Kwa ajili ya kumbukumbu: Magufuli hatojiongezea muda

Kwa ajili ya kumbukumbu: Magufuli hatojiongezea muda

Wizi mkubwa wa kura aliousimamia katika uchaguzi huu ni maandalizi ya project yake ya kubaki madarakani kwa kisingizio cha kusimamia white elephants zake, alishadokeza hilo
Mnyonge mnyongeni, haki yake mpeni.

Let's go with facts.

1. Kulikuwa na wizi mkubwa wa kura. Lakini wizi huu ninkwa ajili ya muhula wa 2020 mpaka 2025.


2. Magufuli amesema mara kadhaa hataki kuongeza muda. Hakuna ushaidi kwamba ataongeza muda. Kumhukumu kwa kosa ambalo hajalitenda bado si sahihi. Magufuli ana makosa mengi sana aliyoyatenda, kaminya upinzani, kaiba kura, kaharibu biashara ya korosho. Mhukumuni kwa makosa ambayo kashayafanya, acheni kumhukumu kwa makosa ambayo mnafikiri atayafanya 2025 bila ushahidi. Mkianza kumhukumu kwa makosa ambayo mnafikiri atayafanya mwaka 2025, mnampa sababu na yeye kutumia kanuni hiyo hiyo ya kuhukumu watu kwa makosa ambayo hawajayafanya.

Atasema nimeota wapinzani watanipindua mwakani. Nawafunga jela wote.

Kumhukumu mtu kwa kosa ambalo hajalifanya kwa sababu unamshuku tu atalifanya ni jambo baya.
 


NN, the 'smirk' on the 2:06 minute speaks volumes, nami nawasilisha kideo hiki kwa minajili ya kumbukumbu tu.
 
Mnyonge mnyongeni, haki yake mpeni.

Let's go with facts.

1. Kulikuwa na wizi mkubwa wa kura. Lakini wizi huu ninkwa ajili ya muhula wa 2020 mpaka 2025.


2. Magufuli amesema mara kadhaa hataki kuongeza muda. Hakuna ushaidi kwamba ataongeza muda. Kumhukumu kwa kosa ambalo hajalitenda bado si sahihi. Magufuli ana makosa mengi sana aliyoyatenda, kaminya upinzani, kaiba kura, kaharibu biashara ya korosho. Mhukumuni kwa makosa ambayo kashayafanya, acheni kumhukumu kwa makosa ambayo mnafikiri atayafanya 2025 bila ushahidi. Mkianza kumhukumu kwa makosa ambayo mnafikiri atayafanya mwaka 2025, mnampa sababu na yeye kutumia kanuni hiyo hiyo ya kuhukumu watu kwa makosa ambayo hawajayafanya.

Atasema nimeota wapinzani watanipindua mwakani. Nawafunga jela wote.

Kumhukumu mtu kwa kosa ambalo hajalifanya kwa sababu unamshuku tu atalifanya ni jambo baya.
Hapo ni sawa na kutwanga maji kwenye kinu.

Hujaandika chochote kilicho kigumu, ila sitoshangaa kama kuna watu hawatokuelewa na kudhani hapo umemtetea Magufuli ilhali ulichokiandika ni ukweli ulio wazi kwa yeyote mwenye macho na akili ya kawaida tu.

Tayari kuna mtu humu keshadai hii mada ni ya kumsifia Magufuli kutokana na ukabila!!
 
Ok, so, me being me. The independent minded guy that I am. Native citizen of Realville. That straight shooter that I am. I am no shrinking violet when it comes to expressing my views.

So I’m going to go out on a limb today and say it. If this means I’ll have to eat crow a couple years from now for being dead wrong, then so be it.

Ni hivi: Rais Magufuli [sidhani] kama atajiongezea muda ili atawale kwa zaidi ya miaka 10.

Minong’ono na hofu iliyopo hivi sasa kwamba atajiongezea muda, ni maneno tu. Ni hewa.

Kwa nini nasema hivyo? Ni kwa sababu zifuatazo:

1. Urais ni mzigo. Ni mzigo mzito wenye kuleta msongo wa mawazo. Ni aina ya mateso flani hivi.

Kwa mtu anayejali kufanya kazi na siyo kula bata, basi mtu wa aina hiyo hawezi kutamani kuwepo madarakani kwa kipindi kirefu kuzidi miaka 10.

Ila kwa mtu mla bata asiyejali kazi, kama alivyokuwa Mobutu wa Zaire au Bokassa wa Afrika ya Kati, atataka aendelee kutawala milele.

Rais Magufuli si mla bata. Jamaa dizaini hata pombe [no pun intended] hanywi. Sidhani kama anavaaga masuti ya bei mbaya.
Jamaa hata mamtoni huwa haendi.

Hata mkewe ukimwangalia unaona kabisa naye si mtu wa bata. Sijawahi kumwona kabeba sijui Birkin bags wala kuvaa red bottoms [Christian Louboutins]. Yeye ni mtu wa magauni ya vitenge tu na tu viatu twa kawaida.

Hata weave [wabongo mnaita weaving] yule mama sijawahi kumwona kashonea.

Hao si aina ya watu wapendao kukaa madarakani kwa muda mrefu.

2. Sidhani kabisa kama atataka kwenda down that rabbit hole.

Yaani yeye ndo aturudishe kule kwa zamani tulikotoka? Sioni kabisa hilo likitokea.

Jamaa atarudi zake Chato kwenda kuchunga ng’ombe.

Kwa hiyo, kwangu mimi hofu iliyopo ya kwamba atajiongezea muda, ni hofu isiyo na msingi wowote ule katika ukweli.

Najua kuwa huwa anapita humu maana kuna wakati aliwahi kunijibu kwenye moja ya hotuba zake baada ya mimi kuuliza humu kama alishawahi kufika Marekani 🤣.

Sasa, kwa jinsi alivyo, anaweza akapita humu na kuona nimesema kuwa hatojiongezea muda wa kubaki madarakani, na yeye akaamua kujiongezea ili tu afanye kinyume na nilivyodai mimi, ili nionekane nimekosea.

Don’t get it twisted, he can be petty like that.

Still, sidhani kabisa kuwa atajiongezea muda wa kubaki madarakani.

Na hii mada/ huu uzi, uwe ni kumbukumbu kuwa ‘NN alisemaga’.

Baadaye ✌🏿
Kweli naona umefilisika siku hizi. Kama urais ni mzigo kilichomfanya atumie kura feki kubaki madarakani ni nini? Si angeachia kura zihesabiwe kihalali ili aone angalau kama atapata nafasi ya kutua huo mzigo? Au angesema tu basi sitaki tena kipindi kingine cha uongozi kwani urais ni mzigo!
BTW Magufuli hataongeza muda wa uongozi ni kweli. Siyo kama hataki ila ataona aibu na kuogopa upinzani atakaokumbana nao kutoka CCM na kila kona ya dunia. Lakini kitu dhahiri atakachofanya ni kutaka kumweka kwa nguvu, mtu aliye loyal kwake atakayem-hand pick! Hili nina uhakika nalo na atatumia nguvu kubwa sana kujaribu kulifanikisha.
 
Kweli naona umefilisika siku hizi. Kama urais ni mzigo kilichomfanya atumie kura feki kubaki madarakani ni nini? Si angeachia kura zihesabiwe kihalali ili aone angalau kama atapata nafasi ya kutua huo mzigo? Au angesema tu basi sitaki tena kipindi kingine cha uongozi kwani urais ni mzigo!
BTW Magufuli hataongeza muda wa uongozi ni kweli. Siyo kama hataki ila ataona aibu na kuogopa upinzani atakaokumbana nao kutoka CCM na kila kona ya dunia. Lakini kitu dhahiri atakachofanya ni kutaka kumweka kwa nguvu, mtu aliye loyal kwake atakayem-hand pick! Hili nina uhakika nalo na atatumia nguvu kubwa sana kujaribu kulifanikisha.
Duh!

Why go personal?

Unaanza bandiko lako kwa kunishambulia kuwa nimefilisika??

Sijui unasumbuliwa na masahibu gani, ila nakupa pole sana.
 
Haudhani au una uhakika? Kudhani bado ni probability
 
Ok, so, me being me. The independent minded guy that I am. Native citizen of Realville. That straight shooter that I am. I am no shrinking violet when it comes to expressing my views.

So I’m going to go out on a limb today and say it. If this means I’ll have to eat crow a couple years from now for being dead wrong, then so be it.

Ni hivi: Rais Magufuli [sidhani] kama atajiongezea muda ili atawale kwa zaidi ya miaka 10.

Minong’ono na hofu iliyopo hivi sasa kwamba atajiongezea muda, ni maneno tu. Ni hewa.

Kwa nini nasema hivyo? Ni kwa sababu zifuatazo:

1. Urais ni mzigo. Ni mzigo mzito wenye kuleta msongo wa mawazo. Ni aina ya mateso flani hivi.

Kwa mtu anayejali kufanya kazi na siyo kula bata, basi mtu wa aina hiyo hawezi kutamani kuwepo madarakani kwa kipindi kirefu kuzidi miaka 10.

Ila kwa mtu mla bata asiyejali kazi, kama alivyokuwa Mobutu wa Zaire au Bokassa wa Afrika ya Kati, atataka aendelee kutawala milele.

Rais Magufuli si mla bata. Jamaa dizaini hata pombe [no pun intended] hanywi. Sidhani kama anavaaga masuti ya bei mbaya.
Jamaa hata mamtoni huwa haendi.

Hata mkewe ukimwangalia unaona kabisa naye si mtu wa bata. Sijawahi kumwona kabeba sijui Birkin bags wala kuvaa red bottoms [Christian Louboutins]. Yeye ni mtu wa magauni ya vitenge tu na tu viatu twa kawaida.

Hata weave [wabongo mnaita weaving] yule mama sijawahi kumwona kashonea.

Hao si aina ya watu wapendao kukaa madarakani kwa muda mrefu.

2. Sidhani kabisa kama atataka kwenda down that rabbit hole.

Yaani yeye ndo aturudishe kule kwa zamani tulikotoka? Sioni kabisa hilo likitokea.

Jamaa atarudi zake Chato kwenda kuchunga ng’ombe.

Kwa hiyo, kwangu mimi hofu iliyopo ya kwamba atajiongezea muda, ni hofu isiyo na msingi wowote ule katika ukweli.

Najua kuwa huwa anapita humu maana kuna wakati aliwahi kunijibu kwenye moja ya hotuba zake baada ya mimi kuuliza humu kama alishawahi kufika Marekani 🤣.

Sasa, kwa jinsi alivyo, anaweza akapita humu na kuona nimesema kuwa hatojiongezea muda wa kubaki madarakani, na yeye akaamua kujiongezea ili tu afanye kinyume na nilivyodai mimi, ili nionekane nimekosea.

Don’t get it twisted, he can be petty like that.

Still, sidhani kabisa kuwa atajiongezea muda wa kubaki madarakani.

Na hii mada/ huu uzi, uwe ni kumbukumbu kuwa ‘NN alisemaga’.

Baadaye ✌🏿
Mkuu muache mzee ata ikiwa miaka 100 mbona unaanza maneno tena wakati hata January Bado ,Mimi nafiki hakuna sababu ya kumpangia bwana ,ikiongezeka sawa, ikibaki iyo sawa , hachana na hayo mkuu
 
Mnyonge mnyongeni, haki yake mpeni.

Let's go with facts.

1. Kulikuwa na wizi mkubwa wa kura. Lakini wizi huu ninkwa ajili ya muhula wa 2020 mpaka 2025.


2. Magufuli amesema mara kadhaa hataki kuongeza muda. Hakuna ushaidi kwamba ataongeza muda. Kumhukumu kwa kosa ambalo hajalitenda bado si sahihi. Magufuli ana makosa mengi sana aliyoyatenda, kaminya upinzani, kaiba kura, kaharibu biashara ya korosho. Mhukumuni kwa makosa ambayo kashayafanya, acheni kumhukumu kwa makosa ambayo mnafikiri atayafanya 2025 bila ushahidi. Mkianza kumhukumu kwa makosa ambayo mnafikiri atayafanya mwaka 2025, mnampa sababu na yeye kutumia kanuni hiyo hiyo ya kuhukumu watu kwa makosa ambayo hawajayafanya.

Atasema nimeota wapinzani watanipindua mwakani. Nawafunga jela wote.

Kumhukumu mtu kwa kosa ambalo hajalifanya kwa sababu unamshuku tu atalifanya ni jambo baya.
Hata mimi hisia zangu zinanifanya niamini kuwa Magufuli hataongeza muda. Ila siyo kama hataongeza muda kwa sababu kazi ya urais ni ngumu kama alivyosema Nyani Ngabu , la hasha. Angekuwa anaona kazi ya urais ni mzigo kihivyo asingetumia nguvu nyingi kuiba kura kishamba kama alivyofanya kwenye huu uchaguzi bali angeacha fate ichukuwe mkondo wake akitegemea pengine atashindwa ili apumzike. Ila jambo naloliona dhahiri ni kuwa atajaribu kwa nguvu zote kuweka a hand picked candidate aliye loyal kwake anayedhani kuwa atamsaidia kufunika uchafu wake. Japo Bongo rais alioyeondoka madarakani hawezi kushtakiwa lakini huyu jamaa amefanya madhambi mengi kiasi ambacho ana wasiwasi siku akiondoka itakuwaje.
 
Mkuu muache mzee ata ikiwa miaka 100 mbona unaanza maneno tena wakati hata January Bado ,Mimi nafiki hakuna sababu ya kumpangia bwana ,ikiongezeka sawa, ikibaki iyo sawa , hachana na hayo mkuu
Sijampangia mtu.

Nimetoa maoni yangu tu.
 
Hapo ni sawa na kutwanga maji kwenye kinu.

Hujaandika chochote kilicho kigumu, ila sitoshangaa kama kuna watu hawatokuelewa na kudhani hapo umemtetea Magufuli ilhali ulichokiandika ni ukweli ulio wazi kwa yeyote mwenye macho na akili ya kawaida tu.

Tayari kuna mtu humu keshadai hii mada ni ya kumsifia Magufuli kutokana na ukabila!!
Sasa mbona mimi Msukuma halafu hakuna wiki inayopita hapa JF bila mimi kumkejeli Magufuli kwa angalau kuandika "Magufuli is a country bumpkin" ?

Mbona nimesema wazi hapo juu kwamba Magufuli ana makosa mengi ambayo kashayafanya, kuanzia kuminya upinzani, kuiba kura, kuharibu biashara ya korosho etc.

Sasa hapo namtetea Magufuli kivipi?

Yani kusem kwamba tusihukumu watu kwa makosa ambayo hawajafanya ila tunafikiri watafanya ni kumtetea Magufuli?

Mtu atakayesema hivyo, nitamuona kama mtu aliyeshindwa kuchambua hoja kwa mantiki na weledi, analeta ushabiki wa kinazi wa "timu yangu vs timu yako, facts be damned".

Give the man a break on this one.

Kumshambulia Magufuli kuhusu yeye kuongeza muda ni ujinga.

Kwa sababu Magufuli ana makosa mengi sana ambayo kashayafanya, hatuhitaji kumtengenezea makosa ya kufikirika ambayo tunafikiri atayafanya.

Kama kuna mtu anataka makosa ambayo Magufuli kashayafanya, kuna makosa zaidi ya 100. Kwa nini uache haya makosa ambayo kashayafanya, uende kuwa obsessed na makosa ambayo unafikiri atayafanya?

Kufanya hivyo, ni sawa na kuwa na mtu tajiri mkubwa sana, bilionea wa dola ana pesa ndefu.

Halafu, badala ya kutumia pesa zake alizonazo, anaenda kukopa hela benki, kwa mkopo wenye riba kubwa sana.

Yani watu wana utajiri wa makosa ya Magufuli, halafu wanaenda benki kukopa makosa ambayo hayapo, kwa riba kubwa sana ya wananchi kuwaona wazushi?

Wanampa Magufuli msemo tu, aweze kusema hawa wamefilisika kisiasa, wanazusha mambo ambayo hayapo.
 
Hata mimi hisia zangu zinanifanya niamini kuwa Magufuli hataongeza muda. Ila siyo kama hataongeza muda kwa sababu kazi ya urais ni ngumu kama alivyosema Nyani Ngabu , la hasha. Angekuwa anaona kazi ya urais ni mzigo kihivyo asingetumia nguvu nyingi kuiba kura kishamba kama alivyofanya kwenye huu uchaguzi bali angeacha fate ichukuwe mkondo wake akitegemea pengine atashindwa ili apumzike. Ila jambo naloliona dhahiri ni kuwa atajaribu kwa nguvu zote kuweka a hand picked candidate aliye loyal kwake anayedhani kuwa atamsaidia kufunika uchafu wake. Japo Bongo rais alioyeondoka madarakani hawezi kushtakiwa lakini huyu jamaa amefanya madhambi mengi kiasi ambacho ana wasiwasi siku akiondoka itakuwaje.
But why go personal with me?

Do I evoke such strong emotion to you each time you see my name?
 
Duh!

Why go personal?

Unaanza bandiko lako kwa kunishambulia kuwa nimefilisika??

Sijui unasumbuliwa na masahibu gani, ila nakupa pole sana.
Nimeshangaa sana sana mtu mweledi kama wewe kuamini kuwa ''ugumu'' wa kazi ya urais unaweza kumfanya Magu asiutake urais tena. Angekuwa anaona kuna ugumu wowote wala asingelazimisha kubaki Ikulu kwa kuiba kura kishamba namna ile. Kitakachomfanya tu asitake kuongeza muda ni aibu na upinzani atakaokutana nao.
 
Mnyonge mnyongeni, haki yake mpeni.

Let's go with facts.

1. Kulikuwa na wizi mkubwa wa kura. Lakini wizi huu ninkwa ajili ya muhula wa 2020 mpaka 2025.


2. Magufuli amesema mara kadhaa hataki kuongeza muda. Hakuna ushaidi kwamba ataongeza muda. Kumhukumu kwa kosa ambalo hajalitenda bado si sahihi. Magufuli ana makosa mengi sana aliyoyatenda, kaminya upinzani, kaiba kura, kaharibu biashara ya korosho. Mhukumuni kwa makosa ambayo kashayafanya, acheni kumhukumu kwa makosa ambayo mnafikiri atayafanya 2025 bila ushahidi. Mkianza kumhukumu kwa makosa ambayo mnafikiri atayafanya mwaka 2025, mnampa sababu na yeye kutumia kanuni hiyo hiyo ya kuhukumu watu kwa makosa ambayo hawajayafanya.

Atasema nimeota wapinzani watanipindua mwakani. Nawafunga jela wote.

Kumhukumu mtu kwa kosa ambalo hajalifanya kwa sababu unamshuku tu atalifanya ni jambo baya.

Watu uhukumu kutokana na mienendo au dalili ambazo magufuli ameonesha.
Kitendo cha kusema ataumaliza upinzani na kutekeleza hilo, kwanini tusihukumu kwamba anafanya hivyo ili ajiwekee mazingira mazuri ya yeye kupata uungwaji mkono wa wabunge wake kuwa aendelee kugombea au kuongeza muda wa kukaa madarakani?

Kwanii tusihukumu kwamba kuua upinzani ni kutaka kuondoa upinzani na ukinzani wa ww kuendelea kufanya kile unachotaka bila upinzani?

Najua upinzani hata kama wasingekuwa wengi huko bungeni lkn zile kelele zao zinatosha kuamsha na hata kuwapa ujasiri wa wabunge wengine wa ccm kusimama nao.

Sasa leo mbunge wa ccm anajua kabisa uchaguzi ungekuwa fair nisinge kuwa hapa bungeni, ubunge wangu umetokana na maagizo ya Rais (alisema mkurugenzi anaempa gari, mshahara mnono asisikie kamtangaza mpinzani) unategemea mbunge huyo kukataa Rais kuongezewa muda au kugombea term nyingine?

Kwahiyo mkuu, mambo mengine tunahukumu kutokana na historia za Ma Rais wa nchi nyingine za Afrika walivyopitia mchakato kama ya Magufuli. Walijihakikishia wana ua upinzani, na kupitisha wabunge wa chama chake kushinda kwa wingi usio halali ili aweze kujiongezea Muda.
 
Sasa mbona mimi Msukuma halafu hakuna wiki inayopita hapa JF bila mimi kumkejeli Magufuli kwa angalau kuandika "Magufuli is a country bumpkin" ?

Mbona nimesema wazi hapo juu kwamba Magufuli ana makosa mengi ambayo kashayafanya, kuanzia kuminya upinzani, kuiba kura, kuharibu biashara ya korosho etc.

Sasa hapo namtetea Magufuli kivipi?

Yani kusem kwamba tusihukumu watu kwa makosa ambayo hawajafanya ila tunafikiri watafanya ni kumtetea Magufuli?

Mtu atakayesema hivyo, nitamuona kama mtu aliyeshindwa kuchambua hoja kwa mantiki na weledi, analeta ushabiki wa kinazi wa "timu yangu vs timu yako, facts be damned".

Give the man a break on this one.

Kumshambulia Magufuli kuhusu yeye kuongeza muda ni ujinga.

Kwa sababu Magufuli ana makosa mengi sana ambayo kashayafanya, hatuhitaji kumtengenezea makosa ya kufikirika ambayo tunafikiri atayafanya.

Kama kuna mtu anataka makosa ambayo Magufuli kashayafanya, kuna makosa zaidi ya 100. Kwa nini uache haya makosa ambayo kashayafanya, uende kuwa obsessed na makosa ambayo unafikiri atayafanya?

Kufanya hivyo, ni sawa na kuwa na mtu tajiri mkubwa sana, bilionea wa dola ana pesa ndefu.

Halafu, badala ya kutumia pesa zake alizonazo, anaenda kukopa hela benki, kwa mkopo wenye riba kubwa sana.

Yani watu wana utajiri wa makosa ya Magufuli, halafu wanaenda benki kukopa makosa ambayo hayapo, kwa riba kubwa sana ya wananchi kuwaona wazushi?

Wanampa Magufuli msemo tu, aweze kusema hawa wamefilisika kisiasa, wanazusha mambo ambayo hayapo.
💯%.
 
Nimeshangaa sana sana mtu mweledi kama wewe kuamini kuwa ''ugumu'' wa kazi ya urais unaweza kumfanya Magu asiutake urais tena. Angekuwa anaona kuna ugumu wowote wala asingelazimisha kubaki Ikulu kwa kuiba kura kishamba namna ile. Kitakachomfanya tu asitake kuongeza muda ni aibu na upinzani atakaokutana nao.
Haya, hewala bwana.

Kama kuna yanayokusibu, nakuombea afueni.
 
Hata mimi hisia zangu zinanifanya niamini kuwa Magufuli hataongeza muda. Ila siyo kama hataongeza muda kwa sababu kazi ya urais ni ngumu kama alivyosema Nyani Ngabu , la hasha. Angekuwa anaona kazi ya urais ni mzigo kihivyo asingetumia nguvu nyingi kuiba kura kishamba kama alivyofanya kwenye huu uchaguzi bali angeacha fate ichukuwe mkondo wake akitegemea pengine atashindwa ili apumzike. Ila jambo naloliona dhahiri ni kuwa atajaribu kwa nguvu zote kuweka a hand picked candidate aliye loyal kwake anayedhani kuwa atamsaidia kufunika uchafu wake. Japo Bongo rais alioyeondoka madarakani hawezi kushtakiwa lakini huyu jamaa amefanya madhambi mengi kiasi ambacho ana wasiwasi siku akiondoka itakuwaje.
Tanzania kuna mambo fulani ya kiutamaduni rais anaweza kusema "not under my watch" hata kama kachoka au haoni mantiki.

Kwa mfano, rais anaweza kuona kuna haja ya kujadili Muungano upya, lakini akasema hataki hili litokee chini ya urais wake.

Au, rais anaweza kuona kashachoka uongozi na anaweza kuacha urais baada ya miaka mitano ya kwanza, lakini akifikiri yeye kuwa rais wa kwanza kuanzisha hilo, anaona atautwaa mzigo wa historia.

Kwa vyovyote vile, sioni sababu ya kumuandama Magufuli kuhusu kuongeza muda wa urais wake, wakati mwenyewe kashasema hataongeza muda.

Hususan kwa sababu kuna mambo mengi sana, makosa aliyoyafanya tayari, tunaweza kumuandama kihalali kabisa bila kuhitaji hili la kubashiri yatakayotokea 2025.
 
Watu uhukumu kutokana na mienendo au dalili ambazo magufuli ameonesha.
Kitendo cha kusema ataumaliza upinzani na kutekeleza hilo, kwanini tusihukumu kwamba anafanya hivyo ili ajiwekee mazingira mazuri ya yeye kupata uungwaji mkono wa wabunge wake kuwa aendelee kugombea au kuongeza muda wa kukaa madarakani?

Kwanii tusihukumu kwamba kuua upinzani ni kutaka kuondoa upinzani na ukinzani wa ww kuendelea kufanya kile unachotaka bila upinzani?

Najua upinzani hata kama wasingekuwa wengi huko bungeni lkn zile kelele zao zinatosha kuamsha na hata kuwapa ujasiri wa wabunge wengine wa ccm kusimama nao.

Sasa leo mbunge wa ccm anajua kabisa uchaguzi ungekuwa fair nisinge kuwa hapa bungeni, ubunge wangu umetokana na maagizo ya Rais (alisema mkurugenzi anaempa gari, mshahara mnono asisikie kamtangaza mpinzani) unategemea mbunge huyo kukataa Rais kuongezewa muda au kugombea term nyingine?

Kwahiyo mkuu, mambo mengine tunahukumu kutokana na historia za Ma Rais wa nchi nyingine za Afrika walivyopitia mchakato kama ya Magufuli. Walijihakikishia wana ua upinzani, na kupitisha wabunge wa chama chake kushinda kwa wingi usio halali ili aweze kujiongezea Muda.
Kuna mambo unaweza kuhukumu kutokana na rekodi ya mtu, kuna mambo unaweza kusema huyu hapa sitegemei aheshimu katiba na demokrasia, kwa sababu kashasema anataka kuua upinzani by 2020.

Hapo una ushahidi wa maneno ya huyo mtu, ukimhukumu unamhukumu kwa fact.

Halafu kuna mambo ya kumhukumu mtu kwa paranoia tu, mtu kashasema mara kadhaa hataongeza muda, unakuwa na inferiority complex tu kuona ataongeza muda.

Kwa sasa, based on facts, kumhukumu Magufuli kwenye hili la kuongeza muda ni paranoia tu.

Na wapinzani wanaoshikia bango hili wanajionesha hawajakoma kisiasa kuchambua mbivu ni zipi na mbichi ni zipi.

Wewe Magufuli ana makosa kedekede ambayo kashayafanya, watu wote wenye akili na wanaoheshimu mantiki wanajua, hayana mjadala.

Unayaacha yote hayo, unaenda kuwa obsessed na makosa ambayo hajayafanya bado?
 
Back
Top Bottom