Kuwekwa kwa somo ya Kiislamu kwenye Tahasusi kunaashiria nini?

Kuwekwa kwa somo ya Kiislamu kwenye Tahasusi kunaashiria nini?

Mimi nimesoma divinity kwenye shule ambayo baba yangu kailipia nje ya ile kodi aliyotoa. Hatuhitaji serikali iingie kwenye kazi ya kufundisha walimu wa dini. Kama hamuwezi kusomesha watu wenu wenyewe tafuteni njia mbadala isiyotumia kodi yangu. Naweza kuwa kafiri lakini si ni kodi yangu? Maana yatawekwa kwenye shule za umma na sisi ndicho kitu hatukitaki. Shule za umma zifundishe masomo ya kawaida. Za dini ziongeze masomo ya dini yake hawakatazwi. Kuna box likiwa na nyoka wakali hutakiwi kulifungua unatakiwa kulichoma.
Haaaaaa,kumbe wewe mfia divinity
Ndio maana unapiga kelele

Madam ya Jana Islamic knowledge, baada yakuwaumbua mnajifanya hamtaki dini zote
 
Wengi nadhani hawajui maana ya Divinity,wamezoea Bible knowledge,limewachanganya wengi wasiofuatilia mambo ya Dini,na kubaki wakristo kwa majina tu,hata X nimekuta post nyingi za kuchekesha.......
Naijua divinity na nimeisoma. Ila niliisomea Sanu seminary na sio kwenye shule ya umma. Sikutumia kodi ya mtu kuisoma. Pia sitaki kodi yangu itumike kumsomesha mtu. Kama unataka kusoma masomo hayo kuna seminari kibao za kuyapata. Shule za umma zifundishe kiswahili, uraia, chemistry, Biology na mengineyo
 
Na sijui kwa nini mnauchukia uislamu mbona sisi hatuwachukii nyinyi.
Wanajifanya wanatupenda (unafiki)

Ni watu wa kulalamika tu kwa Kila kheri na Shari

Nyuzi za kumpondea Bakhresa haziishi humu kisa muislamu
 
Naijua divinity na nimeisoma. Ila niliisomea Sanu seminary na sio kwenye shule ya umma. Sikutumia kodi ya mtu kuisoma. Pia sitaki kodi yangu itumike kumsomesha mtu. Kama unataka kusoma masomo hayo kuna seminari kibao za kuyapata. Shule za umma zifundishe kiswahili, uraia, chemistry, Biology na mengineyo
Kwa unavyoona mtoa post anaijua maana ya divinity??

Waliokuwa wanachangia Tanzania sio nchi ya dini moja, Samia anatugawa, wote wanajua maana ya divinity?
 
Haaaaaa,kumbe wewe mfia divinity
Ndio maana unapiga kelele

Madam ya Jana Islamic knowledge, baada yakuwaumbua mnajifanya hamtaki dini zote
Bro ukisoma kuanzia mwanzo nipo clear. Hata huko kwenye ukristo kuna wanaoamini sanamu na wasioziamini. Kwa ajili ya afya njema ya taifa letu tuondoe vyote. Kila mmoja afundishe watoto wake dini sehemu anayoiona inafaa. Kesho ikitokea shule ya kikristo imekataa kufundisha islamic wakati inao hao wanafunzi si rashba zitaanza? Kuepuka matatizo tufundishane sunday school na madrasa. Siamini kwamba hatuna uwezo huo. Tumefanya kwa miaka 62. Saudia wao ni dini moja, haijuzu somo la dini kuwepo kwenye mtaala. Huku tuna mchanganyiko. Tuache wakati bado tunaweza.
 
Naijua divinity na nimeisoma. Ila niliisomea Sanu seminary na sio kwenye shule ya umma. Sikutumia kodi ya mtu kuisoma. Pia sitaki kodi yangu itumike kumsomesha mtu. Kama unataka kusoma masomo hayo kuna seminari kibao za kuyapata. Shule za umma zifundishe kiswahili, uraia, chemistry, Biology na mengineyo
Unadhani waliofikiria kuweka hawajui wanachokifanya?
 
Kwa hyo dini tu ndo unaona matumizi mabaya ya kodi?
Watu wanajipigia mapesa huko, wanalipana Hadi wake wa viongozi Kisha unaona kwa masomo ya dini ndio Kodi yako inatumika vibaya?

Ule mkataba wenu wa mahospitali hamuoni kama mnatumia vibaya Kodi za serikali?
 
Kwa unavyoona mtoa post anaijua maana ya divinity??

Waliokuwa wanachangia Tanzania sio nchi ya dini moja, Samia anatugawa, wote wanajua maana ya divinity?
Hata kama haijui mimi ni rai yangu kama mmoja wa Watanzania dini tuziache kwenye misikiti na makanisa. Tusizilete kanisani. Nikiangalia udini wa wakenya unanifundisha kitu. Kuna siku yanakuja kuwa makubwa kumbe tungeweza kuyaepuka. Tusiangalie sura zetu, dini zetu au kabila zetu kwenye kufundisha. Tuwaachie walioteuliwa na Mwenyezi Mungu waifanye kazi yao maana wataulizwa
 
Waache wasome. Kuna watu wamesoma tahsusi kwa kufuata Dira ya Maendeleo ya Taifa ya kutaka wataalamu wa aina gani lakini baada ya kugraduate hawana kazi. Hao watakaosoma hayo masomo ya dini kama hayana muelekeo ya wa Dira ya Taifa ya kutaka kujua miaka kadhaa ijayo dunia inataka wataalamu wa aina gani wasome. Ila watambue tu kuwa kwa sasa hata walimu waliokuwa wanapata direct post kuna batch nyingi zipo mtaani sasa wewe n divinity au Islamic yako utakuja kuwa nani? Atheist uweke Arabic kwakuwa nj language uamue kuwa deepest lingualist. Otherwise utakuja kukutana na mkwamo hata wa principle za kuongia chuo.
Wakumbusheni hii kuna statement ya TCU I nasema "three principle amongst neither divinity nor Islamic.
 

Attachments

  • Screenshot_20240321-200843.png
    Screenshot_20240321-200843.png
    131.6 KB · Views: 3
Acha ujinga weka hoja, kwa nini mlalamike Islamic knowledge wakati huo huo kuna divinity?


Muamzisha uzi na wachangiaji ikiwemo wewe mmekurupuka na chuki zenu zilizopitiliza.

Mnajadili why Islamic knowledge??


na mnajifanya hamjui kuwa divinity ipo

Huna hoja bali kuleta kwa screen shot hii ya divinity katika combination kunadhihirisha utahira wenu
• Hoja gani sasa unayotaka, Toka thread hii imeaza hujaona hoja humu,? Hoja zimejitosheleza mkuu..., Ndo maana nasema kama hujaona hoja yoyote humu.. Ujue uwezo wako wa kufikiri ni mdogo.

------------------------

Minong'ono na maneno ya kujigamba kuwa mimi ni nani na wewe ni nani, yaliaza kutokea pale bandari ilipotakiwa kusimamiwa na kampuni isiyoeleweka ya D. P. W, machawa kila pande ya Tanzania waliibuka na kuisifia D. P. W, machawa wengine walifika mbali Zaidi nakufikia hatua ya kutukana viongozi wa dini kule Upande wa pili. INASIKITISHA SANA KUWA NA BINADAMU WA AINA HII HAPA TANZANIA walio kosa weledi wakuchanganua mambo kwa manufaa ya baadae.

TAHASUSI/COMBINATION zina udini ndani yake,
• Mambo haya yanayo husiana na udini, hupandikizwa taratibu taratibu lakini mwisho wa siku hugeuka kuwa bomu lisilozimika hata kwakulimwagia damu.

• Udini, au upendeleo usiofaa kwa dini moja dhidi ya nyingine, unaweza kuleta athari mbaya kwa jamii na nchi kwa ujumla.
Tunaweza tusiyaone haya kwa sasa lakini siku za baadae mambo yatakuwa hatari sana:-
|• Mgawanyiko wa Kijamii, Udini husababisha watu kutengana kulingana na imani zao za kidini, hivyo kuvuruga umoja na mshikamano miongoni mwao

||• Mzozo na Vurugu, udini unachochea migogoro na vurugu, hasa ikiwa makundi ya kidini yanahisi kutengwa au kubaguliwa katika nchi husika.

|||• Ubaya katika Utoaji Haki, unasababisha upendeleo katika nafasi za ajira, elimu, na huduma za serikali, ambapo watu wanapendelewa au kunyimwa fursa kulingana na dini zao.

|V• Kupungua kwa Uaminifu kwa Taasisi, Udini unapokithiri katika serikali na taasisi nyingine, kuna uwezekano wa kupungua imani ya wananchi kwa uadilifu wa taasisi hizo, hivyo kudhoofisha utawala wa sheria na demokrasia.

V• Ukosefu wa Ustawi wa Kiuchumi, Udini uleta kutengwa kwa makundi fulani ya kidini kutoka kwenye shughuli za kiuchumi, kusababisha ukosefu wa usawa na kuzuia maendeleo ya kiuchumi kwenye jamii.

V|• Kupunguza Utalii na Uwekezaji, Migogoro ya kidini inaweza kuathiri taswira ya nchi kimataifa, hivyo kupunguza idadi ya watalii na kuwatia hofu wawekezaji.

V||• Uharibifu wa Mali na Maisha, Migogoro ya kidini inaweza kusababisha uharibifu mkubwa wa mali na hata kupoteza maisha, kugharimu jamii na nchi kwa ujumla.

• Kupambana na udini na kujenga jamii inayovumiliana na kuheshimu tofauti za kidini ni muhimu kuwa na amani, ustawi, usawa kimajukumu na maendeleo endelevu ya jamii.
 
Unadhani waliofikiria kuweka hawajui wanachokifanya?
Hawajui. Kuna wakati zelous ya dini inaweza kukufanya ukashindwa kufanya maamuzi sahihi. Mwelekeo wa taifa sio mali ya kiongozi tu. Inahitaji mjadala mpana wa wote wanaonufaika na kuumizwa kwa maamuzi hayo. Wote tuna sauti sawa kwenye kuamua kesho ya Tanzania. Dini sio kipaumbele chetu maana kiti chetu hajakabidhiwa mungu wa dini yeyote. Tuna nchi yenye wapagani, wakristo na waislambu, mabudha na wahindu. Je tuanze kufundisha ram au ng'ombe ni mungu kwa vile wahindu wanamwabudu? Tuwaachie wenye dini zao.
 
• Hoja gani sasa unayotaka, Toka thread hii imeaza hujaona hoja humu,? Hoja zimejitosheleza mkuu..., Ndo maana nasema kama hujaona hoja yoyote humu.. Ujue uwezo wako wa kufikiri ni mdogo.

------------------------

Minong'ono na maneno ya kujigamba kuwa mimi ni nani na wewe ni nani, yaliaza kutokea pale bandari ilipotakiwa kusimamiwa na kampuni isiyoeleweka ya D. P. W, machawa kila pande ya Tanzania waliibuka na kuisifia D. P. W, machawa wengine walifika mbali Zaidi nakufikia hatua ya kutukana viongozi wa dini kule Upande wa pili. INASIKITISHA SANA KUWA NA BINADAMU WA AINA HII HAPA TANZANIA walio kosa weledi wakuchanganua mambo kwa manufaa ya baadae.

TAHASUSI/COMBINATION zina udini ndani yake,
• Mambo haya yanayo husiana na udini, hupandikizwa taratibu taribu lakini mwisho wa siku hugeuka kuwa bomu lisilozimika hata kwakulimwagia damu.

• Udini, au upendeleo usiofaa kwa dini moja dhidi ya nyingine, unaweza kuleta athari mbaya kwa jamii na nchi kwa ujumla.
Tunaweza tusiyaone haya kwa sasa lakini siku za baadae mambo yatakuwa hatari sana:-
|• Mgawanyiko wa Kijamii, Udini husababisha watu kutengana kulingana na imani zao za kidini, hivyo kuvuruga umoja na mshikamano miongoni mwao

||• Mzozo na Vurugu, udini unachochea migogoro na vurugu, hasa ikiwa makundi ya kidini yanahisi kutengwa au kubaguliwa katika nchi husika.

|||• Ubaya katika Utoaji Haki, unasababisha upendeleo katika nafasi za ajira, elimu, na huduma za serikali, ambapo watu wanapendelewa au kunyimwa fursa kulingana na dini zao.

|V• Kupungua kwa Uaminifu kwa Taasisi, Udini unapokithiri katika serikali na taasisi nyingine, kuna uwezekano wa kupungua imani ya wananchi kwa uadilifu wa taasisi hizo, hivyo kudhoofisha utawala wa sheria na demokrasia.

V• Ukosefu wa Ustawi wa Kiuchumi, Udini uleta kutengwa kwa makundi fulani ya kidini kutoka kwenye shughuli za kiuchumi, kusababisha ukosefu wa usawa na kuzuia maendeleo ya kiuchumi kwenye jamii.

V|• Kupunguza Utalii na Uwekezaji: Migogoro ya kidini inaweza kuathiri taswira ya nchi kimataifa, hivyo kupunguza idadi ya watalii na kuwatia hofu wawekezaji.

V||• Uharibifu wa Mali na Maisha, Migogoro ya kidini inaweza kusababisha uharibifu mkubwa wa mali na hata kupoteza maisha, kugharimu jamii na nchi kwa ujumla.

• Kupambana na udini na kujenga jamii inayovumiliana na kuheshimu tofauti za kidini ni muhimu kwa amani, ustawi, na maendeleo endelevu ya jamii.
Wengi hasa wenzetu wa upande wa pili wanafikiri tuna chuki nao. Hatuna tunatamani tuwe wamoja. Tukianza kubaguana kidini tutakuja kikanda then kikabila. Kenya na Rwanda ni mifano mizuri ya madhara ya ukabila. Ethiopia kuna mapigano ya kidini. Tusipokemea na kupaza sauti zetu leo tutaambulia damu za watoto wetu na wajukuu. Tumeishi kwa amani miaka yote je kimepungua nini? Kama hukuweza kukatazwa kuiba kwenu unafikiri kuisoma biblia kutakusaidia?
 
Wengi hasa wenzetu wa upande wa pili wanafikiri tuna chuki nao. Hatuna tunatamani tuwe wamoja. Tukianza kubaguana kidini tutakuja kikanda then kikabila. Kenya na Rwanda ni mifano mizuri ya madhara ya ukabila. Ethiopia kuna mapigano ya kidini. Tusipokemea na kupaza sauti zetu leo tutaambulia damu za watoto wetu na wajukuu. Tumeishi kwa amani miaka yote je kimepungua nini? Kama hukuweza kukatazwa kuiba kwenu unafikiri kuisoma biblia kutakusaidia?
• Kasumba ya hawa jamaa ni:-

1. Hata liwe baya vipi, akitenda Muslim, wao ni kuchekelea tu.

2. Hata liwe zuri vipi, akitenda Mroma, wao ni kusema sisi tuna chuki, mara makafiri.
 
Back
Top Bottom