Kuuawa kwa Prigozhin na Imani ya Afrika kwa Putin na Washiriki Wake

Kuuawa kwa Prigozhin na Imani ya Afrika kwa Putin na Washiriki Wake

Nimesoma mada zako kadhaa kuhusu mgogoro huu pamoja na Putin na nilihitimisha kwamba una chuki binafsi na Putin pamoja na Russia.

Ulichoandika leo kwa hakika hakina uhalisia na ashakum si matusi, haya ni maneno ya kwenye kahawa na watakaokubaliana nawe sio wafuatiliaji.

Swali moja tu kwako, umethibitisha vipi kuwa ndege hiyo ilitunguliwa kwa amri kutoka Moscow?
 
(1) Prigozhin alikuwa rafiki mkubwa wa Putin tokea utotoni mwao huko St Petersberg na kuna wakati Putin alikuwa anatayarishiwa chakula na mgahawa wa Prigozhin tu; na mara zote Prigozhin mwenyewe ndiye aliyekuwa aneanda kutoa huduma hiyo ya chakula kwa Putin.

(2) Mwanzoni mwa mwaka 2022, shirika la ujasusi la Marekani lilitangaza kuwa Putin anajiandaa kuivamia Ukraine. Viongozi mbalimbali wa nchi za Magharaibi walimtembelea Putin kummwambia asifanye uvamizi huo. Putin aliwaambia kuwa hiyo ilikuwa ni propaganda ya marekani tu yeye hakuwa na mpando wowote wa kuvamia Ukraine

(3) Mwezi wa pili mwaka 2022, Putin aliishambulia Ukraine kinyume kabisa na vile alivyokuwa anawaambia viongozi wa nchi za Magharibi waliomuomba sana asifanye uvamizi huo kwa sababu za usalama wa dunia

(4) Prigozhin kwa kutumia kampuni yake ya Wagner alimsaidia rafiki yake katika uvamizi wa Ukraine kwa kupigana sana kule Bakhmut na kupoteza askari wake wengi sana akiwamo mtanzania mmoja. Kibaya zaidi kwa Prigozhin ilikuwa ni kwamba jeshi halisi la Urusi lilikuwa halitoi ushirikiano kwa jeshi lake la Wagner japo wote walikuwa wanapigana vita moja kwa ajili ya Putin. Prigozhin alilalamika sana kuhus kukosekana kwa ushirkiano huo

(5) Baada ya kukosekana kwa ushirikiano huo wa namba (4) hapo juu, Prigozhin alitishia kupeleka jeshi lake kwenda Moscow kuwabana waziri wa ulinzi na mkuu wa majeshi wa urusi. Tishio hilo lilionekana kama ni uasi akalistisha. Baada ya kulistisha, Putin akatangza kuwa mfarakano umekwisha na wale askari wote wa Wagner wanatakiwa waijunge na Jeshi, halafu Prigozhin aendelee na biashara zake nyingine lakini siyo ya PMC Wagner tena.

(6) Wakati Putin alipowakaribisha viongozi wa Afrika kwenye mkutano wake, alimruhusu Prigozhin akutane na viongzi wa kiafrika wa nchi ambako ana biashara zake. Hiyo ikionyesha kuwa hana mfarakano na bwana Prigozhin tena.

(7) Majuzi tu Prigozhin alikuwa anasafiri kwenda nyumbani kwake St. Petersrbeg; usafiri wake hutumia ndege mbili au tatu zinazofanana, na anaweza kuingia kwenye ndege yoyote kati ya hizo mbili/tatu bila kuulizwa atatumia ndege gani. Hata hivyo siku hiyo ya tukio, mamlaka zilitaka atamke ataondoka na ndege gani, akachagua ndege ya kwanza. Baada ya ndege hiyo kuondoka mamlaka zilichelewesha ile ndege yake ya pili kuondoka hadi ndege yake ya kwanza ilipokaribia na Tver ambapo kuna Air Defense system installation za jijeshi, ndipo ile ndege ya pili ikaruhusiwa kuondoka Moscow.

(8) Ndege ya kwanza ya bwana Prigozhin ilipoingia kwenye malengo mazuri ya Air Defense System ya Tver, ikatunguliwa; halafu ile ndege ya pili ambayo ilikuwa na mawasiliaono na ile ya kwanza iliposikia mlipuko wa ndege nyeza ya kwanza aikaamua kurudi Moscow; hata hivyo baada ya kuruhusiwa kutua Moscow, watu wote waliokuwa kwenye ndege hiyo ya pili wakatiwa nguvuni.

Matumizi ya zana za kijeshi Urusi yanahitaji kibali cha Putin tu; kwa hiyo utunguzi wa ndege ya Prigozhin ulikuwa na baraka za bwana Putin. Swali langu: Hivi kweli viongozi wa Afrtika tunajiamini nini kukubali maneno ya Putin ambaye hajaonyesha punje ya kusema ukweli siyo tu kwa viongozi wenzake wa nchi nyingine bali hata kwa marafiki zake wa karibu wa tangu utotoni?


Hata sisi tuna facts' kama una chuki na Putin mtafute mrekebishe tofauti zenu, kuna vitu umepotosha hapo.
 
Unaweza nitajia mwanasiasa yeyote unayedhani ni mkweli na mimi nitakwambia uongo wake aliowahi kuusema hadharani.
Haya tupe uongo aliousema hadharani bwana JFK (Join Forces with the Kings)
 
Haaaaa. Kichuguu Ndugu yangu Dunia Kote Ukimwona mwanasiasa anazungumza mbele ya umma ukweli ni % ndogo sana kama 10%.

Viongoz wa Kisiasa huzungumza ukweli wote wawapo kwenye Vikao Vya siri na washirika wao wa wakati huo. KWENYE SIASA UKWELI HUZUNGUMZWA SIRINI TU na ndani ya nafisi zao.
Kwel kabisa,hakunaga mwanasiasa mkweli
 
Putin amefanya vibaya sana kumuua mwenzake.Yule hata ukimuangalia usoni anatisha.Ni swala la muda Putin atakuja kufa kifo kibaya na watakaomuua hawatatoka mbali.Kumuondoa mwenzake sio kupunguza maadui bali anaongeza maadui kumbuka Prighozin alikuwa na watu wanaomtii na kumpenda.Ni swala la muda tu.
 
(1) Prigozhin alikuwa rafiki mkubwa wa Putin tokea utotoni mwao huko St Petersberg na kuna wakati Putin alikuwa anatayarishiwa chakula na mgahawa wa Prigozhin tu; na mara zote Prigozhin mwenyewe ndiye aliyekuwa aneanda kutoa huduma hiyo ya chakula kwa Putin.

(2) Mwanzoni mwa mwaka 2022, shirika la ujasusi la Marekani lilitangaza kuwa Putin anajiandaa kuivamia Ukraine. Viongozi mbalimbali wa nchi za Magharaibi walimtembelea Putin kummwambia asifanye uvamizi huo. Putin aliwaambia kuwa hiyo ilikuwa ni propaganda ya marekani tu yeye hakuwa na mpando wowote wa kuvamia Ukraine

(3) Mwezi wa pili mwaka 2022, Putin aliishambulia Ukraine kinyume kabisa na vile alivyokuwa anawaambia viongozi wa nchi za Magharibi waliomuomba sana asifanye uvamizi huo kwa sababu za usalama wa dunia

(4) Prigozhin kwa kutumia kampuni yake ya Wagner alimsaidia rafiki yake katika uvamizi wa Ukraine kwa kupigana sana kule Bakhmut na kupoteza askari wake wengi sana akiwamo mtanzania mmoja. Kibaya zaidi kwa Prigozhin ilikuwa ni kwamba jeshi halisi la Urusi lilikuwa halitoi ushirikiano kwa jeshi lake la Wagner japo wote walikuwa wanapigana vita moja kwa ajili ya Putin. Prigozhin alilalamika sana kuhus kukosekana kwa ushirkiano huo

(5) Baada ya kukosekana kwa ushirikiano huo wa namba (4) hapo juu, Prigozhin alitishia kupeleka jeshi lake kwenda Moscow kuwabana waziri wa ulinzi na mkuu wa majeshi wa urusi. Tishio hilo lilionekana kama ni uasi akalistisha. Baada ya kulistisha, Putin akatangza kuwa mfarakano umekwisha na wale askari wote wa Wagner wanatakiwa waijunge na Jeshi, halafu Prigozhin aendelee na biashara zake nyingine lakini siyo ya PMC Wagner tena.

(6) Wakati Putin alipowakaribisha viongozi wa Afrika kwenye mkutano wake, alimruhusu Prigozhin akutane na viongzi wa kiafrika wa nchi ambako ana biashara zake. Hiyo ikionyesha kuwa hana mfarakano na bwana Prigozhin tena.

(7) Majuzi tu Prigozhin alikuwa anasafiri kwenda nyumbani kwake St. Petersrbeg; usafiri wake hutumia ndege mbili au tatu zinazofanana, na anaweza kuingia kwenye ndege yoyote kati ya hizo mbili/tatu bila kuulizwa atatumia ndege gani. Hata hivyo siku hiyo ya tukio, mamlaka zilitaka atamke ataondoka na ndege gani, akachagua ndege ya kwanza. Baada ya ndege hiyo kuondoka mamlaka zilichelewesha ile ndege yake ya pili kuondoka hadi ndege yake ya kwanza ilipokaribia na Tver ambapo kuna Air Defense system installation za jijeshi, ndipo ile ndege ya pili ikaruhusiwa kuondoka Moscow.

(8) Ndege ya kwanza ya bwana Prigozhin ilipoingia kwenye malengo mazuri ya Air Defense System ya Tver, ikatunguliwa; halafu ile ndege ya pili ambayo ilikuwa na mawasiliaono na ile ya kwanza iliposikia mlipuko wa ndege nyeza ya kwanza aikaamua kurudi Moscow; hata hivyo baada ya kuruhusiwa kutua Moscow, watu wote waliokuwa kwenye ndege hiyo ya pili wakatiwa nguvuni.

Matumizi ya zana za kijeshi Urusi yanahitaji kibali cha Putin tu; kwa hiyo utunguzi wa ndege ya Prigozhin ulikuwa na baraka za bwana Putin. Swali langu: Hivi kweli viongozi wa Afrtika tunajiamini nini kukubali maneno ya Putin ambaye hajaonyesha punje ya kusema ukweli siyo tu kwa viongozi wenzake wa nchi nyingine bali hata kwa marafiki zake wa karibu wa tangu utotoni?
Inasemekana hiyo Wagner mmoja wa waanzilishi wake ni Putin, hivyo haikuwa mali ya Prigozhin kwa asilimia zote.

Putin hasamehi kamwe wasaliti, hivyo kwa kilichompata Prigozhin kilitarajiwa.... hatimaye Wagner imemezwa na wizara ya ulinzi ya Urusi.
 
Kwenye Geopolitics hatuangalii yupi adui na yupi rafiki, au yupi mwema au yupi muovu.

Kwenye Geopolitics tunaangalia yupi "Maslahi" yake yanaendana au hayapingani na yetu bila kujali internal politics au foreign policies zake as long as hazina mahusiano yoyote au hazipingani na maslahi yetu

Russia ni key geopolitical player kwenye uasisi na mafanikio ya BRICS,
BRICS ni jina mwamvuli kwa nchi zote ambazo "maslahi" yao hayaendani na Western economic system pamoja na capitalistic & neo colonial institutions zake zote kama Petro dollar system, IMF, World Bank etc.

Russia kama ilivyo Africa, China, India na nchi nyingi zinazotaka kuwa sehemu ya BRICS ni wahanga wakubwa wa Western led World kwa mda mrefu, so "maslahi" yao yanaendana bila kujali tofauti zao za kisiasa au kijamii

So anachokifanya Putin Russia, sisi Africa hakituhusu, hata akiua raia wake

Tunachopaswa jali ni "Maslahi" yetu, inapaswa tutoke kwenye utumwa wa kiuchumi, na BRICS ni hatua moja wapo

Kuhusu mahusiano ya Russia (au USSR) na Africa, hujasoma historia?

Russia wamepita viongozi wehu kuliko Putin, lakini nitajie nchi moja ya Afrika iliyotawaliwa au kunyonywa na Warusi? Au Wachina? Au Wahindi?
 
ukweli ni kwamba, hata kama alikuwa rafiki yake wa utotoni, kitendo cha uasi alichokuwa amekionyesha ilikuwa ni tishio la kutomwamini tena na ingekuwa ujinga kama putin asingefanya alichofanya. kwa upande wa putin kwa africa, ukienda kwa kuaminiana hana shida, ila ukienda kwa usaliti au mguu mmoja ukiwa western countries lazima kuna siku utaona makucha yake tu.
 
Viongozi wa Afrika wanaomkumbatia Putin kama kwamba anawathimini wao sana ilihali akiua ndugu zake wa karibu sana na kufuta makaburi ya askari wa Wagner ambao ni warusi kama yeye waliomsiadia sana kwenye hiyo special military Operation ni viongozi wenye upungufu mkubwa sana wa akili. Watu wa Ukraine wako karibu sana na warusi kwa vile wanaongea lugfha moja na wana historia inayoshabihiana sana lakini anawaua bila huruma yoyote. Waafrika nyingi mtakuwa mna thamani gani kwake? Angalia hapa alivyofuta makaburi ya wagner baada ya kumuua Prigozhin. Ni mtu wa aina gani huyo kuheshimiwa na viongozi wetu?


View: https://rumble.com/v3bmx7q-wagner-cemeteries-being-paved-over.html?mref=1psd20&mc=6ztjq
 
(1) Prigozhin alikuwa rafiki mkubwa wa Putin tokea utotoni mwao huko St Petersberg na kuna wakati Putin alikuwa anatayarishiwa chakula na mgahawa wa Prigozhin tu; na mara zote Prigozhin mwenyewe ndiye aliyekuwa aneanda kutoa huduma hiyo ya chakula kwa Putin.

(2) Mwanzoni mwa mwaka 2022, shirika la ujasusi la Marekani lilitangaza kuwa Putin anajiandaa kuivamia Ukraine. Viongozi mbalimbali wa nchi za Magharaibi walimtembelea Putin kummwambia asifanye uvamizi huo. Putin aliwaambia kuwa hiyo ilikuwa ni propaganda ya marekani tu yeye hakuwa na mpando wowote wa kuvamia Ukraine

(3) Mwezi wa pili mwaka 2022, Putin aliishambulia Ukraine kinyume kabisa na vile alivyokuwa anawaambia viongozi wa nchi za Magharibi waliomuomba sana asifanye uvamizi huo kwa sababu za usalama wa dunia

(4) Prigozhin kwa kutumia kampuni yake ya Wagner alimsaidia rafiki yake katika uvamizi wa Ukraine kwa kupigana sana kule Bakhmut na kupoteza askari wake wengi sana akiwamo mtanzania mmoja. Kibaya zaidi kwa Prigozhin ilikuwa ni kwamba jeshi halisi la Urusi lilikuwa halitoi ushirikiano kwa jeshi lake la Wagner japo wote walikuwa wanapigana vita moja kwa ajili ya Putin. Prigozhin alilalamika sana kuhus kukosekana kwa ushirkiano huo

(5) Baada ya kukosekana kwa ushirikiano huo wa namba (4) hapo juu, Prigozhin alitishia kupeleka jeshi lake kwenda Moscow kuwabana waziri wa ulinzi na mkuu wa majeshi wa urusi. Tishio hilo lilionekana kama ni uasi akalistisha. Baada ya kulistisha, Putin akatangza kuwa mfarakano umekwisha na wale askari wote wa Wagner wanatakiwa waijunge na Jeshi, halafu Prigozhin aendelee na biashara zake nyingine lakini siyo ya PMC Wagner tena.

(6) Wakati Putin alipowakaribisha viongozi wa Afrika kwenye mkutano wake, alimruhusu Prigozhin akutane na viongzi wa kiafrika wa nchi ambako ana biashara zake. Hiyo ikionyesha kuwa hana mfarakano na bwana Prigozhin tena.

(7) Majuzi tu Prigozhin alikuwa anasafiri kwenda nyumbani kwake St. Petersrbeg; usafiri wake hutumia ndege mbili au tatu zinazofanana, na anaweza kuingia kwenye ndege yoyote kati ya hizo mbili/tatu bila kuulizwa atatumia ndege gani. Hata hivyo siku hiyo ya tukio, mamlaka zilitaka atamke ataondoka na ndege gani, akachagua ndege ya kwanza. Baada ya ndege hiyo kuondoka mamlaka zilichelewesha ile ndege yake ya pili kuondoka hadi ndege yake ya kwanza ilipokaribia na Tver ambapo kuna Air Defense system installation za jijeshi, ndipo ile ndege ya pili ikaruhusiwa kuondoka Moscow.

(8) Ndege ya kwanza ya bwana Prigozhin ilipoingia kwenye malengo mazuri ya Air Defense System ya Tver, ikatunguliwa; halafu ile ndege ya pili ambayo ilikuwa na mawasiliaono na ile ya kwanza iliposikia mlipuko wa ndege nyeza ya kwanza aikaamua kurudi Moscow; hata hivyo baada ya kuruhusiwa kutua Moscow, watu wote waliokuwa kwenye ndege hiyo ya pili wakatiwa nguvuni.

Matumizi ya zana za kijeshi Urusi yanahitaji kibali cha Putin tu; kwa hiyo utunguzi wa ndege ya Prigozhin ulikuwa na baraka za bwana Putin. Swali langu: Hivi kweli viongozi wa Afrtika tunajiamini nini kukubali maneno ya Putin ambaye hajaonyesha punje ya kusema ukweli siyo tu kwa viongozi wenzake wa nchi nyingine bali hata kwa marafiki zake wa karibu wa tangu utotoni?
Chawa mmagharibi at work
 
Putin amefanya vibaya sana kumuua mwenzake.Yule hata ukimuangalia usoni anatisha.Ni swala la muda Putin atakuja kufa kifo kibaya na watakaomuua hawatatoka mbali.Kumuondoa mwenzake sio kupunguza maadui bali anaongeza maadui kumbuka Prighozin alikuwa na watu wanaomtii na kumpenda.Ni swala la muda tu.
To assassinate Putin is next to impossible ndugu yangu. Huyo ni wa kiwango juu sana ktk security technology. Sijui Boris Yeltsin alipekua vipi hata akapata huyo Putin. Hatari sana. Putin has made Russia Great Again.
 
Kama ni kweli Prigozhin ameuliwa (assassinated) , basi muuaji alitaka mpost content kama hii ya mleta mada.
 
Back
Top Bottom