Kwa hili alilolifanya Diamond, litamgharimu sana katika safari yake ya kimuziki

Kwa hili alilolifanya Diamond, litamgharimu sana katika safari yake ya kimuziki

Jamani mbona wasanii wengi Tu wanashabikia CCM? Mwanafa,Lina, Shilole,Mwasiti Na wengine wengi mbona anaandamwa Diamond? Kweli Diamond nyota inawka!

Hawana madhara kama baba tiffah na hawara yake wa zamani.
 
Mimi nimeisha mu unfollow kila mahali, siipendi ccm na vitu vyote vinavyofanana na ccm. Yale ma nzi ya kijani nyumbani kwangu nimeyaua yote!

Mimi nimesema Diamond ana haki ya kuchagua chama chochote, unfortunately amechagua chama kinachotia kinyaa na kuchefua wengi.Sasa anaonekana kama msaliti fulani ivii amaiziing!
Kwa kweli bora nitazame picha za mazombie kuliko mapicha ya CCM.
 
This is too childish.... Tujifunze kukubaliana kutokubaliana katika mtizamo.... Siku nyingine mtamchagulia muda wa kujamiana na mwanamke wake kisa tu nyinyi huwa mnajamiana muda huo
 
Sasa mashabiki zake wapenda maendeleo hawajapendezwa na hilo... na wameamua kujitoaa kutomsopport..
Maana haiwezekani awatukane mashabiki zake ikiwa anajua kila mtu now ni UKAWA

kila mtu now ni ukawa....(nimegundua una upungufu mkubwa sana wa kufikri)

Sawa unapenda maendeleo...Je Diamond ni waziri mkuu au Raisi??... he is just exercising his civic right
 
Diamond hakubebwa ili kufika hapo alipo, so hakuna kitakacho mshusha as long as ataendelea kuwa na juhudi binafsi, juhudi zake ndo ziliwafanya mumpende, nadhani msingempenda kama kazi zake zingekuwa mbovu
 
Wewe kwa sababu umevurugwa huwezi elewa. Yeye alitakiwa kama msanii alitakiwa apige hela apite hivi, mambo ya kuanza kupaka watu jukwaani na kwenye instagram maana yake ameingia kwenye siasa rasmi. Na mimi sera yangu mtu yoyote wa ccm kwangu hatakiwi. Kwanza sijui kama hata uliisikia hiyo nyimbo aliyoimba kwenye Kampeni au unaropoka tu kama mtu alievurugwa utumbo mpana!

na nimevurugwa hasaaa wala sio kidogo, so kwa akili yako ukawa ni akina nani? kama siyo mvinyo wa zamani kwenye chupa mpya?? hivi kuna mtu alishawahi kujaza watu kama nyuki kwenye harakati za kutafuta wadhamini kama lowasa? HAPO ALIKUWA CCM, na sera za ccm, kidumu chama chamapinduzi na misifa kibao, watu walikuwa wanampigia shagwe haijapata kutokea,akapata wadhamini wakapitiliza hata waliokuwa wanahitajika kwa kila mkoa, huyu lowasa huyu,baada ya kukatwa tuu akahamia ukawa, sasa hapa kwa mtu ambaye amevurugwa kama mimi lazima ajiulize nyie watu mnataka nini?? mnamtaka lowasa au ukawa ndio sasa mumpangie diamond cha kufanya, je amsupport lowasa au upinzani? na upinzani unaouona wewe ni upi??
 
Kwanza sio ajabu mtu mwenyewe hata hujawahi kumpigia kura diamond sema umeona wivu ulipomwona jukwaani

alafu ID zinazosema hapa nilikuwa nampigia sana kura diamond lakini kuanzia sasa sitampigia tena kwanza zote ni mpya, ni ID moja tu naijui alikuwa diamond damu na ameweka wazi kusitisha support the rest ni changamsha genge tuu
 
Hivi wewe ulietoa mada unaweza kutafuta pesa au bado mwanafunzi..unajuwa pesa inavyotafutwa kweli wewe ndugu yangu...usirudie tena ku post vitu kabla ya kujiuliza na kujijibu ndiyo ulete mada mezani...Pesa inatafutwa kivyovyote vile wewe unachotakiwa ni kupanda dau
 
alafu ID zinazosema hapa nilikuwa nampigia sana kura diamond lakini kuanzia sasa sitampigia tena kwanza zote ni mpya, ni ID moja tu naijui alikuwa diamond damu na ameweka wazi kusitisha support the rest ni changamsha genge tuu

Ahahaha Team kiba nishawashtukia siku nyingiiiii!!wanataka kuaminisha watu kwamba diamond amekosea bahati mbaya shabiki zake tuko ngangari kinomaaaa,tumejipanga hasaaa!!

Ney wa Mitego daily anadiss watu huko Insta,lakini hajadiliwi huku JF,ni hiviii Hamtuwezi na hamtokuja kumuweza Diamond!

Endeleeni na akili zenu za kushikiwa na uvivu wenu team kiba na haters wote wa chibu,ndio kwanzaaaa diamond anang'araaa
 
Mwenzako anapiga pesa wewe unalialia wewe nenda kwenye mafuriko ya ukawa kwa wanuka kwapa ukakomboe nchi nani kakukataza maybe utaingiza chochote maana siku hiyo vitecno nje nje.
 
Napenda kumjulisha msanii diamond platinumz, kuwa kwa tukio lile la jana pale uwanja wa jangwani kuwabeza na kuwakashifu upinzani umejimaliza rasmi! Kumbuka sio ccm pekee ndo waliokuwa wanahudhuria katika matamasha yako, wala kukupigia kura ulipokuwa unawania tuzo mbalimbali, ni watanzania wa itikadi zote. Sasa kwasababu umeamua kuchagua upande, basi ni upande huo ndo watakao kusupport. Sifa zimejaza kichwa chako mpaka umejisahau na kuona hakuna wa kukuporomosha wala kukufanya chochote. Ungekuwa na busara ungejifunza kwa yaliyomkuta Marlow baada ya kufanya kama ulivyofanya wewe, leo hasikiki tena. Nimeshangaa wewe kuwepo kwenye kundi la watu wanaowaona vijana kama sisi ni wapumbavu, malofa na vibaka! Mimi Naamini pamoja na watanzania wengine tumechukua hatua ya kukuunfolow katika mitandao mbalimbali ya kijamii. Pia sitokaa kukupigia kura wala kushiriki kwenye tamasha lako lolote. Ni hayo tu na maamuzi yangu ya kipumbavu na kilofa. Asante

Mtoto wa kiume unalalamika kama msichana. Let a boy live and enjoy his life and choices. Why diamond kila siku na anazidi kufanikiwa. Lofa indeed
 
wanatamani mno anguko la Domo lakini haliji!kilichompandisha ndicho kitakachomshusha..kuna wengi wanaanza kumzingatia pale wanaposikia anapondwa zaidi.kaitwa na CCM,kapiga hela kaenda zake.
kuhusu maoni yake juu ya masuala ya kisiasa ni haki yake kama mtanzania.kusema hutampigia kura sababu anaamini tofauti na wewe ni upuuz...kwani mna dini za kufanana?kabila je?umri?elimu?we pia una date mtu mzima sana kukuzidi kama yeye?
fuatilia muziki wake...bhaas.anachofanya nje ya muziki hakikuhusu ni maisha yake binafsi.hutaki kumshabikia....pita hiv....
 
Diamond hajawahi kumpigia kampeni lowasa

Aliitwa kutumbuiza akatumbuiza akasepa

Tusibishane sana...Muda ni jibu la kila kitu

Vijana ndio sisi...Na wengine hapa tumekuwa mashabiki wake wakubwa hata humu jukwaani inajulikana

Sasa tutaona....lwts wait and see....Ninyi wa CCM mtaendelea kum support hadi huko kwenye nominations zake
Mkuu umetema madini matupu, yeye ni mjinga hajui kizazi chake wanashabikia upande gani, asinge take sides, angefanya kama alivyo fanya kwa lowassa, angepiga show avute mkwanja aende zake. Sasa ameamua kutake side, side ya chama ambacho asilimia kubwa ni waakina mama watu wazima na wazee. Sasa hivi hawezi ona, matokeo atayapata baada ya mwaka. Halaf amejiona amekuwa super star sana, kama jana anaongea live kwenye radio anamwambia DIVA ningekuwa NIMEKUKAZA ungeniheshimu. Katika umri wangu wote huu sijawahi msikia msanii anaongea hivyo radioni. Ndo yale yale ya mkapa kuwaita watanzania wanaotaka mabadiliko ni wapumbavu na malofa. Wamelewa hawa hela tunazowapa wenyewe
 
Mkuu umetema madini matupu, yeye ni mjinga hajui kizazi chake wanashabikia upande gani, asinge take sides, angefanya kama alivyo fanya kwa lowassa, angepiga show avute mkwanja aende zake. Sasa ameamua kutake side, side ya chama ambacho asilimia kubwa ni waakina mama watu wazima na wazee. Sasa hivi hawezi ona, matokeo atayapata baada ya mwaka. Halaf amejiona amekuwa super star sana, kama jana anaongea live kwenye radio anamwambia ningekuwa NIMEKUKAZA ungeniheshimu. Katika umri wangu wote huu sijawahi msikia msanii anaongea hivyo radioni. Ndo yale yale ya mkapa kuwaita watanzania wanaotaka mabadiliko ni wapumbavu na malofa. Wamelewa hawa hela tunazowapa wenyewe

The guy is hopeless....naanza kuelewa
 
napenda kumjulisha msanii diamond platinumz, kuwa kwa tukio lile la jana pale uwanja wa jangwani kuwabeza na kuwakashifu upinzani umejimaliza rasmi! Kumbuka sio ccm pekee ndo waliokuwa wanahudhuria katika matamasha yako, wala kukupigia kura ulipokuwa unawania tuzo mbalimbali, ni watanzania wa itikadi zote. Sasa kwasababu umeamua kuchagua upande, basi ni upande huo ndo watakao kusupport. Sifa zimejaza kichwa chako mpaka umejisahau na kuona hakuna wa kukuporomosha wala kukufanya chochote. Ungekuwa na busara ungejifunza kwa yaliyomkuta marlow baada ya kufanya kama ulivyofanya wewe, leo hasikiki tena. Nimeshangaa wewe kuwepo kwenye kundi la watu wanaowaona vijana kama sisi ni wapumbavu, malofa na vibaka! Mimi naamini pamoja na watanzania wengine tumechukua hatua ya kukuunfolow katika mitandao mbalimbali ya kijamii. Pia sitokaa kukupigia kura wala kushiriki kwenye tamasha lako lolote. Ni hayo tu na maamuzi yangu ya kipumbavu na kilofa. Asante

binadamu yeyote anakuwa na msimamo wake
usilazimishe diomond afuate unachotaka wewe .kilichompandisha ni ubora wa muziki wake si kingine..
 
Back
Top Bottom