Kuelewa mbongo anataka nini ni kazi kwelikweli.
Kipindi cha JK tulikua tunamponda na kumtukana kwelikweli, majina yote ya hovyohovyo tukampachika tukafikia mpaka kutamani siku moja nchi yetu itawaliwe kidikteta.
Mungu si Athumani akasikia kilio chetu akatuletea Jiwe tena Jiwe kwelikweli hacheki kabisa na kima yoyote, Wabongo tukaanza vilio na kusaga meno, tukampachika majina ya hovyohovyo lakini Mwamba alifunga macho na akaziba kabisa masikio yake.
Kelele zikaanza mpaka mjengoni za kummisi JK na kila sifa nzuri akapewa na walewale waliokua wanambeza, wanamkebehi na kumtukana.
Leo hii baada ya Mwamba kutangulia mbele za haki walewale waliokua wanambeza, wanamkebehi na kumtukana JPM ndio haohao wamekua wapiga zumari wa kumsifia na kumuona yeye ndie alikua haswa mkombozi wa hii nchi, wamegeukia upande wa pili kumtukana na kumsimanga Mama pamoja na viongozi waliopita wa awamu ya nne.
Mimi ninachosema Mama aendelee tu kuupiga mwingi asisikilize kelele za chura maana chura akiwa majini analalamika maji ni ya baridi sana halafu pia ni machafu yanamsababishia ngozi yake kushambuliwa na wadudu ndio maana mwili wake unapata mabaka mabaka,
Chura huyohuyo akiwa nchi kavu pia analalamika nchi kavu jua ni kali sana linamchoma mpaka ngozi yake inababuka na mwili wake wote unajaa mabaka mabaka.