Last emperor
JF-Expert Member
- Mar 22, 2015
- 10,351
- 9,855
Mleta uzi wivu unakudumbua. Kwenye kujirusha hakuna chama acha hizo bhana
Jamani mbona wasanii wengi Tu wanashabikia CCM? Mwanafa,Lina, Shilole,Mwasiti Na wengine wengi mbona anaandamwa Diamond? Kweli Diamond nyota inawka!
Mimi nimeisha mu unfollow kila mahali, siipendi ccm na vitu vyote vinavyofanana na ccm. Yale ma nzi ya kijani nyumbani kwangu nimeyaua yote!
Sasa mashabiki zake wapenda maendeleo hawajapendezwa na hilo... na wameamua kujitoaa kutomsopport..
Maana haiwezekani awatukane mashabiki zake ikiwa anajua kila mtu now ni UKAWA
This is too childish.... Tujifunze kukubaliana kutokubaliana katika mtizamo.... Siku nyingine mtamchagulia muda wa kujamiana na mwanamke wake kisa tu nyinyi huwa mnajamiana muda huo
Wewe kwa sababu umevurugwa huwezi elewa. Yeye alitakiwa kama msanii alitakiwa apige hela apite hivi, mambo ya kuanza kupaka watu jukwaani na kwenye instagram maana yake ameingia kwenye siasa rasmi. Na mimi sera yangu mtu yoyote wa ccm kwangu hatakiwi. Kwanza sijui kama hata uliisikia hiyo nyimbo aliyoimba kwenye Kampeni au unaropoka tu kama mtu alievurugwa utumbo mpana!
Kwanza sio ajabu mtu mwenyewe hata hujawahi kumpigia kura diamond sema umeona wivu ulipomwona jukwaani
alafu ID zinazosema hapa nilikuwa nampigia sana kura diamond lakini kuanzia sasa sitampigia tena kwanza zote ni mpya, ni ID moja tu naijui alikuwa diamond damu na ameweka wazi kusitisha support the rest ni changamsha genge tuu
Napenda kumjulisha msanii diamond platinumz, kuwa kwa tukio lile la jana pale uwanja wa jangwani kuwabeza na kuwakashifu upinzani umejimaliza rasmi! Kumbuka sio ccm pekee ndo waliokuwa wanahudhuria katika matamasha yako, wala kukupigia kura ulipokuwa unawania tuzo mbalimbali, ni watanzania wa itikadi zote. Sasa kwasababu umeamua kuchagua upande, basi ni upande huo ndo watakao kusupport. Sifa zimejaza kichwa chako mpaka umejisahau na kuona hakuna wa kukuporomosha wala kukufanya chochote. Ungekuwa na busara ungejifunza kwa yaliyomkuta Marlow baada ya kufanya kama ulivyofanya wewe, leo hasikiki tena. Nimeshangaa wewe kuwepo kwenye kundi la watu wanaowaona vijana kama sisi ni wapumbavu, malofa na vibaka! Mimi Naamini pamoja na watanzania wengine tumechukua hatua ya kukuunfolow katika mitandao mbalimbali ya kijamii. Pia sitokaa kukupigia kura wala kushiriki kwenye tamasha lako lolote. Ni hayo tu na maamuzi yangu ya kipumbavu na kilofa. Asante
Mkuu umetema madini matupu, yeye ni mjinga hajui kizazi chake wanashabikia upande gani, asinge take sides, angefanya kama alivyo fanya kwa lowassa, angepiga show avute mkwanja aende zake. Sasa ameamua kutake side, side ya chama ambacho asilimia kubwa ni waakina mama watu wazima na wazee. Sasa hivi hawezi ona, matokeo atayapata baada ya mwaka. Halaf amejiona amekuwa super star sana, kama jana anaongea live kwenye radio anamwambia DIVA ningekuwa NIMEKUKAZA ungeniheshimu. Katika umri wangu wote huu sijawahi msikia msanii anaongea hivyo radioni. Ndo yale yale ya mkapa kuwaita watanzania wanaotaka mabadiliko ni wapumbavu na malofa. Wamelewa hawa hela tunazowapa wenyeweDiamond hajawahi kumpigia kampeni lowasa
Aliitwa kutumbuiza akatumbuiza akasepa
Tusibishane sana...Muda ni jibu la kila kitu
Vijana ndio sisi...Na wengine hapa tumekuwa mashabiki wake wakubwa hata humu jukwaani inajulikana
Sasa tutaona....lwts wait and see....Ninyi wa CCM mtaendelea kum support hadi huko kwenye nominations zake
Mkuu umetema madini matupu, yeye ni mjinga hajui kizazi chake wanashabikia upande gani, asinge take sides, angefanya kama alivyo fanya kwa lowassa, angepiga show avute mkwanja aende zake. Sasa ameamua kutake side, side ya chama ambacho asilimia kubwa ni waakina mama watu wazima na wazee. Sasa hivi hawezi ona, matokeo atayapata baada ya mwaka. Halaf amejiona amekuwa super star sana, kama jana anaongea live kwenye radio anamwambia ningekuwa NIMEKUKAZA ungeniheshimu. Katika umri wangu wote huu sijawahi msikia msanii anaongea hivyo radioni. Ndo yale yale ya mkapa kuwaita watanzania wanaotaka mabadiliko ni wapumbavu na malofa. Wamelewa hawa hela tunazowapa wenyewe
napenda kumjulisha msanii diamond platinumz, kuwa kwa tukio lile la jana pale uwanja wa jangwani kuwabeza na kuwakashifu upinzani umejimaliza rasmi! Kumbuka sio ccm pekee ndo waliokuwa wanahudhuria katika matamasha yako, wala kukupigia kura ulipokuwa unawania tuzo mbalimbali, ni watanzania wa itikadi zote. Sasa kwasababu umeamua kuchagua upande, basi ni upande huo ndo watakao kusupport. Sifa zimejaza kichwa chako mpaka umejisahau na kuona hakuna wa kukuporomosha wala kukufanya chochote. Ungekuwa na busara ungejifunza kwa yaliyomkuta marlow baada ya kufanya kama ulivyofanya wewe, leo hasikiki tena. Nimeshangaa wewe kuwepo kwenye kundi la watu wanaowaona vijana kama sisi ni wapumbavu, malofa na vibaka! Mimi naamini pamoja na watanzania wengine tumechukua hatua ya kukuunfolow katika mitandao mbalimbali ya kijamii. Pia sitokaa kukupigia kura wala kushiriki kwenye tamasha lako lolote. Ni hayo tu na maamuzi yangu ya kipumbavu na kilofa. Asante