Kwa hoja hizi Zitto hafai kuwa kiongozi ACT.

Allen Kilewella

JF-Expert Member
Joined
Sep 30, 2011
Posts
21,470
Reaction score
40,593
Sifa mojawapo ya kuwa kiongozi wa umma ni kuwa na maadili yanayokubalika kwa wananchi. Kiongozi wa chama cha siasa ni yule mtu anayesimama mbele kwa niaba ya chama chake kwenye maslahi ya wananchi wote bila ya kujali kama ni wanachama wake ama la.

Kama kiongozi anaona kuawa kwa watu ni jambo la kawaida sana na anaona ni sawa kukaa na watu walioua wanachama wake, ni mtu wa hatari sana. Mbele ya safari Zitto anaweza kufanya au kukubali jambo lolote lile ili mradi yeye maslahi yake yalindwe.

Kauli hii imenisiktisha sana. Yaani mtu aliyemiminiwa risasi 38 kama Tundu Lissu ama aliyechapwa mijeledi kama Godbless Lema unawezaje kudhani kuondoka kwao ili kuwa ni kwa kujipendea. Yeye anayedai alibaki kupambana alipambana kivipi na kuhusu nini ambacho sisi hatukijui?

 
Hayo ndio majibu toka kwa heche na huyo masabo?!
 
Zitto kabwe aliokolewa na Mshauri wa Askofu mkuu wa Canterbury mh Ndugai pale Bungeni siku aliyojificha akiwaogopa polisi
 
Zitto ndio mnafiki namba moja kwa wanasiasa wa hicho kinachoitwa upinzani Tanzania. Hao 21 ,anaodai waliuawa ilikuwa wakati wa CUF sio ACT hivyo zitto hawezi kudai credit; afadhali hata, Lipumba ,adai credit maana, ndiye alikuwa kiongozi wa CUF. Pili wakqti wa maandamano ya mwqka 2020 Unguja anbapo wakina Jussa walipigwa hqdi kuumizwa ambapo viongozi karibia wote wa juu walishiriki na kuonja shubiri ya kukamatwa na kupigwa zitto hakushiriki hayo maandamano. ivyo pia hawezi kudai credit. Zitto hajawahi kupata msukosuko wowote mkubwa wa dola hata ndani ya chama chake .

Zitto aendelee kuwauza wenzake hafi watakapomstukia.
 
Kwani Maslahi gani tumepata kwa waliokimbia nchi mpaka sasa!
 
Zitto aendelee kuwauza wenzake hafi watakapomstukia.
Kajisahaulisha kwamba Mwaka 2001 (Enzi kabla baadhi ya viongozi wa CUF kujivika koti la ACT) mamia ya watu walikimbilia Mombasa. Kwa ivo kwa mtazamo wake watu wale walishindwa kubaki kupambana??
 
Reactions: RMC
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…