Kwa maafa ya Hanang' serikali iwe inasikiliza wazee

Kwa maafa ya Hanang' serikali iwe inasikiliza wazee

Kazi ipo... kwa hyo unaamini wale wazee wangefanya kitu... hii haina tofauti kusikia mganga analia katepeliwa... hao wazee km kwel walikuwa na nguvu ya kuzuia wangewanyoosha hao watu wa maliasili...ili kulinda kizazi chao, cos familia za mali asili hazijaumia kulikk hao wazee...

Kk land slide inatokea sanaaa.. tuwe tunachukua tahadhali sio kuanza kufikiria mazingaombwe kuokoa maisha yako..
 
😂🙌hakika
Babu zetu na bibi zetu walizaliwa wakayakuta waliyoyakuta hapa duniani, wakaishi hivyo hivyo hadi siku zao za kuondoka zilivyofika wakaondoka na kuyaacha waliyoyakuta.

Halikadhalika wazazi wetu nao wakaja wakayakuta walioyakuta bibi na babu zetu, wakaishi nayo hivyo hivyo wakisubiri kuondoka na kuyaacha.

Sisi pia tumezaliwa na kuyakuta Nina imani pia tutaondoka na kuyaacha kama tulivyoyakuta. So ndomaana nasema Dunia ina mengi wewe ukijua hili na mungine anajua lile.

The world's very complicated 🤣🤣
 
1. Mizimu ni uongo
2. Matambiko ni uongo.
3. Wanaofanya matambiko ni wazushi na waongo.

Mtu akishakufa hajiwezi yeye mwenyewe sembuse kusaidia waliohai?

Yaani kuna Watu ni wajinga wa kiwango cha juu kabisa.
Ni Watu ambao wapo karne hii kimakosa.

Unazungumzia Majini unaita mizimu
 
Yaani hata taarifa hukuskia kwenye vyombo vya habari waathirika walivyohojiwa asubui waliskia sauti ya muungurumo kama volcano,nyinyi mnoishi kwa niaba ya hisani ya Facebook,Instagram, TikTok mnashida
Mihemko.
 
Kazi ipo... kwa hyo unaamini wale wazee wangefanya kitu... hii haina tofauti kusikia mganga analia katepeliwa... hao wazee km kwel walikuwa na nguvu ya kuzuia wangewanyoosha hao watu wa maliasili...ili kulinda kizazi chao, cos familia za mali asili hazijaumia kulikk hao wazee...

Kk land slide inatokea sanaaa.. tuwe tunachukua tahadhali sio kuanza kufikiria mazingaombwe kuokoa maisha yako..
Ndo mana nimekujibu,nyinyi mliokulia mnapanda daladala mwendo wa mita 300 mnashida sana,iyo ni azabu ya mizimu sio hao wazee,wazee kazi Yao ni kuongea na mizimu kwa luga Yao wanaambiwa mizimu inataka Nini wanaitambikia ili kuweka mambo sawa,wazee hawahusiki na kutoa adhabu kwa wananchi wa Hanang' ,iyo azabu imetolewa na asili ya mlima baada ya wanadamu kushindwa kutimiziwa haja zao

Kama mungu aliua watu wake kipindi Cha nuhu mizimu ni nani asimalize kwa kushindwa kutimiziwa haja zao

Wewe uliekulia kwenye dunia ya Facebook na kutype kwa simu utashangaa na kudhihaki sana,amini nakwambia ulimwengu wa nguvu za asili upo na unafanya kazi mda wote,

Usione vyaelewa jua viliundwa,
 
Shida nyinyi mkikaaga mitandaoni mnajikuta ujuaji mwingi,nimekwambia mtafte mtu wa Hanang' mndani akupe abc za mlima Hanang' ,sio Kila kitu ni kuleta ujuaji
Hao watu wa misitu wapo masaa 24 huko mlimani kusubiri kufukuza wazee wa kimila, acha fix mzee....
 
Acheni kupingana na nature Ata kama wangechinja ng'ombe ishirini Bado isingesaidia
 
VOLCANIC ERUPTION.

BAHATI MVUA ILINYESHA LAVA ONHEKUWA YA MOTO WATU WANHEYEYUKA.
Volcanic eruption haiwezi zuiliwa na kitu dhaifu cha kijinga kama mvua. Ile lava ikitoka kwa mlipuko, moshi wake unatanda kuzidi usawa wa mawingu ya mvua. Lava inayeyusha mawe, inayeyusha nyumba ukirudi unakuta tope jekundu ije ishindwe na muunganiko wa manyunyu unaoitwa mvua?

Lava inakaa siku nne haijakauka, ukirudi baada ya wiki ukakanyaga kiholela unaungua unakatwa mguu hiyo ndio izuiliwe na mvua. Volcanic eruption inazuiwa na mvua hadi haitoi moshi?
Ungekuwa unaujua moto wa volcano usingewaza hata. Yeyote anayeitaja volcano kwenye suala la Hanang ajipe muda aisome inavyokuwa.
 
Kilichotokea Hanang' mlima ulianza kuunguruma Toka mwez wa 9 na kutikisika kidogo,kama kawaida ya Mila na desturi lazima tambiko lifanyike

Wazee wakajipanga wakati wanaenda mlimani wakakutana na watu wa misitu(maliasili) wakafukuzwa milimani

Wazee waliapa kitachotokea mwaka huu lazima nchi itikisike ,baada ya siku 3 likatokea la kutokea watu zaidi ya 80 wamekufa

Hakuna Cha mudflow,land slide,debris flow ,ni kukaidi Mila na desturi za eneo husika zisifanyike ,
Hao maafisa wa misitu wamesalimika?
 
Shida nyinyi mkikaaga mitandaoni mnajikuta ujuaji mwingi,nimekwambia mtafte mtu wa Hanang' mndani akupe abc za mlima Hanang' ,sio Kila kitu ni kuleta ujuaji
Kama walijua umuhimu wa hilo tambiko lao, walishindwa njia nyingine ya kufika huko mlimani au hao maafisa misitu walitanda mlima mzima na wakakaa masaa 24 kuzuia wazee wa kimila.......punguza fix.
 
Mzee mmoja yule anasema,wale wazee wa matambiko walopofukuzwa na TANAPA,usiku huo huo au kesho yake,hii varangati ikatokea. Mwingine anasema walifukuzwa na kuchapwa viboko. TANAPA wanakanusha kumchupa mtu yeyote.
Mwingine anasema mwaka 1954,Dec 3.,volcano ilitokea. Hii ni well- nigh impossible kuthibitisha.
The last volcano there took place in the pleistocene age(250,000,000 years to 11,700 years ago).
It is not important. Lakini wapo waandishi wa habari kule. Kwa nini wasiwatafute wale watu ambao inadaiwa walifukuzwa. Kwa sababu hawa watu wamekuwa gumzo sasa.
Kwa sababu,remember mtu akiweka sattellite juu anaweza kuona watu wanatimuliwa na TANAPA. Ataona quite clearly kama unavyotazama television pictures.
 
1. Mizimu ni uongo
2. Matambiko ni uongo.
3. Wanaofanya matambiko ni wazushi na waongo.

Mtu akishakufa hajiwezi yeye mwenyewe sembuse kusaidia waliohai?

Yaani kuna Watu ni wajinga wa kiwango cha juu kabisa.
Ni Watu ambao wapo karne hii kimakosa.

Unazungumzia Majini unaita mizimu
Mkuu unasema hivyo wakati unatumia ubin wa babu yako hujistukii
 
Kama walijua umuhimu wa hilo tambiko lao, walishindwa njia nyingine ya kufika huko mlimani au hao maafisa misitu walitanda mlima mzima na wakakaa masaa 24 kuzuia wazee wa kimila.......punguza fix.
We ni boya kweli,ao maafisa misitu unawajua vizuri,taarifa za misituni za watu kuuwawa na hao jamaa unazijua vizuri,

Wazee walitaka wakafanye Yao kulituliza jambo lijalo kwa Mila na desturi

Sasa kama wametimuliwa yanini waendelee kulazimisha ACHA NCHI ITIKISIKE NA IWE FUNZO KWA VIZAZI VIJAVYO,

Na ndio maana mnaletewa mtaala mpya mjifunze historian ya Tanzania,Africa huenda hata kazi ya machifu huijui umekalili Berlin conference
 
Back
Top Bottom