Kuzaliana kunamsaidia nini kiumbe anayezaa?

Kwa sababu genes zake zinamsukuma katika subconscious kuwa na muendelezo wake hapa duniani.
Kuna mambo ni magumu kuelewa. Na kwanini mtu anapenda kuwa na mtoto?
 
Tukitafakari kijuujuu tutakosa majibu lakini tukitafakari kwanini Mungu aliumba dunia tutapata jibu.Iko hivi,kila kitu alichokiumba Mungu humu duniani kiko kwa sababu,kuna tunavyo ona sasa kwamba vimeumbwa na tukajua sababu yake,na vingine kwa uwezo wetu mdogo bado hatujajua kwanini vipo,lakini ni swala la muda tu,itafika mahali tutajua sababu,kwani sio kila kilichopo hapa duniani sisi kama binadamu mpaka sasa tumeweza kugundua kazi yake au sababu ya kuwapo kwake ni nini,ni swala la muda utakapofika tutajua.

Ni topic ndefu sana tukitaka kudadavua ili ieleweke,lakini tukikaa vizuri katika imani tutaanza kuelewa taratibu....
 
Hata usipozaa au ng'ombe asipozaa anakufa tu. Kuendelea kwa ng'ombe kuwepo duniani yeye kunamsaidia nini?
Kutokuwepo kwa ng'ombe duniani kuna hasara gani kwa ng'ombe? Na uwepo wako duniani unafaida gani kwako? Yaani maswali yako ni sawa na kusema uwepo wa viumbe hai hauna faida jambo ambalo si kweli. Life is beautiful. Na changamoto zake still bado ni jambo jema maisha kuwepo kuliko kutokuwepo.
 
Hizi faida zipo kwa wote, ng'ombe, samaki, paka, vyura, panzi, miti, nk nk? Maana hapa hatuongelei binadamu tu.
 
Ni kweli. Maisha ni mazuri. Ndiyo maana sina tatizo na miili yetu kupambana kusurvive. Lakini kunafaida gani kutumia resources nyingi za kiafya na kiuchumi na muda kuzalisha viumbe wengine. Cheki kama kuku.

Anatumia muda kuatamia na virutubisho vyake kuzalisha mayai. Inamsaidia nini? Maana kufanya hivyo kunaenda hata kinyume na kusurvive kwake, kwanza anazalisha competitor wa resources zilizopo. Ng'ombe anazaa. Ananyonyesha na kulinda mtoto hadi anakua. Inamsaidia nini?
 
Ushasema maisha ni mazuri. Na ili maisha yaendelee kuwepo lazima kuzaliana kuwepo.

Sasa usingezaliwa ukanyonyeshwa ukakua ungekuaje sehemu ya kuendeleza uzuri wa maisha?
 
Ushasema maisha ni mazuri. Na ili maisha yaendelee kuwepo lazima kuzaliana kuwepo.

Sasa usingezaliwa ukanyonyeshwa ukakua ungekuaje sehemu ya kuendeleza uzuri wa maisha?
Mazuri kwa huyo kiumbe. Ndiyo maana anapambana kusurvive. Sasa anapata faida gani kuzalisha viumbe wengine?
 
Mtoto ni assests hebu waza wazazi wa leonel messi, wa Diamond Platnumz,
Mtoto ni uwekezaji wa uzeeni kama pension yaani
Ndgu kama bado huna mtoto tafadhari usitafute kabisa.

Yaani mtoto ni Asset?? Unamtengeneza mtoto kwa manufaa yako binafsi?
Mwache aishi maisha yake sio kutegemea na yeye aje akusaidie wakati nae atakua na malengo yake.
 
Mazuri kwa huyo kiumbe. Ndiyo maana anapambana kusurvive. Sasa anapata faida gani kuzalisha viumbe wengine?
Faida ni kutoa kile ambacho alipewa ili kuendeleza uzuri wa maisha. Kwani yeye alijileta duniani na kuona uzuri wake? Ili uione faida jiulize viumbe watapoteza nn wasipozaliana?
 
.... ungekuwa mwanaume usiye na uwezo wa kuzalisha au mwanamke usiye na uwezo wa kutunga mimba usingewaza haya, siku zote aliyeshiba hamfikirii mwenye njaa...kiafya binadamu anasaidiwa na kuzaa sababu moja ya kazi ya mifumo ya mwilini ni kutengeneza viini vya uzazi wa binadamu mwingine na zoezi zima uitimishwa na Sex kati ya mwanaume na mwanamke na ndiyo maana kutokuwa na uwezo wa kuzaa au kuzalisha ni tatizo la kiafya.!
 
Bila kuzaliana kungekua hakuna uhai wa kiumbe chochote duniani maana tungekufa wote...faida ya kuzaliana ndo uhai wa dunia.
 
Tunazaana ili tuteseke kisha tukachomwe moto😳😳😳
 
So how did you know that we are here for that mission mentioned above while you don't what the mission is?
it's just an assumption, so don't take it as a conclusion.

let me ask you, what is the purpose of humans on earth?.
 
it's just an assumption, so don't take it as a conclusion.

let me ask you, what is the purpose of humans on earth?.
What you are asking is the same question the man asked above
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…