Kuweka au Kutokuweka WhatsApp status: Kuna uhusiano na mtu kuwa smart, msomi au tajiri?

Kuweka au Kutokuweka WhatsApp status: Kuna uhusiano na mtu kuwa smart, msomi au tajiri?

Haya mambo YA status waachieni wanawake.
Wanawake huwa wanatumia status kuchambana na show offf za kijinga

Mimi binafsi status sijawahi kuweka na sina muda wa kuangalia status ya mtu

Watu wamekuwa watumwa kwenye mitandao. Vitu wanvyovitafuta kwenye hizo posts au status ni likes, followers, views, comments kutoka kwa watu.

Wengine wanapokosa hivyo vitu wanaanza kujiona hawana thamani au hawapendwi (inferiority) na depression inaanza. Huu ni utumwa ambao umejificha

Mtu anapost halafu kila wakati anatembelea post yake kuona kuna likes ngapi au je watu wanacomment? Au anapost kutafuta attention ili aongeze followers. Huu ni utumwa
 
Kuna mtu humu nina namba zake huu mwaka unaenda wa pili, ila hata siku moja sijawahi muona akiweka status ama akiview zangu.

Siku nyingine naweka naset aone yeye mwenyewe lakini zitamaliza masaa 24 sioni akiview

Watu wa hivyo wana shida gani? Ni utu uzima au ndio wako busy hawana muda na status??

Bado nawashangaaa aisee
Si utu uzima ,Wala ushamba au chochote!Ni maamuzi tu. Mfano Mimi siweki kabisa status,kwa sababu naziona irrelevant,hazina maana.Hivyo tu.
 
Kuna kasumba naona imezidi kushamili kuwa mtu aliweka status kwenye simu ni mtu ambaye sio smart maana mwanaume au mwanamke mwenye heshima zake humkuti na mambo ayo ya status kwenye simu au kuwa online mara kwa mara au pia kuwepo kwenye magroup. Je, hili lina uhalisia wowote?
We sema tu kuwa hupendi kuweka status..!! Sasa usichokipenda usitutake tukusaidie kukichukia..!!
 
Kuna kasumba naona imezidi kushamili kuwa mtu aliweka status kwenye simu ni mtu ambaye sio smart maana mwanaume au mwanamke mwenye heshima zake humkuti na mambo ayo ya status kwenye simu au kuwa online mara kwa mara au pia kuwepo kwenye magroup. Je, hili lina uhalisia wowote?
Sio kuweka ila kuna wale wanaoweka kama mipasho na kuchamba watu, so hapo akili ndogo utaijua tu
 
Mimi siweki sana status, naweza kukaa hata miezi sita sijaweka, sio nataka kuonekana matured huwa naona tu uvivu, halafu huwa nahisi kama nikiweka najichoresha tu lakini za watu naangalia na kuzifurahia.
 
Kupitia Whatsapp utajua watu smart na Hawa wenzangu na Mimi

1. Mtu smart huwezi mkuta kaweka DP ya picha yake Whatsapp

2. Mtu smart huwezi kuta anaweka mastatus mara kwa mara na akiweka basi ujue ni jambo muhimu sana ambalo anataka kufikisha ujumbe kwa njia hiyo

3. Mtu smart hana muda wa ku view status za watu, ila hapa Kuna wa aina 2 Kuna ambao Hawa view kabisa na Kuna wale ambao wana view lakini wakiona unapost pumba au unajipost sana wanakukataa Hawa view tena

Wale wenzangu na Mimi wanaenda kinyume chake
Kwamba mtu smart ni yule anaeweka mistari ya bibilia na picha za Yesu?
 
Kwangu status ni sehemu ya kuwachanganya watu wasiyajue maisha yangu halisi japo sivimbi wala kufanya showoffs ila ninachopost kwa mtu anaetarajia kujua maisha yangu basi ataniona ni mtu wa hali ya chini sana mda mwingine post zangu zinatoa fundisho kwakua hata akionyesha ulicho nacho haibadili kitu chochote zaidi utajiletea marafiki wasio na tija maishani. status zangu zimenifanya niwe na marafiki wachache wasio thamini vitu ambao ni wakweli na wako makini[emoji41]
 
Kuna mtu humu nina namba zake huu mwaka unaenda wa pili, ila hata siku moja sijawahi muona akiweka status ama akiview zangu.

Siku nyingine naweka naset aone yeye mwenyewe lakini zitamaliza masaa 24 sioni akiview

Watu wa hivyo wana shida gani? Ni utu uzima au ndio wako busy hawana muda na status??

Bado nawashangaaa aisee
Sio anatumia gb watsup ana view lakini wewe huoni
 
Mimi siweki sana status, naweza kukaa hata miezi sita sijaweka, sio nataka kuonekana matured huwa naona tu uvivu, halafu huwa nahisi kama nikiweka najichoresha tu lakini za watu naangalia na kuzifurahia.
Tumefanana akili

Tofauti yetu ni moja tu mimi nime hide view kwahyo nikiziangalia hawajui kama nimeangalia halafu siangalii zote naangalia zile za wapenda kupost meme
 
Back
Top Bottom