Kuuliza si ujinga, Mtu akifariki watu wanasema Apumzike kwa Amani huwa wanamwambia marehemu au wanamaanisha nini?

Marehemu Wanajua bhana, kinachokufa ni mwli sio roho zao, roho zao still zinaishi.
hakuna hicho kitu, shetani anatumia hiyo fursa kudanganya watu
wewe chukua hilo andiko kwamba wafu hawajui lolote

FUNDISHO LA BIBLIA KUHUSU “NAFSI”​

Kwanza, tuzungumzie nafsi. Huenda unakumbuka kwamba mwanzoni Biblia iliandikwa katika Kiebrania na Kigiriki. Waandishi wa Biblia walitumia neno neʹphesh la Kiebrania au psy·kheʹ la Kigiriki walipoandika kuhusu nafsi. Maneno hayo mawili yanapatikana zaidi ya mara 800 katika Maandiko, na Tafsiri ya Ulimwengu Mpya huyatafsiri yote kuwa “nafsi.” Unapochunguza jinsi neno “nafsi” linavyotumiwa katika Biblia, utaona kwa wazi kwamba neno hilo humaanisha (1) watu, (2) wanyama, au (3) uhai wa mtu au mnyama. Na tuzungumzie baadhi ya Maandiko yanayoonyesha mambo hayo matatu.
Watu. “Katika siku za Noa . . . watu wachache, yaani, nafsi nane, walichukuliwa salama kupitia maji.” (1 Petro 3:20) Kwa wazi neno “nafsi” katika andiko hilo linamaanisha watu, yaani, Noa, mkewe, wanawe watatu, na wake zao. Andiko la Kutoka 16:16 lina maagizo kwa Waisraeli kuhusu kuokota mana. Waliambiwa: “Okoteni kiasi chake . . . kulingana na hesabu ya nafsi ambazo kila mmoja wenu anazo katika hema lake.” Kwa hiyo, kiasi cha mana kilichookotwa kilitegemea kiasi cha watu katika kila familia. Maandiko yafuatayo ya Biblia yanaonyesha matumizi ya neno “nafsi” kumaanisha watu, Mwanzo 46:18; Yoshua 11:11; Matendo 27:37; na Waroma 13:1.
Wanyama. Tunasoma hivi katika masimulizi ya Biblia kuhusu uumbaji: “Mungu akaendelea kusema: ‘Maji na yajawe na nafsi hai na viumbe vinavyoruka viruke juu ya dunia kwenye uso wa anga la mbingu.’ Mungu akaendelea kusema: ‘Dunia na itokeze nafsi zilizo hai kulingana na aina zake, mnyama wa kufugwa na mnyama anayetambaa na mnyama-mwitu wa dunia kulingana na aina yake.’ Ikawa hivyo.” (Mwanzo 1:20, 24) Katika andiko hilo, samaki, wanyama wa kufugwa, na wanyama-mwitu wote wanaitwa kwa neno lilelile—“nafsi.” Ndege na wanyama wengine wanaitwa nafsi kwenye Mwanzo 9:10; Mambo ya Walawi 11:46; na Hesabu 31:28.
Uhai wa mtu. Wakati mwingine neno “nafsi” humaanisha uhai wa mtu. Yehova alimwambia Musa: “Watu wote waliokuwa wakiiwinda nafsi yako wamekufa.” (Kutoka 4:19) Adui za Musa walikuwa wakiwinda nini? Walitaka kumuua Musa. Raheli alipokuwa akimzaa mwanawe Benyamini, ‘nafsi yake ilitoka (kwa sababu alikufa).’ (Mwanzo 35:16-19) Wakati huo Raheli alipoteza uhai wake. Fikiria pia maneno ya Yesu: “Mimi ndiye mchungaji mwema; mchungaji mwema huitoa nafsi yake kwa ajili ya kondoo.” (Yohana 10:11) Yesu alitoa nafsi au uhai wake kwa ajili ya wanadamu. Katika maandiko hayo ya Biblia, ni wazi kwamba neno “nafsi” linamaanisha mtu. Utapata mifano mingine yenye maana hiyo ya neno “nafsi” kwenye 1 Wafalme 17:17-23; Mathayo 10:39; Yohana 15:13; na Matendo 20:10.
Unapoendelea kujifunza Neno la Mungu utaona kwamba hakuna popote katika Biblia ambapo neno “nafsi” linahusianishwa na “kutoweza kufa” au “kuishi milele.” Badala yake, Maandiko yanasema kwamba nafsi inaweza kufa. (Ezekieli 18:4, 20) Kwa hiyo, katika Biblia mtu ambaye amekufa huitwa ‘nafsi iliyokufa.’—Mambo ya Walawi 21:11.

MAANA YA “ROHO”​

Hebu tuzungumzie jinsi Biblia inavyotumia neno “roho.” Watu fulani hufikiri kwamba “roho” ni neno lingine linalomaanisha “nafsi.” Lakini, si kweli. Biblia inaonyesha wazi kwamba “roho” na “nafsi” ni vitu viwili tofauti. Vinatofautianaje?
Waandishi wa Biblia walitumia neno la Kiebrania ruʹach au neno la Kigiriki, pneuʹma waliporejelea “roho.” Maandiko yenyewe yanaonyesha maana ya maneno hayo. Kwa mfano, andiko la Zaburi 104:29 linasema: “[Yehova] ukiiondoa roho [ruʹach] yao, wanakata pumzi, na kurudi katika mavumbi yao.” Andiko la Yakobo 2:26 linasema kwamba “mwili bila roho [pneuʹma] umekufa.” Katika andiko hilo “roho” inamaanisha kile ambacho huupa mwili uhai. Bila roho, mwili umekufa. Kwa hiyo, katika Biblia neno ruʹach halitafsiriwi tu “roho” bali pia “nguvu” au kani ya uhai. Kwa mfano, Mungu alisema hivi kuhusu Mafuriko ya siku ya Noa: “Ninaleta gharika ya maji duniani ili kuharibu kutoka chini ya mbingu wote wenye mwili walio na nguvu [ruʹach] za uhai ndani yao.” (Mwanzo 6:17; 7:15, 22) Hivyo, “roho” inarejelea nguvu isiyoonekana, inayotendesha viumbe vyote vilivyo hai.

Nafsi na roho hutofautiana. Mwili unahitaji roho kama vile redio inavyohitaji umeme ili kufanya kazi. Kwa mfano, unapotia betri katika redio na kuiwasha, nguvu zilizo katika betri huiwezesha redio kufanya kazi. Hata hivyo, redio haiwezi kufanya kazi bila betri. Hali kadhalika, redio ambayo imeondolewa kwenye umeme haiwezi kufanya kazi. Vivyo hivyo, roho ni nguvu ambayo hutendesha mwili wetu. Kama umeme, roho haiwezi kuhisi wala kufikiri. Ni nguvu isiyo na utu. Lakini bila roho au kani ya uhai, “tunakata pumzi na kurudi kwenye udongo,” kama mtunga-zaburi alivyosema.
Andiko la Mhubiri 12:7 linasema hivi linapozungumzia kifo cha mwanadamu: “Mavumbi [mwili wake] huirudia nchi kama yalivyokuwa, nayo roho yenyewe humrudia Mungu wa kweli aliyeitoa.” Roho au kani ya uhai inapoondoka mwilini, mwili hufa na kurudi ulipotoka, yaani, kwenye udongo. Vivyo hivyo, nguvu ya uhai hurudi ilipotoka, yaani, kwa Mungu. (Ayubu 34:14, 15; Zaburi 36:9) Hiyo haimaanishi kwamba nguvu ya uhai huenda mbinguni kihalisi. Badala yake, inamaanisha kwamba mtu akifa, tumaini lolote la kuishi tena linamtegemea Yehova Mungu. Ni kana kwamba uhai wake uko mikononi mwa Mungu. Ni kupitia nguvu za Mungu tu ndipo roho au nguvu ya uhai inaweza kurudishwa ili mtu aweze kuishi tena.
Inafariji kama nini kujua kwamba hivyo ndivyo Mungu atakavyofanya kwa wote wanaopumzika ndani ya “makaburi ya ukumbusho!” (Yohana 5:28, 29) Wakati wa ufufuo, Yehova atamfanyizia mwili mpya yule anayelala katika kifo na kuuhuisha kwa kutia roho, au nguvu ya uhai ndani yake. Itakuwa siku ya shangwe sana.
 
acha fix mkuuu
 
Sayansi unayoizungumzia imeshatoa majibu kuhusu kifo labda wewe ndio unajizima data kwa tamaa yako ya kwenda mbinguni , ukifa kazi zote za mwili zinasimama na mchakato wa kuoza unaanza rasmi , na kubadilika kama nishati ndani ya udongo ili kurutubisha mchicha na mchicha kitukuu chako kitaula na kupata nishati ya kupata manii ili atungishe mimba ya kuzaa kilembwe chako.
 
Ngoja nikae pembeni niangalie hii mtanange DR Mambo Jambo nipo pale nasubiri watu watwangane kwa hoja
 
Mkuu bila shaka wewe ni mashahidi wa yehova😁
 
Kwani Hakuna watu waliokuja ku modify gregor mendel theory? Vipi Copernicus hakuja baadae Galileo Galilee kuja kumodify alichokisema?😂😂
Nafikiri ni umeelewa ila tu Basi unaamua kukwepa swali🤣
Siku njema
 
Kwani Hakuna watu waliokuja ku modify gregor mendel theory? Vipi Copernicus hakuja baadae Galileo Galilee kuja kumodify alichokisema?😂😂
Nafikiri ni umeelewa ila tu Basi unaamua kukwepa swali🤣
Siku njema
Mkuu na mimi nmekuja kumodify, kuna theories zangu nyingi tu zinafanyiwa tafiti au kwa sababu mimi ni mmatumbi mwenzako, tena mtangagiza , ndio maana hauniamini mpaka galileo?
 
Ni kama vile tunakumbushana kuwa huku duniani tunahangaika na mapumziko ni ukifa.
Mkuu kabla ya kuzaliwa si ulipumzika mabilioni ya miaka sasa unataka upumzike nini tena na maisha ni miaka 50 tu ukiwa na nguvu ni 60!!
 

R.I.P eti, wanafikiri kule kaburini maiti anaenda kula bata au kutalii

R.I.P❌❌❌❌❌
إنا لله وإنا إليه راجعون ✔✔✔✔✔✔✔
 
Kwanini unasema hakuna kitu chochote kile kipo baada ya kifo?
Baada ya kifo wapi?

Kifo ndio mwisho wa uwepo wa kitu hapa duniani.

Sasa kama unadhani kuna kitu kipo baada ya kifo, inabidi ueleze kinakuwepo sehemu gani tofauti na hii Universe ambayo ipo.
Hakuna kitu nje ya space, time na universe kwa ujumla.

Kila kitu hata kifo kipo ndani ya universe, time and space.

Nje ya hapo hakuna kitu.
 
Mkuu na mimi nmekuja kumodify, kuna theories zangu nyingi tu zinafanyiwa tafiti au kwa sababu mimi ni mmatumbi mwenzako, tena mtangagiza , ndio maana hauniamini mpaka galileo?
labda sababu upo na fake ID huenda nakufahamu . Kama unayo ikawa tested na verified lazima watu was mini na tuanze kutumia.
Hao wote walifanya chunguzi baadae watu wakaja kuziboresha zaidi. Na wapo waliokuja na theories nyingi zikawa criticised na watu wakaja kuzifanyia tafiti Ilya na zikazaa matunda.
Ndio maana nikakuuliza Kwanini unasema sayansi ilishatoa majibu wakati sayansi ya mwaka 1800 si hii ya mwaka 2023. Sababu ya kukua kwa teknolojia Kwanini unahitimisha kwamba hakuna kitu? Kwanini usiseme hatujui sababu maendeleo ya sayansi yanavyokua May be somedays in future miaka 500 kutakuwa na majibu?
Sijui kama unaelewa lakini🤣🤣
 
Kuuuuuuuuuuba babake weka weka wekaaaaaaaa
Humu tu humu tu
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…