Kwa madereva: Tuliowahi kutokewa na mauzauza barabarani tupeane uzoefu

Kwa madereva: Tuliowahi kutokewa na mauzauza barabarani tupeane uzoefu

Hahahahahhahahaaaa Huu uzi umenikumbusha kitu. Siko upande wa mauza uza ila nilifahamiana na dereva mmoja wa malori wa kukatiza nchi kama 4 hivi barani Africa. Siku moja tukiwa Bukoba akawa ananisimulia vitu anavyokutana navyo barabaeani kama dereva mchana na usiku.

Kikubwa wizi, majambazi na majangiri kuna eneo ukiacha kioo wazi wanakutupia kopo la nyuki au nyoka. Ndani ya Salina kadhaa lazima usimamishe gari kama so kulidondosha. Kifuatacho ni kupakua mizigo kisha wanakuacha uwe mzima ah umeumia hawana habari na wewe kisha wanapotelea maporini.

Kuna moja hiyo nilicheka nusura nijikojolee, naomba nisimulie kisa chenyewe kama alivonisimulia.

Jamaa yangu miaka hiyo aliajiriwa kwenye kampuni ya usafirishaji mizigo ya mwarabu mmoja wa mwanza japo alikuwa dereva tayari na alijua kuendesha. Wakiondoka na mzigo tajiri aliwaasa njiani kuna majambazi na majangiri na hawaishii kuiba tuu wanabaka pia aka kuwasodomise. Kweli wakaondoka na dreva wake kufika katikati ya pori wakawekewa kizuizi na majangiri dereva akashuka kujaribu kuwasihi wawaachie wapite na Yule utingo alibaki kwenye gari. Wakaja wakamshusha utingo wakawaambia mkitaka muende na mzigo tunachukua roba moja na tunambaka mmoja wenu. Daah wakiwa na hamaki wakasema tumshughulikie dereva utingo Rudi kwenye hadi fastaa. Kweli dereva akashughulikiwamaana aliendesha kwa tabu sana mzigo ukafika salama lakini hawakupata mzigo wa kurudi nao hivi hawakuwa na hela Yaani lori lilirudi tupu.

Siku wanarudi na mwanza yule dereva alimwambia utingo, endesha wewe mimi nipumzike kufika pori lilelile wakasimamishwa na majangiri walewale wakasema, mnarudi haya leo tumshughulikie utingo dereva pumzika, bila kusubiri wakaenda upande wa abiria wakamshusha yule jamaa na kumsodomise tena......(wakati ananisimulia nilicheka hatariii)

Yule dereva kufika kwa mwarabu akarudisha funguo kazi imemshinda.

Kisa kingine alichokutana nacho huyo jamaa yangu safari za mwanza bukoba hadi mpakani Uganda akiwa bado utingo alipata dereva ambae mkewe alikuwa na wivu balaa halafu mzigo na mtata. Maana siku majangiri wanaobaka wakiwepo kwenye pori mojawapo huwa malori wanaambiana na kukaa vituo eneo kabla ya pori na wakiondoka basi safari huendelea. Ilimpa wakati mgumu maana alimuaga mkewe naondoka jumatatu tunarudi alhamis Ila wakikutana na changamoto kama hizo za kuwakwepa majangiri wabakaji anakaa muda mrefu zaidi matokeo yake mkewe anahisi amepita nyumba ndogo. Akirudi hata na zawadi bado anakuwa na kibarua cha kumuelewesha mkewe kuwa kazi yao ni ngumu na mambo wanayokutana nayo barabarani hawezi kuelezea yote.

Siku ya siku mkewe akamwambia leo tutasafiri wote nione hizi changamoto mnazokutana nazo. Akamsihi sana mkewe bakii mkewe kagoma basi kishingo upande jamaa akakubali mkewe wasafiri wote. Hamad kati ya pori majangiri wabakaji hasa hapa, wakawashusha wote, wakasema leo mna mwanamke.... Basi nyie rudini kwenye gari leo acha tufaidi mbele na nyuma. Dereva machozi yalimtoka akiahidi day la hela kubwa Hata akope waapi sanasana aliambulia kupigwa na ubapa wa mapanga mgongoni. Mkewe kuona mmewe anataka kuuwawa, analogs kelele, basi muacheni navua nchi zote, walipomaliza mke karudi kwenye gari hoiii. Walipofika walikokuwa wanapeleka mzigo, mke akamwambia dereva, mume wangu nisamehe kweli kazi yenu in a changamoto, pole sana. Naomba nirudi na basi nyie hata mkikaa wiki mbili sina wivu tena. Alikuwa mpole maana alihisi jamaa atamuacha. Dereva akamwambia tulia tunarudi wote uzuri saa ya kurudi pori lilikuwa shwari.

Safari moja kwenye vilima vya iringa kuna maiti ya mwizi mmoja wa mizigo ya malori walimkamata wamapiga hadi akafa halafu wakamuweka kwenye kilima chenye kina kali yaani ukija na gari unastukia huyu hapa alikanywagwa na magari hadi akapotelea kwenye lami. Hilo eneo pakajaa mafuta meusiii.....

Kasinde.
Kwahiyo dereva aliendelea na uyo mke au alimwacha!?
 
Mauza uza yapo kuna mwaka nilitoka South Africa na fortuner old model ndio zinatoka nikapita Mozambique kuna sehemu kuna pori kubwa nikawaona watu wawili wamevaa mashuka hawajavaa viatu usiku kama saa sita hivi ukiwapita unakuja kuwaona mbele tena wako upande ule ule nilipokaribia tete nikasimama mara akaja jamaa na D4D akasimama akaniuliza kuna vitu umeviona bara barani maana mimi nilidhani nina usingizi naota nikamwambia ndio alikua Kaburu nikamshauri atafute hotel alale maana aliingiza woga tayari nikaendelea na safari huko mbele sikukutana nao tena na sijapita tena ile bara bara..
 
Ndoto, usingizi na imani za kishirikina.

Hakuna kitu. Why usiku na si mchana??

Why barabarani tu na si njia ya train, Angani au Majini??.

Story za abunwasi na changamsha genge.

Nishasafiri Barabara nyingi, masaa yote kuspan 24 hours sijashuhudia hayo.

Ulongo tu na kutiana woga, kuwapa ulaji waganga wa kienyeji wafanye zindiko.
Usichokiona au usichokiweza katu usimalize kusema hakuna kitu cha namna hiyo. Kuwa na akiba ya maneno, nyie yakiwakuta ndio huwa mnakuwa ma deadliest witnessess
 
Japo si dereva, lakini nakumbuka wakat tuko moshi dereva amekabidhi gari kwa baba mbele ya gari imepondeka kabisa baba akauliza kulikoni akawaambia et kagonga kuku aliniacha njia panda wallah
 
--ngoja nifupishe,

Nakumbuka kuna siku 2012 nimepanda basi ya kampuni ya Satelite kutoka tanga kuelekea dar nikiwa nimekaa siti za karibu na mbele niliona dereva amepiga mabreki mengi gari ikayumba na tukasikia mlio mkubwa kwenye eneo la engine,a ila akaimudu na kuiweka sawa na akaweza kupaki pembeni ya barabara.

Wadau tukamgeukia dereva , "kulikoni unataka kutumwaga ?"
Akatujibu kuwa alikua ameona Kanga (ndege jamii ya kuku) na akamgonga ndio yule tulisikia kwenye engine,
Tukashuka na eneo la mbele la engin likafunguliwa, hatukukuta damu, manyoya wala dalili zozote za kugongwa kitu ila kitu pekee tulichokikuta ni fan belt iliokatika.

Tukajaribu kukagua huku na kule hatukukuta kitu chochote na safari yetu ikawa ndio mwisho mpaka ilipoletwa basi nyingine kutuchukua.

Mpaka leo hii sijaweza kujua ni kitu gani kilitokea japo dereva alikomalia msimamo wake
kumbe ulinusurika mhenga mwenzangu.
 
Ni hatari tupu ila huwezi acha kusafiri kwa kuogopa mauza uza

Sent using Jamii Forums mobile app
Ni safari moja tu ndio nimewah kufika home late saa saba halaf home sikusema kama nakuja na niko hivo hua wananishtukia tu nipo, lakini sijawah kukumbwa na hiyo kadhia tena napenda sana kufika home usiku sema sio wa manane

Kuna siku pia tulienda shamba la moja la mkonge liko mnazi, ni mbali tulikua kama watu wanne nikiwa mwanamke alone kwenye ule msafara, wakat tunarud dereva akasema tuchanje mbuga kwa mbuga tusipite ya lami tutazunguka sana tulipokua mbugan gari sjui ilikanyaga nn ikaserereka karib iingie kwenye kidaraja tukashuka hatukuona chochote tukaendelea kuja tokea sehem kunaitwa maramba tayar usiku saa mbili hivi, tukatembea hapo hakuna alieku na waswas kuhusu nn tulikanyaga kufika eneo linaitwa gombero alitoka nyoka upande wa dereva anavuka dereva akamkanyaga tena nikapiga kelele nyoka ikabidi tuangalie hatukuona kama amekanyagwa sikua na waswas kabisa leo ninesoma hapa nimerecall hayo matukio maybe yawezekana n hayo mauza uza au ilikua kweli
 
Ndoto, usingizi na imani za kishirikina.

Hakuna kitu. Why usiku na si mchana??

Why barabarani tu na si njia ya train, Angani au Majini??.

Story za abunwasi na changamsha genge.

Nishasafiri Barabara nyingi, masaa yote kuspan 24 hours sijashuhudia hayo.

Ulongo tu na kutiana woga, kuwapa ulaji waganga wa kienyeji wafanye zindiko.
Binadamu bhana, Sasa kwa vile hujaona ndo unapinga?
Kama hujawahi kutana na hayo mauza uza si kigezo cha kusema hayapo.
Kimya pia ni akili unaweza ukaambulia hata moja

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Mauza uza ni nini hayo? nataka siku nikutane nayo nimeendesha sana night kali na napenda sababu ya speed so nipite njia gani nikutane hata na jini, nije kusimulia masela.
 
Back
Top Bottom