Kwa madereva: Tuliowahi kutokewa na mauzauza barabarani tupeane uzoefu

Hapo Kwedikwazu ni noma kwa hayo mambo,Handeni hiyo Mzee.

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Hivi vitu vipo, ilikuwa mwaka 1998 nikitokea South Africa kupitia njia ya Zimbabwe - Msumbiji, tukiwa katikati ya mapori ya Msumbiji mchana wa saa 7 tulimkuta mzee katikati ya barabara amevaa kanzu nyeupee akiwa anatusumamisha, tukaambiana na mwenzangu hakuna kupunguza mwendo, kule kitendo cha kutaka kumgonga alifanya kama watoto wanavyocheza mchezo wao wa rede, akakwepa gari, basi hatukufika hata mita 100 gari ikazima, kusimama hayupo na gari ikawa imenoki engine palepale.

Sent using Jamii Forums mobile app
 

[emoji3][emoji3][emoji3][emoji3][emoji3][emoji3]mabusu mara tatu bora lingekua busu moja aiseeee[emoji3][emoji3][emoji3][emoji3]
 
Hapa jukwaani nani anavifahamu vyombo vya kioo? Ni Vitombe na Sahani za kioo! Basi siku moja natoka SHY kwenda Mhunze, kabla ya daraja nikakuta katikati ya barabara hivyo vyombo vimewekwa ugali ndani yake na kufunikiwa kama mtu ametengewa chakula, kikombe kimejaa maziwa! Cha ajabu kabla ya eneo hilo nilipishana na lori lakini halikuvigonga vile vyombo, sasa Mimi nikapunguza mwendo nikapita pembeni. Kama hatua ishirini hivi nikasimama nikarudi kucheki tukio, hamaaadi.sijakuta kitu chochote!!
 
Duuh!
 
Mkafanyaje baada ya hapo

Sent using Jamii Forums mobile app
 
MKUU KUNA siku nilikuwa nakwenda TANGA,,,nipo na jamaa kama 4 kwenye GARI ndogo nikiwa naendesha ,, nakumbuka tulitoka hapa DAR ,mapema kama SAA 12 jioni,,tukaenda mdogo mdogo kufika CHALINZE tukatulia SEHEM vurugu za MABASI NA MAFUSO ZIPUNGUWE,,,kufika kama SAA 4 USIKU tukaanza safari ya kwenda NGAMIANI TANGA,,,TUKIWA kwenye gari story ziliendelea kama kawaida ili DEREVA NISILALE.,,tukaipita MSATA,,salama,,WAMI,,, MKATA,,SEGERA hyo,,,,Salama salmini, HALE ,, tukatoboa MUHEZA SAA nane USIKU,muda huo wenzangu wote nilihisi wamelala,maana ilikuwa kmya,,nlikuwa nasikiliza MVUMO WA INJINI YA GARI NA UPEPO TU,,, sasa balaa likaanza TUMEFIKA kuna SEHEM inaitwa MKANYAGENI,,nikaona mbele kama mita 50 kuna MWANAMKE katikati ya Barabara,,kakaa chini tena yupo UCHI WA MNYAMA,,,amekaa mkao wa kunyoosha miguu kuangalia tulipokuwa tunakuja,,Nikasikia KELELE MMOJA,,,wa JAMAA yangu aliyokuwa mbele ananambiya KANYAGA MAFUTA,,USIFUNGE brake TUTAKUFA,,MCHAWI YULE,,,,,jamaa wote waliamka,,,wakati huo nilikuwa nipo SPEED KAMA 120 HIVI...basi nikakanyaga mafuta nikampitia yule MAMA katikati ,,,means NIMEMGONGA,,,lakini sikusikia DALILI YEYOTE YA KUGONGA,,,,muda huo watu wote walikuwa macho,,,,huku tukiwa na Taharuki ya kugonga MTU,,,nilizidisha speeds ya gari hadi NGAMIANI MJINI,kwa kuwa ilikuwa ni USIKU ilibidi kusubiri kukuche, ,ilipofika ASUBUHI nikaanza kuikaguwa GARI,,AJABU haikuonyesha DALILI YEYOTE YA KUGONGA MTU,,aisee tulishangaa sana,,wala hakuna DALILI KWAMBA TULIGONGA MTU PALE,,PIA,,TULISHANGAA SANA,,, KUNA SIKU ingine nipo PEKE YNGU kwenye GARI,,,ilikuwa kama SAA NANE za USIKU ,, Barabara ya MOROGORO maeneo ya MAGARI SABA DARESALAM , ,,njia ilikuwa imetulia sana muda huo,,,NIKIWA SPEEDS PEKE YNGU BARABARANI,,,,,,mbele kidogo nikaona LORI LINAKUJA KWA KASI WRONG SITE,,means limehama UPANDE wake linakuja kwngu,,ikabidi NIHAME UPANDE wa pili KULIPISHA,,,kuangalia kulia naona kuna LORI LINGINE limewasha taa nalo linakuja kwa speed,,Duu,yaani nipo katikati UPANDE wa kushoto kuna LORI LINAKUJA UPANDE WNGU,,na kulia pia KUNA Lori kwa kifupi niliwekwa katikati ya magari mawili yanayokuja mbele yngu kwa KASI KUBWA,,nilihisi mikono imekufa GANZI,,,pale pale nikapata UJASIRI NIKASEMA MIMI hapa SIENDI PEMBENI,,maana huko pembeni kuna MAKORONGO ,, wakati natafakari ZILE LORI hizi hapa karibu yngu,,yaani zinakuja kwa pamoja mbele yangu,,,,zikiwa zimewasha taa fully..basi na Mimi sijuwi nilipata ujasiri GANI,, nikajikuta nimeng'ang'ania steering huku nakanyaga mafuta,,,kufumba na kufumbuwa nikajiona nimepita katikati ya yale malori lakini sijasikia kishindo,,au DALILI ya KUGONGA,,, na sehemu niliyopita katikati YAKE hata BODABODA HAIPITI..NIKAGEUKA NYUMA SIKUONA HATA DALILI YA GARI KUPISHANA NALO,,..HAPO nilikuwa natetemeka na gari ilizima kwa woga,,,,KESHO,,, nilipo muhadithia jamaa yng mmoja akaniuliza HIVI UNAJUWA YALE MARINGI YA SHABA,, WANAYOVAA MADEREVA WA MASAFA MAREFU MKONONI NI YA KAZI GNI? MFANO MADEREVA WA MALORI AU MABASI MAKUBWA YA MIKOANI,,,,WENGI WAO WANA MARINGI YA SHABA MKONONI,, nikamwambiya sijuwi,,akasema WAULIZE,,vinginevyo usipende kutembea usiku wa manane,,especially peke YAKO,, nikakumbuka kuna kitu natakiwa nikifanye kama DEREVA WA USIKU....

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Mpenyo wa kwenda kwa mgangaa huo

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Kuna ndugu yangu mmoja anaendesha magari makubwa, ilikua trip ya kutoka wilayani kuelekea mwanza (approx 200Km)
alianza safari saa 12 jioni mpaka kunakucha hajafika alikua anakutana na barabara nyingi ambazo akizifuata zinaishia mitoni
wachawi pumbavu zao
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…