Kwa hili la Inyala, Mbeya ninampinga Makamu wa Rais Dr. Mpango kwa agizo lake "quick fix" na kumsihi awe serious na maisha ya Watanzania

Kwa hili la Inyala, Mbeya ninampinga Makamu wa Rais Dr. Mpango kwa agizo lake "quick fix" na kumsihi awe serious na maisha ya Watanzania

Unalionaje agizo la Dr. Mpango?

  • Zuri linafaa sana

    Votes: 4 21.1%
  • Halifai kabisa

    Votes: 15 78.9%

  • Total voters
    19
Nimeona taarifa ya Mkuu wa Mkoa Mbeya, Homera, akisema DED na dereva wake waliambiwa na polisi wa usalama barabarani wasubiri kwanza, wao wakalazimisha kwenda wakisema walikuwa na haraka.

Naona hiyo haraka yao ndio iliyosababisha mwendo kasi ulioleta ile ajali, ndio maana ile gari ya DED imechakaa vibaya sana. Hawa viongozi wa serikali waache kutumia vyeo vyao kulazimisha mambo hadi kwenda kinyume na taratibu, wataisha.
Yaani madereva wa gari serikali na za viongozi Tz , wengi wao huwa ni ku' jimwambafy' bila sababu za msingi..... matokeo yake ndio haya...RIP Mkurugenzi.
 
Najaribu kuwaza nje ya bokisi. Wakati ule wa biashara ya viungo vya wenye ulemavu wa ngozi/ alibino ilipopamba moto sababu ilikuwa ni nini?
 
Mwisho, ninawaomba sana viongozi wetu jaribuni kuwa serious na matatizo yanayowakabili Wananchi, hasa yale yanayosababisha vifo. Msitangulize kukimbia gharama za kutatua matatizo kama haya na kupendekeza majibu ya kisiasa ambayo hayatatusaidia. Kama tatizo ni fedha, tunakatwa sana tozo, tumieni hizo pale Inyala kama suala la emergency.
Ili upate suluhisho la tatizo kwa usahihi ni lazima nawe uingie uonje au uwe sehemu ya tatizo hilo, viongozi wetu hawaliwezi hilo la kujaribu kuzama kwenye matatizo ili kufeel namna sahihi ya kutatua matatizo.

Hili unaloshauri ni sahihi kabisa nakupa heko, TANROADS walitakiwa kumshauri hivi VP ili kauli yake iwe na mashiko, hao wanaoambiwa wakague malori siyo mafundi na hawana uelewa wowte wa mifumo ya magari makubwa, alichofanya hapo VP ni kupanua wigo wa rushwa.

Nchi hii ina shida kwenye uongozi, haya maamuzi ya kipuuzi ndiyo yaleyale yanayowatesa wananchi mijini kwa kuzuia mabasi kushusha abiria kwenye vituo vya katikati ya miji ukiuliza sababu ni vile wanakuuza ajira kwa bodaboda bajaji guta na daladala wanazomiliki wao which is a very wrong ideology and fixed mindset of politicians
 
Mnaosema gari ikaguliwe kabla ya kushuka mlima mnauhakika kuwa kabla ya gari hiyo kuanza kushuka haikuwa na brake?, je mnajua chanzo kikuu cha magari kufeli brake hapo inyala?.

Kwa nini mlima nyoka hakuna sana ajali zaidi ya hapo inyala/pipe line?.

Gari ishuke mlima nyoka vizuri halafu inyala kumaliza hapo ujue ni uendeshaji pia unachangia na barabara kwa sasa imeshakuwa ndogo hiyo haikidhi vigezo vya kuhimili wingi wa magari yanayopita kwa sasa.

Climbing lane zinahitajika,lay bay na njia za kuepuka ajali kama zile za migodini au hapo imhotep kaweka clip, hayo ndiyo yanayohitajika kwa sasa na wala si sababu za kila siku kusema brake brake.

Madereva wetu wa sasa sio kama wale wa zamani wa kuendesha tani 70 nk siku hizi wanyoa viduku nao wapo kwenye malori na hawa ni tatizo na wala hawashauriki na wala kutaka kujifunza mambo mapya.
 
Ili upate suluhisho la tatizo kwa usahihi ni lazima nawe uingie uonje au uwe sehemu ya tatizo hilo, viongozi wetu hawaliwezi hilo la kujaribu kuzama kwenye matatizo ili kufeel namna sahihi ya kutatua matatizo.

Hili unaloshauri ni sahihi kabisa nakupa heko, TANROADS walitakiwa kumshauri hivi VP ili kauli yake iwe na mashiko, hao wanaoambiwa wakague malori siyo mafundi na hawana uelewa wowte wa mifumo ya magari makubwa, alichofanya hapo VP ni kupanua wigo wa rushwa.

Nchi hii ina shida kwenye uongozi, haya maamuzi ya kipuuzi ndiyo yaleyale yanayowatesa wananchi mijini kwa kuzuia mabasi kushusha abiria kwenye vituo vya katikati ya miji ukiuliza sababu ni vile wanakuuza ajira kwa bodaboda bajaji guta na daladala wanazomiliki wao which is a very wrong ideology and fixed mindset of politicians
Siku tukiamua kuanza kutumia wataalamu wa gani husika kwenye matatizo mengi ya nchi hii ili kupata ufumbuzi, hakika mambo mengi sana yatabadilika.
 
Katika taarifa yake kuhusu ajali ya pale Inyala Mkoani Mbeya iliyoua watu kadhaa pamoja na DED wa Igunga, Gazeti la Mwananchi limetoa taarifa kwamba ajali hiyo imetokea ikiwa ni siku tatu zimepita baada ya Makamu wa Rais Dkt. Mpango kutoa maagizo kwa Jeshi la Polisi Mkoa wa Mbeya kuanza ukaguzi wa magari ya mizigo katika eneo hili.

Sasa nashindwa kuelewa busara ya Makamu wetu wa Rais kwamba suluhisho la kuzuia ajali pale Inyala ni kuyakagua magari ya mizigo kabla hayajapita kile kipande cha barabara. Hili nalipinga kwa dhati. Nimeshindwa na hata kuchukizwa na jinsi watu walio na madaraka nchini kama Dkt. Mpango wanavyoyachukulia mambo mazito kirahisi namna hivi.

Hili ni eneo ambalo karibu kila wiki panatokea ajali mbaya sana, na Dkt. Mpango anasema kagueni magari kabla hayajapita hapa. Hii ni busara kweli?

Anapaswa kuelewa nini kinasababisha ajali pale kabla ya kutoa kile tunaita utatuzi wa kisiasa kwa tatizo la kisayansi.

Kwa kumsaidia tu na kumpa ushauri wa bure usio wa kisiasa, ni kwamba kuna sababu kubwa tatu zinazosababisha ajali pale;
  1. Barabara imeharibika sana na kuweka matuta ya lami kudidimia ambayo mara nyingi yanakulazimu kupita upande usio wako wa barabara au kupoteza control ya gari unapopanda tuta kwa sababu gari zinayumba sana kwenye haya matuta
  2. Hiyo sehemu ina mlima/mteremko wa umbali mrefu
  3. Hiyo sehemu ni ya solid line ambayo huwezi ku-overtake gari nyingine (japo madereva wa mabasi hawajali hili)
Sasa Dkt. Mpango anapaswa kutoa wazo la kuzuia ajali pale kwa kuangalia hizo sababu tatu. Na kwa mawazo tu, haya yanapaswa kufikiriwa na Serikali ili kuzuia vifo na ajali za kila wakati eneo hili;
  1. TANROAD waamrishwe kutengeneza hili eneo haraka sana. Matengenezo yanayotakiwa hapa ni kama yale yaliyofanyika mteremko wa Kitonga katika kuzuia barabara kuweka matuta kutokana na uzito wa malori.
  2. Kwa kuwa hili ni eneo la mlima/mteremko wa umbali mrefu, pawekwe climbing lane ili kuwepo na njia tatu na ambayo moja itatumiwa zaidi na malori yanayopanda taratibu sana eneo hili
  3. Zaidi ya kuweka climbing lanes, eneo hili liwekwe "lay-by" kadhaa (yaani michepuko katika barabara iliyo kama sehemu ya kituo cha basi) ili madereva wanaopanda au kuteremka wawe na eneo la kuingia pale wanapoona gari lao linaanza kuleta matatizo na kulifanyia marekebisho, badala ya kusimamisha lori barabarani eneo la hatari.
Mwisho, ninawaomba sana viongozi wetu jaribuni kuwa serious na matatizo yanayowakabili Wananchi, hasa yale yanayosababisha vifo. Msitangulize kukimbia gharama za kutatua matatizo kama haya na kupendekeza majibu ya kisiasa ambayo hayatatusaidia. Kama tatizo ni fedha, tunakatwa sana tozo, tumieni hizo pale Inyala kama suala la emergency.
We ndiyo hujielewi ht umeandika nn. Ajali ya jana Lori ilifeli breki. Ajali nyingi ubovu wa malori
 
VP kila uchao analishwa matango pori tu, tuwaache wataalamu waje na suluhisho hilo eneo hata mtu wa kawaida tu anaweza kuja na solution, barabara ni mbovu sana na nyembamba.
 
Katika taarifa yake kuhusu ajali ya pale Inyala Mkoani Mbeya iliyoua watu kadhaa pamoja na DED wa Igunga, Gazeti la Mwananchi limetoa taarifa kwamba ajali hiyo imetokea ikiwa ni siku tatu zimepita baada ya Makamu wa Rais Dkt. Mpango kutoa maagizo kwa Jeshi la Polisi Mkoa wa Mbeya kuanza ukaguzi wa magari ya mizigo katika eneo hili.

Sasa nashindwa kuelewa busara ya Makamu wetu wa Rais kwamba suluhisho la kuzuia ajali pale Inyala ni kuyakagua magari ya mizigo kabla hayajapita kile kipande cha barabara. Hili nalipinga kwa dhati. Nimeshindwa na hata kuchukizwa na jinsi watu walio na madaraka nchini kama Dkt. Mpango wanavyoyachukulia mambo mazito kirahisi namna hivi.

Hili ni eneo ambalo karibu kila wiki panatokea ajali mbaya sana, na Dkt. Mpango anasema kagueni magari kabla hayajapita hapa. Hii ni busara kweli?

Anapaswa kuelewa nini kinasababisha ajali pale kabla ya kutoa kile tunaita utatuzi wa kisiasa kwa tatizo la kisayansi.

Kwa kumsaidia tu na kumpa ushauri wa bure usio wa kisiasa, ni kwamba kuna sababu kubwa tatu zinazosababisha ajali pale;
  1. Barabara imeharibika sana na kuweka matuta ya lami kudidimia ambayo mara nyingi yanakulazimu kupita upande usio wako wa barabara au kupoteza control ya gari unapopanda tuta kwa sababu gari zinayumba sana kwenye haya matuta
  2. Hiyo sehemu ina mlima/mteremko wa umbali mrefu
  3. Hiyo sehemu ni ya solid line ambayo huwezi ku-overtake gari nyingine (japo madereva wa mabasi hawajali hili)
Sasa Dkt. Mpango anapaswa kutoa wazo la kuzuia ajali pale kwa kuangalia hizo sababu tatu. Na kwa mawazo tu, haya yanapaswa kufikiriwa na Serikali ili kuzuia vifo na ajali za kila wakati eneo hili;
  1. TANROAD waamrishwe kutengeneza hili eneo haraka sana. Matengenezo yanayotakiwa hapa ni kama yale yaliyofanyika mteremko wa Kitonga katika kuzuia barabara kuweka matuta kutokana na uzito wa malori.
  2. Kwa kuwa hili ni eneo la mlima/mteremko wa umbali mrefu, pawekwe climbing lane ili kuwepo na njia tatu na ambayo moja itatumiwa zaidi na malori yanayopanda taratibu sana eneo hili
  3. Zaidi ya kuweka climbing lanes, eneo hili liwekwe "lay-by" kadhaa (yaani michepuko katika barabara iliyo kama sehemu ya kituo cha basi) ili madereva wanaopanda au kuteremka wawe na eneo la kuingia pale wanapoona gari lao linaanza kuleta matatizo na kulifanyia marekebisho, badala ya kusimamisha lori barabarani eneo la hatari.
Mwisho, ninawaomba sana viongozi wetu jaribuni kuwa serious na matatizo yanayowakabili Wananchi, hasa yale yanayosababisha vifo. Msitangulize kukimbia gharama za kutatua matatizo kama haya na kupendekeza majibu ya kisiasa ambayo hayatatusaidia. Kama tatizo ni fedha, tunakatwa sana tozo, tumieni hizo pale Inyala kama suala la emergency.
Good analysis Dr Mpango kanogewa na asali siku hizi anajiongelea tu bora liende. Anataka kuwatengenezea Polisi mfereji wa rushwa kwa kisingizio cha kukagua malori wakati hata Sasa wanakagua na ajali ziko pale pale majibu rahisi kwa maswali magumu.
 
Miundombinu Inaruhusu kujihami? Unajihami vp kwenye single carriage road kwenye mteremko? Gari nyingine ikifeli break na kuja kwako unaenda wapi? Unapajua Inyala au?

Common sense isn't common hakika
K 5.
KUONA
Kutambua
Kutabiri
Kuamua
Kutekeleza
 
Mnaambiwa subirini,wao wanajifanya wana haraka

Ova
 
Mnaosema gari ikaguliwe kabla ya kushuka mlima mnauhakika kuwa kabla ya gari hiyo kuanza kushuka haikuwa na brake?, je mnajua chanzo kikuu cha magari kufeli brake hapo inyala?.

Gari ishuke mlima nyoka vizuri halafu inyala kumaliza hapo ujue ni uendeshaji pia unachangia na barabara kwa sasa imeshakuwa ndogo hiyo haikidhi vigezo vya kuhimili wingi wa magari yanayopita kwa sasa.
Mie sijaona gari inakaguliwa breki kabla ya kuanza kupanda mlima!

Halafu, Dr. Mpango anasema magari ya mizigo yakaguliwe pale. Ukifika kwenye sehemu za kupima uzito malori yanakuwa mengi sana kusubiri kupima uzito, kitu kinachotumia mashime. Sasa amefikiri hao mafundi , na sijui watakuwa nani, watachukua muda gani kukagua breki? Tutajikuta lori zinakaa pake siku mbili zikisubiri kukaguliwa ili zitelemke au kupanda Mlima wa Inyala! Sasa hilo wazo nalo ni akili kweli?
 
We ndiyo hujielewi ht umeandika nn. Ajali ya jana Lori ilifeli breki. Ajali nyingi ubovu wa malori
Sasa hayo maneno kamwambie Dr Mpango, maana kama lilifeli breki ina maana lingekaguliwa breki zikiwa hazijafeli na lingeruhusiwa kupita. Huwezi hata kufikiri kama tu yule jamaa
 
Mnaambiwa subirini,wao wanajifanya wana haraka

Ova
Mie sidhani wao kuamua kupita ni tatizo. Tusitafute tatizo la karibu. Kwani magari yanapita pale kwa zamu kwa kuwa malori huwa yanafeli breki? Jiulize hilo

Ila najiuliza, huyu dereva nae alikuwa mzanzibari? Hawajazoea mikiki ya barabara kama hizi hawaa, wao trip zao sana sana ndefu kuliko yote ni masaa matatu kama sikosei, hakuna hata kupishana na lori, hakuna milima. Hawa viongozi wanaoletwa bara toka Zanzibar kuja bara wasiwe wanaleta madereva wao.
 
Marlezo yote haya ni hofu ya ukaguzi kwani mnabeba vitu gani?
Hebu tumia akili kidogo wewe. Yaani wewe umefikiria ukaguzi wa kuzuia ajali Inyala ni kukagua lori limebeba nini? I say kuna watu mnajifinya na kulalamika. Halafu unakuta mtu kama wewe eti unaruhusiwa kupiga kura kutuchagulia viongozi!
 
Inasikitisha sana jinsi tusivyoweza kuwa na majawabu sahihi huku kuna lundo la Wataalamu
Kwanza Dr Mpango amejiuliza ukiweka utaratibu wa kukagua malori pale atapata wapi wakaguzi wa kutosha ili kutosababisha msongamano wa malori? Hajafikiria kwamba tunaweza kukuta lori linakaa pale siku mbili likisubiri kukaguliwa ili lishuke au kupanda mlima? Hebu atembelee mizani kwanza aone ikiwa mizani hali ndio hiyo, kukagua breki za malorii itakuwaje. Yatapaki wapi ili yakaguliwe? Nani watakagua? Watalala wapi? Watakula, kunywa na kunya wapi wakiwa katika zoezi hilo? Okay, na lori likikutwa lina tatizo, then what, tutaanzisha magereji pale? Yaani viongozi wanaongea tu, wanatoa tu maagizo "impractical" kirahisi!
 
Back
Top Bottom