Kuwe na mkakati maalumu wa kupunguza idadi ya Wakazi katika mkoa wa Dar es Salaam

Kuwe na mkakati maalumu wa kupunguza idadi ya Wakazi katika mkoa wa Dar es Salaam

Nilisema population Tanzania ni ticking timebomb.

Tanzania ina average annual population increase ya 3%.

Na hapa hujaona kitu, population ya Dar inaenda ku double in the next 10 years.

Ila kuna watu ukiwaambia habari za uzazi wa mpango unagombana nao.

Wanasema Tanzania ni nchi kubwa inahitaji watu.
Pia dar inaongezeka watu kwa sababu ya watu kuhamia ila rate ya kuzaliana kwa dar ni ndogo sana.. ifanyike namna watu wapende kuhamia na miji mingine... kama walivyofanya Dodoma
 
Serikali itengeneze mazingira rafiki mkoa wa pwani ili mji utanuke... kwa kiasi flani wamefanikiwa kwa kata ya mapinga.. ipo bagamoyo lakini ina vibe ya dar.. hata hivyo dar bado sana kuna miji kama kinshassa au cairo ina population za mil 20 huko
Cairo Wamisri wanajenga mji mpya kupunguza watu.

Kinshasa hatuwezo kuiga matatizo.

Kuna haja ya kuwa na miji mingi mizuri yenye huduma zote na fursa watu wasikimbilie kuishi Dar.

Jana nilikuwa naangalia nguminza Mike Tyson, akatokea Shaquille O'Neal anahojiwa. Akaukizwa umekuja lini Dallas Texas kuangalia ngumi. Akasema naishi Dallas. Yani huyu ni mtu wa Newark/New York City, kaamua tu aende kuishi Dallas na anapata kila kitu anachotaka huko.

Tatizo Tanzania kuishi hivyo ni vigumu, karibu kila kitu kipo Dar. Huko kwingine miji bado saana.
 
Nilisema population Tanzania ni ticking timebomb.

Tanzania ina average annual population increase ya 3%.

Na hapa hujaona kitu, population ya Dar inaenda ku double in the next 10 years.

Ila kuna watu ukiwaambia habari za uzazi wa mpango unagombana nao.

Wanasema Tanzania ni nchi kubwa inahitaji watu.
Wanakuambia kilichoifikisha China haipo ilipo (big economy) ni watu! Tuzaliane kwa kasi na sisi tuwe kama China.

Ndivyo wanavyosema vibarazani huko wakiungwa mkono na wanasiasa ambao mwisho wao wa kuona ni next election.
 
Kuna umasikini wa fikra na kukosa ubunifu.

Miji kama Tanga na Mtwara ina kila kitu, mpaka bandari, hakuna sababu iwe underdeveloped kama ilivyo sasa.
Ukii-develop kasi ya kuzaliana inajiongeza automatically kuhakikisha inai-underdevelop. The root cause is uncontrolled population increase.
 
Pia dar inaongezeka watu kwa sababu ya watu kuhamia ila rate ya kuzaliana kwa dar ni ndogo sana.. ifanyike namna watu wapende kuhamia na miji mingine... kama walivyofanya Dodoma
Nakuelewa.

Tatizo ni kwamba, Dar hata kama rate ya kuzaliana ni ndogo, kwa watu wengi rate ndogo ni watu wengi.

Ukiwa na watu milioni 7 kwa Dar na vitongoji vyake, na una rate ya kuzaliana %2.8, ambayo ndiyo tunaita ndogo kwetu, kwa mwaka hapo unaongeza watu karibu laki mbili kwa kuzaliana tu, kabla hata ya wahamiaji.

Miji mingine watu hawawezi kuhamia kama hakuna fursa za kiuchumi na huduma za jamii zinazofuatwa Dar.
 
Nilisema population Tanzania ni ticking timebomb.

Tanzania ina average annual population increase ya 3%.

Na hapa hujaona kitu, population ya Dar inaenda ku double in the next 10 years.

Ila kuna watu ukiwaambia habari za uzazi wa mpango unagombana nao.

Wanasema Tanzania ni nchi kubwa inahitaji watu.
tanzania ina watu mil 70+, china ni bil 2 hio bomb unayoongelea iko wap
 
Wanakuambia kilichoifikisha China haipo ilipo (big economy) ni watu! Tuzaliane kwa kasi na sisi tuwe kama China.

Ndivyo wanavyosema vibarazani huko wakiungwa mkono na wanasiasa ambao mwisho wao wa kuona ni next election.
Hapana.

China haijafika hapo ilipo kwa kuwa na watu wengi.

China imekuwa na watu wengi kwa siku nyingi sana, mpaka watu wengi wakafa kwa njaa kwenye The Big Leap Forward na The Cultural Revolution chini ya Mao.

Watu wamekufa kwa njaa, watu walikuwepo wengi, lakini hakukuwa na mpango mzuei wa kutumia nguvukazi yao.

Kilichoifikisha China hapo ilipo ni kujipanga kwenye teknolojia na viwanda kujua kuwatumia watu wake kuzalisha kwa ufanisi kwenye uchumi wa dunia.

Kwa maneno mengine, ukiongeza watu tu kwa kutegemea kuongeza watu ndiyo kuongeza uchumi, bila mkakati wa kujua utawatumiaje hao watu, unaweza kuongeza midomo ya kulisha tu, watu wakafa kwa njaa.

Inatakuwa kabla hujaongeza watu ujue utawasomesha wapi, utawatibu vioi, watafanya kazi gani, uwe na mipango ya kuitumia hiyo nguvukazi, usiende kwa kudra tu.
 
Serikali itekeleze baadhi ya mambo tunayoyasoma vyuoni kuna cozi tumesoma zinazungumzia namna ya kuwa na balansi kwenye idadi ya watu kwenye miji ya nchi husika sasa ukicheki hakuna balansi mfano jiji kama mbeya halina international school hata moja halina mall halina hotel ya nyota tano hospital ya mkoa unakuta ina ct scan machine mbili nazo hazifanyi kazi kwa hivi vitu baadhi vimefanya watu kadhaa waamua kujazana dar kufuata vitu hvyo sasa balance itatoka wapi

Jiji linalofuqtia baada ya dar lilitakiwa liwe na at least nusu ya idadi ya watu wa dar lkn sivyo
Peleka the best social services kwenye miji mingine automatically population will distribute normally.

If I were the government for example, kwa majiji yote ningejenga the best referral hospitals halafu all government primary schools medium of instruction would be English huku nikiilazimisha Dar es Salaam kubaki Kiswahili. Mbona watu wangehama wenyewe!
 
tanzania ina watu mil 70+, china ni bil 2 hio bomb unayoongelea iko wap
Sasa unataka kulinganisha Tanzania na China kweli?

Tanzania ambayo haina hata maandishi yake na China yenye civilization ya maelfu ya miaka?

Unaelewa hata kanuni za kulinganisha vitu?

Unaelewa kuwa kuna vitu havilinganishiki na ukivilinganisha unachekesha?
 
Ukii-develop kasi ya kuzaliana inajiongeza automatically kuhakikisha inai-underdevelop. The root cause is uncontrolled population increase.
Mkuu,

Trend ya dunia nzima inaonesha development inasababisha kasi ya kuzaana kupungua.

Ndiyo maana Eurooe na North America wana low fertility rate.

Development inaenda na wanawake kusoma zaidi, wanawake kusoma zaidi kunaenda na umri wa kuolewa kuongezeka, umri wa wanawake kuilewa kuongezeka kunasababisha wanawake kuzaa watoto wachache zaidi.

Hata hapo Tanzania fertility rate ya Dar ni 2.8 wakati Simiyu ni 6.6.
 
Kuna mikoa mingi ya kui endeleza lakini hakili zao wao zipo dar
Ile sera ya majimbo ilibezwa but they had vision. Mahali ambao no competetion hakuna maendeleo. China for example, kuishi Guangzhou, au Hong Kong, au Nanjing, an Shanghai, au Beijing, and elsewhere it does make any difference in any aspect. Ubora wa huduma utakayoipata mji A ndio ile ile utaipata mji B. Kwanini watu warundikane sehemu moja kama viazi.
 
Serikali itengeneze mazingira rafiki mkoa wa pwani ili mji utanuke... kwa kiasi flani wamefanikiwa kwa kata ya mapinga.. ipo bagamoyo lakini ina vibe ya dar.. hata hivyo dar bado sana kuna miji kama kinshassa au cairo ina population za mil 20 huko
Una kichaa wewe


Unalinganisha Cairo yenye square kilometers 4000 na far yenye square kilometers 1500
 
Mkuu,

Trend ya dunia nzima inaonesha development inasababisha kasi ya kuzaana kupungua.

Ndiyo maana Eurooe na North America wana low fertility rate.

Development inaenda na wanawake kusoma zaidi, wanawake kusoma zaidi kunaenda na umri wa kuolewa kuongezeka, umri wa wanawake kuilewa kuongezeka kunasababisha wanawake kuzaa watoto wachache zaidi.

Hata hapo Tanzania fertility rate ya Dar ni 2.8 wakati Simiyu ni 6.6.
Ha ha ha! Wasukuma kwa uzazi tumetisha!
 
Serikali kupitia mamlaka husika hasa mipango miji, ingepunguza au kuweka idadi kamili ya wakazi katika mkoa wa Dar es Salaam.

Dar es Salaam watu wamerundikana sehemu moja kuanzia makazi hadi vyombo vya usafiri.

Sasa kwa nia njema kwanini kusiwe na mpango wa ku zuwia ongezeko la idadi ya watu kuhamia Dar na badala yake wapelekwe maeneo mengine kwani nchi yetu ni kubwa kijografia.

Hii itasaidia hata wakati wa majanga iwe rahisi maeneo mengi kufikika kwaajili ya kutoa msaada kwa haraka na kuokoa maisha ya watu na mali zao.

Watu waende kama ni kwaajili ya shughuli za biashara na kuondoka na si kujenga makazi.

Wakazi wa Dar karibuni Tandaimba, Handeni, Kasulu, Biharamulo, Nachingwea, Newala, Same na maeneo mengine.

Maisha bila kukimbilia na kujazana Dar es Salaam yanawezekana.
Hata ingekua wewe ni wa daslam ungekubali kweli uende nje ya TANZANIA?
Maana mikoani kote hadi duniania ukitaja mzizima ndo unaongelea Tz
Uko kwenu mpitimbi/chululumo wanahisi unawatoa watu nje ya dunia kwanza wanaogopa hata kuulizia ni wapi!?
 
Hatari, usukumani mtaji ni watu, Geita ingekua bado ipo Mwanza basi dar ingekua ishiapitwa kwa watu na mwanza.
Yani huko simiyu kwa wastani nyumba moja ina watu watano+ .. huku town mageto ya mtu mmoja mmoja kibao
Watoto watano walio hai; na wengine kama nane hivi kwa mama huyo huyo walikufa at infancy kwa sababu mbalimbali including imani potofu. Kule watu wanabeba mimba sio mchezo.
 
Na hiyo ingekuwa si tatizo kama watu wanaokuja Dar wangekuwa productive, kama kungekuwa kuna viwanda wanafanyia kazi, kama wangekuwa wamejiingiza katika digital/information economy wanafanya kazi kwenye mitandao na kuingiza fedha nchini.

Lakini, hata hao wanaokija Dar wengi wao ni Wamachinga na wabangaizaji tu.

Yani hata mtu akitaka kujiingiza kwenye uchumi wa mitandaoni, serikali imedhibiti hata njia za kumlipa ni tatizo. Watanzania inawabidi wawalipe Wakenya ili kutumia Paypal accounts za Kenya, wengine wanalipa as much as 30% ili kuweza kulipwa Paypal. Hii ni kodi inawafanya Wakenya wafaidi bila kufanya lolote.

Yani serikali si tu haisaidii wananchi kujijenga kiuchumi, hata pale wananchi wanapojiongeza wenyewe bila kusaidiwa na serikali, serikali inawazibia wasiendelee.
Humu mbugila wengi mzee hakuna uthubutu na hakuna viongozi wenye mipango na matazamio mapya. Tanzania kwa ushubwada ndo nyumbani
 
Viongozi wameweka vitu vyote vizuri huko Dar - hospital, barabara, n.k na hawataki kuondoa.
Mfano ndogo, kila mbunge hata wa Nanjilinji hujenga huko Dar.
 
Back
Top Bottom