Kwa maneno haya ya Polepole inamaanisha kifo cha Magufuli kina mchezo mchafu ndani yake?

chinchilla coat

JF-Expert Member
Joined
May 16, 2016
Posts
5,107
Reaction score
10,969
Alikuwa akihojiwa na Dar24 na kuulizwa kuhusu minong'ono ya watu kuwa Magufuli huenda hakufariki kwa ugonjwa uliotajwa kweli na kuwa huenda aliuawa

Polepole akakwepa kujibu swali hilo na kusema mtu akishakufa yeye hamzungumzii tena (hata Rais wa nchi?)

Polepole ambaye alikua moja ya watu wa karibu sana na Magufuli kabla hajafa, na kwa sababu hiyo lazima atakuwa anajua mengi kuhusu kuumwa hadi kufariki kwa Magufuli

Na wafuasi wengi wenye hii minong'ono ni wale wanamuunga mkono na kumuamini Polepole kama mfuasi wa kweli wa Magufuli aliyebaki, angesema ndio ni matatizo ya moyo yalimuondoa basi ingepungua sana kama sio kuisha

Kwa nini anashikwa na kigugumizi ku back up taarifa aliyotoa Rais kuwa Magufuli alifariki kwa ugonjwa wa moyo wakati anajua ni kweli kuna minong'ono?

Kusema hawezi kuzungumzua kifo cha Magufuli kuugua kwake kuliambatana na usiri mkubwa haoni kuwa anazidi kuongeza nguvu kwenye hiyo minong'ono?

Video

Your browser is not able to display this video.
 
Ila Chakubanga ameongea kwa weledi sana hapo mbona. Yani yeye alichomaanisha ni kuwa hana mamlaka ya kuzungumzia hilo jambo kwakuwa yeye sio mwanafamilia.

Basi. Msipende kukuza mambo. Mwacheni marehemu aendelee kula mahewa huko motoni.
 
Pole pole alikuwa amefikia juu sana. Alikuwa na mamlaka makubwa sana ya kumhoji yeyote ndani ya taifa hili.

Wakati huo alikuwa na kipindi chake Channel Ten anajifanya anatatua shida za wananchi, anampigia simu kiongozi yeyote wakati wowote hata usiku wa manane kumhoji atoe majibu.

Sasa hayo madaraka yamemponyoka ghafla sana. Hapo alipo kiakili hayuko sawa, bado ana HANG OVER ya MADARAKA.

Na kibaya zaidi bado anaihitaji SIASA lakini akiangalia haoni FUTURE. Maana hayuko kwenye Chama wala serikalini na hata akienda kugombea huko CCM kwenye kura za maoni hawezi kupita.

Sasa sasa hivi anachofanya ni kutafuta mashabiki kwa kujifanye yeye ni mtetezi wa watu.

Hakuma kingine cha maana.
 
aisee magufuli sio wa kwanza kufa humu duniani, hata sisi tulishafiwa na ndugu zetu tutoleeni upumbavu humu, yeye alikua na hatimiliki ya kuishi daima?
Kama mnalijua hilo mbona mnafurahi kifo chake na kusema Mungu fundi
 

Anatumia mbinu ile ile ya mwendazake kujifanya yeye mtu wa watu sio
 
Hizi mada zenye maudhui haya zipumzisheni sasa.....tugange mengine..
 
Wajinga tu ndo hawawezi jua hii movie ilichezwaje, changa la macho ili tujuwe corona kisa watu wake wa karibu wamekufa .
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…