Kwa hili la Ndugai na Rais, linaonesha watanzania ndio tuna matatizo makubwa

Kwa hili la Ndugai na Rais, linaonesha watanzania ndio tuna matatizo makubwa

THE FIRST BORN

JF-Expert Member
Joined
Apr 24, 2019
Posts
2,224
Reaction score
4,472
Habarini!

Hii vita inayoendelea inaonyesha Jinsi gani watanzania ndio tuna shida kubwa na ndio sababu hatuendelei.

Ndugai kasemea Juu ya jambo ambalo lina maslahi kwa Nchi lakini anakuja Mtu ana mjibu kwa kuangalia Maslahi yake tena kwa kejeli watu Wooooteee wanashangilia Kweli Mpo serious?

Yeah ni kweli kuna sehemu nyingi Ndugai kateleza sana huko Nyuma ila Kuna msemo unasema "Mnyonge Mnyongeni Ila Haki yake Mpeni" Ndugai ana haki ya kujibiwa Sio kwa Njia ya personal attack ila kwa njia ileile aliyotumia kuelezea Issue yake.

Hili suala la Ndugai tuweke Makosa yake pembeni tumhoji Rais sio tufurahi kifo cha Ndugai.

NOTE:
Swala la Msamaha alioomba Ndugai to Me usiulete hapa, ule alileta Njaaa zake tu na hizo ndio errors zake Kila siku tujadili Issue.
 
Tumbocracy ndicho kilichopo. Kaanza lini kujali maslahi yangu, wewe na WaTZ wenzetu? Kumbe angekiri huko nyuma kwamba anasutwa na MIDOLA aloyeyusha kujitibia kwa pesa zetu huku wengine hata panadol ya mia hawaimudu! Ingeanzia hapo. Mengineyo ni maslahi binafsi, TUMBOCRACY tu
 
Hatuwezi kutafakari mambo. Sisi ni mapunguani.
Ndugu zangu wazaramo kama sikosei, wanasema mchelea mwana kulia, mwisho Julia yeye, Sasa no sababu ya matatizo ya watanzania, tumsamehe ili tuendelee kukosea vizuri🤔.
 
Bora Samia ametoa joto lake,amehisi dharau zinazidi kila kukicha,heshima yake inavunjwa na walio karibu nae,aliowaamini ,

Hivi kama hili .Ndugai arapu kwa Magu unazani Ndugai angekuwa bado hajafika kusiko julikana kwa watu wasiojulika,yaani wangekwishampa na uraia kabisa.

samia yupo sawa ,hakuweka donge rohoni amemueleza Ndugai mchana kweupe ili kazi iendelee au mlitaka ,style za Raisi Yule.
 
Kauli za Ndugai hazivumiliki....kusema nchi itakuja kupigwa mnada hapa anamaanisha huyu anaeongoza nchi ni hovyo...

Kauli ya kusema 2025 mtachagua wenyewe kuendelea na hawa wa kukopa kopa ama la...bado ni ya Kumsimanga Rais kwamba hafai kuongoza nchi inafaa abadilishiwe..

Ndio maana jana Mama Samia kasema kuna watu walitilia shaka uwezo wake wakati anaapishwa kuongoza, Sasa wanaona aibu kwa mambo makubwa anayoyafanya...
 
Back
Top Bottom