Kwa kauli hii ya Rais Samia, ni wazi kwamba watu wanamdharau (wanamchukulia poa)

Watazania bwana hamna shukrani mkipewa uhuru wa kuongea na kutoa maoni juu ya serikali mnasema Rais wanamdharau akiamua kutumia nguvu za Urais mnaaza kulialia mnaonewa ndugai anatumia haki yake kikatiba kuonge
 
Mbona unaongea vitu ambavyo sijakuuliza? Nimekwambia kasimamia mradi gani wa kimkakati ukakamilika? Maana ukiongelea hayo nitakuambia na mama nae ndani ya miezi saba kajenga vituo vya afya zaidi ya 100 , vyumba vya madarasa elfu 15 na miradi kadhaa inayoendelea kujengwa. Huyu mama msiseme kwa chuki zenu kafanya mambo makubwa kwa muda mfupi sana muweke ushabiki wa magufuli pembeni.
 
Atajijua aliwakaribisha mwenyewe alitaka aonekane mwamba kuliko Jpm ona sasa

USSR
 
Angalia hata akiwa anaongea yy ni kuomba omba tu. Haya ndiyo madhara yake.
 
Huwez kuuliza swali kama wakati Una jua haku maliza muda wake wa uongoz na mirad ya kimkakati ina chukua miaka mingi miradi ya kimkakati radhima kiongoz na akili siyo kiongoz anaye fikilia kwenda kutembeza bakuli Tu na kuja kujenga darasa na vyoo

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Mbongo bila mkwara mzito na kutumbuana kila kukicha haendi ni kama punda bila kiboko haendi sasa kila uongozi na zama zake mama hataki hayo mambo anataka watu wafanye kazi lakini anawaona live kabisa jinsi wanavyomjaribu.
 
Kikwete alisafiri na alifanya makubwa sana, ikiwemo uwekezaji na ajira nje nje, so mwacheni azurule huko nje kuliko kujifungia ndani ka kuku anayeatamia
Mama yako hana analofanya, yupo tu analalamika kama raia wake tu!
 
Kumbe mnajua miradi ya kimkakati inachukua miaka mingi sasa kinachowafanya muwashwe washwe ni nini?
 
Watanzania huwa hatueleweki tunataka nini ni ungrateful people
Hana analofanya! Analalamika tu kama mimi wa mtandaoni. Ungrateful indeed, unless afanye kama raisi anavyotakiwa kufanya.
 
Mama yeye anaota na kuweweseka mbowe tu
 
Huyu si ndiye alisema watu wamevuruga kwenye awamu iliyopita alafu jumba bovu anaangushiwa yeye???
Mm mwenywe nimemshangaa kwa kauli yake hii ina maana hana kumbukumbu kabisa kuwa alituambia awamu iliyopita watu walivuruga mno😲 leo anatuambia eti hawezi kuvumilia ubadhilifu unaoendelea Inamaana kibao kimegeuka kwake 🤔 wahuni sio watu😁
 
Kipindi kile Zackia Menghji nae alilalamika kuandamwa na watu sababu ya jinsia yake alipotunukiwa moja ya wizara nyeti za nchi hii. Leo namsikia tena Mama
Mama ndio anatetea sana jinsia yake mm naona ni kama anatafuta Huruma tuu😁 ukitaka kuongoza lazima uwe sura ya mbuzi
 
Hana analofanya! Analalamika tu kama mimi wa mtandaoni. Ungrateful indeed, unless afanye kama raisi anavyotakiwa kufanya.
Watanzania hata mkiletewa malaika hamriziki kikubwa kiongozi afanye anachojiskia bila kujali malalamiko Ili walalamike vizuri Hadi mate yawakauke
 
Mi nakumbuka mama yetu ametuzibua sana makofi, makonzi, fimbo na vile vifinyo vya ngozi kuvilia damu.
Mama alikua anatupenda sana watoto wake ila tukizingua alikua mkali kwelikweli hana simile.
Nashangaa Mama yetu wa sasa kaamua kutulea ki Junior Junior na mitoto ishaanza kua minunda na mifedhuli.
Mi namkumbusha tu mama ya kwamba kuna msemo wa wahenga usemao
"Mchelea mwana kulia, hulia yeye"
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…