pa kuanzia anayejua ni Maulana.

Wananchi tuombwe radhi. Na iwe ni mwisho kutokea timu yoyote inayopata nafasi kushindwa kusafiri kwa kukosa pesa au mipango mibovu.

Ukitaka kujua uzito wa jambo hili jiulize kwanini Biashara FC inapata adhabu. Na utashangaa hapa kwetu hakuna atakaye wajibishwa kama vile jambo hilo ni la kawaida.

Nimetema nyongo!
 
Acha kupoteza muda kuelewesha taahira
 
Hapana. Kuna sababu mbili za Biashara Utd kutolewa ni:-
  • Laana ya kula njama na Yanga kutaka kuifunga Simba kwenye mechi ya ligi.
  • Nuksi ya Happi kuitunuku vijihela vyake
Wewe ndio bogus kabisa, Yaani Simba kufungwa ni laana? Watu wanaongea point za maana wewe unaleta mashudu.
 
Simba inaonekana ndio mmeihujumu biashara

Kwa kauli zenu inaonyesha mna bifu na Hawa watu.

Kwamba up ushaidi umeshindwa kupeleka takukuru waufanyie kazi?

Kwamba nyie mtashinda kila mechi na litimu libovu ?
Libovu libovu raundi ya kwanza nje ndani limegongwa na mimba ya faini juu kweli libovu[emoji16][emoji16][emoji16]

Sent from my Nokia C1 Plus using JamiiForums mobile app
 
Hakika... Sijaona kazi ya wizara ya Michezo... Sijui wanafanya kazi gani mpaka timu ishindwe kusafiri... Timu inayowakilisha nchi
 
Kazi ya tff ni kudafirisha team ?
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…