Kuuliza si ujinga, Mtu akifariki watu wanasema Apumzike kwa Amani huwa wanamwambia marehemu au wanamaanisha nini?

ukifariki unakua umerara tu umerest zako, kwa wa imani ndo kunakua na peace na kwa upande wa ndg zetu kuna nyundo na Scorpion tena
 
Mkuu ,kikawaida binadamu huwa anatamni kuishi milele bila kufa ,bila kujua kifo pia ni sehemu ya uhai , yani kifo ndio uhai wenyewe , unakufa mwili wako unaoza tunapata nishati kwa viumbe wengne ,yani hicho kinachoitwa uhai ni wewe katika hali zote, dini zinawapa matumani ya kijinga mno ,ndio maana zinawaiteni kondooo, vuka kwenye hivyo viwango vya kushikiwa ufahamu wako mkuu, kwa hofu ya kifo na ahadi za peponi.
 
Hata swali nililouliza sijajibiwa nimeambiwa vitu vingineπŸ˜‚πŸ˜‚
Asante kwa kushiriki mkuu.
 
May the soul of the.....rest in peace.
.....................................
Kondooo ukiwaambua rohoo wanachekelea ila ukiwaambia ukifa unakuwa nishati ya uhai katika maumbile mengne wananuna, 🀣🀣🀣
 
kivip mkuu Elezea?
Roho ni ya Mungu, humrejelea aliyeitoa
Mwili uliumbwa kwa udongo, utarejea udongoni.
Nafsi Ina sifa kama roho ila siyo roho na ndiyo inayoweka mawasiliano kati ya mwili na roho.

Nafsi ndiyo inayotangatanga
 
Kwanza sayansi haipo kwenye tafiti za kugundua nini kipo baada ya kifo.

Kwa sababu hakuna sehemu au kitu chochote kile ambacho kipo baada ya kifo.

Sayansi ipo kwenye tafiti na harakati za kuweza kuzuia kifo.
 
Lugha za kufarijiana tu hizo, mtu akishakufa kila kitu kimeisha hapo. Anapumzikaje kwa amani sasa.
 
Kwanza sayansi haipo kwenye tafiti za kugundua nini kipo baada ya kifo.

Kwa sababu hakuna sehemu au kitu chochote kile ambacho kipo baada ya kifo.

Sayansi ipo kwenye tafiti na harakati za kuweza kuzuia kifo.
Kwanini unasema hakuna kitu chochote kile kipo baada ya kifo? Kwanini usiseme bado hatujui? Kwanini ni lazima kwamba hakuna kitu wakati tunaona Exactly miaka mingi nyuma teknolojia ilikuwa ndogo na watu hawakuweza kuamini kwamba unaweza kutoka Dar mpaka dodoma kwa dakika45. Kwanini tusiseme hatujui na tunalazimisha kwamba hakuna kitu?πŸ˜‚πŸ˜‚
 
Unashangaa hilo hujaona matangazo ya TV na magazeti unakuta inawekwa picha ya marehemu kwenye gazeti au TV hakafu maelezo yanafuata fulani ni miska kadhaa toka umetutoka unakumbukwa sana na nduguzo fulani fulani na fulani

Sasa huyo marehemu huko aliko huwa anaangalia TV na kusoma magazeti ? Ili aone anavyokumbukwa?
 
Hao siyo Waislaam.
.Waislaam tunatakiana tuwe kwenye amani kila tunapokutana "Asalaam Alaikum" na tunapopatwa na msiba tunafarijiana kwa kukumbushana kuwa sote ni wa Allah na kwake ni marejeo.
 
Wewe ndio umeshindwa kupata jibu lako kwenye maelezo yangu 😁😁
Hata sayansi kwenye masuala ya mungu ipo neutral haisimami upande wowote sababu kila siku tafiti zinaendelea.
Mimi mekuuliza swali jepesi ukaleta stori zingine. Kwanini ni rahisi kusema hakuna kitu lakini si rahisi kusema kwamba hatujui? TutajuJe maendeleo ya sayansi miaka 200 inayokuja itakuwa na majibu kiasi chake au kuna vitu vitakuwa vimevumbuliwa?πŸ˜‚πŸ˜‚
Kwanini ni lazima kwamba baadda yakifo hakuna kitu na si kwamba hatujui sababu sayansi inaweza kuvumbua kitu fulani miaka 500 baadae kuhusu kifo?

Kwanini unahitimisha hakuna kitu?
 
πŸ˜‚πŸ€£πŸ€£πŸ€£πŸ€£.
Hii inakuwaga TBC nilimuuliza kaka yangu siku moja sikupewaga majibu zaidi ya kuambiwa ndio anaona.
Kweli Imani zinafurahisha sana ila ni namna ya kujaribu kutuliza hisia zetu
 
Neno linalostahili sio Rest in Prace au pumzika kwa amani neno linalotakiwa kutamkwa ni

" Mungu muweke mahali panapomstahili"

Kama atanuweka pema au pabaya ni yeye mwenyewe ndie ajua
 
Marehemu ni mtu aliyekufa mwili but roho yake inaishi - ipo. Mwili wako unaweza uka-shut down (ukafa) na roho yako isipate pumziko - May his/her soul rest in peace - ni kuitakia matashi mema tu...

Ni sawasawa na kumwambia mtu - safari njema, ufike salama, ulale salama, kazi njema n.k Hizi ni good wishes tu
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…