Kwa machungu nasema 'Kwaheri mji wangu Dar es Salaam'

Kwa machungu nasema 'Kwaheri mji wangu Dar es Salaam'

Teknocrat

JF-Expert Member
Joined
Oct 20, 2018
Posts
4,967
Reaction score
11,056
Kama maudhui ya mada yangu inavyosema, nimeona nikubali hali ya sasa ya maisha yangu na jiji la Dar es salaam.

Kwa kukubali Dar es salaam sio tena ule mji au jiji niliwahi kuishi na kuwa na marafiki na ndugu. Baada ya kukulia, kusoma na kufanya kazi jijini Dar es salaam tangu nilivyozaliwa.

Niliweza kuishi na kusoma maeneo tofauti ya jiji, kuanzia Kurasini wilaya ya Temeke, Upanga wilaya ya Ilala, na Msasani, Oysterbay na Masaki wilaya ya Kinondoni.

Katika maisha yangu niliweza kuwa na marafiki kutoka mashuleni na wengine tuliojuana kutokana na maeneo niliyoshi.

Kwa sasa baada ya kuwa nje ya nchi kwa zaidi ya miaka 25, ilikuwa nikipata fursa ya kurudi na kutembea ilikuwa ikiwa ni furaha iliyoje kila nikirudi kutembea Dar es salaam nakukutana na ndugu na marafiki tuliosoma nao na kukua nao maeneo niliyowahi kuishi, na hali ilikuwa ikibadilika kwa kadri muda unavyoenda kila napo pata fursa kuja kutembelea nyumbani jijini Dare es salaam.

Kwa sasa hii hali ya mabadiliko ninayokutana nayo ni kutoweza kukutana na marafiki na ndugu kutokana aidha nao wao pia wahama jijini, au wameenda kutafuta maisha nje ya nchi na wengine wametangulia mbele yetu.

Hii imefikia mpaka sasa nikirudi, nakuwa sina sehemu ya kwenda kutembelea marafiki wala ndugu na kujikuta muda wote niko peke yangu au niko na familia yangu binafsi, na imekuwa mpaka watoto wangu wananiuliza kuwa baba uliiishi na kusoma huu mji, wako wapi marafiki zako uliosoma nao au uliocheza nao utotoni, kwa kweli nimekuwa sina jibu zaidi ya wote wamehamia nchi zingine au miji mingine ya mbali.

Kwa kweli na jiji limebadilika, kuna maeneo mabadiliko ni chanya yaliyoleta maendeleo kama Kigamboni na Mbweni ndio maeneo ya makazi mapya ya kisasa, na kuna maeneo yamebadilika kwa kuvurugika kama Upanga, Oysterbay na Masaki kwa kuharibika na kuanza kufanana na uswahili baadhi ya maeneo.

Kwa sasa nahitimisha jiji la Dar es Salaam sio tena lile jiji langu nililokulia, nililokuwa na marafiki kutoka kila tabaka la kimaisha kuanzia kuwa na marafiki kutoka familia zakishua niliokuwa nao maeneo ya Upanga, Oysterbay na Masaki ambao wote aidha wanaishi nje ya nchi au wametangulia mbele yetu na pia watoto wa familia za kimasikini niliosoma nao na kuwa marafiki wa kutembeleana na walikuwa wananishangaa badala ya kujichanganya na mabrazameni wa Oysterbay, mimi nilikuwa nakwenda kukaa nao maskani maeneo ya Temeke, Mtoni kwa Aziz Ali, Manzese Magomeni na Mwananyamala, leo hii hawa wote hawapo tena, wengi walieenda South Africa na wengine walifanikiwa mpaka kufika US na Italy, na wengine wametangulia mbele yetu, kwa hiyo hata haya maeneo yamekuwa mageni kwangu kwa sasa.

Natumai nikizeeka, nitarudi nyumbani kwenye kibanda changu nilichojitahidi kujenga huko Kigamboni na kuyaanza maisha ya upweke bila rafiki

Kwaheri Dar es Salaam,
 
Upweke ni ugonjwa mbaya ukikosa umakini unaweza kubaki na rafiki mmoja tu ambaye ni mkeo tena uombe Mungu asiwe kisilani.

Ukiwa mtu wa ibada hasa muislamu, basi marafiki zako watakuwa unaofanya nao ibada msikitini na baada ya swala hasa muda wa jioni mnapata kahawa na kubadilishana mawazo.

Ukiwa mlevi jioni unafika bar unapata moja mbili mnabadilishana mawazo na wenzio.
 
Kwakweli mm kila baada ya miezi mitatu lazima nilidi kijijini kwa wazazi wangu nilipo mzika mzee na babu zangu.Nayaandaa maisha ya kijijini kwakuwa karibu na wanakijiji nafahamu kama mungu ata niweka hai nikifikisha miaka 55 naamia kabisa kijijini vulugu za mjini nawaachia vijana. N.B akikisha unawekeza kwenu maisha ya mjini yanaitaji akili nyingi ukizeeka.
 
P
Kama maudhui ya mada yangu inavyosema, nimeona nikubali hali ya sasa ya maisha yangu na jiji la Dar es salaam.

Kwa kukubali Dar es salaam sio tena ule mji au jiji niliwahi kuishi na kuwa na marafiki na ndugu. Baada ya kukulia, kusoma na kufanya kazi jijini Dar es salaam tangu nilivyozaliwa.

Niliweza kuishi na kusoma maeneo tofauti ya jiji, kuanzia Kurasini wilaya ya Temeke, Upanga wilaya ya Ilala, na Msasani, Oysterbay na Masaki wilaya ya Kinondoni.

Katika maisha yangu niliweza kuwa na marafiki kutoka mashuleni na wengine tuliojuana kutokana na maeneo niliyoshi.

Kwa sasa baada ya kuwa nje ya nchi kwa zaidi ya miaka 25, ilikuwa nikipata fursa ya kurudi na kutembea ilikuwa ikiwa ni furaha iliyoje kila nikirudi kutembea Dar es salaam nakukutana na ndugu na marafiki tuliosoma nao na kukua nao maeneo niliyowahi kuishi, na hali ilikuwa ikibadilika kwa kadri muda unavyoenda kila napo pata fursa kuja kutembelea nyumbani jijini Dare es salaam.

Kwa sasa hii hali ya mabadiliko ninayokutana nayo ni kutoweza kukutana na marafiki na ndugu kutokana aidha nao wao pia wahama jijini, au wameenda kutafuta maisha nje ya nchi na wengine wametangulia mbele yetu.

Hii imefikia mpaka sasa nikirudi, nakuwa sina sehemu ya kwenda kutembelea marafiki wala ndugu na kujikuta muda wote niko peke yangu au niko na familia yangu binafsi, na imekuwa mpaka watoto wangu wananiuliza kuwa baba uliiishi na kusoma huu mji, wako wapi marafiki zako uliosoma nao au uliocheza nao utotoni, kwa kweli nimekuwa sina jibu zaidi ya wote wamehamia nchi zingine au miji mingine ya mbali.

Kwa kweli na jiji limebadilika, kuna maeneo mabadiliko ni chanya yaliyoleta maendeleo kama Kigamboni na Mbweni ndio maeneo ya makazi mapya ya kisasa, na kuna maeneo yamebadilika kwa kuvurugika kama Upanga, Oysterbay na Masaki kwa kuharibika na kuanza kufanana na uswahili baadhi ya maeneo.

Kwa sasa nahitimisha jiji la Dar es Salaam sio tena lile jiji langu nililokulia, nililokuwa na marafiki kutoka kila tabaka la kimaisha kuanzia kuwa na marafiki kutoka familia zakishua niliokuwa nao maeneo ya Upanga, Oysterbay na Masaki ambao wote aidha wanaishi nje ya nchi au wametangulia mbele yetu na pia watoto wa familia za kimasikini niliosoma nao na kuwa marafiki wa kutembeleana na walikuwa wananishangaa badala ya kujichanganya na mabrazameni wa Oysterbay, mimi nilikuwa nakwenda kukaa nao maskani maeneo ya Temeke, Mtoni kwa Aziz Ali, Manzese Magomeni na Mwananyamala, leo hii hawa wote hawapo tena, wengi walieenda South Africa na wengine walifanikiwa mpaka kufika US na Italy, na wengine wametangulia mbele yetu, kwa hiyo hata haya maeneo yamekuwa mageni kwangu kwa sasa.

Natumai nikizeeka, nitarudi nyumbani kwenye kibanda changu nilichojitahidi kujenga huko Kigamboni na kuyaanza maisha ya upweke bila rafiki

Kwaheri Dar es Salaam,
Pole mkuu,ndio maisha yetu.
 
Kama maudhui ya mada yangu inavyosema, nimeona nikubali hali ya sasa ya maisha yangu na jiji la Dar es salaam.

Kwa kukubali Dar es salaam sio tena ule mji au jiji niliwahi kuishi na kuwa na marafiki na ndugu. Baada ya kukulia, kusoma na kufanya kazi jijini Dar es salaam tangu nilivyozaliwa.

Niliweza kuishi na kusoma maeneo tofauti ya jiji, kuanzia Kurasini wilaya ya Temeke, Upanga wilaya ya Ilala, na Msasani, Oysterbay na Masaki wilaya ya Kinondoni.

Katika maisha yangu niliweza kuwa na marafiki kutoka mashuleni na wengine tuliojuana kutokana na maeneo niliyoshi.

Kwa sasa baada ya kuwa nje ya nchi kwa zaidi ya miaka 25, ilikuwa nikipata fursa ya kurudi na kutembea ilikuwa ikiwa ni furaha iliyoje kila nikirudi kutembea Dar es salaam nakukutana na ndugu na marafiki tuliosoma nao na kukua nao maeneo niliyowahi kuishi, na hali ilikuwa ikibadilika kwa kadri muda unavyoenda kila napo pata fursa kuja kutembelea nyumbani jijini Dare es salaam.

Kwa sasa hii hali ya mabadiliko ninayokutana nayo ni kutoweza kukutana na marafiki na ndugu kutokana aidha nao wao pia wahama jijini, au wameenda kutafuta maisha nje ya nchi na wengine wametangulia mbele yetu.

Hii imefikia mpaka sasa nikirudi, nakuwa sina sehemu ya kwenda kutembelea marafiki wala ndugu na kujikuta muda wote niko peke yangu au niko na familia yangu binafsi, na imekuwa mpaka watoto wangu wananiuliza kuwa baba uliiishi na kusoma huu mji, wako wapi marafiki zako uliosoma nao au uliocheza nao utotoni, kwa kweli nimekuwa sina jibu zaidi ya wote wamehamia nchi zingine au miji mingine ya mbali.

Kwa kweli na jiji limebadilika, kuna maeneo mabadiliko ni chanya yaliyoleta maendeleo kama Kigamboni na Mbweni ndio maeneo ya makazi mapya ya kisasa, na kuna maeneo yamebadilika kwa kuvurugika kama Upanga, Oysterbay na Masaki kwa kuharibika na kuanza kufanana na uswahili baadhi ya maeneo.

Kwa sasa nahitimisha jiji la Dar es Salaam sio tena lile jiji langu nililokulia, nililokuwa na marafiki kutoka kila tabaka la kimaisha kuanzia kuwa na marafiki kutoka familia zakishua niliokuwa nao maeneo ya Upanga, Oysterbay na Masaki ambao wote aidha wanaishi nje ya nchi au wametangulia mbele yetu na pia watoto wa familia za kimasikini niliosoma nao na kuwa marafiki wa kutembeleana na walikuwa wananishangaa badala ya kujichanganya na mabrazameni wa Oysterbay, mimi nilikuwa nakwenda kukaa nao maskani maeneo ya Temeke, Mtoni kwa Aziz Ali, Manzese Magomeni na Mwananyamala, leo hii hawa wote hawapo tena, wengi walieenda South Africa na wengine walifanikiwa mpaka kufika US na Italy, na wengine wametangulia mbele yetu, kwa hiyo hata haya maeneo yamekuwa mageni kwangu kwa sasa.

Natumai nikizeeka, nitarudi nyumbani kwenye kibanda changu nilichojitahidi kujenga huko Kigamboni na kuyaanza maisha ya upweke bila rafiki

Kwaheri Dar es Salaam,
They say you never cross the same river twice.

Marafiki wenyewe ndio sisi tuko London, New York etc.

Kuna siku nilirudi Dar likizo nikawa nawatafuta marafiki. Nikapata experience kama yako. Vijiwe vimekufa. Watu wametapakaa dunia nzima. Vichochoro vyote tulivyokuwa tunakatiza vimejengewa kuta.

Abby Spartan hayupo, chimbo long time. Mani yuko South Carolina. Ngoto Spy hayupo, kazamia Vietnam. Baba Kiaro hayupo kashavuna maokoto ya Baba Ben na kukimbilia Nairo. Emma Jo hayupo yupo Chuga. Papii katembea mbele South. Mpaka Buddha Monk karuka Joburg. King Louis XIV katambaa . Tesha hayupo kajimix Mwanza. Pisholi yupo Dar lakini kapotea tu anasukuma mzigo.

Mzee wa Gala (RIP) kajenga tuta baada ya kupiga ukuta maskani kulinda Mercedes Benz yake. Ngati boy kajimix UK long time.

Nikamkuta Zico tu kabaki katikati ya wadosi anapepea flag bado.

Nimerudi kiwanja changu watoto wananishangaa wananiona mimi mgeni. Wakati nimetimba magulu hapo tangu Yoweri Museveni na Tito Okello (the real Museveni and Okello, sio majina ya maskani tu) wanagongea fegi maskani na kukimbia bill za madereva teksi wa Muhimbili.

Kwa sasa naona kama Dar imekuwa overpopulated.

Nimefikiria sana nikija naweza kukaa nje kabisa ya mji, Bagamoyo au Tanga.
 
They say you never cross the same river twice.

Marafiki wenyewe ndio sisi tuko London, New York etc.

Kuna siku nilirudi Dar likizo nikawa nawatafuta marafiki. Nikapata experience kama yako. Vijiwe vimekufa. Watu wametapakaa dunia nzima. Vichochoro vyote tulivyokuwa tunakatiza vimejengewa kuta.

Abby Spartan hayupo, chimbo long time. Mani yuko South Carolina. Ngoto Spy hayupo, kazamia Vietnam. Baba Kiaro hayupo kashavuna maokoto ya Baba Ben na kukimbilia Nairo. Emma Jo hayupo yupo Chuga. Papii katembea mbele South. Mpaka Buddha Monk karuka Joburg. King Louis XIV katambaa . Tesha hayupo kajimix Mwanza. Pisholi yupo Dar lakini kapotea tu anasukuma mzigo.

Mzee wa Gala (RIP) kajenga tuta baada ya kupiga ukuta maskani kulinda Mercedes Benz yake. Ngati boy kajimix UK long time.

Nikamkuta Zico tu kabaki katikati ya wadosi anapepea flag bado.

Nimerudi kiwanja changu watoto wananishangaa wananiona mimi mgeni. Wakati nimetimba magulu hapo tangu Yoweri Museveni na Tito Okello (the real Museveni and Okello, sio majina ya maskani tu) wanagongea fegi maskani na kukimbia bill za madereva teksi wa Muhimbili.

Kwa sasa naona kama Dar imekuwa overpopulated.

Nimefikiria sana nikija naweza kukaa nje kabisa ya mji, Bagamoyo au Tanga.
Mkuu, kwa kweli ndio uhalisia wenyewe huu

Huu mji sio tena ule tuliokuwa tunaoujua, na sasa hata wale watu waliokuwa karibu yetu kama marafiki na ndugu pia wameshapotea na kupotea.
Nakumbua Oysterbay tulikuwa na Joseph Kabila(mwenyewe) kabisa mitaani alikuwa kijana mpole.
Nilienda mpaka Don Bosco, Vijana, kushangaa tu kujikumbusha.
Nilibahatika kukutana na Coach Evarist Mapunda mitaa, anafundisha new generation.
Mtaa wa Mindu umejaa maghorofa tupu, zile msajili almost zote walinunua na kuvunja.
Pale mbele ya Diamond Jubilee kile kiwanja walikokuwa wazungusha gari wadosi wa upanga, naona jeshi wamefungia uzio.
Halafu kutokana na mji kuwa overpopulated, maeneo mengi yaliyokuwa na public access wameyafunga.

Ndio hivyo, nimekubali nikirudi , ni kukaa huko mbali na mji na kuwa hobbyist wa kilimo binafsi kwa matumizi yangu.
na project ndogo ndogo za kuniweka busy.
 
Nimekuonea huruma..huna hata magroup ya watsup ya mliosoma nao? At least kidogo inasaidia kutokupotezana sana...au nyie ni wale wa kizazi za analojia...mpk chuo unafika hamjaianza digitali..
Nilitokaga mkuku kwenye haya magurupu ya wasap ya wale niliosoma nao
Huko ni michango kila siku, nikaona isiwe tabu , nikasepa kimyakimya kwa kubadilisha namba
 
Back
Top Bottom