Kwa miezi 12 sasa moyo wangu unateketea. Nahisi huyu Mtoto sio wangu

Kwa miezi 12 sasa moyo wangu unateketea. Nahisi huyu Mtoto sio wangu

Bush Dokta

JF-Expert Member
Joined
Apr 11, 2023
Posts
24,831
Reaction score
45,154
Wakuu mganga hajigangi, mimi kama Bush Dokta sio dokta wa mauzauza bali ni dokta Herbalist yaani wa mitishamba.

Sasa nina mtoto amezaliwa miezi 12 iliyopita. Mimi ni mweusi Tii, Mama ni maji ya kunde ila mtoto amekuwa maji ya kunde zaidi ya Mama yake.

Hata kama mimi sio msomi wa sayansi kubwa lakini naamini mchanganyiko wa mbegu nyeusi na maji ya kunde lazima ije zao ya kati kati.

Sasa nikawa najipa muda labda atabadilika kadiri muda unavyosonga lakini wapi ndio kwanza anazidi kuwa white. Sasa kuna siku Mama kaja kutembea na kumuona mtoto akiwa na kama miezi miwili hivi.

Nikiwa nimelala ndani nikasikia Mama anahoji Mke wangu akimuuliza kama stori tu kuwa huyo mjukuu anafanana na nani mbona ana kiwaraza? Mimi sina na mama yake hana. Tena akahoji mbona mweupe sana?

Ni kama kulikuwa na mahojiano serious ikafika mahali akamuuliza leta picha za wajomba zake tuone.

Hapa inaonekana Wife alimwambia anafafanana ujombani. Mama alimkomalia ndio wife akaja ndani kuniuliza kama nina picha za shemeji zangu kwenye simu. Nikamwambia sina basi ikaishia hapo.

Niliendelea kuwaza na kuwazua. Nikifikiria nimefanya uwekezaji mkubwa kwenye familia yangu na msimamizi amekuwa yeye siku zote.

Sijawahi mwambia ila tangu hapo sina hamu naye kabisa. Ni miezi 12 sasa. Hata uwezo wangu wa kuchapa kazi sasa unapungua nina stress kiasi.

Nimejaribu kuvumilia nimeona nije hapa nipate mawazo mawili matatu nianzie wapi?
 
Wakuu mganga hajigangi mimi kama Bush Dokta sio dokta wa mauza uza bali ni dokta Herbalist yaani wa mitishamba.

Sasa nina mtoto amezaliwa miezi 12 iliyopita....

Mimi ni mweusi Tii, Mama ni maji ya kunde ika mtoto amekuwa maji ya kunde zaidi ya Mama yake.

Hata kama mimi sio msomi wa sayansi kubwa lakini naamini mchanganyiko wa mbegu nyeusi na maji ya kunde lazima ije zao ya kati kati.

Sasa nikawa najipa muda labda atabadirika kadiri muda unavyosonga lakini wapi ndio kwanza anazidi kuwa white.

Sasa kuna siku Mama kaja kutembea na kumuona mtoto akiwa na kama miezi miwili hivi.

Nikiwa nimelala ndani nikasikia Mama anahoji Mke wangu akimuuliza kama stori tu kuwa huyo mjukuu anafanana na nani mbona ana kiwaraza? Mimi sina na mama yake hana. Tena akahoji mbona mweupe sana?

Ni kama kulikuwa na mahojiano serious ikafika mahali akamuuliza leta picha za wajomba zake tuone.

Hana inaonekana Wife alimwambia anafafanana ujombani.
Mama alimkomalia ndioo wife akaja ndani kuniuliza kama nina picha za shemeji zangu kwenye simu.

Nikamwambia sina basi ikaishia hapo.

Niliendelea kuwaza na kuwazua.
Nikifikiria nimefanya uwekezaji mkubwa kwenye familia yangu na msimamizi amekuwa yeye siku zote.

Sijawahi mwambia ila tangu hapo sina hamu naye kabisa.
Ni miezi 12 sasa. Hata uwezo wangu wa kuchapa kazi sasa unapungua nina stress kiasi.

Nimejaribu kuvumilia nimeona nije hapa nipate mawazo mawili matatu nianzie wapi?
Mama yako ana usahihi wa 98% na mashangazi pia.
Inawezekana mtoto sio wako, nakushauri kapime DNA uache mashaka na kukisia.
Ikigundulika sio wako mpeleke huyo mtoto Kwa baba yake, kama hujamuoa huyo mwanamke, piga chini mapema sana.
Afya yako ya akili ni muhimu na Taifa inakutegemea.
 
Back
Top Bottom