Kwa maoni ya Dkt. Slaa, inawezekana Ben Saanane na wengine walitekwa na kupotezwa na Chadema

Kwa maoni ya Dkt. Slaa, inawezekana Ben Saanane na wengine walitekwa na kupotezwa na Chadema

Synthesizer

Platinum Member
Joined
Feb 15, 2010
Posts
12,699
Reaction score
22,598
Kuna vitu vingine ni bora kukaa kimya badala ya kuongea, kwa kuwa unapoongea watu wataweza kujua kina cha busara zako kama ni kirefu au kifupi sana. Katika maisha, ni bora kukaa kimya watu wadhani una busara, kuliko wewe kudhani una busara ukaongea hadharani na kufanya hata wale waliodhani una busara watambue kuwa huna busara.

Mfano ni hili la Lissu na suala zima la kupigwa risasi. Ni kweli hatuna ukweli wote, lakini pia kuna viashiria vingi kwamba vyombo vya usalama vya Serikali havikulipa uzito unaostahili katika kulipeleleza. Na pia kumekuwa na circumstantial evidence nyingi sana kwamba kwa namna moja au nyingine Serikali ilihusika. Sasa pale Dr. Slaa anaposema hawezi kuongelea hili, kisha anaeleza kisa cha mtu alietekwa na watu wa CHADEMA wenyewe, ni wazi ana nia ya kuufanya umma uamini kwamba kuna uwezekano Lissu alipigwa risasi na watu wa CHADEMA.

Lakini sasa, hili wazo la Dr. Slaa lingekuwa na circumstantial evidence nje ya huyo alietekwa na Chadema wenyewe, labda ndio angepaswa kuliunganisha na hicho kisa kingine. Na Dkt Slaa, anajuaje kwamba huyo aliesema aliongoza kumteka mtu wa CHADEMA yote hiyo haikuwa part ya plan ya kuwavuruga CHADEMA kwa kuwagonganisha wao kwa wao? Hivi Dr. Slaa hajui dirty politics zinavyochezwa, kampuni ya soda hii kuweka kondomu kwenye chupa ya kampuni ya soda ile ili watu waione ni kampuni ya soda chafu?

Kwa mfano, hivi Dr Slaa anajua kwamba muda mfupi baada ya Lissu kupigwa riasi Magufuli alimpigia simu Mwigulu Nchemba kama waziri wa Mambo ya Ndani atoe tamko kwamba serikali haikuhusika na jaribio la kumuua Lissu? (Mwigulu baada ya kupata ushauri wa wazee fulani wa CCM hakufanya hivyo, ikawa sababu mojawapo ya Magufuli kumchukia na hatimae kumtoa uwaziri). Muulize Mwigulu atakuambia, na utaelewa kwa nini pia Magufuli aliwachukia wazee fulani wa CCM.

Je, Dr. Slaa anajua kwamba Lissu alikuwa shadowed kwa muda mrefu kabla ya tukio? Je, anajua CCTV recordings ziliondolewa pale kwenye eneo la tukio? Je, Dr. Slaa anajua kwamba barabara zilifanywa tupu ili gari lililotumika kwenye jaribio liweze kupita bila pingamizi kuondoka sehemu ya tukio? Je, Dr. Slaa anajua gari mpya ya Nissan Patrol ilitumika na kuchomwa moto ili kuharibu ushahidi? Sasa nani ndani ya CHADEMA anaweza ku-mount operation ya namna hiyo dhidi ya Lissu?

Nani ndani ya CHADEMA anaweza ku-mount operation za aina ya utekaji na uuaji uliofanywa na kuufanikisha bila kuwa na support ya Serikali, na vyombo vya usalama vikae kimya bila kuwakamata kwa kutumia kila aina ya nguvu? Operation za namna hiyo ambazo nyingine zilifanyika mchana kweupe, zinaweza tu kufanyika ikiwa wanaozifanya wanajua Serikali na vyombo vya usalama viko nyuma yao. Yaani hili ni gumu sana kwa Dr. Slaa kulielewa?

N wazi sana Dr. Slaa amekuwa currupted na zawadi ya ubalozi aliyopewa na Magufuli, na sasa inamfanya kuwa shabiki namba moja wa Magufuli. In fact anaonyesha hata silka ya kumshutumu na kumpiga Rais Samia vijembe kichinichini kwa huu ushabiki wake kwa Magufuli. Dr. Slaa amekuwa psychologically bribed and corrupted na zawadi ya ubalozi kiasi kwamba sasa anajisahau kabisa, he is becoming so naive to the extent of forgetting to be clever. Poor Dr Slaa.
 
Haipo Serikali duniani inayoweza kufanya mambo ya kijinga kwa jinsi hii kama yanayodhaniwa kufanyika awamu ya 5 ya Hayati JPM. In fact JPM na Serikali yake hawakuhusika

Huko mbele ya safari mimi naamini kabisa kuwa ukweli wote utakuja kujulikana tu. Vita kati ya ukweli na uongo, uongo huwa unaanza unashinda kwanza, halafu ukweli ndiyo unakuja kumalizia kwa kushinda mwisho.
 
Slaa ametupatia mwanga kwenye mambo ya muhimu sana.

Chadema walikalia kumtuhumu Magufuli kwamba amemteka na kumpoteza Ben kumbe ni internal operation ya chama, kuua na kupoteza watu na kisha kutupia lawama serikali.

Sasa naanza kupata mashaka na walioshambulia Lisu, sasa naanza kuwaamini waliosema hii ni vita ya mamlaka vyeo ndani ya chama.

Ahsante sana mzee Slaa.
 
Na kama Chadema ni wauaji wakubwa, basi sijui tutasemaje kuhusu CCM - tuanze ka kina Sokoine, Mwaikambo, nk
This is very simple than you think: Tuombe USA au Uingereza watupe wapelelezi wafanye uchunguzi. Kuna mengi sana wanaweza kutusaidia. Kupigwa risasi Mh. Lissu, Azori Gwanda na Ben Saanane kutoweka nk....
 
Slaa ametupatia mwanga kwenye mambo ya muhimu sana.

Chadema walikalia kumtuhumu Magufuli kwamba amemteka na kumpoteza Ben kumbe ni internal operation ya chama, kuua na kupoteza watu na kisha kutupia lawama serikali.

Sasa naanza kupata mashaka na walioshambulia Lisu, sasa naanza kuwaamini waliosema hii ni vita ya mamlaka vyeo ndani ya chama.

Ahsante sana mzee Slaa.
Kabisa. Ndiyo maana tunapiga kelele kila siku tuombe mataifa yaliyobobea kwenye upelelezi kama USA au Uingereza watusaidie eli hao Chadema waumbuke.
 
Huyu mzee ni mjinga sna, kwao ni Karatu toka ametoka Ulaya hajawahi kufika Karatu, anakinyongo sn na CHADEMA
 
Babu mihogo dish lishayumba tumsamehe, kumwongelea hapa ni kumpa millage za bure !!
Yule mzee ana matatizo makubwa. Ni wa kuonea huruma. Sijui ni mke wake anamwendesha au ni maisha yamempiga lakini naona kuna kitu ambacho hakiko sawa hata kidogo.
 
Kabisa. Ndiyo maana watu wanasema mtu kama huyu mwanzisha thread na Dr Slaa ni wapumbavu kwani hawajui kwamba wanaposema mtu kama Ben Saanane alipotezwa na na Chadema basi wanalazimisha uchunguzi ambao utaanika kila kitu hadharani
Huyu mzee ni mpumbafu sn hana akili
 
Haipo Serikali duniani inayoweza kufanya mambo ya kijinga kwa jinsi hii kama yanayodhaniwa kufanyika awamu ya 5 ya Hayati JPM. In fact JPM na Serikali yake hawakuhusika

Huko mbele ya safari mimi naamini kabisa kuwa ukweli wote utakuja kujulikana tu. Vita kati ya ukweli na uongo, uongo huwa unaanza unashinda kwanza, halafu ukweli ndiyo unakuja kumalizia kwa kushinda mwisho.
Kama serikali haijahusika wameshindwa nini kufanya uchunguzi??, Kwamba chadema ina nguvu kuliko usalama wa Taifa au jeshi la polisi??. Huu upuuzi wakutetea vitu ambavyo hata mtoto wa darasa la saba anavifahamu ni ukichaa.
 
Back
Top Bottom