Elisha Sarikiel
JF-Expert Member
- Aug 29, 2020
- 905
- 1,540
- Thread starter
-
- #161
Naamini bado kuna wanawake wengi, walio tayari kufunga ndoa bila hata sherehe kama hawa waliofunga ndoa kwa askofu Zachary Kakobe.Ni Jambo jema lakini kwa Karne hii mtihani mkubwa ni kumpata mwanamke atakayekubali kufunga ndoa bila sherehe kubwa. Wengi wanataka sherehe ya kifahari, msafara wa magari na miosho mingi ili mji mzima wajue kuwa ameolewa. Ukigusia swala la ndoa bila sherehe wanakukimbia
Muulize kama anazifahamu ndoa za mkeka zina gharama kubwa ⁉️Halafu wewe jamaa siyo muelewa kabisa,watu wameshaamua kufanya hivyo wewe unakomaa siyo sawa,wewe kama nani? Acha kupangia watu maisha
Hakika wapendeza bila mambo ya mchina na nduguzeNimewapenda bure Hakika wamependeza Sana
Inatwa roho ya ....................Hatukosi kukosoa
Naunga mkono hojaHongera zao, Ila kwa mfululizo wa picha naona tukio nalo lilikuwa staged
Sio mbaya Ila Kuna namna wangeweza kuwa cheap zaidi.
Uliza uambiwe kabla ya kuandika upotoshaji mbele ya umma kama huu. Nenda YEHODAYA kanisa la Full Gospel Bible Fellowship utafundishwa kweli ya neno la Mungu kwa usahihi.Inatia huruma nilichokiona hapo ni kuwa maharusi wanajioza hawaozwi na wazazi wala ndugu tofauti na makanisa mengine
Hiyo si nzuri kwa mahusiano ya wazazi na ndugu .Yaani kweli watu wanaoana hawana hata mzazi au ndugu wa kuwasindikiza wakishaoana wanaondoka kama wakiwa au yatima.Hivi kwa mtindo huo kuna hata mkwe au mzazi au ndugu atakwenda kukanyaga nyumbani kwa maharusi?
Huo mfumo unaua kabisa undugu.Wanatakiwa kuozwa sio kujioza ndio maana hata michango huwa haiitishwi na wanaooana huitishwa na wazazi au ndugu
Hata kipindi cha Yesu harusi zilikuwa sherehe mfano harusi ya kana
Hilo la watu kujiondokea tu utafikiri vibaka na kukimbilia daladala na bodaboda ni kudhalilisha ndoa
Ni kweli kabisa kwamba baraka ziwe nao maisha yao yoteHii ni nzuri sana, gharama za harusi huacha watu na madeni, hongereni sana maharusi na Mungu awabariki
Anastahili zaidi tano Chukwuemeka TakpoKwahili nampa tano kakobe
Askofu Kakobe aliwahi kufungisha ndoa 50 kwa wakati mmoja miaka mingi iliyopita.Issue siyo namna walivyofanya Kwasababu Kwasababu binafsi najua ndoa siyo gharama.
Gharama huwa zinakuja kwenye Sherehe kitu ambacho ni option.
Kila siku watu wanafunga ndoa kwa wakuu wa wilaya kwabkujaza tu fomu na kusepa.
Hili tukio linaonekana ni staged, na kiki zinahusika. There is no way unaweza kui-entertain umasikini kwa namna yoyote kama hawa wanavyotaka kufanya.
Kwanza wamesema, ndoa zilizofungwa ni 21, then why this couple ?????
Hakuna mzazi au ndugu mwendawazimu wa kutofurahia mtoto wake kufunga ndoa labda mjumbe mpigaji fedha wasiokosa kila kamati za harusi atalalamika kukosa dili la pesa.Huo uondokaji wa maharusi unajieleza wenyewe kuwa hakuba cha ndugu wala jirani wala wazazi wala marafiki wa kusindikiza watoto wao baada ya ndoa kanisani!!! aisee yaani hata waumini wenzao tu kuwasindikiza hakuna!!!! Hii kali.Mungu awasaidie kwenye maisha yao ya upweke waliyoanza nayo kanisani kwenye ndoa yao
Hii kitu wazazi na ndugu na marafiki na majirani wanaowafahamu wakiziona hizi picha wengi roho zitawauma sana yaani siku ya ndoa watu wanakuwa wakiwa hivyo inatia huruma
Fundisho zuri kwa jamiiNimewapenda bure
Wewe Muuza simu used ndiye unayepotosha umma si MIMI.Mkuu unajaribu kupotosha uma!,hii inaitwa kubariki ndoa na wala sio ndio,hii ni kwa wale wanaoishi uchumba sugu na wanapika na kupakua,utakuwa hauelewi vizuri ndoa ni nini na kubariki ndoa ni nini !
Kwa amani na upendo safiiiiiiiiiiiiiiiiiiiiiiiiiiiiiiiiiiiiiiii !!!!!!!!!Hahahahahah daaah Safi Sana very simple hakuna mbwembwe Wala majotroo[emoji1]
Hongera kubwaSafi sana, hongera zao
Ukweli wamependezaNimependa walivyovaa
Ilikuwa siku ya Ijumaa 19.2.2021, ni siku nyingine ya kukumbukwa, katika Kanisa la Full Gospel Bible Fellowship (FGBF), Dar-Es-Salaam, lililoko Barabara ya Sam Nujoma; pale ambapo jumla ya wahusika 84 waliposhiriki katika kufungwa kwa Ndoa 21, zilizofungwa kwa pamoja katika Ibada ya Ndoa iliyoanza saa 5 asubuhi. Wahusika hao 84, walikuwa ni Mabwana Arusi 21, na Mabibi Arusi 21, ambao hawajawahi kuishi pamoja; na jumla ya Mashahidi 42 (waume 21 na wake zao 21).
Kama ilivyo ada, katika Arusi hizo, viwango vya mavazi ya Mabwana na Mabibi Arusi, vilikuwa ni vilevile ambavyo vimekuwa vikizingatiwa, katika Ndoa mamia kwa mamia, zilizofungwa katika Kanisa la FGBF, kwa miaka zaidi ya 30; hususan tangu Askofu Mkuu Zachary Kakobe alipoliasisi Kanisa hili, tarehe 30.4.1989.
Katika Ibada hiyo ya Ndoa, Askofu Kakobe alihubiri kwanza ujumbe wa Neno la Mungu lisiloghoshiwa, wenye kichwa, "WALA MSIIFUATISHE NAMNA YA DUNIA HII" (WARUMI 12:2); kisha ndipo alipofungisha Ndoa hizo 21 kwa pamoja.
Suala lililowavutia sana wageni, waliohudhuria kwa mara ya kwanza, katika Ibada za Ndoa za Kanisa la FGBF, ni jinsi walivyowashuhudia Maarusi hao, wakitumia usafiri uleule wa kawaida ambao wamekuwa wakiutumia, wanapokwenda Kanisani, katika Ibada nyingine za kawaida. Baada ya kufunga Ndoa zao, Bwana Arusi mmoja mwenye gari lake, alikwenda na mkewe, nyumbani kwake, na gari lake hilohilo, huku akiliendesha mwenyewe.
Baadhi ya Maarusi, walikwenda kwao, kwa kutembea tu kwa miguu, huku wameshikana mikono kwa upendo na furaha isiyoelezeka; na kuwasisimua watu wengi. Siyo hilo tu, Maarusi wengine wengi walitembea kwa miguu, huku wamejaa bashasha, mpaka kwenye kituo cha daladala kilichoko jirani na Kanisa hilo, na kupanda daladala hizo zilizowapeleka majumbani kwao. Taarifa zilizopatikana baadaye, zinaeleza jinsi baadhi yao walivyokuwa wakihubiri Injili ndani ya daladala hizo walizozipanda.
Bwana Arusi mmoja, ambaye hutumia pikipiki (bodaboda) yake kuja Kanisani, alimvisha helmet (kofia ngumu) mkewe, kisha akampakia mkewe (Bibi Arusi), kwenye bodaboda hiyo, na kuondoka naye kwenda nyumbani, huku watu wengi walioshuhudia tukio hilo, wakishangilia kwa nderemo, vifijo na vigelegele !
"Basi atukuzwe Yeye (Mungu) awezaye kufanya mambo ya ajabu mno kuliko yote tuyaombayo au tuyawazayo, kwa kadiri ya nguvu itendayo kazi ndani yetu; naam atukuzwe katika Kanisa na katika Kristo Yesu hata vizazi vyote vya milele na milele. Amina" (WAEFESO 3:20-21). MARANATHA !!!
Tazama picha zao
View attachment 1708770
View attachment 1708771View attachment 1708772View attachment 1708773View attachment 1708774View attachment 1708775View attachment 1708776View attachment 1708777View attachment 1708778View attachment 1708779View attachment 1708780View attachment 1708781View attachment 1708782View attachment 1708783View attachment 1708785View attachment 1708786View attachment 1708787View attachment 1708788View attachment 1708789View attachment 1708791View attachment 1708792View attachment 1708793View attachment 1708794View attachment 1708795View attachment 1708796View attachment 1708797View attachment 1708798View attachment 1708800View attachment 1708801View attachment 1708802
Mkuu na wale walioamua kuishi bila kuoana, je mke akifa washawahi kosa majirani wa kuja msibani?? Maana hawajawahi kuwa na ubwabwa ni sogea tukaeWatu wa aina yako tunawajua shida zao unawanyima watu sherehe ya harusi yako hakafu huyo nkeo akifariki huko ndani kelele unapiga mtaa nzima kuwa umefiwa na mjeo waje msibani wakati kwrnye harusi hukuwaalika unajifanya mtu wa principle usiyetaka kuingiliwa personal affairs zako na mkeo!!!