Kuweka Records Sawa: Utaratibu alioupendekeza Shabiby ndio uliokuwepo kabla, Haufai

Kuweka Records Sawa: Utaratibu alioupendekeza Shabiby ndio uliokuwepo kabla, Haufai

Brother,
Hapa ni rahisi tu. Kwenye gharama mbalimbali za mafuta kuna vitu ni constant/fixed, na kuna vitu ni variable.

Mfano wauzaji mbalimbali wanaweza kua na bei tofauti, au pia wasafirishaji nao wanaweza kua na bei tofauti pia kwa kila ujazo fulani. Lakini yakifika hapa Tanzania gharama za hapa ni constant kwa kila lita. Yaan TBS, TRA, Ewura, TPA, etc hatutaokoa chochote.

Sasa kama Shabiby anaweza kushusha kwa 50% means atacheza kwenye Muuzaji au Msafirishaji au wote wawili. Anaweza kua sahihi kama tu kuna uzembe unafanyika kwenye ku bargain bei ya hivi vitu viwili. Yaani Inawezekana hawa wanaoagiza mzigo mkubwa (Say 100mil litres kwenye mfano wangu wa awali) wanashindwa ku negotiate bei nzuri then akienda yeye na 10mil litres zake wamsikilize.

Au tuje pale pale kua yeye anaweza kupata ya bei rahisi zaidi bila kujali ubora wake tofauti na Wale wa Bulk ambao wanaweza kua too much selective kwenye ubora.

Ubora weka pembeni hilo kama ulivyoweka fixed costs kama zilivyo hapa:

IMG_20220408_065739_529.jpg


Issue ni CIF bargaining, usafiri na wapi yananunuliwa.

Umesahau kuwa yawezekana tunapigwa.

Timu kuagiza yaweza kuwa imesheheni wahuni mtupu!
 
Bei inaweza kuwa za chini na himilivu lakini ametoa tahadhari hapo kuwa mfumo anaopendekeza shabbiby ,kuna kampuni zinaweza agiza mafuta ya ubora wa kiwango cha chini .

Ubora ni kisingizio mjomba. Kwani TBS ana kazi gani?
 
Ubora ni kisingizio mjomba. Kwani TBS ana kazi gani?
Tbs wangekuwa wanakagua ubora kweli na wapo makini kusingekuewa na vitu feki kariakoo..
Tbs haina msaada kwa mwananchi wa kawaida ,
 
Hakuna bidhaa unaweza kuicontrol price yake kama huizalishi na wewe kwa kiasi kikubwa consumer tu.... Dunia haitutegemei kwa chochote il kwa kiasi kikubwa mpaka sasa tunaitegemea sana dunia watu wetu waweze kuishi..... Tuache ubwanyenye na kulialia, tuhimizane kuchapa kazi na kuweza kujifanyia mambo mengi either kwa kuwa na mitaji au technolojia..

Leo hii tunalialia bei ya mafuta wakati huko baharini tuna gas yakutosha, yapo maeneo kibao yameonyesha dalili za kuwa na mafuta, pale Songea kuna Uranium, kule Mbeya kuna helium...Ziwa Nyasa kuna mafuta pale live..Tuna mabwawa na mito kila mahala..

Tuache kulialia, Kizazi hiki na kingine kijitoa mhanga kuleta heshima, watu wafanye kazi na wafie huko kwenye kazi kuijenga Tanzania, Taifa halijengwi kwa watu kulialia na comedians, Taifa linajengwa kwa ushupavu na kujitolea kwa muda mrefu..

Leo hii mnataka mafuta ya bei rahisi wakati yanachimbwa na wengine huko vidume, mnataka urahisi wa maisha wakati nyie ni consumers tu, Mnajivunia rasilimari wakati hamuonyeshi dalili zozote za kuichakata zaidi ya kutegemea watu walete mitaji na akili zao...

Shida ya Africa na Tanzania ni watu wake wengi kuwa legelege na kuwaza maisha mazuri huku hakuna aliyeyaandaa zaidi ya siasa na ujinga ujinga tu..

Mnataka mafuta yashuke bei?, hata serikali leo hii ikitoa kodi zote kwenye mafuta bado tutaona ni gharama tu na tutataka wanaotuletea watupe bure maana tunapenda burebure.....Ukiwa masikini duniani utaonewa, utadharaulika, utadhulumiwa na kila aina ya uhuni utafanyiwa..... Russia yule asingekuwa strong leo angeshapotea, lakini babu zao akina Stalin na Lenin walipiga kazi kwelikweli na kulifia Taifa na hatimaye wakaleta vizazi strong kama akina Putin, Lavrov, Abrahamovic nk..

Acha uongo mjomba kodi ni zaidi 100% kwenye mafuta:

IMG_20220408_065739_529.jpg


Na hapo wahuni bado hamjafanya yenu.
 
Sasa ndugu mdau hebu tueleze . juzi tumeambiwa mafuta yapo ya kutufikisha siku 27. Lakini juzi ewura wametangaza bei mpya na zimeanza kutumika hapohapo , kwanini isingesubiriwa hizo siku 27 ziishe Ndo bei zibadilike?
Mafuta yaliyoletwa yanatosha hizo siku, huwezi leta meli moja kwa wakati, zinakuja nyingi kwa muda fulani

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Basi na bidhaa za kariakoo ziagizwe kwa uagizaji wa pamoja kama mafuta.
Tbs wangekuwa wanakagua ubora kweli na wapo makini kusingekuewa na vitu feki kariakoo..
Tbs haina msaada kwa mwananchi wa kawaida ,
 
Tbs wangekuwa wanakagua ubora kweli na wapo makini kusingekuewa na vitu feki kariakoo..
Tbs haina msaada kwa mwananchi wa kawaida ,

Hii ndiyo inahalalisha sasa kuwa kwa mawazo ya Shabiby tutaelewana mafuta feki?

Uchakachuaji si huwa unafanyika humu humu nchini?

Kama TBS haina kazi kwanini kuendelea kuwa mzigo kwetu?
 
Hii ndiyo inahalalisha kuwa kwa mawazo ya Shabiby tutaelewana mafuta feki?

Uchakachuaji si huwa unafanyika humu humu nchini?
Ukimsoma mtoa mada kuna sababu nyingi zaidi ya uchakachuaji
 
Ukimsoma mtoa mada kuna sababu nyingi zaidi ya uchakachuaji

Una maslahi yoyote na bei kubwa kwenye mafuta ndugu?

Kwanini nguvu kubwa hivi kuhalalisha bei kubwa hata pasipokuwa sababu?
 
Tafuta Bei za 2011 kurudi nyuma, anachosema shabiby ni kweli Ila serikali ilikua inashindwa kuwabana kwenye mapato.
2008 kama sijakosea tulivuka 2250 kwa Lita na kukikuwa hamna vita huko Ukraine...
 
Una maslahi yoyote na bei kubwa kwenye mafuta ndugu?

Kwanini nguvu kubwa hivi kuhalalisha bei kubwa hata pasipokuwa sababu?
Sina maslahi yoyote kwenye bei kubwa, ila pia sio mtu wa kusikikiza na kukubali kika ninaloambiwa just because nipo kwenye shida au hali ngumu,

Bei za mafuta zipo juu, lakini hao kina shabiby ni wapigaji tu kama wapigaji wengine , kuna kitu wameona kunawabana kwenye mfumo huu wa kuagiza kwa pamoja , kwa mfumo ukiopo sasa tuna access na mafuta bora sana maana hakuna loopholes
Kuna madudu mengi sana kwenye ule mfumo wa kika mtu kuagiza , na wala bei haitashuka kama anavyosema shabiby .
Sana sana serikali itapoteza mapato
 
Kwa nini kuandikia mate? Shabiby anaahidi bei kupungua chini ya 50%?

Kwanini asipewe nafasi kama Masudi Kipanya ku prove gari lake la umeme?
Sasa anashindwaje kuleta mafuta ya bei chee hata sasa? Mfumo wa BPS unashindanisha kampuni zote interested kuingiza mafuta na unatoa tenda kwa kampuni iliyo na bei ya CHINI kupita zote. Kwa akili za kawaida hapo Shabiby anazuiwa vipi kampuni yake kuomba kwa bei ya chini (lowest bidding price) ili kuingiza mafuta kwa bei ya chini? Kwanini kwenye mchango wake hakuelezea sababu za serikali kuachana na mpango wa zamani (anaoupendekeza) na kuingia kwenye mpango mpya?
 
Sina maslahi yoyote kwenye bei kubwa, ila pia sio mtu wa kusikikiza na kukubali kika ninaloambiwa just because nipo kwenye shida au hali ngumu,

Bei za mafuta zipo juu, lakini hao kina shabiby ni wapigaji tu kama wapigaji wengine , kuna kitu wameona kunawabana kwenye mfumo huu wa kuagiza kwa pamoja , kwa mfumo ukiopo sasa tuna access na mafuta bora sana maana hakuna loopholes
Kuna madudu mengi sana kwenye ule mfumo wa kika mtu kuagiza , na wala bei haitashuka kama anavyosema shabiby .

Kwanini kuandikia mate? Kwanini umeng'ang'ania kuandikia mate? Kwamba bei hazitashuka kwa ubora ule ule kwani wewe ni Kerubi?
 
2008 kama sijakosea tulivuka 2250 kwa Lita na kukikuwa hamna vita huko Ukraine...
Hawaelewi hawa vijana wa juzi akili zao ziko whatsapp na Facebook tu. Shabiby anajua vizuri anachokisema ila anajua watanzania mazwazwa hivyo atapata wafuasi wengi tu. Infact, kama sio mfumo huo wa pamoja mafuta yangekuwa yamefika 5000 kwa lita siku nyingi.
 
Back
Top Bottom