Kwa Mara ya kwanza Napongeza Ubunifu alioufanya Makonda Arusha

Kwa Mara ya kwanza Napongeza Ubunifu alioufanya Makonda Arusha

Malkia wa Nguvu ni jambo zuri. Sikuwahi jua kuwa alihusika au ilikuaje ila kwa impact haliwezi kuandaliwa na hii Land Rover Festival.

Tamasha hili lilichapishwa vizuri na kutangazwa hadi vyombo vya kimataifa mwaka kesho kuna uwezekano mkubwa sana wakaja hata watu wawili wawili kutoka nje ya Tanzania kuja kushiriki.

publicity hiyo ikawafanya Kampuni ya Land Rover kuja kufungua kiwanda cha kutengeneza magari yake hapa.

Likitumika vizuri na kupewa publicity ya ukweli kimataifa impact ni kubwa sana kiutalii naujumla kwa ujumla huko mbeleni.
Kiwanda kingine?
.Si alisema kwa sasa zinatengenezwa Arusha na wanaziuza hadi Uingereza?
 
Oooh sawa. Ila hata kwa kulichukua na kulifanya liwe namna lilivyofanywa anastahili pongezi zetu.

Nategemea kuwaona Mawaziri wa Utalii na Habari wakishiriki kulipa publicity kubwa hili tukio ili liwe na manufaa tuliyoyasema humu.
Hivi unajua rushwa aliyovuta kulibeba hili swala? yule huwa haendi bure
 
Sidhani kama ni kiwanda cha Land Rover wenyewe. Nimezungumza kama kampuni husika wenyewe wataamua kufungua kiwanda chenyewe hapa nchini.
Uongozi wa Tanzania ni wa hovyo hakuna mtu atakuja kufungua kiwanda kikubwa hapa maana sera za hapa zinategemea matamko ya Rais aliyepo madarakani, alijaribu Dangote lakini mwisho anasua sua tu sababu ya sera mbovu na kodi za kijinga.
 
Uongozi wa Tanzania ni wa hovyo hakuna mtu atakuja kufungua kiwanda kikubwa hapa maana sera za hapa zinategemea matamko ya Rais aliyepo madarakani, alijaribu Dangote lakini mwisho anasua sua tu sababu ya sera mbovu na kodi za kijinga.
Hilo halina ubishi. Ila kama wameweza wale kiwanda cha ndege ndogo kule Morogoro hata hawa wanaweza kuja
 
Royal tour imeleta nini mpk leo na mabilioni iliyotumia? kila RC/DC ndiyo ilikuwa habari ya mjini
Sizingumzii Royal Tour kama Royal Tour. Ila kwa takwimu zilizopo kwenye ukanda wa Afrika sisi ni moja ya nchi zilizofanya vizuri sana kwenye sekta ya utalii kwa mwaka huu kama sikosei. Limerushwa sana kwenye blogs za kimataifa wiki kadhaa zilizopita.
 
Sidhani kama kiwanda cha Land Rover wenyewe. Nimezungumza kama kampuni husika wenyewe wataamua kufungua kiwanda chenyewe hapa nchini.
Lakini ulimsikia aliposema zinatengenezwa hapa Arusha na wanaenda kuwauzia Waingereza?
Hakusema zinakarabatiwa.
 
Hilo halina ubishi. Ila kama wameweza wale kiwanda cha ndege ndogo kule Morogoro hata hawa wanaweza kuja
Baadae kitakufa, wakati nakuwa nilikutana na kilimo kwanza ikafa, ikaja BRN ikafa, serikali ya viwanda ikafa(viwanda mia 3 kila mkoa ya Jafo), royal tour ikafa, leo maigizo ya land rover sijui hakuna lolote, ukiambiwa budget na kitakachopatikana ni mbingu na ardhi, TRA huwa wanasema wamekusanya 3T lakini huwezi kusikia wanasoma mapato na matumizi hata siku moja ni utapeli tapeli tu
 
Baadae kitakufa, wakati nakuwa nilikutana na kilimo kwanza ikafa, ikaja BRN ikafa, serikali ya viwanda ikafa(viwanda mia 3 kila mkoa ya Jafo), royal tour ikafa, leo maigizo ya land rover sijui hakuna lolote, ukiambiwa budget na kitakachopatikana ni mbingu na ardhi, TRA huwa wanasema wamekusanya 3T lakini huwezi kusikia wanasoma mapato na matumizi hata siku moja ni utapeli tapeli tu
Let's hope for the best!
 
Sizingumzii Royal Tour kama Royal Tour. Ila kwa takwimu zilizopo kwenye ukanda wa Afrika sisi ni moja ya nchi zilizofanya vizuri sana kwenye sekta ya utalii kwa mwaka huu kama sikosei. Limerushwa sana kwenye blogs za kimataifa wiki kadhaa zilizopita.
Broo nimezaliwa kaskazini Arusha haijawahi kushuka kiutali isipokuwa kipindi cha corona 2020-2021 na sera mbovu za Magu, ndiyo maana Arusha ina hoteli nyingi sn za kitalii kuliko mji wowote hapa EAC
 
Broo nimezaliwa kaskazini Arusha haijawahi kushuka kiutali isipokuwa kipindi cha corona 2020-2021 na sera mbovu za Magu, ndiyo maana Arusha ina hoteli nyingi sn za kitalii kuliko mji wowote hapa EAC
Takwimu zinaonesha mwaka jana na mwaka huu Tanzania ndo tumefanya vizuri na hii ni kwa mujibu wa vyombo vya habari na takwimu kutoka nje ya Tanzania.

So hata kama tulikuwa tunafanya vizuri ila hivi karibuni tumekuwa tunafanya vizuri zaidi.
 
Mimi sio mshabiki wa Makonda, kutokana na namna ninavyomjua. Tabia zake binafsi na hulka zake ndo chanzo kikuu cha mimi kutokuwa shabiki wake na kila siku kumpinga kwenye masuala mengi sana.

Katika kumfuatilia kwangu tangu akiwa mkuu wa Wilaya ya Kinondoni, then Mkuu wa Mkoa wa Dar es Salaam, mpaka alivyokuwa Katibu Mwenezi wa Chama cha Mapinduzi na sasa Mkuu wa Mkoa wa Arusha nadhani amefanya jambo moja tu ambalo naliona kama jambo la maana lenye impact chanya kwenye uchumi wa nchi.

Jambo hili ni huu ubinifu wa Land Rover Festival!

Pamoja na Rais Samia kuanza kusemwa vibaya na media za kimataifa ila tunakumbuka kuwa kwa muda wa miaka 3 sasa media hizi zilikuwa zikimsema vizuri sana hadi kuleta impact kubwa sana kwenye sekta ya utalii ambayo ndo chanzo chetu kikuu cha fedha za kigeni zinazotunisha mfuko wetu wa Benki Kuu bila kusahau uwekezaji wa kigeni (FDI)

Ni dhahili sasa kuwa, suala hili la Land Rover Festival ni ubunifu mkubwa sana katika kupiga chapuo ukuaji wa Utalii nchini Tanzania na kuufanya ukue zaidi katika siku za mbeleni na kuongeza mapato ya Taifa.

Nimependa publicity ya hili tukio na kusema kweli publicity hii ikienda hewani hadi kimataifa inaweza kuja kufanya mwaka kesho wakaja hadi waingereza na wajerumani kuja kushiriki hili Tamasha kwa kuleta magari yao.

Soma Pia: RC Makonda: Oktoba 2024 tuna maonesho ya Landcruiser, Range na Landrover 1000

Mwisho pamoja na kumpongeza Makonda kwa hii creativity na publicity yenye matokeo chanya kwenye uchumi wa nchi.

Napendekeza pia Festival hii ihusishe matukio ya burudani kama vile mziki na maonyesho ya vyakula mbalimbali vya kitanzania.

Hili kusema kweli litakuza sana Utalii wetu na miaka ya mbeleni linaweza kuja kuwa Tamasha kubwa kama yale ya Carnival (Brazil) na mengineyo tunayoyafahamu Duniani.

Pili najua huu ni mwanzo ila ni vizuri Tamasha hili likawa linafanyika hata kwa Wiki nzima ili kuweka nafasi ya matukio mengi kufanyika.


Hongera Makonda. Huu ndo ubunifu tunaoutaka sio yale mambo yako ya kijinga ya kuchongea watu, ufitini, wivu wa madaraka, ufisadi, na kutafuta cheap popularity!

Keep it up!

Lord denning

Samia ajaleta impact yeyote kwenye utalii, hayo wanayasema ambao hawaujui utalii!
 
Takwimu zinaonesha mwaka jana na mwaka huu Tanzania ndo tumefanya vizuri na hii ni kwa mujibu wa vyombo vya habari na takwimu kutoka nje ya Tanzania.

So hata kama tulikuwa tunafanya vizuri ila hivi karibuni tumekuwa tunafanya vizuri zaidi.
Soma ripoti za kuanzia 2000-2016 ndiyo ulinganishe na leo, kumbuka nyuma matumizi ya internet, social media kwa Tanzania yalikuwa chini sn
 
Back
Top Bottom