Kuweni makini na hakikisheni mkitoa pesa benki mnapata ujumbe wa salio lililobaki

Wacha kutumia atm ...pia waambie wakupe video ya saa ambayo pesa imetolewa kwenye atm kuna camera ....benki sikuizi zimekuwa kama ccm kuna organise crime ya wafanyakazi wao ndiyo wanafanya huo uhuni
Itakuwa kwa wakala. ATM huwezi kutoa 500k, unatoa kwa mafungu ya laki nne nne tu.
Ila kuwa Makini na msg unayotumiwa, 50,000 inasomeka kirahisi kama 500,000.
Wasiliana na benk yako uwe unapata msg Kila unapotoa hela
 
Bank wezi. Two weeks nmejitumia $200 kwenye akaunti ila ajabu wamedeposite kwa akauntu 400000 tu.
 
Elimu...elimu...elimu

Kuna haja ya mabenk kutoa elimu ya kutosha kwa wateja wao.

Ile statement pia inahitaji elimu kwenye kuisoma....
 
Watu mna hela sana yaan uibiwe laki5 usijue miezi mitatu?😂 alaf cha kushangaza unalia lia kuhusu hiyo 12k.

Anyway.. kuna mawili mtu ana pass zako au ww umejichanganya maybe ni mlevi etc, ingawa ukitoa hela huw kuna ujumbe unatumwa ktk namba yako ya simu. (Kama huna hii huduma sikupi pole ni uzembe wako).

Kiuhalisia wizi ambao utafanywa na wahudumu wa Banks ambao wapo smart ni wa kuchomoa kiasi kidogo mnoo cha hela ambacho ww hutaweza kugundua au kufatilia..

Mfano kwa kila mwezi anafilter accounts zenye zaidi ya laki 1+ kisha anachomoa tsh 100 tu kwa kila account.

Mfano, ktk hiyo process akichomoa Tzs 100 ktk accounts 100k ina maana atakuwa na mil 10 ambazo hazina maswali. Huo ndio wizi smart unaofanyika kila mara..
 
Si waangalie kwenye camera jamani, mbona roho mbayaa hivyoo
 
Kama ni chini ya million 60 Rudi ukachukue zote zilizobaki uweke kwenye laini 4 za simu
 
Ha ha ha hii ilimkutaga demu wangu wakati anasoma chuo hakuwa na bom alikuwa Analipiwa na kakaake yupo nje ya nchi alikuwa anamtumia pesa kwa western union kisha anakuja anaziweka bank alikuwa anatumia Akiba ya pale MWANANYAMALA komakoma akawa anatoa pesa kwenye zile ATM za umoja hakuwa anaangalia salio yaan alikuwa achukui list
Sasa siku hiyo akachukua list kucheck ndio anakuta zaidi ya laki mbili hakuna
Ikawa mzozo mkubwa kanipigia simu kwenda kumsaidia ikabidi tufanye mpango wa kuacess CAMERA kuangalia ni mdogo wake ndo alikuwa anatoa hizo ela km mara tano hivi alianza na 10000 akawa kila akiishiwa anapandusha dau mara ya mwusho alitoa 5000
akasema basi yaishe atafanyaje unadhani atampeleka mdogo wake polisi

Timbwili ndo akaenda kimuazishia mdogo wake DOGO akajifanya kukataa weee walipigana halafu walikuwa wamepishana miaka 5 wote wanawake
Mama yao ndo aliamua huo ugomvi
Mimi ugomvi wa ndugu sikuingila
 
Pole Sana, kuna system itakuwa haipo Sawa, pia nilipatwa na tatizo Hilo kwenye simu, hela unapotea tu lakini nilipofatilia inaonyesha ni mimi mwenyewe natoa wakati siyo hivyo, kuna system itakuwa inajivuruga.
 
Kwenye statement inaonesha alietoa alitoa kwa njia gani, ATM wakala au ndani.

Kama ndani au ATM kuna camera iyo siku, lipia elfu 15 kisha wa access.

Kama ni kwa wakala ndio ujue wakala gani wa wapi na alietoa alikua nani na alitumia simu au card.
Mtoa mada chukua hii
 
Ilinitokea hiyo, Nilitoa kwa card NMB Wakala hapo Kariakoo yule wakala mpaka leo namkumbuka, baada ya kutoa fedha kiasi cha 300,000 nikaondoka baada ya kuona message imeingia kwenye simu kwamba umetoa kiasi cha sh 300,000 kutoka kwa wakala ABC... sasa kumbe message zimeingia mbili za miamala ya 300k, ila kwasababu ya haraka utaona ile message moja tu, au hata ukiona mbili utasema labda ni mtandao tu, Sasa kumbe yule wakala amefanya miamala miwili ya laki tatu jumla 600k ila cash aliyonipa mkononi ni 300k. Sikuhangaika kuwaza au kuangalia salio. Baada ya siku kadhaa kupita nikasema ngoja niangalio salio, Lahaula! Nakuta 300k haipo na sielewi imeenda wapi! Chap nikaenda NMB Bank nikaomba statement, kuangalia nakuta ile siku niliyotoa 300k kumbe ilikuwa 600k! Yaani miamala inaonekana miwili imefuatana.Wakanipa barua nikafuate hiyo 300k iliyobaki kwa yule wakala, wakaniambia au kama nimepasahau wao wanaweza kuwasiliana naye, bahati nzuri nikapakumbuka, nikarudi nikamuonyesha vielelezo vyote, wala hakua mbishi, chap akanivutia 300k yangu nikatembea.

Fikiria wangapi wanaofanya miamala midogo wala hawaangalii salio au bank statement wanaibiwa kiasi gani? Ina maana nisingeshtuka ndiyo ingekuwa basi tena😀
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…