Lusungo
JF-Expert Member
- Jan 4, 2014
- 28,259
- 41,416
Morogoro kesho ofisi za umma na binafsi wameelekezwa kufunga ofisi mchana ili watumishi wakajaze jamhuri stadium. Mashule kesho kazi ni hiyo hiyo pamoja na kusomba watu toka wilaya za karibu..Ndugu zangu watanzania,
Huu ni zaidi ya Upendo, Ni zaidi ya kukubalika, ni zaidi ya kila kitu. Rais Samia ni Mpango wa Mungu Mwenyewe. Kwa mafuriko yanayoendelea kushuhudiwa katika ziara za Mheshimiwa Rais wetu mpendwa, kwa hakika hakuna sababu Ya yeye kuanza kuzunguka Nchi nzima kupiga kampeni za Urais Mwakani.
Mama anapendwa na kukubalika mpaka wapinzani wanatetemeka kama wagonjwa wa homa kali. Wapinzani kwa sasa wamechanganyikiwa na kuvurugwa kabisa akili baada ya kuona mapokezi mazito ambayo hayajawahi kushuhudiwa hapa Nchini.
Kama Afrika ingekuwa ni nchi moja basi Rais wetu mpendwa na Jemedari wetu kipenzi Mheshimiwa Daktari Mama Samia ndiye angekuwa Rais kwa sasa.Anakubalika kwa watu mpaka Watu wanatokwa na Machozi ya furaha utafikiri wamepakwa pilipili machoni.View attachment 3062519View attachment 3062520View attachment 3062521View attachment 3062522
Kazi iendelee, Mama Ametufikia na kuwafikia watanzania kwa utumishi wake uliotukuka wa kugusa maisha ya watanzania wanyonge wasio na Sauti.
Lucas Hebel Mwashambwa, Mama ANATOSHA kuendelea kuliongoza Taifa letu kwa muhula wa pili.View attachment 3062523
Najiuliza tu huyu mama haya yanayofanyika anayajua dhahiri au watu wanamla kisogo? Ni huruma sana!! Imagine hadi vyo visivyo vya umma wafanyakazi kuamriwa wafanye kazi nusu siku!!