Kwa la Bandari, Pongezi TLS. Katiba yetu imenajisiwa. Bunge limetunga Sheria batili. Haki za Watanzania zimeporwa. Kwanini TLS wamenyamaza kimya?

Kwa la Bandari, Pongezi TLS. Katiba yetu imenajisiwa. Bunge limetunga Sheria batili. Haki za Watanzania zimeporwa. Kwanini TLS wamenyamaza kimya?

DP World Dubai ni mkoloni pacha mithili ya kampuni ya VOC (Verenigde Oostindische Compagnie) ya Uholanzi.
...
DP World ya Dubai na The Dutch East India Company VOC, Verenigde Oostindische Compagnie) agenda zao ni za kikoloni na mikataba yote inayoingiwa imo kwa minajili ya kuwakilisha watawala wa nchi zao ndogo kidiplomasia, kijeshi, kutwaa ardhi nchi za mbali na kuingia mikataba kama vile wao (kampuni) ni nchi hasahasa na nchi duni za dunia hii.

Ukiusoma mkataba wa IGA, kwa umakini hata kama wewe siyo Mwanasheria, utagundua kuwa hoja yako iko sahihi.

KWAMBA:

Kwa mkataba wa IGA, ambao DPW inataka kuutumia Tanzania kuwekeza, tofauti na nchi zingine km UK wakisajiri kama DPW Southampton Gateway au DPW London Gateway, inajivika koti la Dubai, nchi yake. Na taarifa ni kwamba DPW ni mali ya Sultani wa Dubai na familia yake. Kwa msingi huo tunamkaribisha Tanzania atutawale kupitia moja ya njia kuu (Maji - bandari, Ardhi, na Anga) za kuingia nchini.

KARIBU Sultani na familia yako
 
mkuu walikaa kimya kwa sababu tayari walikuwa wamesha pewa ahadi Fulani fulani , Ila kilichowatoa shimoni hata hao TLS ni aibu . so wapichokifanya kwa Sasa ni at least kutoa aibu kiaina . Kama wametubu kwa kumaanisha pongezi kwao!!
 
wanasheria

Na wanasheria wasomi walio na uelewa mpana wa historia ya ubeberu na mikataba tata iliyowahi kufanywa baina ya mataifa beberu na nchi nyonge zisizo na uelewa wa Geopolitics na ukoloni yaliyofanya kwa njiaza hila na kilaghahi kupata makoloni kupitia vibaraka au viongozi / machifu waliodanganywa kuhusu wanachosaini ni mahusiano ya makubaliano rafiki kumbe ni kuuzwa moja kwa moja sovereignty ya nchi.
 
Hongera kwa uchambuzi mzuri mkuu, wenye madaraka wanadharau sana raia ndio maana hawaogopi kuivunja katiba.

JokaKuu Nguruvi3 zitto junior Kalamu Mag3
Huwa sisomi magazeti ya huyo mkuu, kwa hiyo huwa mara nyingi sishiriki kwenye mada zake.

Nimekwishasoma na kushiriki kwenye mjadala wa hayo yaliyojadiliwa na hao TLS.

Nimeheshimu sana mchango wao katika swala hili la Bandari.

Nashukuru kwa kunikaribisha huku.
 
Pascal tuanue kwanza mkataba wa TICTS wa Gati namba 8 Hadi 11pale bandarini Ilikuwaje
Mimi ni mtu wa maslahi ya taifa mbele
Kwenye hili la Bandari, msimamo wangu ni very open, kuna vitu sisi Watanzania hatuwezi, lazima tusaidiwe!. Watanzania tujifunze kukubali kuna vitu hatuwezi, tunaposhindwa tukubali kusaidiwa au tukomae? Baada ya Bandari ni ATCL na SGR au Tusubirie?

Ila katika kusaidiwa lazima tusaidiwe kwa haki na wote tufaidike na sio kusaidiwa kwa janja janja, hili pia nimeliweka wazi Japo Bunge Limeridhia, DPW Kuendesha Bandari Zetu, ni Makubaliano Tu, Tukithibisha Kuna Matatizo, Tunarekebisha Mkataba wa HGA, Kazi Nzuri Iendelee!

P
 
Katika sheria ambazo ni ngumu kueleweka hata kwa wanasheria wengi ni PUBLIC INTERNATIONAL LAW. Ubaya zaidi linapokuja suala zima la mikataba ya kimataifa ndiyo mambo yanazidi kuwa makubwa kwasababu kipengele ambacho kinahusika ni THE LAW OF TREATIES, kama umesoma sheria utafahamu kwamba hii ni mada ngumu na ndefu mno kama ilivyo THE LAW OF THE SEA.

Linapokuja suala zima la uwekezaji ndiyo mambo yanazidi kuwa magumu zaidi kwasababu mada ambazo zinahusika sana ni THE LAW OF TREATIES, INVESTMENT LAW, DISPUTE RESOLUTION. Unaweza kukuta mtu kasoma PhD ya sheria lakini hizi mada bado haziwezi. Ndiyo maana hata ukija hapa Tanzania wanasheria wanaofanya INTERNATIONAL COMMERCIAL ARBITRATION ni wachache mno.

Kuweza kuelewa vizuri ule mkataba inahitaji uwe zaidi ya mwanasheria. Inahitaji kwanza kabisa uifahamu vizuri PUBLIC INTERNATIONAL LAW, bila hivyo utaingia chaka. Tafasiri za vifungu vya sheria za kimataifa hasahasa mikataba (Treaties), ni tofauti kabisa na tafasiri ya kwenye mikataba ya kawaida (Contracts). Kuna mambo kadhaa wa kadhaa ambayo kifalsafa mwanasheria anahitaji kuyafahamu kabla ya kuanza kutafasiri vifungu vya mkataba kama ule wa DP World.

Sasa ndugu zetu wametafasiri wenyewe, sijui tafasiri zao wamezitoa wapi. Leo hii mambo yamelipuka vibaya mno. TLS wamekuja na tafasiri yao, AG yuko na tafasiri yake, SPEAKER yuko na tafasiri yake, BUSH-LAWYER MBARAWA naye yuko na tafasiri zake. Kiufupi ni vurugu mechi tupu. Nchi za wenzetu suala kama hili lingekuwa limefanyiwa mjadala mpana, huenda hata kupelekwa kwenye mahakama ya katiba uli kupatiwa ushauri. Huku wanazima mjadala kwa nguvu.

Binafsi waache wanasheria wajadili hoja ili tufahamu nani ameliingiza taifa chaka....
Unajaribu kufanya mambo yaonekane kuwa magumu sana kuliko yalivyo. Sielewi wewe unasimamia wapi hasa kuhusu swala hili.

Hizo sheria ngumu unazozungumzia zipo kwa manufaa ya nani kama haziwezi kueleweka na pande zinazohusika?

Sasa sijui tufanyeje, maana kama hatuna uwezo wa kuzielewa hizi sheria, tukubali tu kuingia kichizi bila ya kujua jambo tunaloliingia?

Artificial Intelligence bado ni eneo changa sana, ambalo nalo hatujawa nalo uwezo na hatuwezi kusubiri tulitegemee hilo kwenye haya mambo unayosema wewe ni magumu sana kuyaelewa.

Uhitaji wetu ni sasa, kama kuna jambo tusiloweza kulielewa kwa kukosa uwezo nalo, na wala hatuwezi hata kuajiri wenye uwezo nalo toka nje, ina haja gani ya kujihusisha kwenye jambo lenyewe?

Kifupi ni kwamba, sikubaliani na maudhui ya hoja yako.
 
Wanabodi,

Nikiwa ni mwanachama wa TLS, nimeisoma taarifa ya TLS kuhusu issue ya Bandari na DPW, kiukweli kabisa TLS inastahili pongezi za dhati!, imefunga huu mjadala, ingekuwa mimi ni Mnyamwezi, Kinyamwezi hii inaitwa "funga kalomo", yaani funga mdomo!. Taarifa hii ya TLS ni funga kazi, na huu ndio uzalendo!, hongera sana TLS kwa kutanguliza mbele maslahi ya taifa.

Kama mwanachama mwaminifu wa TLS, kwa heshima ya chama changu cha wanasheria wa Tanganyika, naomba nisikosoe jambo lolote kwenye taarifa ya TLS, ila sio vibaya kuzungumzia baadhi ya hoja ambazo TLS haikuzigusia kabisa!.

Ni baada ya kuisoma taarifa ya TLS, ndipo nikagindua mtu mwandishi wa habari kwanza, halafu ukaingia kwenye sheria, unakuwa na jicho kali zaidi kuliko jicho la mwanasheria mwanasheria tuu ambaye sio mwanahabari!.

Jicho la Mwanasheria linaangazia vifungu vya katiba, sheria, taratibu na kanuni, jicho la mwanahabari linaangalia mtazamo wa jamii, Mwananchi wa kawaida, anaona nini, anataka nini, hivyo jicho la mwanahabari linaona kuliko jicho la mwanasheria.

Baada ya Bunge letu kuridhia, niliandika makala hii, Japo Bunge Limeridhia, DPW Kuendesha Bandari Zetu, ni Makubaliano Tu, Tukithibisha Kuna Matatizo, Tunarekebisha Mkataba wa HGA, Kazi Nzuri Iendelee! humo niliainisha mapungufu ya IGA hiyo kisheria kwa jicho la kiuanahabari.

TLS katika taarifa yao, kuna maeneo mengi wamepita mule mule nilimopita mimi, ila lile kubwa kuliko, "The Capacity" to contract, TLS wamelikwepa na kuliweka kiporo kusubiria wawasiliane na Dubai.

TLS hawakuyaona yale niliyo yaona mimi!. Tanzania ni nchi, inakwenda kuingia mkataba wa kimataifa wa nchi na nchi, yaani Tanzania na UAE, lakini signatories wa Tanzania ni nchi, halali signatories wa UAE ni kampuni ya DPW!, tena imesaini bila POA yoyote toka UAE!.

Kwa maneno mengine ni kampuni ya DPW imejigeuza ni nchi ya Dubai wakati ni kampuni binafsi!, sio nchi, Dubai sio nchi, nchi ni UAE!, nchi yetu haiwezi kuingia mkataba wa kimataifa wa kuwa ratified na Bunge letu kama an international Treaty wakati signatories ni kampuni na sio nchi na hakuna POA yoyote ya UAE kuruihusu DPW to transact an international Treaty on behalf of UAE!.

Nimeipongeza TLS kwa uzalendo kwenye hili, ila nikiri kuwa nimeshangazwa na umakini huu wa TLS katika hili la Bandari.

Sheria Kuu kuliko zote nchini kwetu ni katiba, katiba ndio sheria Mama, sheria nyingine yoyote inayokwenda kinyume cha katiba ni sheria batili!. Kinachoibatilisha hiyo sheria yoyote kinyume cha katiba, ni katiba yenyewe!.

  1. Serikali yetu ime draft sheria batili, inayokwenda kinyume cha katiba, ikaipeleka Bungeni kutungwa kuwa sheria!, kwanini TLS walikaa kimya?!.
  2. Bunge letu likaitunga hiyo sheria batili inayokwenda kinyume cha katiba, kwanini TLS walikaa kimya?.
  3. Rais wa JMT akaisaini hiyo sheria batili kuwa ni sheria!, kwanini TLS walikaa kimya?!.
  4. Mahakama Kuu kupitia kesi ya Mtikila, ikatamka sheria hiyo ni batili na kuitaka serikali iifute. Kwanini TLS walikaa kimya?!.
  5. Ubatili wa sheria batili yoyote unabatilishwa na katiba, Mahakama Kuu ikiisha tamka sheria fulani ni batili kwa kwenda kinyume cha katiba, automatically sheria batili hiyo inakuwa imebatilika from there and then. Kazi ya serikali ni procedures tuu za kuifuta!. Kwanini TLS walikaa kimya na sheria batili hiyo mpaka sasa bado iko kwenye sheria zetu licha ya Mahakama Kuu kutangaza ni batili?.
  6. Serikali yetu ikakata rufaa kupinga uamuzi huo wa Mahakama Kuu, ikashidwa!, kwanini TLS walikaa kimya?!.
  7. Serikali yetu baada ya kubwebwa, ikafanya kubwa kuliko, ikapeleka Bungeni mabadiliko ya katiba kwa hati ya dharura, batili ile ikachomekewa kiubatili ndani ya katiba yetu!. Kwanini TLS walikaa kimya?!.
  8. Bunge letu likafanya mabadiliko ya katiba na kuichomeka hiyo batili ndani ya katiba yetu!. Hivyo katiba yetu imenajisiwa kwa kuchomekewa ubatili!, kwanini TLS walikaa kimya?!.
  9. Mchungaji Mtikila hakukubali katiba yetu inajisiwe, akafungua shauri kupinga mabadiliko hayo ya katiba, Mahakama Kuu ikampa ushindi na kutangaza mabadiliko hayo ni batili!, kwanini TLS walikaa kimya?!.
  10. Serikali yetu ikakata rufaa Mahakama ya Rufani kupinga uamuzi huo wa Mahakama Kuu, serikali ikashinda, kwanini TLS walikaa kimya?!.
Mpaka leo ninapoandika hapa, Katiba yetu bado inacho kifungu batili hicho!, sheria zetu bado zina ubatili huo na TLS wako kimya!.

Nimalizie kwa pongezi tena, TLS kwa hili la Bandari, ila kuna makubwa kuliko hili la Bandari, TLS bado hamjachelewa!.

Mungu ibariki TLS
Mungu Ibariki Tanzania

Paskali
Paskali wewe ni mwanachama mwaminifu wa TLS, na mimi nakuuliza "kwanini mkikaa kimya?"
 
Unajaribu kufanya mambo yaonekane kuwa magumu sana kuliko yalivyo. Sielewi wewe unasimamia wapi hasa kuhusu swala hili.

Hizo sheria ngumu unazozungumzia zipo kwa manufaa ya nani kama haziwezi kueleweka na pande zinazohusika?
Mambo ni magumu sana hata bila ya mimi kuyafanya magumu. Yangekuwa marahisi kama wewe unavyotaka kulazimisha hapa, basi huenda kila mtu ikiwemo wewe angekuwa ni mwanasheria wa sheria za mikataba na uwekezaji. YOU CAN TAKE THIS TO THE BANK!

Kifupi ni kwamba, sikubaliani na maudhui ya hoja yako.
 
Back
Top Bottom