black hawk87
JF-Expert Member
- Jan 25, 2020
- 678
- 1,244
Vp Bado hajafumaniwa na vitoto vya watu akiwala mzigo ,hujapata kesi za kuandikia watoto za watu barua za uchumbakweli mkuu,
huyu dogo anamazuri yake licha ya hasara alizosababisha na tumejitahidi kuweka vitu mbali na kutojisahau kwa kadili inavyowezekana.
1: Hajinyei wala hajawahi kujinyea tangu alipofikisha mwaka na nusu. akitaka kukata gogo anaita ''mama poti'' analetewa.
2: Hazugi kula, hata ukimpa ugali bila mboga anakula hadi tumbo linajaa, na anaomba maji ya Kunywa.
3:analala mara mbili kwa siku ukiacha usiku.
4:Mimi Baba yake, naweza kwenda naye popote bila mama yake hata siku nzima na asinipe shida yoyote, Juzi nimejaribu kumtembeza kwa mguu tumetembea karibu kilometer moja bila kumbeba. anashangaa tu magari.
5:Ukimtuma kitu anakileta.
kilicho akilini kitumie