Kwa maswali haya sensa imefeli kabla haijafanyika!

Kwa maswali haya sensa imefeli kabla haijafanyika!

Kwanza maswali ni mengi bila sababu ya msingi halafu mengi ni ya kijinga na kipuuzi. Ingewezekana kabisa kuwa na dodoso lenye maswali machache na ya msingi. Baadhi ya maswali wangeachiwa watendaji wa mitaa/vijiji wakisaidiwa na wenyeviti wao kwani ni ya kifamilia zaidi na yanahitaji utulivu.

Kwa ufupi hii itakuwa sensa ya hovyo kabisa kufanyika nchini na itachukuwa muda mrefu bila sababu yo yote. Wananchi wengi watayakwepa au kuyapuuza baadhi ya maswali kwa kusema uongo!

PIA, SOMA:
- Maswali 100 ya sensa ya watu na makazi ya mwaka
Kuna swali nimeulizwa umiliki wa kompyuta ya mezani au mpakato nikajibu sijawahi miliki kwa mda wanaotaka wao...swali lililofuata nimeulizwa je nimetumia hizo compyuta za mezani au mpakato kwa mda huo? Kujibu yes ikagoma ikabidi karani aanze mwanzo....Sasa Ina maana kitu Kama hukimiliki huwezi kutumia hata kwa mtu mwingine au maofisini? Mbona taarifa wanazozitaka zitakuwa za uongo Sana?
 
Wenzetu wanawekeza kwenye Civil Registration and Vital Statistics (CRVS) ili kupunguza gharama za kufanya Sensa kila baada ya miaka 10
NI kweli ndugu ndio maana wenye tu huwa wakati kwa wanaoingia au vizuri vipya na wanaofariki hii hausaidia kuestimate watu wako hata kama usipofanya sensa.
 
kwa wingi wa haya maswali zoezi litachukuwa siku 30,
Note my words. hivyo serekali itapata mzigo mkubwa kweli wa kulipa watendaji wa sensa.
Niamini mimi hawatalipwa kwa siku zote lazima watadhulumiwa na hawatakuwa na mahali po pote pa kupeleka malalamiko yao!
 
Tunapozungumza kuhusu Mashirika/Taasisi/Wizara Nyingi za Serikali zinaongozwa na watu wenye uwezo mdogo sana(Kutathimini,Kuchambua,kuchanganua,kutafakari,kufikiri,kutunga sera na mikakati,kusimamia utekelezaji.nk);Maswali mengi ya Sensa ni ya kijinga/kipuuzi na kubwa yanaaingilia "Life privacy"ya mtu. Hata kuyajadili na kuyachambua ni aibu: "JUDGE A MAN BY HIS QUESTION'S RATHER THAN HIS ANSWER'S" By voltaire:
Mkuu acha kutukana watendaji wa hii nchi.
 
Tunafanya sensa mara moja tu kila baada ya miaka 10....na bado watu wanaona maswali mengi! Issue hapa ni maswali ya msingi, yatasaidia kutambua ukubwa wa mahitaji ya msingi, by the way...huhitaji haya certificate ya darasa la 7 kuyajibu!
Ni kweli. Maswali ya kawaida sana ni madodoso muhimu kufahamu mambo ya kiuchumi katika kaya husika. Ukijumlisha na teknolojia sasahivi baadhi ya maswali hata uliza na pia mengine hayatahusika kwa kila mtu.

Hofu iliyopo ni je taarifa hizo zitatumika kwa nia njema ya maendeleo au ni zaidi ya hapo.
 
Mkuu acha kutukana watendaji wa hii nchi.
Hapana hiyo ni moja ya tathimini/majawabu katika mengi maswali-Kwanini Africa na baadhi ya nchi dunia y a tatu tu maskini sana na tunakwenda kwa mwendo wa konokono kuyafikia "Maendeleo".
 
Ni kweli. Maswali ya kawaida sana ni madodoso muhimu kufahamu mambo ya kiuchumi katika kaya husika. Ukijumlisha na teknolojia sasahivi baadhi ya maswali hata uliza na pia mengine hayatahusika kwa kila mtu.

Hofu iliyopo ni je taarifa hizo zitatumika kwa nia njema ya maendeleo au ni zaidi ya hapo.
Kwa hali inavyoendelea wengi hawatahesabiwa kama ilinyopangwa!
 
Uko sahihi mkuu mimi nimejibu yasiyopungua matano kwanza serikali inataka kujua elimu elimu ya wanangu ili iweje iwapo haikuusika na karo wala mkopo wa elimu ya juu? Hali ya mahusiano yangu na mke wangu ili iweje? Maswali ya kijinga siweziyajibu mie
 
Uko sahihi mkuu mimi nimejibu yasiyopungua matano kwanza serikali inataka kujua elimu elimu ya wanangu ili iweje iwapo haikuusika na karo wala mkopo wa elimu ya juu? Hali ya mahusiano yangu na mke wangu ili iweje? Maswali ya kijinga siweziyajibu mie
😁😁😁 Labda serikali inataka kutoa ushauri nasaha!
 
Swali namba 59.
Una mtaji wa Shilingi ngapi na uliutoa wspi?
Hili swali watapewa majibu ya uongo tupu
..Wewe ni Alibino?....Jamani! Karani SI ananiona Kabisa kwamba Mimi ni Mweusi tii...Kushinda Giza!!
 
Back
Top Bottom