Kwa hili la mwaka mmoja wa kifo cha Magufuli, Kanisa Katoliki linapaswa kuona aibu

Kwa hili la mwaka mmoja wa kifo cha Magufuli, Kanisa Katoliki linapaswa kuona aibu

Mwandishi huelewi kuwa hiyo ni sherehe ya kusherekea kifo cha huyo mnyambuda kiaina. Hapo watu wa kanisa wanasherehekea kinamna.
 
Kwani wewe ni muumini wa kanisa katoliki? Mbona kama hujielewi,kanisa linasimama kwasababu ya neno msamaha.
Madayako umeanza na kanisa katoliki alafu humondani umechanganyachanganya mara kakobe blabla blabla.

Kama hujui kusamehe then hujui hata maana ya ukristo.
Msamaha sio kuwasafisha hawa waovu
 
Kila kitu kilichoandikwa hapo Magufuli alikifanya hadharani kabisa, sio tuhuma.
Labda kama ulikuwa hufuatilii siasa
Wewe inaonesha wazi sio mfuasi wa imani ya kikristo.
Ni nani wewe hata uwe na nguvu ya kumhukumu mwenzio?!

Kanisa liko sahihi. Kazi ya kuhukumu ni ya Mungu peke yake.
 
Wewe inaonesha wazi sio mfuasi wa imani ya kikristo.
Ni nani wewe hata uwe na nguvu ya kumhukumu mwenzio?!

Kanisa liko sahihi. Kazi ya kuhukumu ni ya Mungu peke yake.
Yaani Leo hii kule Italia wanaweza kumuadhikisha Mussolini Lisa wakristo hawatakiwi kuhukumu?
 
Mlidhani angechukiwa Milele, mlijiaminisha ni Dikteta sababu aligusa Maslahi yenu ila deep down mnamkumbuka, mnatamani arudi walau sekunde moja tu mumwambie 'Samahani', Haiwezekani,

Mna Maumivu ya Nafsi, mnacheka lakini Roho zinawasuta, Magufuli Kipenzi cha Wengi,

Continue to Rest Easy Mzalendo halisi.
Kipenzi ??😂😂😜
Basi pole kwa kipenzi chako kuwa kuzimu
 
Ndio Kila mtu atakufa, Ila Kuna vifo vingine lazima tuvisheherekee kwa kuwa vimeleta unafuu kwa binadamu waliobaki
Unafuu wa maisha kwa lipi mkuu ,inaonekana unaishi Marekani sio Tanzania yetu hii ambayo vifaa vya ujenzi viko juu,maisha magumu na watu wanakula mlo mmoja ,wamachinga wanatamani kutoka Dar kurudi shamba ,ajira wanapewa kwa michongo , ..... tatizo muda .
 
Sitaki kuzungumzia maovu ya kisiasa aliyoyafanya kwa Taifa huyu mtu, maana hata ukurasa huu hautatosha, nataka nizungumzie tu maovu aliyowafanyia kanisa Katoliki na Makanisa Mengine, halafu leo hii wanaadhimisha mwaka mmoja tangu kifo chake

Kwanza kabisa kulikuwa na mauaji na watu kupotea kulivyoshamiri mwaka 2017 Kanisa Katoliki lilitoa waraka wa kulaani mambo hayo na kuliombea Taifa lirudi kwenye mstari, alichojibu bwana huyu ni kulikejeli Kanisa katoliki na kusema kuwa halikukemea mauaji ya Kibiti (Kitu ambacho ni uongo, Kanisa lilikemea) na hata kama halikukemea kweli ndio itafanya mauaji ya watu wale kuwa sahihi? Ni mtu muovu namna gani anayeweza kuwaza hivi? Kanisa halioni aibu kumuadhimisha mtu kama huyu?

Pili, Baraza la Maaskofu wa Makanisa ya Kiprotestanti nao wakatoa waraka wa kukemea mauaji yaliyokuwa yameshamiri nchini kipindi kile, lakini mtu huyu alivyokuwa wa ajabu alitoa wa notisi kwa makanisa hayo kufuta waraka huo ama yatafutiwa usajili, hii ilileta sekeseke hadi aliyekuwa waziri wa mambo ya ndani kipindi kile Mwigulu Nchemba kuondolewa

Tatu, Askofu Kakobe, aliposema kuwa Tanzania ni nchi ya vyama vingi na vyama vyote vinapaswa kupewa nafasi, askofu huyu alitukanwa na kudhihakiwa sana na vijana wa kazi wa huyu mzee, na kunyang’anywa paspoti yake na kuambiwa sio raia wa Tanzania, haikuishia hapo askofu Kakobe alitishiwa kufilisiwa mali zake na za kanisa endapo ‘asingeunga juhudi’ . Huytu ndiye mtu Kanisa Katoliki linamuadhimisha?

Nne, Askofu Niwemugizi aliposema kudai katiba mpya sio uchochezi, mtu huyu bila chembe ya aibu alimuundia zengwe kuwa sio raia wa Tanzania na akapokjonywa paspoti, japo Askofu huyu ndio alikuwa Askofu wake tangu kabla hajawa Rais..!

Tano, Kulipokuwa na Wimbi la ugonjwa Corona, mtu huyu kwa siasa zake za kilaghai akasema Corona imeondolewa kwa maombi ya siku 3, Kanisa Katoliki ambalo linajua kuwa Mungu katupa Sayansi ya kukabiliana na majanga, likasisitiza watu kuchukua tahadhari za kisayansi na kushauri Serikali ifuate njia zilizothibitishwa Kisayansi kukabiliana na hili Janga.

Kanisa lilienda mbali na kutoa takwimu za watumishi wake kama maaskofu, mapadri, masista n.k waliokufa wengi kwa kipindi kifupi kwa dalili za ugonjwa wa Covid. Mtu huyu mnakumbuka alifanyaje?

Alikejeli vibaya viongozi wa Dini na kusema wanapotosha watu kiimani, kuna kipindi aliingia kanisani na kumkejeli padre mmoja aliyekuwa anazingatia kanuni za kujikinga na Corona. Mtu huyu leo ndio Kanisa..Au linataka kumtangaza Mtakatifuu?

Nimechagua baadhi tu ambayo yalifanyika hadharani na mtu fmfuatiliji wa siasa atayajua, ila yapo mengi sana mtu huyu aliwafanyia viongozi wa Dini kama yale ya akina Mwingira, na kukamata mapadri huko Moshi, ila niishie hapa

Najua baadhi wanaweza kuteta na kusema alikuwa kiongozi mkubwa wa nchi aliyefanya mambo makubwa hivyo lazima wamuadhimishe.

Lakini Mkapa, ambaye ni kiongozi aliyekuwa na mapungufu yake pia japo hayakufikia kiwaongo hiki, alifanya mambo makubwa sana na alipofikisha mwaka mmoja tangu kifo chake, Kanisa Katoliki halikufanya chochote
Weweee...Halafu unaonekana utakuwa na Shida saaana KIMAISHA. Watu kama wewe huwa mnakufa Maskini.
 
Sitaki kuzungumzia maovu ya kisiasa aliyoyafanya kwa Taifa huyu mtu, maana hata ukurasa huu hautatosha, nataka nizungumzie tu maovu aliyowafanyia kanisa Katoliki na Makanisa Mengine, halafu leo hii wanaadhimisha mwaka mmoja tangu kifo chake

Kwanza kabisa kulikuwa na mauaji na watu kupotea kulivyoshamiri mwaka 2017 Kanisa Katoliki lilitoa waraka wa kulaani mambo hayo na kuliombea Taifa lirudi kwenye mstari, alichojibu bwana huyu ni kulikejeli Kanisa katoliki na kusema kuwa halikukemea mauaji ya Kibiti (Kitu ambacho ni uongo, Kanisa lilikemea) na hata kama halikukemea kweli ndio itafanya mauaji ya watu wale kuwa sahihi? Ni mtu muovu namna gani anayeweza kuwaza hivi? Kanisa halioni aibu kumuadhimisha mtu kama huyu?

Pili, Baraza la Maaskofu wa Makanisa ya Kiprotestanti nao wakatoa waraka wa kukemea mauaji yaliyokuwa yameshamiri nchini kipindi kile, lakini mtu huyu alivyokuwa wa ajabu alitoa wa notisi kwa makanisa hayo kufuta waraka huo ama yatafutiwa usajili, hii ilileta sekeseke hadi aliyekuwa waziri wa mambo ya ndani kipindi kile Mwigulu Nchemba kuondolewa

Tatu, Askofu Kakobe, aliposema kuwa Tanzania ni nchi ya vyama vingi na vyama vyote vinapaswa kupewa nafasi, askofu huyu alitukanwa na kudhihakiwa sana na vijana wa kazi wa huyu mzee, na kunyang’anywa paspoti yake na kuambiwa sio raia wa Tanzania, haikuishia hapo askofu Kakobe alitishiwa kufilisiwa mali zake na za kanisa endapo ‘asingeunga juhudi’ . Huytu ndiye mtu Kanisa Katoliki linamuadhimisha?

Nne, Askofu Niwemugizi aliposema kudai katiba mpya sio uchochezi, mtu huyu bila chembe ya aibu alimuundia zengwe kuwa sio raia wa Tanzania na akapokjonywa paspoti, japo Askofu huyu ndio alikuwa Askofu wake tangu kabla hajawa Rais..!

Tano, Kulipokuwa na Wimbi la ugonjwa Corona, mtu huyu kwa siasa zake za kilaghai akasema Corona imeondolewa kwa maombi ya siku 3, Kanisa Katoliki ambalo linajua kuwa Mungu katupa Sayansi ya kukabiliana na majanga, likasisitiza watu kuchukua tahadhari za kisayansi na kushauri Serikali ifuate njia zilizothibitishwa Kisayansi kukabiliana na hili Janga.

Kanisa lilienda mbali na kutoa takwimu za watumishi wake kama maaskofu, mapadri, masista n.k waliokufa wengi kwa kipindi kifupi kwa dalili za ugonjwa wa Covid. Mtu huyu mnakumbuka alifanyaje?

Alikejeli vibaya viongozi wa Dini na kusema wanapotosha watu kiimani, kuna kipindi aliingia kanisani na kumkejeli padre mmoja aliyekuwa anazingatia kanuni za kujikinga na Corona. Mtu huyu leo ndio Kanisa..Au linataka kumtangaza Mtakatifuu?

Nimechagua baadhi tu ambayo yalifanyika hadharani na mtu fmfuatiliji wa siasa atayajua, ila yapo mengi sana mtu huyu aliwafanyia viongozi wa Dini kama yale ya akina Mwingira, na kukamata mapadri huko Moshi, ila niishie hapa

Najua baadhi wanaweza kuteta na kusema alikuwa kiongozi mkubwa wa nchi aliyefanya mambo makubwa hivyo lazima wamuadhimishe.

Lakini Mkapa, ambaye ni kiongozi aliyekuwa na mapungufu yake pia japo hayakufikia kiwaongo hiki, alifanya mambo makubwa sana na alipofikisha mwaka mmoja tangu kifo chake, Kanisa Katoliki halikufanya chochote
Achana na Mambo ya kanisa, wewe unaweza kumhubiri Mungu bila kuogopa hata kama unaua??? Unaweza kusema Mungu oyeeeeee mbele za watu wa dini mbalimbali. Mwacha mtu wa Mungu aendelee kuenziwa. Kikubwa dunia nzima ilihubiriwa habari za Mungu kwa mwaka mmoja. Kama unaona wivu kesho jifungie ndani.
 
Ndio Kila mtu atakufa, Ila Kuna vifo vingine lazima tuvisheherekee kwa kuwa vimeleta unafuu kwa binadamu waliobaki
Unafuu wakati wa mateso yako upo pale pale!?. Wakati wa kulala juu ya kitanda cha hospitalini kwa miezi sita ukitumia mipira kupumua?.

Mkuu usifurahie sana kifo cha mwenzako ukawa unamkufuru Mungu.
 
Uzi wako umetuhumu tu, hakuna sehemu umeweka uthibitisho, hebu tuwekee hapa ili uwe credible.
Huu
1647437506375.jpg
 
Kanisa katoliki jimbo kuu la mwanza ni kanisa linaloongozwa kisiasa hasa, John magufuli alikuwa na matendo mengi mabaya kuliko mazuri. magufuli alikuwa hana moyo wa kitanzania na kibinadamu. hafai kutengewa siku kwa ajili ya kumuombea. kumbuka matendo yake yameathiri wengi hasa.
 
Back
Top Bottom