Kwa anachokifanya Israel huko Syria, nimehitimisha kuwa Bashar al Assad alikuwa mtu sahihi ila wananchi walipatwa tu na mzuka na wivu

Sio kwasababu ya kutafuta sifa wala kujikweza. wayahudi na US wameshawazidi maarifa. Muda hauna baya. Utaongea
 
Huna ujualo wewe, so endelea kupenga/kumeka makamasi huju ukilia
 
Anachokifanya Israel ndani ya Syria kinaonyesha kuwa ukiwa mnyonge mbele ya Israel anakuwa anajibondea tu. Kama siyo uwepo wa Hizbollah ndani ya lebanon sasa hivi Israel ingekuwa imeshamega South Lebanon nzima.
 
Punguza uongo. Assad alikuwa nuksi Syria ndio maana raia wamesherekea kuondoka kwake.
Hivi haujui watu wanaweza kusherehekea na kufurahia ujinga. Wengine hata hawajui kwa nini wanarukaruka kwa furaha.

Nikuambie tu hata Tz kuna wapinzani wanapinga mambo mengi ya serikali lakini wamo wasiojua wanapinga nini na kwa nini, bali ni bendera fuata upepo.

Hivyo hivyo, hata wafuasi wa CCM hufuraia kila uchaguzi kushinda kwa kishindo lakini ukiwauliza ni kishindo gani wakati mmeiba kura au kujizolea viti vingi kwa kigezo cha kupita bila kupingwa huku watu wakipotezwa, na kura kuibiwa waziwazi, hawawezi kukupa majibu wao wamekalili tu kuwa ilimradi tumeshinda kwa kishindo haijalishi. So, watu km hawa hufuraia wasichokiruhia na hawajui wanafurahia nini. Fraha ya mtu inatofasili nyingi kwa taswira ya ndani ya moyo na nje. Nadhani umenielewa km bado basi wewe haufundishiki.
 

IZRAEL YAENDELEZA UBABE SYRIA/YASHAMBULIA MELI ZA KIVITA NA MAGHALA YA SILAHA.​


View: https://www.youtube.com/watch?v=CjP7Wi9zPOc
 
Wewe siyo ridhiki kwa wazazi wao. Na pengine ulizaliwa kabla baba na mama yako hawajafunga I ndoa.
Kumbe unapakwa makamssi na wenzio? Nilikuwa sijui hilo, ahsante kwa kutujuza, ndiyo maana ukiona makamasi unslegeza macho. Watu mna siri sans
 
Hakuna nchi yenye uhasama na Israel itakayokuwa imara hapo mashariki ya kati.

Nchi zote zinazoizunguka Israel inatakiwa aidha iwe inauhusiano mwema na Israel au iwe dhaifu kiasi ambacho haitakuwa tishio kwa israel.

Hapo Syria hata Kama wataanzisha serikali ya kidemokrasia bado marekani na Israel watafanya wanaloweza kuingiza mgogoro mpaka wachapane na kwa kuwa waarabu ni wabinafsi kuwagombanisha ni rahisi sana
 
Good contribution with no emotions. Nyie ndo mnatakiwa kuwa jf, kuna wengine humu watoto HARAMU wanatoa matusi hadi wanatufanya na sisi tusiozea matusi kuyaporomosha. Hivi hapo ulivyochangia kistaarabu na kimamantic umrpingukiwa nini. Ebu jaribu kuwaelimisha na hawa watoto HARAMU. Have a good day.
 
Kwa namna hali ya usalama ilivyo Tata kwa Sasa huko, iwe Israel au warabu endapo mna nguvu zakijeshi za kutosha Ni heri kupambana kufa kupona ili tu kujihakikishia usalama wakutosha. Maana watu wa ukanda huo hawana huruma Wala hawajui kwa kina Ni Nini maana ya amani. Ndicho anachofanya Israel kwa Sasa.
Na hapa kwa jicho la mbali tunaona huu ndio ushindi ambao Israel aliuhitaji.
 
Israel inaweza kufurahia kuanguka kwa utawala wa Bashir Assad kwa sababu mbalimbali za kimkakati na kiusalama, zikiwemo:
  1. Kupunguza Ushawishi wa Iran: Utawala wa Assad umekuwa mshirika mkubwa wa Iran katika eneo la Mashariki ya Kati. Kuanguka kwake kunaweza kudhoofisha ushawishi wa Iran nchini Syria, na hivyo kupunguza tishio la moja kwa moja kwa Israel kutoka kwa vikundi vinavyoungwa mkono na Iran kama Hizbollah.​
  2. Kudhoofisha Vikundi vya Uadui: Syria chini ya Assad imekuwa njia kuu ya kupeleka silaha na msaada wa Iran kwa Hizbollah, ambayo ni adui mkubwa wa Israel. Kuanguka kwa Assad kunaweza kuvuruga njia hii.​
  3. Fursa za Kuimarisha Ushawishi wa Kikanda: Kuondoka kwa Assad kunaweza kuipa Israel fursa ya kuimarisha mahusiano na wapinzani wa Assad ndani ya Syria, ikiwa ni pamoja na makundi ya waasi au serikali mpya inayoweza kuwa na msimamo wa wastani.​
  4. Kupunguza Uwezekano wa Vita vya Baadaye: Assad ameendeleza hali ya uhasama na Israel kwa muda mrefu, na utawala mpya unaweza kutoa nafasi ya mazungumzo au angalau kupunguza uhasama kati ya pande hizo mbili.​
  5. Usalama wa Mpaka: Israel imekuwa na wasiwasi mkubwa juu ya uwepo wa vikosi vya Iran na Hizbollah karibu na mpaka wa Golan. Kuondoka kwa Assad kunaweza kusababisha mabadiliko ya hali hiyo, na kuimarisha usalama wa mpaka wa Israel.​
Hata hivyo, ni muhimu kutambua kwamba Israel inaweza pia kuwa na wasiwasi kuhusu ombwe la madaraka ambalo linaweza kuzalisha machafuko au kuibuka kwa makundi yenye msimamo mkali zaidi baada ya kuondoka kwa Assad
 
Hajui kiswahili
 
Ni mpumbavu pekee ndo anashabikia vita,mtu mwenye akili timamu hawezi shabikia vita kama ushabiki wa Simba na Yanga

Mostly ni wajumapili ndo hua wanasifia Israel mara marekani nakubali wana za kuvuukia tu
 
sikubaliani nawe kama rais assad alikuwa bora syria ,,,,,,,,,kiongozi yoyote awapo madarakani akawa anafunga watu,anapoteza watu huyo si kiongozi........awape uhuru wa kujieleza wananchi wetu
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…