Kwa Mara ya kwanza Napongeza Ubunifu alioufanya Makonda Arusha

Kwa Mara ya kwanza Napongeza Ubunifu alioufanya Makonda Arusha

Lord denning

JF-Expert Member
Joined
Jun 3, 2015
Posts
15,819
Reaction score
33,255
Mimi sio mshabiki wa Makonda, kutokana na namna ninavyomjua. Tabia zake binafsi na hulka zake ndo chanzo kikuu cha mimi kutokuwa shabiki wake na kila siku kumpinga kwenye masuala mengi sana.

Katika kumfuatilia kwangu tangu akiwa mkuu wa Wilaya ya Kinondoni, then Mkuu wa Mkoa wa Dar es Salaam, mpaka alivyokuwa Katibu Mwenezi wa Chama cha Mapinduzi na sasa Mkuu wa Mkoa wa Arusha nadhani amefanya jambo moja tu ambalo naliona kama jambo la maana lenye impact chanya kwenye uchumi wa nchi.

Jambo hili ni huu ubinifu wa Land Rover Festival!

Pamoja na Rais Samia kuanza kusemwa vibaya na media za kimataifa ila tunakumbuka kuwa kwa muda wa miaka 3 sasa media hizi zilikuwa zikimsema vizuri sana hadi kuleta impact kubwa sana kwenye sekta ya utalii ambayo ndo chanzo chetu kikuu cha fedha za kigeni zinazotunisha mfuko wetu wa Benki Kuu bila kusahau uwekezaji wa kigeni (FDI)

Ni dhahili sasa kuwa, suala hili la Land Rover Festival ni ubunifu mkubwa sana katika kupiga chapuo ukuaji wa Utalii nchini Tanzania na kuufanya ukue zaidi katika siku za mbeleni na kuongeza mapato ya Taifa.

Nimependa publicity ya hili tukio na kusema kweli publicity hii ikienda hewani hadi kimataifa inaweza kuja kufanya mwaka kesho wakaja hadi waingereza na wajerumani kuja kushiriki hili Tamasha kwa kuleta magari yao.

Soma Pia: RC Makonda: Oktoba 2024 tuna maonesho ya Landcruiser, Range na Landrover 1000

Mwisho pamoja na kumpongeza Makonda kwa hii creativity na publicity yenye matokeo chanya kwenye uchumi wa nchi.

Napendekeza pia Festival hii ihusishe matukio ya burudani kama vile mziki na maonyesho ya vyakula mbalimbali vya kitanzania.

Hili kusema kweli litakuza sana Utalii wetu na miaka ya mbeleni linaweza kuja kuwa Tamasha kubwa kama yale ya Carnival (Brazil) na mengineyo tunayoyafahamu Duniani.

Pili najua huu ni mwanzo ila ni vizuri Tamasha hili likawa linafanyika hata kwa Wiki nzima ili kuweka nafasi ya matukio mengi kufanyika.


Hongera Makonda. Huu ndo ubunifu tunaoutaka sio yale mambo yako ya kijinga ya kuchongea watu, ufitini, wivu wa madaraka, ufisadi, na kutafuta cheap popularity!

Keep it up!

Lord denning
 
Mimi sio mshabiki wa Makonda, kutokana na namna ninavyomjua. Tabia zake binafsi na hulka zake ndo chanzo kikuu cha mimi kutokuwa shabiki wake na kila siku kumpinga kwenye masuala mengi sana.

Katika kumfuatilia kwangu tangu akiwa mkuu wa Wilaya ya Kinondoni, then Mkuu wa Mkoa wa Dar es Salaam, mpaka alivyokuwa Katibu Mwenezi wa Chama cha Mapinduzi na sasa Mkuu wa Mkoa wa Arusha nadhani amefanya jambo moja tu ambalo naliona kama jambo la maana lenye impact chanya kwenye uchumi wa nchi.

Jambo hili ni huu ubinifu wa Land Rover Festival!

Pamoja na Rais Samia kuanza kusemwa vibaya na media za kimataifa ila tunakumbuka kuwa kwa muda wa miaka 3 sasa media hizi zilikuwa zikimsema vizuri sana hadi kuleta impact kubwa sana kwenye sekta ya utalii ambayo ndo chanzo chetu kikuu cha fedha za kigeni zinazotunisha mfuko wetu wa Benki Kuu.

Ni dhahili sasa kuwa, suala hili la Land Rover Festival ni ubunifu mkubwa sana katika kupiga chapuo ukuaji wa Utalii nchini Tanzania na kuufanya ukue zaidi katika siku za mbeleni na kuongeza mapato ya Taifa.

Nimependa publicity ya hili tukio na kusema kweli publicity hii ikienda hewani hadi kimataifa inaweza kuja kufanya mwaka kesho wakaja hadi waingereza na wajerumani kuja kushiriki hili Tamasha kwa kuleta magari yao.


Mwisho pamoja na kumpongeza Makonda kwa hii creativity na publicity yenye matokeo chanya kwenye uchumi wa nchi.

Napendekeza pia Festival hii ihusishe matukio ya burudani kama vile mziki na maonyesho ya vyakula mbalimbali vya kitanzania.

Hili kusema kweli litakuza sana Utalii wetu na miaka ya mbeleni linaweza kuja kuwa Tamasha kubwa kama yale ya Carnival (Brazil) na mengineyo tunayoyafahamu Duniani.

Pili najua huu ni mwanzo ila ni vizuri Tamasha hili likawa linafanyika hata kwa Wiki nzima ili kuweka nafasi ya matukio mengi kufanyika.


Hongera Makonda. Huu ndo ubunifu tunaoutaka sio yale mambo yako ya kijinga ya kuchongea watu, ufitini, wivu wa madaraka, ufisadi, na kutafuta cheap popularity!

Keep it up!

Lord denning
Hapo unakula buku 7 au 10 kabisa ???
 
Kusifu kikupendezajo ni wajibu lakini maudhi y maudhui ya kisifiwacho ni muhimu. Kwa mtazamo wangu tamasha ni la kutangaza gari aina ya LANDROVER kwanza na utalii inafuata. Tamasha ni la LANDROVER Vs LANDCRUISER. Lilitakiwa kuwa tamasha la UTALIII gari LANDROVER , LANDRUISER na MAPUTO ni vikolezo/nyenzo za kutalii. Anglia nyenzo historia ya utalii kuanzia 1980 hadi sasa.

Nawaza tu!!
 
Mimi sio mshabiki wa Makonda, kutokana na namna ninavyomjua. Tabia zake binafsi na hulka zake ndo chanzo kikuu cha mimi kutokuwa shabiki wake na kila siku kumpinga kwenye masuala mengi sana.

Katika kumfuatilia kwangu tangu akiwa mkuu wa Wilaya ya Kinondoni,
Akiwa DC wa Kinondoni kwa ushirikiano na Ruge Mutahaba alianzisha Malkia wa Nguvu na yeye kuvishwa taji ya Balkia wa Nguvu na hapa ndipo akina sisi watu wa “Kauli Umba” tukamtolea kauli humu humu JF, iliyomuumbia u RC
wa DSM Nimemkubali Sana DC Makonda, anafaa kuwa Mkuu wa Mkoa Dar es Salaam
nadhani amefanya jambo moja tu ambalo naliona kama jambo la maana lenye impact chanya kwenye uchumi wa nchi.

Jambo hili ni huu ubinifu wa Land Rover Festival!

Keep it up!

Lord denning
Naomba kuheshimu mawazo yako hata kwa kuliona hili moja tuu ni mwanzo mzuri wa kumuangazia Konda Boy with positive prospective outlook kutoka kwa mtu kama wewe, it does something good for him and his endeavors on the aspect the power of positive thinking that will make this festival a big thing in future, wasiwasi wangu ni kitu kinachoitwa continuity on the part of mamlaka yake ya uteuzi, ”ukipata tuu a "limelight” kosa!, utaonekana you are trying to steals the show!unang'olewa!. Inferiority complex ni tatizo on her part!, kuna mtu alitumbuliwa uwaziri kwa kosa la kupiga picha na rais fulani!. Baada ya mwenezi kung'ara, akaonekana ana overshine, akaondolewa!, baada ya Jerry Slaa kushine ardhi, akaondolewa!, baada ya Mtaka kushine Dodoma, akatupwa Njombe!, hivyo dogo akishine sana Arachuga, huchelewi kusikia amehamishwa kuwa RC Lindi au Singida, where is the continuity?

P
 
Leo lazima tusikie vilio vya bundi mahali fulani. Wewe kabisa kumsifia na kumpongeza mtu pro-shujaa? Mhhhh, ama kweli kua mwanangu uyaone!
🤣🤣🤣🤣 najua hata Makonda baada ya kusoma uzi wangu lazima akatoe sadaka kesho kanisani!

Ni jambo la kawaida tu. Sinaga bifu za kishamba.

Uadui wangu na Sukuma Gang ni kutokana na mambo yao ya kijinga na kishamba hasa kipindi kile.

Otherwise kwenye mambo mazuri sote ni Watanzania.
 
Akiwa DC wa Kinondoni kwa ushirikiano na Ruge Mutahaba alianzisha Malkia wa Nguvu na yeye kuvishwa taji ya Balkia wa Nguvu na hapa ndipo akina sisi watu wa “Kauli Umba” tukamtolea kauli humu humu JF, iliyomuumbia u RC
wa DSM Nimemkubali Sana DC Makonda, anafaa kuwa Mkuu wa Mkoa Dar es Salaam
Malkia wa Nguvu ni jambo zuri. Sikuwahi jua kuwa alihusika au ilikuwaje ila kwa impact haliwezi kinganishwa na hii Land Rover Festival.

Hii Festival ikiwa published vizuri na kutangazwa hadi vyombo vya kimataifa mwaka kesho kuna uwezekano mkubwa sana wakaja hata watu laki mbili au tatu kutoka nje ya Tanzania kuja kushiriki.

Inawezekana publicity hiyo ikawafanya Kampuni ya Land Rover kuja kufungua hata kiwanda Tanzania na kuanza kutengeneza magari yake hapa.

Likitumika vizuri na kupewa publicity ya ukweli kimataifa impact ni kubwa sana kiutalii na kiuchumi kwa ujumla huko mbeleni.
 
"Anapenda makiki kama msanii" -Weusi
Hapana hii sio Kiki ya kishamba kama zile zingine za sijui clinic za matatizo mara kuwachongea watu sijui kuwadhalilisha watumishi wa umma n.k.

Hii kitu tukitumia akili imekaa vizuri sana kimkakati.

Vikiletwa vyombo vya kimataifa pale sijui CNN, BBC, AL Jazeera, DW, France 24, Wion, Firstpost, CCGTV, African News, VOA, TRT na vinginevyo na wakarusha lile tukio nakwambia mwaka kesho hapatakalika pale chugani kwa hiyo nyomi ya wageni kushiriki ile Festival!

Na nyomi ikiwa kubwa basi ndo mapato ya nchi yataongezeka.
 
Mimi sio mshabiki wa Makonda, kutokana na namna ninavyomjua. Tabia zake binafsi na hulka zake ndo chanzo kikuu cha mimi kutokuwa shabiki wake na kila siku kumpinga kwenye masuala mengi sana.

Katika kumfuatilia kwangu tangu akiwa mkuu wa Wilaya ya Kinondoni, then Mkuu wa Mkoa wa Dar es Salaam, mpaka alivyokuwa Katibu Mwenezi wa Chama cha Mapinduzi na sasa Mkuu wa Mkoa wa Arusha nadhani amefanya jambo moja tu ambalo naliona kama jambo la maana lenye impact chanya kwenye uchumi wa nchi.

Jambo hili ni huu ubinifu wa Land Rover Festival!

Pamoja na Rais Samia kuanza kusemwa vibaya na media za kimataifa ila tunakumbuka kuwa kwa muda wa miaka 3 sasa media hizi zilikuwa zikimsema vizuri sana hadi kuleta impact kubwa sana kwenye sekta ya utalii ambayo ndo chanzo chetu kikuu cha fedha za kigeni zinazotunisha mfuko wetu wa Benki Kuu.

Ni dhahili sasa kuwa, suala hili la Land Rover Festival ni ubunifu mkubwa sana katika kupiga chapuo ukuaji wa Utalii nchini Tanzania na kuufanya ukue zaidi katika siku za mbeleni na kuongeza mapato ya Taifa.

Nimependa publicity ya hili tukio na kusema kweli publicity hii ikienda hewani hadi kimataifa inaweza kuja kufanya mwaka kesho wakaja hadi waingereza na wajerumani kuja kushiriki hili Tamasha kwa kuleta magari yao.

Soma Pia: RC Makonda: Oktoba 2024 tuna maonesho ya Landcruiser, Range na Landrover 1000

Mwisho pamoja na kumpongeza Makonda kwa hii creativity na publicity yenye matokeo chanya kwenye uchumi wa nchi.

Napendekeza pia Festival hii ihusishe matukio ya burudani kama vile mziki na maonyesho ya vyakula mbalimbali vya kitanzania.

Hili kusema kweli litakuza sana Utalii wetu na miaka ya mbeleni linaweza kuja kuwa Tamasha kubwa kama yale ya Carnival (Brazil) na mengineyo tunayoyafahamu Duniani.

Pili najua huu ni mwanzo ila ni vizuri Tamasha hili likawa linafanyika hata kwa Wiki nzima ili kuweka nafasi ya matukio mengi kufanyika.


Hongera Makonda. Huu ndo ubunifu tunaoutaka sio yale mambo yako ya kijinga ya kuchongea watu, ufitini, wivu wa madaraka, ufisadi, na kutafuta cheap popularity!

Keep it up!

Lord denning
Hii kitu inaweza kugeuka kuwa kitu kikubwa hata majirani wakaanza kushiriki.
Simkubali ila hii inaweza kuvutia watalii kama ulivyosema. Sema aache kujifanya wazir wa nchi eti trafiki akikukamata mwambie anipigie mimi. Yani utoke mbeya na gari bovu trafiki wakuache kisa makonda kasema.
 
Hii kitu inaweza kugeuka kuwa kitu kikubwa hata majirani wakaanza kushiriki.
Simkubali ila hii inaweza kuvutia watalii kama ulivyosema. Sema aache kujifanya wazir wa nchi eti trafiki akikukamata mwambie anipigie mimi. Yani utoke mbeya na gari bovu trafiki wakuache kisa makonda kasema.
Saaana. Nimeona TBC watu kutoka Kenya wamevuka kuja kushiriki. Kwa muono wa mbele ni jambo lenye impact kubwa sana tukilichukulia serious na kuliwekea mikakati mizuri.

Hayo ya kuwasema Trafiki hadharani ndo ujinga wake ninaousema kila siku hapa. All in All pamoja na hili zuri lake ila still anabaki kuwa liability kwa sehemu kubwa.
 
Hili hata siyo wazo la Makonda ni wazo la wafanyabiashara wa utalii Arusha yeye ametumika tu sababu ni mpenda sifa
Oooh sawa. Ila hata kwa kulichukua na kulifanya liwe namna lilivyofanywa anastahili pongezi zetu.

Nategemea kuwaona Mawaziri wa Utalii na Habari wakishiriki kulipa publicity kubwa hili tukio ili liwe na manufaa tuliyoyasema humu.
 
Back
Top Bottom