Kwa hili la Ndugai na Rais, linaonesha watanzania ndio tuna matatizo makubwa

Kwahio mkuu tunaangalia Mvurugano au point ilipo?
 

 
Msamaha wa Ndugai si wa hiari, ni shinikizo toka CCM. Tukikubali kusikiliza maoni tofauti, hata kama yanakinzana na yetu, nchi itaneemeka.
 
Can't disagree...na nadhani maza anatakiwa kummaliza kabisa hivi kashaelekea kibla...politics is about timing as well.
 
Kila tukio lina sababu. Nchi haina mwongozo rasmi- katiba-na iliopo imekuwa ikiwekwa viraka kwa maslahi ya watawala. Leo kuna mlolongo wa wenye kinga za kutoguswa na sheria, matokeo ni mnyukano wa viongozi kwa maumivu ya wananchi.
 
Ndugai amejibu kwa maslahi yake mwenyewe na siyo ya nchi.

Kama alikuwa na huruma na nchi hii angetumia mabilioni ya fedha kwenda kwenye matibabu yake mtu mmoja wakati hospitali nyingi hapa zina upungufu wa vifaa na dawa za kutibu wagonjwa wa hali ya chini?

Na ilipowekwa kama audit query akazua ya kuzua kwa CAG mpaka akaondolewa. Leo hii ndiyo amekuwa mtetea nchi ati!
 
Mtu akisema jambo zuri kwa Taifa tuweke mapungufu yake pembeni ndio kwa Ndugai
 
Ndugai haondoki ng'o ingawa aliteleza kidogo kwenda public kusema nchi itapigwa mnada wakati yeye ana uwezo wa kumuona Mhe.Rais 24/7 tofauti na sisi wengine tunaosemea hapa.

Kumpinga Rais na kumrushia madongo ni kuyatafuta tu
Yeye awapige fimbo hao wengine hata kumpa za uso waziri ila sio Rais

Kujipima nguvu na Rais tena
Hivi angekuwa aliepita mbona walikuwa wanalazimisha kucheka ingawa hawana sura za ucheshi?
 
Siku viwanja vya ndege, bandari na Tanesco vinachukuliwa na waliotukopesha ndipo tutakumbuka maneno ya Job Ndugai, wakati huo tumeishachelewa saaaaana!
Aibu yetu watanzania.
 
Alikuwa anavunjiwa, lakini sasa naona kajivunjia
 
Kosa la Ndugai ni lipi?
 
Katiba ni muhimu isomwe na waTanzania mashuleni ili tujuwe mgawanyo wa mipaka, uhuru na mamlaka za mihilili ya urais, bunge na mahakama inaishia wapi.

Hapa wabunge nao waelimishwe kutetea maoni ya wananchi kuhusu mikopo na mwenendo wa matumizi wanasemaje. Maana urais / executive umeshasisitiza utaendelea kukopa bila kusema mikopo hiyo itajikita ktk miundombinu au madawati na vyumba vya madarasa


El poder ejecutivo está separado del legislativo y el judicial en una democracia
 
Kwa hio uchungu na maslahi ya nchi anayo awamu hii tu?
Kipindi cha mwendazake ashawahi kupanua domo lake kulalamikia mikopo ya muda mfupi tena yenye riba kubwa?
Ndani ya kijani kuna makundi mawili
-Kundi la kwanza ni wale wanaounga mkono juhudi ya mama kutuletea maendeleo
-Kundi la pili ndio hilo la kina Nduguyai na wenzake ambao wao ni against, lengo lao ni kumkwamisha mama ili 2025 wakaimu nafasi.
 
Watanzania japo Kuna kundi kubwa linaloishi kwa kuyumbayumba kwasababu ya kutumika na uelewa wao mdogo lakini bado Kuna kundi la wachache waliofunguka fahamu zao na wanaohitaji matokeo yatakayoakisi muda tuliopo na kuhitaji mambo yafanyike kwa haraka na yalingane na muda, pia lile kundi lililokwamisha mambo kwa uwazi kabisa na Sasa likija kwa njia nyingine ya kukwamisha mambo na kujiwekea unafiki mwingine Ili kuinua majina yao yawe juu hao wanaojielewa wameamua kuyapinga na kusimama na maendeleo ya wakati huu Ili aliyepewa dhamani tuje tumpime kama atatufaa tena, huko kuchamba alikochamba siyo shida kabisa maana wanawake wenye kujielewa huwa wanajua kufanya mambo mengi mazuri kwa wakati mmoja na ndo maana ukipata mke Bora unakuwa umepata mafanikio ya maisha yako, Sasa Mama Raisi ameanza kuonyesha kwa mfano kujenga madarasa kwa wakati mmoja Nchi nzima na hela ya tozo akaona haitoshi na itaendelea kutuweka nyuma akaongeza huo mkopo umalize wapi wanafunzi watasomea kitu ambacho kitafanya wasaidizi wake wajitume kwenye mambo mengine na Kila mtu au mkoa utatoa matokeo ya nini wamewaletea wanachi kuliko walivyofanya zamani kuchungulia eneo shule moja Nchi nzima na huku sehemu zingine zikiwa zimetulia tu, Sasa njia hii ya kutatua tatizo moja Nchi nzima na kila mkoa ukaleta tathimini yake ya kiwango cha pesa ilichopewa kikiwa sawa na muda ukiwa sawa utaleta matokeo mazuri mengi maana wale wavivu na wale wanaotumika kukwamisha watajulikana kwa wepesi baada ya matokeo yao kuwa mabaya Sasa basi ndo maana hiyo nguvu na Hekima aliyopata Raisi ndo imewaumiza wale waliopenda kuishi kwa unafiki na matokeo hafifu yasiyo na faida zaidi ya kudanganya toto kwa pipi huku mtoto anahitaji chakula ashibe muda huo.
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…