Kuvunja undugu na ndugu zako wa damu wanaokutakia mabaya ni kosa?

Kuvunja undugu na ndugu zako wa damu wanaokutakia mabaya ni kosa?

Mwizukulu mgikuru

JF-Expert Member
Joined
Oct 21, 2021
Posts
5,715
Reaction score
13,739
Wasalam ndugu zangu wana JamiiForums, ni mara nyingine naleta kwenu mada nyingine.

Vitabu vya dini vimekuwa vikituhusia sana tusivunje undugu kwa matatizo au changamoto za hapa na pale zinazotokea aidha kwenye jamii zetu au familia zetu, lakini kumekuwa na sababu nyingi zinazopelekea ndugu kuchukiana na kupelekea kuchukiana maisha na hata wengine kufikia kutokuzikana.

Kwa mfano mimi miaka 10 nyuma niliwahi kupata kupewa kesi mbaya sana ya jinai iliyonifanya nikae gerezani miezi 6 lakini kuna baadhi ya ndugu walikuwa wanashangilia huku wakisema Mwizukulu Mgikuru ndio basi tena mshenzi yule.

Huyo anaeshangilia matatizo yako hujawahi kulala au kula kwake na pia hujawahi kumuomba msaada wa aina yoyote! Sasa ndugu wa aina hii wa nini wakuu? Ipo haja ya kuwa nae?
 
Habari wanajamii forum...naomba kuuliza tena kwa mara nyingine hawa jamaa wanaojiita ndugu zangu wa damu siwahitaji kabisa , japo imani yangu inanikataza nisiweke kinyongo kwa ndugu, moja ya mambo waliowahi kunifanyia ni kushangiria nilipopata matatizo, siku nimekamatwa nikapelekwa gereza moja kubwa huko kanda ya ziwa jamaa walifanya party😁😁 ..wakawa wanatangaza mwizukulu mgikuru ndio basi tena kwisha habari yake, nauliza watu kama hawa kuvunja huu ujamaa uchwara si ni sawa kabisa😎
 
Habari wanajamii forum...naomba kuuliza tena kwa mara nyingine hawa jamaa wanaojiita ndugu zangu wa damu siwahitaji kabisa , japo imani yangu inanikataza nisiweke kinyongo kwa ndugu, moja ya mambo waliowahi kunifanyia ni kushangiria nilipopata matatizo, siku nimekamatwa nikapelekwa gereza moja kubwa huko kanda ya ziwa jamaa walifanya party😁😁 ..wakawa wanatangaza mwizukulu mgikuru ndio basi tena kwisha habari yake, nauliza watu kama hawa kuvunja huu ujamaa uchwara si ni sawa kabisa😎
Uliwaona we mwenyewe wakifurahia shida zako au ulisimuliwa?
 
Habari wanajamii forum...naomba kuuliza tena kwa mara nyingine hawa jamaa wanaojiita ndugu zangu wa damu siwahitaji kabisa , japo imani yangu inanikataza nisiweke kinyongo kwa ndugu, moja ya mambo waliowahi kunifanyia ni kushangiria nilipopata matatizo, siku nimekamatwa nikapelekwa gereza moja kubwa huko kanda ya ziwa jamaa walifanya party😁😁 ..wakawa wanatangaza mwizukulu mgikuru ndio basi tena kwisha habari yake, nauliza watu kama hawa kuvunja huu ujamaa uchwara si ni sawa kabisa😎
Wamekuonyesha kwamba wao ni ndugu Jina hivyo fanya mambo yako kwa usahihi ila usiwashilikishe mambo yako kiundani sana.Ahsante
 
Hata wasipokutakia mabaya unaruhusiwa kuvunja undugu tu, ni haki yako ya kikatiba.

Kwani kuna mtu kakulazimisha undugu?
 
Back
Top Bottom