Kuweka Records Sawa: Utaratibu alioupendekeza Shabiby ndio uliokuwepo kabla, Haufai

Kuweka Records Sawa: Utaratibu alioupendekeza Shabiby ndio uliokuwepo kabla, Haufai

Wakuu Kwema?

Mimi kwa kiasi fulani ni mdau wa mafuta, kwani hapo kabla miaka ya nyuma nilishawahi kufanya kazi katika kampuni ya mafuta Kwa kama miaka kadhaa Hivi

Hivi karibuni Mbunge wa Gairo Bw. Ahmed Abdallah Shabiby amependekeza kua ili Bei ya mafuta iweze kushuka basi Serikali iruhusu Wafanyabiashara binafsi waagize mafuta hayo.

Napenda kuweka taarifa sawa tu kua Utaratibu huu anaoupendekeza Bw. Shabiby utumike ndio uliokuwepo hapo awali. Serikali ilikuja kuubadilisha huu utaratibu kutokana na sababu au mapumgufu yake kadhaa, na chache nitazitaja hapa chini.

Kwanza ni ku avoid "Transfer Pricing". Yaani kampuni A iliyopo Tanzania ni tawi la Kampuni B iliyopo labda S.A. Sasa kampuni B ndio inayonunua mafuta inakokujua kisha inaiuzia kampuni A ya hapa nchini kwa bei kubwa kuliko bei ya soko.

Sasa kampuni A ya hapa katika hesabu zake za kodi ya faida 30%x (Mapato - Matumizi) inajikuta inalipa kodi kidogo sababu gharama za uendeshaji zimekua kubwa kutokana na gharama kubwa za manunuzi ya mzigo. Kwa mtindo huu kampuni zingine hufikia hata kuandika wamepata hasara (Manunuzi + Gharama zingine vimezidi Mapato). Kifupi kampuni hukwepa kodi kwa kusingizia gharama kubwa za manunuzi kumbe humo humo anapomlipa Kampuni Mama na faida au dividend anasafirishia hapo hapo kinyemela.

Sababu ya pili Mpaka Serikali ikaondoa utaratibu huu ni kufaidi "Discount on Bulk Purchases". Yaani kampuni 10 zikinunua labda lita million 10 kila moja ni tofauti na kampuni moja ikinunua lita 10mil x 10 = Lita 100mil. Huyu anaenunua lita nyingi ni rahisi ku bargain na kupewa Discount kubwa tofauti na yule anaenunua kidogo. Discount hiyo hupelekea unafuu wa bei Mwishowe kwa finale user.

Tatu ni kua na records za mafuta yaliyoko nchini. Yaani soko likiwa holela kila mtu anaagiza mnaweza kushindwa kujua hata mahitaji ya nchi kwa kipindi husika ni kiasi gani. Hii pia huwezesha Serikali kukadiria (bajeti) Kodi itakayokusanywa kutokana na mafuta haya.

Nne ni kupata bidhaa iliyo bora na standard. Kutokana na Bei mbalimbali zinazosababishwa na ubora mbalimbali basi wengine wanaweza kuchukua au kuagiza hata yale yenye ubora wa chini sababu tu ya unafuu wa bei bila kujali athari zake kwenye matumizi yake. Standard hapa ni viwango vifanane kati ya kampuni moja na ingine. Kusiwe na tofauti kati ya anaejazia BP/Puma au yule anaejazia Oilcom (Ceteris Peribus).

Tano ni kuondoa mafuta ya magendo kwenye soko. Since Mnunuzi wa kutoka nje atakua ni mmoja tu na ndie atakaewasambazia Makampuni ya ndani then kunapunguza uwezekano wa mafuta mengine yasiyolipiwa ushuru kuingia kwenye soko.

Sita, Kwa kuagiza pamoja kunaleta uniformity kwenye Bei. Ingawa Labor na Other Overhead Expenses zaweza kua tofauti lakini bei ya kununulia bidhaa ambayo ndio huchukua sehemu kubwa ikiwa sawa basi Bei hazitapishana sana. Ingawa bei Hupangwa na Ewura lakini kipindi hicho huu utaratibu unawekwa ni Makampuni yenyewe yalikua yanajipangia Bei baada ya kukukokotoa Gharama mbalimbali za kuanzia Manunuzi na Undeshaji pia.

Saba, Kuzuia kuficha mafuta. Kampuni zingeweza kusema hazina mafuta (lower supplies) ili kutengeneza Demand kubwa then bei zipande. Lakini since uagizaji na/kisha ugawaji wa mafuta hufanywa Kwa pamoja then ni rahisi kujua stock ya kila kampuni. Hivyo si rahisi kwa Kampuni husika kuficha taarifa za mafuta iliyo nayo.

Sababu zilikuwa nyingi, nimejaribu kukumbuka chache. Inawezekana mazingira ya wakati ule yangechochea tuhamie kwenye uagizaji wa pamoja labda sababu hizo sio valid anymore so turudi tu kule kule tena. Nimeona kama (nilieliekua) mdau wa mafuta basi nisikae kimya watu wafikiri kua hatujawahi kua katika huo utaratibu alioupendekeza Bwana Shabiby.

Muwe na Siku njema.
Sababu zilikuwa na mashiko kipindi hicho ila kwa sasa hakuna maana kwa sababu kama ni Kodi kuna valuation systems mpya,kila taarifa unaipata kwenye mtandao kwa hiyo janja janja inakuwa imepunguzwa..

Pili swala la quality kuna TBS,ishu ya kuficha mafuta Ili bei zipande halina msingi kwa sababu mafuta yanayoingia yanajulikana na yanayotumika yanajulikana.. kampuni zikiwa nyingi hiyo cartels ni ngumu Sana..

Hili la mafuta ya magendo inawezekana ila yakiingia hayawezi kuuzwa Kwa bei ya Juu,lakini pia hayawezi kuwa mengi kwa kiasi hicho maana utayasafitishaje bila kugundulika?..

All in all kinachotakiwa ni mafuta yauzwe Kwa bei ya chini ambapo chini ya bulk procurement imeshindikana kupata huo unafuu na in fact bei inakua moja..

Mwisho hivi kampuni za biashara ya mafuta zitakua vipi kwa staili hii ya bulk procurement ikiwa mnalazimishwa kununua kwa wauzaji wakubwa wachache na Kwa bei ambayo wamepanga wao na Serikali?..

Huu utaratibu licha ya kutotoa nafuu ya bei kwa wananchi unawanufaisha makampuni makubwa wachache na maofisa wa serikali, wengine nyie mtaishia kama kuwa mawaka wao..

Duniani kote mafuta yanaagizwa na kampuni binafsi tofauti tofauti,suala la kuwa na mafuta ya akiba ni la serikali kupitia tpdc/puma hao ndio wawe na reserves za kuja ku offset in case kuna scenarios kama ya kuficha mafuta au upungufu wa kawaida...

Mwaka juzi somewhere around 2018 mafuta yaliadimika na bulk procurement ilikuwepo so hii sio sababu ya msingi Ili mafuta yasiadikike.
 
Ukitumia common sense vizuri utaona analosema shabbiby haliwezekani, bei kushuka kwa 50% maana yake ni kuwa mafuta yauzwe sh 1400 kwa lita ya diesel!! Bei hii haipo kokote duniani, Epra Kenya ambao ndio leguratory board kama ilivyo ewura kwetu , wametangaza bei mbaya sana kwa mafuta kwa mwezi huu huko kenya
Shabiby anasema mafuta yauzwe 1,400 lakini kodi za Serikali takriban TZS 1,000 au zaidi zisiguswe sababu ndizo zinazolipa au kununua madawa. Means kuna uwezekano wa kupata mafuta ya mpaka TZS 300/Litre CIF.

"Burden of Proof" hapa ni iko kwa Shabiby kutuambia wapi tutapata kwa hii Bei. Amesema Deep See unaweza kupata kwa mpaka 1/4 price ya world market price, Serikali umuombe awasaidie details za huko wakayachukue wakishajiridhisha ubora na Usalama wake .
 
K
Shabiby mpigaji tu!
Kumbe ! Mafuta ni Kila kitu,mazao shambani,uzalishaji viwandani,usafiri na usafirishaji, tunataka bei nafuu ya mafuta.hiyo Bulk imeundwa na kina nani?isije kuwa wanaofanya biashara ya mafuta ndio wanaajaza kwa pamoja na sisi tunasema ni Bulk kumbe ni cartel.hatutaki 'monopoly' kama si kwa ushindani,basi serikali iunde kampuni ya kununua na kusambaxza mafuta ,si. TIPPER !,kwa nini hapo TU bei ili hali kwani wap eaweze na sisi tushindwe_why !
 
Nimeiskiliza kwa umakini mkubwa clip ya Shabiby. Kwa wakati huu wa vita ya urusi bulk procurement sio njia sahihi ya kuagiza mafuta nje! Kwa sababu kampuni inayotumika inachukua mafuta iliyowagonga vikwazo Russia. Hii ina maana wamebadili soko na hivyo hili likampuni ni la EU.
Hii ni fursa kwa kampuni kuagiza nje mafuta kwa bei nafuu...kwani huyo Mrusi tu kwa sababu ya vikwazo ameshusha bei ya mafuta yake up to 600 per litre.
Sasa 600 tukaweka na vikodi uchwara vyao hapo. Yakauzwa 1200 siye wananchi tutakuwa na shida gani?
Shabiby kasema wazi kuwa hako kakamati kanakosiamamia bulk procurement na kenyewe kanapiga cha juu vizuri tu kwenye hizo bei za kuagiza.

Faida ulizozielezea hapo kwa bulk procurement ni nzuri lakini haziondoi ukweli kuwa bulk procurement kwa kipindi cha vita inaumiza wananchi.
 
Nimeiskiliza kwa umakini mkubwa clip ya Shabiby. Kwa wakati huu wa vita ya urusi bulk procurement sio njia sahihi ya kuagiza mafuta nje! Kwa sababu kampuni inayotumika inachukua mafuta iliyowagonga vikwazo Russia. Hii ina maana wamebadili soko na hivyo hili likampuni ni la EU.
Hii ni fursa kwa kampuni kuagiza nje mafuta kwa bei nafuu...kwani huyo Mrusi tu kwa sababu ya vikwazo ameshusha bei ya mafuta yake up to 600 per litre.
Sasa 600 tukaweka na vikodi uchwara vyao hapo. Yakauzwa 1200 siye wananchi tutakuwa na shida gani?
Shabiby kasema wazi kuwa hako kakamati kanakosiamamia bulk procurement na kenyewe kanapiga cha juu vizuri tu kwenye hizo bei za kuagiza.

Faida ulizozielezea hapo kwa bulk procurement ni nzuri lakini haziondoi ukweli kuwa bulk procurement kwa kipindi cha vita inaumiza wananchi.
Watanzania mnapenda sana magendo!
 
Wakuu Kwema?

Mimi kwa kiasi fulani ni mdau wa mafuta, kwani hapo kabla miaka ya nyuma nilishawahi kufanya kazi katika kampuni ya mafuta Kwa kama miaka kadhaa Hivi

Hivi karibuni Mbunge wa Gairo Bw. Ahmed Abdallah Shabiby amependekeza kua ili Bei ya mafuta iweze kushuka basi Serikali iruhusu Wafanyabiashara binafsi waagize mafuta hayo.

Napenda kuweka taarifa sawa tu kua Utaratibu huu anaoupendekeza Bw. Shabiby utumike ndio uliokuwepo hapo awali. Serikali ilikuja kuubadilisha huu utaratibu kutokana na sababu au mapumgufu yake kadhaa, na chache nitazitaja hapa chini.

Kwanza ni ku avoid "Transfer Pricing". Yaani kampuni A iliyopo Tanzania ni tawi la Kampuni B iliyopo labda S.A. Sasa kampuni B ndio inayonunua mafuta inakokujua kisha inaiuzia kampuni A ya hapa nchini kwa bei kubwa kuliko bei ya soko.

Sasa kampuni A ya hapa katika hesabu zake za kodi ya faida 30%x (Mapato - Matumizi) inajikuta inalipa kodi kidogo sababu gharama za uendeshaji zimekua kubwa kutokana na gharama kubwa za manunuzi ya mzigo. Kwa mtindo huu kampuni zingine hufikia hata kuandika wamepata hasara (Manunuzi + Gharama zingine vimezidi Mapato). Kifupi kampuni hukwepa kodi kwa kusingizia gharama kubwa za manunuzi kumbe humo humo anapomlipa Kampuni Mama na faida au dividend anasafirishia hapo hapo kinyemela.

Sababu ya pili Mpaka Serikali ikaondoa utaratibu huu ni kufaidi "Discount on Bulk Purchases". Yaani kampuni 10 zikinunua labda lita million 10 kila moja ni tofauti na kampuni moja ikinunua lita 10mil x 10 = Lita 100mil. Huyu anaenunua lita nyingi ni rahisi ku bargain na kupewa Discount kubwa tofauti na yule anaenunua kidogo. Discount hiyo hupelekea unafuu wa bei Mwishowe kwa finale user.

Tatu ni kua na records za mafuta yaliyoko nchini. Yaani soko likiwa holela kila mtu anaagiza mnaweza kushindwa kujua hata mahitaji ya nchi kwa kipindi husika ni kiasi gani. Hii pia huwezesha Serikali kukadiria (bajeti) Kodi itakayokusanywa kutokana na mafuta haya.

Nne ni kupata bidhaa iliyo bora na standard. Kutokana na Bei mbalimbali zinazosababishwa na ubora mbalimbali basi wengine wanaweza kuchukua au kuagiza hata yale yenye ubora wa chini sababu tu ya unafuu wa bei bila kujali athari zake kwenye matumizi yake. Standard hapa ni viwango vifanane kati ya kampuni moja na ingine. Kusiwe na tofauti kati ya anaejazia BP/Puma au yule anaejazia Oilcom (Ceteris Peribus).

Tano ni kuondoa mafuta ya magendo kwenye soko. Since Mnunuzi wa kutoka nje atakua ni mmoja tu na ndie atakaewasambazia Makampuni ya ndani then kunapunguza uwezekano wa mafuta mengine yasiyolipiwa ushuru kuingia kwenye soko.

Sita, Kwa kuagiza pamoja kunaleta uniformity kwenye Bei. Ingawa Labor na Other Overhead Expenses zaweza kua tofauti lakini bei ya kununulia bidhaa ambayo ndio huchukua sehemu kubwa ikiwa sawa basi Bei hazitapishana sana. Ingawa bei Hupangwa na Ewura lakini kipindi hicho huu utaratibu unawekwa ni Makampuni yenyewe yalikua yanajipangia Bei baada ya kukukokotoa Gharama mbalimbali za kuanzia Manunuzi na Undeshaji pia.

Saba, Kuzuia kuficha mafuta. Kampuni zingeweza kusema hazina mafuta (lower supplies) ili kutengeneza Demand kubwa then bei zipande. Lakini since uagizaji na/kisha ugawaji wa mafuta hufanywa Kwa pamoja then ni rahisi kujua stock ya kila kampuni. Hivyo si rahisi kwa Kampuni husika kuficha taarifa za mafuta iliyo nayo.

Sababu zilikuwa nyingi, nimejaribu kukumbuka chache. Inawezekana mazingira ya wakati ule yangechochea tuhamie kwenye uagizaji wa pamoja labda sababu hizo sio valid anymore so turudi tu kule kule tena. Nimeona kama (nilieliekua) mdau wa mafuta basi nisikae kimya watu wafikiri kua hatujawahi kua katika huo utaratibu alioupendekeza Bwana Shabiby.

Muwe na Siku njema.
Good analysis. Inaonekana ni sekta yako unayoielewa vizuri.

JF ndivyo ilivyostahili kuwa. Kuna mambo kama member wa JF umatakiwa kuwasikiliza wataalam au wenye uelewa wa kutodha kwenye eneo hilo, japo haizuiwi kuuliza.

Bahati mbaya, siku hizi, JF kuna virukia njia, kila wakiona kitu, hata kama hawajui, wanarukia tu, tena kwa jeuri, jeuri ya kijinga.
 
Shabiby anasema mafuta yauzwe 1,400 lakini kodi za Deep See unaweza kupata kwa mpaka 1/4 price ya world market price, Serikali umuombe awasaidie details za huko wakayachukue wakishajiridhisha ubora na Usalama wake .
Serikali haiwezi kwenda deep sea

Kifupi kuna machinga wauza mafuta mengine ya wizi 'magendo nk huko deep sea.Mengine yanatoka nchi zilizowekewa vikwazo hivyo wenye business vya mafuta huamua kuyauza kwa magendo .Serikali na magendo wapi ns wapi

Shabby alichoshauri watu binafsi waachie hiyo shughuli Serikali isubiri Meli bandarini kachukue kodi zao mafuta bei rahisi waingie

Hizo meli zinaitwa Ro Ro kama sikosei ziko nyingi deep ni machinga waliochangamka ambao huuza bidhaa nyingi tu ikiwemo.mafuta

Huu no wakati muafaka Serikali iruhusu sekta binafsi waingize mafuta itashangaa. Mafuta ya bei chee yataingia
 
Safi sana. Nchi hii haija hawahi pungukiwa wazalendo. Mh Shabibu hakutaka kuweka wazi kitu kilicho sababisha serikali kuamua bulk procurement. Uzuri wenyewe alikiri Watanzania wa leo si wale wa mwaka 47.
hili aliliweka wazi kinaga ubaga

Shabiby kasema sababu ya kuletwa Bulk Procument System ni Wazungu wa TOTAL kulalamika ku loby serikalini kwamba Wahindi wa JAMNAGAR (walionunua GapOil na GapCo) wameshusha bei ya mafuta kupindukia walipokuja Tanzania.

BPS ilipoanzishwa JAMNAGAR akaona hakuna ushindani, business plan yake ya kuja Tanzania ilikuwa kushusha bei kuteka soko, akaondoka zake.

Bei zikafumuka tena.
 
Wakuu Kwema?

Mimi kwa kiasi fulani ni mdau wa mafuta, kwani hapo kabla miaka ya nyuma nilishawahi kufanya kazi katika kampuni ya mafuta Kwa kama miaka kadhaa Hivi

Hivi karibuni Mbunge wa Gairo Bw. Ahmed Abdallah Shabiby amependekeza kua ili Bei ya mafuta iweze kushuka basi Serikali iruhusu Wafanyabiashara binafsi waagize mafuta hayo.

Napenda kuweka taarifa sawa tu kua Utaratibu huu anaoupendekeza Bw. Shabiby utumike ndio uliokuwepo hapo awali. Serikali ilikuja kuubadilisha huu utaratibu kutokana na sababu au mapumgufu yake kadhaa, na chache nitazitaja hapa chini.

Kwanza ni ku avoid "Transfer Pricing". Yaani kampuni A iliyopo Tanzania ni tawi la Kampuni B iliyopo labda S.A. Sasa kampuni B ndio inayonunua mafuta inakokujua kisha inaiuzia kampuni A ya hapa nchini kwa bei kubwa kuliko bei ya soko.

Sasa kampuni A ya hapa katika hesabu zake za kodi ya faida 30%x (Mapato - Matumizi) inajikuta inalipa kodi kidogo sababu gharama za uendeshaji zimekua kubwa kutokana na gharama kubwa za manunuzi ya mzigo. Kwa mtindo huu kampuni zingine hufikia hata kuandika wamepata hasara (Manunuzi + Gharama zingine vimezidi Mapato). Kifupi kampuni hukwepa kodi kwa kusingizia gharama kubwa za manunuzi kumbe humo humo anapomlipa Kampuni Mama na faida au dividend anasafirishia hapo hapo kinyemela.

Sababu ya pili Mpaka Serikali ikaondoa utaratibu huu ni kufaidi "Discount on Bulk Purchases". Yaani kampuni 10 zikinunua labda lita million 10 kila moja ni tofauti na kampuni moja ikinunua lita 10mil x 10 = Lita 100mil. Huyu anaenunua lita nyingi ni rahisi ku bargain na kupewa Discount kubwa tofauti na yule anaenunua kidogo. Discount hiyo hupelekea unafuu wa bei Mwishowe kwa finale user.

Tatu ni kua na records za mafuta yaliyoko nchini. Yaani soko likiwa holela kila mtu anaagiza mnaweza kushindwa kujua hata mahitaji ya nchi kwa kipindi husika ni kiasi gani. Hii pia huwezesha Serikali kukadiria (bajeti) Kodi itakayokusanywa kutokana na mafuta haya.

Nne ni kupata bidhaa iliyo bora na standard. Kutokana na Bei mbalimbali zinazosababishwa na ubora mbalimbali basi wengine wanaweza kuchukua au kuagiza hata yale yenye ubora wa chini sababu tu ya unafuu wa bei bila kujali athari zake kwenye matumizi yake. Standard hapa ni viwango vifanane kati ya kampuni moja na ingine. Kusiwe na tofauti kati ya anaejazia BP/Puma au yule anaejazia Oilcom (Ceteris Peribus).

Tano ni kuondoa mafuta ya magendo kwenye soko. Since Mnunuzi wa kutoka nje atakua ni mmoja tu na ndie atakaewasambazia Makampuni ya ndani then kunapunguza uwezekano wa mafuta mengine yasiyolipiwa ushuru kuingia kwenye soko.

Sita, Kwa kuagiza pamoja kunaleta uniformity kwenye Bei. Ingawa Labor na Other Overhead Expenses zaweza kua tofauti lakini bei ya kununulia bidhaa ambayo ndio huchukua sehemu kubwa ikiwa sawa basi Bei hazitapishana sana. Ingawa bei Hupangwa na Ewura lakini kipindi hicho huu utaratibu unawekwa ni Makampuni yenyewe yalikua yanajipangia Bei baada ya kukukokotoa Gharama mbalimbali za kuanzia Manunuzi na Undeshaji pia.

Saba, Kuzuia kuficha mafuta. Kampuni zingeweza kusema hazina mafuta (lower supplies) ili kutengeneza Demand kubwa then bei zipande. Lakini since uagizaji na/kisha ugawaji wa mafuta hufanywa Kwa pamoja then ni rahisi kujua stock ya kila kampuni. Hivyo si rahisi kwa Kampuni husika kuficha taarifa za mafuta iliyo nayo.

Sababu zilikuwa nyingi, nimejaribu kukumbuka chache. Inawezekana mazingira ya wakati ule yangechochea tuhamie kwenye uagizaji wa pamoja labda sababu hizo sio valid anymore so turudi tu kule kule tena. Nimeona kama (nilieliekua) mdau wa mafuta basi nisikae kimya watu wafikiri kua hatujawahi kua katika huo utaratibu alioupendekeza Bwana Shabiby.

Muwe na Siku njema.
Shabiby anataka fursa atupige. Ule utaratibu uliondolewa sababu ulileta shida sana kwenye controls. Naona wanataka kuanza kumdanganya spika wapenyeze upigaji wao
 
Shabiby anasema mafuta yauzwe 1,400 lakini kodi za Serikali takriban TZS 1,000 au zaidi zisiguswe sababu ndizo zinazolipa au kununua madawa. Means kuna uwezekano wa kupata mafuta ya mpaka TZS 300/Litre CIF.

"Burden of Proof" hapa ni iko kwa Shabiby kutuambia wapi tutapata kwa hii Bei. Amesema Deep See unaweza kupata kwa mpaka 1/4 price ya world market price, Serikali umuombe awasaidie details za huko wakayachukue wakishajiridhisha ubora na Usalama wake .
Unaona. Sasa!!!
Mafuta ya deep see yanayouzwa rahisi ni mafuta ya magendo na hayana constant flow, kwamba utayapata kila siku,
Ni sawa tu na kununua simu ya dili kinondoni
 
hili aliliweka wazi kinaga ubaga

Shabiby kasema sababu ya kuletwa Bulk Procument System ni Wazungu wa TOTAL kulalamika ku loby serikalini kwamba Wahindi wa JAMNAGAR (walionunua GapOil na GapCo) wameshusha bei ya mafuta kupindukia walipokuja Tanzania.

BPS ilipoanzishwa JAMNAGAR akaona hakuna ushindani, business plan yake ya kuja Tanzania ilikuwa kushusha bei kuteka soko, akaondoka zake.

Bei zikafumuka tena.
Muhindi anapata wapi mafuta ya bei nafuu ilhali source ya mafuta ni moja na bei zinajulikana?
Nyanya sokoni zina bei tofauti sababu zinatoka sehemu mbali mbali na gharama za kuzilima zinatofautina , mafuta yana source moja mtu anaposema ana ya bei tofauti kabisa na ya soko , ni either ameyachakachua au ni ya deal.
 
Mafuta kufikia 3000 lazima itafutwe njia mbadala.
Ndio sababu ulaya zamani sanq walianza na hybrid car , electric nk. Ilikuwa ni swala la muda tu kabla hayajalipuka bei
 
Serikali haiwezi kwenda deep sea

Kifupi kuna machinga wauza mafuta mengine ya wizi 'magendo nk huko deep sea.Mengine yanatoka nchi zilizowekewa vikwazo hivyo wenye business vya mafuta huamua kuyauza kwa magendo .Serikali na magendo wapi ns wapi

Shabby alichoshauri watu binafsi waachie hiyo shughuli Serikali isubiri Meli bandarini kachukue kodi zao mafuta bei rahisi waingie

Hizo meli zinaitwa Ro Ro kama sikosei ziko nyingi deep ni machinga waliochangamka ambao huuza bidhaa nyingi tu ikiwemo.mafuta

Huu no wakati muafaka Serikali iruhusu sekta binafsi waingize mafuta itashangaa. Mafuta ya bei chee yataingia
Mkuu umepotoka kidogo , you may want to edit your post .
Roro sio meli za mafuta , ni meli ya kubeba mizigo hasa magari yanayotembea
Terminology Roro ina maana ya' Roll on and roll off' kwa maana gari litaingia na kutoka kwenye meli hiyo likiwa linatembea
Swaum njema
 
Mkuu umepotoka kidogo , you may want to edit your post .
Roro sio meli za mafuta , ni meli ya kubeba mizigo hasa magari yanayotembea
Terminology Roro ina maana ya' Roll on and roll off' kwa maana gari litaingia na kutoka kwenye meli hiyo likiwa linatembea
Swaum njema
Ok mfano meli kwa meli yenye mafuta na ingine haina mafuta zikisogeleana meli yenye mafuta ikipump mafuta kuingiza meli ingine inayopokea mafuta deep sea na kuondoka nayo kwenda nchi husika hiyo meli ina pump mafuta sio Roro?
 
Pambaneni na hali yenu na Sisi tupambane na hali yetu
IMG_6261.jpg
 
Back
Top Bottom