Kuzaa mapema sio kupata msaada/ suluhu za uzeeni

Kuzaa mapema sio kupata msaada/ suluhu za uzeeni

Japokuwa maisha yenyewe hayana fomula maalum ila ikija Kwenye suala la kuzaa lazima vigezo Fulani vizingatiwe;

1.Ukomavu wa kiakili na kihisia
2.Uwezo wa kiuchumi
3.Utayari wa kuzikabili changamoto zitakazotokea kwenye uzazi na mengineyo.
 
Mkuu jamaa pale mwanzo kaichambua dhana ya kuchelewa kuzaa, ila wengi wenu naona mmekomalia kwenye umri hamgusii uchumi na afya ya akili.

Mtu anaweza kua na 30 yrs lakini akili ya kitoto, kujisimamia yeye tu hawezi huyo anaachwa akue kwanza. Akizaa akiwa na akili hizo atatafsiriwa kama kazaa mapema.
Hata kama tukitazama suala la uchumi na afya ya akili, nayo kwangu bado nayaona mepesi vile vile.

Mfano ukizungumzia uchumi, hebu niambie, ni muda gani ambao una hakika ukifika, mtu fulani atakuwa amefanikiwa kiuchumi? baada ya kumaliza chuo na kupata ajira? hiyo ajira itapatikana lini? isipopatikana huyu mtu aendelee kusubiri tu mpaka siku ifike yakufanikiwa asiyoijua?!

Hata kama ni biashara, tunaona biashara ngapi zinakufa kila siku? kwa hiyo hawa waendelee kusubiri tu mpaka siku mifuko yao itakapotuna ndio wapate watoto? hii hoja yenu kwangu haina maana.

- Afya ya akili, ukiondoa mazezeta na machizi, binafsi sioni kama kuna mtu mwingine tofauti na hao mwenye tatizo la afya ya akili, mnachofanya hapa kinaweza kuwa ni sawa na kuingilia maamuzi ya wengine, nothing else.
 
Mkuu, kwani baba anatakiwa awe na muonekano gani? Ni muonekano gani sahihi kwa mtu anayeitwa baba?
Kiuhalisia kuna baba na babu, huo ndio mpangilio wa kibinadamu, sasa nyie kama wengine mtataka kubadilisha baba ndio awe babu, hiyo ni uamuzi wenu, lakini kimsingi umri wa baba hauwezi kufanana na ule wa babu.
 
Hata kama tukitazama suala la uchumi na afya ya akili, nayo kwangu bado nayaona mepesi vile vile.

Mfano ukizungumzia uchumi, hebu niambie, ni muda gani ambao una hakika ukifika, mtu fulani atakuwa amefanikiwa kiuchumi? baada ya kumaliza chuo na kupata ajira? hiyo ajira itapatikana lini? isipopatikana huyu mtu aendelee kusubiri tu mpaka siku ifike yakufanikiwa asiyoijua?!

Hata kama ni biashara, tunaona biashara ngapi zinakufa kila siku? kwa hiyo hawa waendelee kusubiri tu mpaka siku mifuko yao itakapotuna ndio wapate watoto? hii hoja yenu kwangu haina maana.

- Afya ya akili, ukiondoa mazezeta na machizi, binafsi sioni kama kuna mtu mwingine tofauti na hao mwenye tatizo la afya ya akili, mnachofanya hapa kinaweza kuwa ni sawa na kuingilia maamuzi ya wengine, nothing else.
Afya ya Akili ni muhimu hii watu hawajui Mimi dada zangu wote wamezalia nyumbani na hawana kipato wanategemea sisi wajomba zao so usichukulie powah swala la Afya ya Akili .
 
Kwa
Kiuhalisia kuna baba na babu, huo ndio mpangilio wa kibinadamu, sasa nyie kama wengine mtataka kubadilisha baba ndio awe babu, hiyo ni uamuzi wenu, lakini kimsingi umri wa baba hauwezi kufanana na ule wa babu.
Hamna chochote ebu angalia Maisha ya Sugu au Jay z
 
Zaa Kwa wakati hiyo ndio meaning.
Kwa nini uwahi mapema au uchelewe?
Wewe hueleweki na hiki ulichoandika, umeandika kwa mafungu ndio maana kinapoteza maana.

Mfano unaposema mtu azae kwa wakati, huo wakati ni upi? atakapofanikiwa kiuchumi? lini? kwamba aendelee kusubiri tu mpaka siku isiyojulikana afanikiwe kiuchumi ndio awe na familia? huku ndiko kunasababisha baba aje kuitwa babu na watoto wake wa kuwazaa mwenyewe, hope mmenielewa na wenzio wenye mtazamo kama wako.
 
Afya ya Akili ni muhimu hii watu hawajui Mimi dada zangu wote wamezalia nyumbani na hawana kipato wanategemea sisi wajomba zao so usichukulie powah swala la Afya ya Akili .
Hao dada zako kwanini msiwaambie wapeleke hao watoto kwa baba zao? dada zako ni wajinga, na nyie ni wazembe, hilo sio tatizo la afya ya akili.
 
Wewe hueleweki na hiki ulichoandika, umeandika kwa mafungu ndio maana kinapoteza maana.

Mfano unaposema mtu azae kwa wakati, huo wakati ni upi? atakapofanikiwa kiuchumi? lini? kwamba aendelee kusubiri tu mpaka siku isiyojulikana afanikiwe kiuchumi ndio awe na familia? huku ndiko kunasababisha baba aje kuitwa babu na watoto wake wa kuwazaa mwenyewe, hope mmenielewa na wenzio wenye mtazamo kama wako.

Wakati WA MTU na mtu unatofautiana ndio maana nikaandika kuwa Ukomavu WA kiumri katika hisia na Akili, na kujitegemea na kutegemewa ndio Wakati Sahihi.

Sasa sijui ulitaka niandike miaka 20-30 au 40-45
 
Kiuhalisia kuna baba na babu, huo ndio mpangilio wa kibinadamu, sasa nyie kama wengine mtataka kubadilisha baba ndio awe babu, hiyo ni uamuzi wenu, lakini kimsingi umri wa baba hauwezi kufanana na ule wa babu.
Kuna dhana unashindwa kuielewa.

Wewe ni mtu mzima sasa hivi, je baba yako utamuita babu kwasababu umri wake umeenda?
 
Ukichelewa sana watoto wako watakuja kukuita babu badala ya baba.
Ukizaa mapema ndo unazeeka mapema angalia Kuna yule mzee yupo 70 hana Mtoto wala familia ila yupo poa.

Angalia Kuna msanii moja hapa bongo wa kike maarufu na ana pesa yupo 40's hana Mtoto ila kama kijana .


Unapozaa ndo unazee kwa majukumu
 
Kweli kabisa kiongozi nakubaliana na wewe. Kuzaa mapema kunakufanya uwezo kuwajibika malezi ilihali unanguvu lakin sio uzae mapema halafu mzigo wa malezi unaupeleka kwa wazazi.

Naishi kwenye jamii moja unakuta kijana hana kazi wala shughuli yoyote familia inamtafutia mke na mahari ili aoe kwa kigezo tu amefika wa kuoa. Baada ya ndoa anamleta mke nyumbani lkn anayehudumia familia ni wazazi. Kwa kiasi fulani ndo maana hata umasikini haupungui kwa sababu ya mila na desturi zilizopitwa na wakati.

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Kweli kabisa kiongozi nakubaliana na wewe. Kuzaa mapema kunakufanya uwezo kuwajibika malezi ilihali unanguvu lakin sio uzae mapema halafu mzigo wa malezi unaupeleka kwa wazazi.

Naishi kwenye jamii moja unakuta kijana hana kazi wala shughuli yoyote familia inamtafutia mke na mahari ili aoe kwa kigezo tu amefika wa kuoa. Baada ya ndoa anamleta mke nyumbani lkn anayehudumia familia ni wazazi. Kwa kiasi fulani ndo maana hata umasikini haupungui kwa sababu ya mila na desturi zilizopitwa na wakati.

Sent using Jamii Forums mobile app

Hapo lazima kuna mmoja lazima alambe mchanga. Hasa huyo muolewaji
 
Hakuna kitu kisicho na formula.
HAPANA Hapa Umekosea Kidogo Kipo Kitu Ambacho Hakina Formula Kinaitwa "MAISHA" Maisha Hayana Formula Mkuu MAISHA YANGEKUWA NA FORMULA WOTE TUNGEKUWA MATAJILI MANA HAKUNA ANAE UPENDA UMASIKINI.... KWA MFANO HUU TU MIMI NIMEJIFUNZA KWAMBA MAISHA HAYANA FORMULA

"MAISHA SIO HESABU ZA KUGAWANYA ZILE... MANA MTU UNAWEZA KUTA JANA ALIKUWA NA HELA NYINGI MARA KESHO HANA HATA MIA"
 
HAPANA Hapa Umekosea Kidogo Kipo Kitu Ambacho Hakina Formula Kinaitwa "MAISHA" Maisha Hayana Formula Mkuu MAISHA YANGEKUWA NA FORMULA WOTE TUNGEKUWA MATAJILI MANA HAKUNA ANAE UPENDA UMASIKINI.... KWA MFANO HUU TU MIMI NIMEJIFUNZA KWAMBA MAISHA HAYANA FORMULA

"MAISHA SIO HESABU ZA KUGAWANYA ZILE... MANA MTU UNAWEZA KUTA JANA ALIKUWA NA HELA NYINGI MARA KESHO HANA HATA MIA"

Huwezi sema Maisha hayana Formula, sema Watu wengi hawajui formula ya Maisha.
Ikiwa Jambo Fulani haujui formula yake haimaanishi Jambo Hilo halina Formula.

Kama huijui Formula ya maisha, aliyeyaleta Maisha anaijua formula yake.
 
Back
Top Bottom