Kwa muda mrefu ujao Tanzania haitaweza kupata maendeleo ya maana

Kwa muda mrefu ujao Tanzania haitaweza kupata maendeleo ya maana

Fumadilu Kalimanzila

JF-Expert Member
Joined
Dec 10, 2016
Posts
1,770
Reaction score
5,423
Nimejaribu kuichunguza Nchi yetu inavyoongozwa na mikakati tuliyonayo najiridhisha kuwa ni vigumu sana kupata maendeleo ya maana hata kwa miongo mitatu ijayo yaani comes 2050!
Sababu zangu ni hizi;

1. Elimu yetu ni duni sana kwa maana ya maudhui (contents) na inazalisha watu wenye maarifa madogo sana ambao hawajitambui na wasio na uwezo wa kuona mbali.

2. Viongozi wetu walioko katika nafasi za uongozi katika taasisi mbalimbali wana maarifa madogo sana (sisemi hawana vyeti) na hawana uwezo wa kuiangalia Tanzania baada ya miaka 50 au 100 ijayo ambapo tunakadiriwa kuwa na watu zaidi ya milioni 120.

3. Hatuna itikadi ya maana inayotuongoza katika mwelekeo wa Nchi yetu na viongozi wengi hawalijui hili ndo maana unaweza kukuta leo mwanasiasa huyu yuko chama hiki na kesho amehamia chama kile na unaona kabisa hakuna anachokiamini au kukisimamia ni bora kunakucha na ugali wake unaupata basi!

4. Tumezidiwa maarifa na mataifa yenye nguvu kiasi kwamba sasa wanatupangia hadi ni vitu gani tunapaswa kuvifikiria.Nguvu kazi ya Taifa (hasa vijana) haiko katika uzalishaji iko katika ku-bet na kujadili mambo ambayo hawana uwezo wa kubadili chochote kama mipira inayochezwa ulaya n.k.

5. Tumeshindwa kujenga mifumo imara inayoweza kujiendesha yenyewe bila kuingiliwa na watu wenye nia mbaya au malengo binafsi.
 
Dah umeniharibia siku kabsa Uzi wa Kwanza kufungua una kitimoto...

Linchi hili Nyerere alikosea Sana kujimegea maeneo mengi linchi likubwa with lack of visionable leaders..
Wazungu sio mafala kujigawa vi nchi vidogo vidogo , Sisi tung'ang'ania kuwa li nchi likubwa ambalo ni useless, Raisi atokee namtumbo huko hawez kumthamini mtu wa Namanga hata iweje , two different ethnic group , na hii ni nature ...!!
 
Tutachelewa kupata maendeleo kwa sababu ya watu kama nyinyi manaoishia kuona tatizo na kulalamika badala ya kutoa suluhu ya namna ya kutatua Hilo tatizo, shame on you
wasukuma wana msemo wao: kiongozi wa msafara akikosea njia basi wote walio nyuma yake hupotea njia pia. nadhani kuna makosa yalifanyika tangu tarehe 9 Disemba 1961.
 
Katiba inawaruhusu viongozi darasa la saba watunge sheria, viongozi wanateuliguliwa na rais kwa hisani, bila kujali uwezo, hivyo wanamtumikia rais. What do we expect?
 
Uko sahihi brother, we tunatakiwa kujitathmini kwa dhati ili kuijenga nchi yetu kiukweliukweli
 
Waafrika tuna roho mbaya sana.
Ndiyo maana nasema kila siku kujitawala tunajitawala ila bado sana, angalia mifumo yetu na mipango.
 
Hapo kwenye namba 3 ndio panakatisha matumaini kabisa, kwa sababu wale wanasiasa ambao ndio pengine tunategemea watakuwa ni mbadala wa viongozi hawa waliyotufikisha hapa ila unakuta wao nao hawana dira hawaeleweki wanasimamia nini. Huwezi ukawa na matumaini ya mabadiliko kupitia wanasiasa hao hawana tofauti sana na viongozi tuliyonao sasa.
 
Wazungu sio mafala kujigawa vi nchi vidogo vidogo , Sisi tung'ang'ania kuwa li nchi likubwa ambalo ni useless, Raisi atokee namtumbo huko hawez kumthamini mtu wa Namanga hata iweje , two different ethnic group , na hii ni nature ...!!
Ni ujinga ujinga mtupu na ubatili mtupu..

Huwa najiuliza tutatumia miaka ngapi kupita stage of development km walizopita UK & USA..Yaan naona mpk Sasa hatufika initial stage...hata ukipitia MPANGO PLAN WA TAIFA upo kisiasa siasa ndio Mana kila Rais akiingia hutenda apendalo..

Kiufupi tuna safari ndefu...
 
Katiba inawaruhusu viongozi darasa la saba watunge sheria, viongozi wanateuliguliwa na rais kwa hisani, bila kujali uwezo, hivyo wanamtumikia rais. What do we expect?
Ajabu kuna watu walikuwa wanajenga hoja kwamba Samia avunje baraza la mawaziri ili kusiwe na mawaziri ambao hawajaapa kwake Samia kana kwamba hao mawaziri wanafanya kazi binafsi za Samia.
 
Tutachelewa kupata maendeleo kwa sababu ya watu kama nyinyi manaoishia kuona tatizo na kulalamika badala ya kutoa suluhu ya namna ya kutatua Hilo tatizo, shame on you
hivi ni suluhu gani utaitoa kama wewe si sehemu ya watunga sera.makazini ukiwa na msimamo unatafutiwa kosa ili wakufukuze kazi kwa kweli nchi hii haina ambao visionary .mfano rahisi angalia bungeni mambo yanayofanyika halafu wewe unasema toa suluhisho,unatoa wapi na kwa nani.kwani issue ya mandege watu wengi walishauri lkn nani alikubali ushauri huo.hapakuwa na bajeti ya ngege lkn zilinunuliwa.
 
Huo ndio ukweli, tutaendelea kupiga mark time kwa muda mrefu sana.
 
hivi ni suluhu gani utaitoa kama wewe si sehemu ya watunga sera.makazini ukiwa na msimamo unatafutiwa kosa ili wakufukuze kazi kwa kweli nchi hii haina ambao visionary .mfano rahisi angalia bungeni mambo yanayofanyika halafu wewe unasema toa suluhisho,unatoa wapi na kwa nani.kwani issue ya mandege watu wengi walishauri lkn nani alikubali ushauri huo.hapakuwa na bajeti ya ngege lkn zilinunuliwa.
Anza kwa kubadili mtazamo wako kuhusu hayo matatizo kisha shirikisha watu wako wa karibu wanaokuamini na kuheshimu mawazo yako. Duniani kote watu walioleta mabadiliko walianza kubadilika wenyewe kabla ya kubadili jamii yao
 
Mkuu umegusa kwenye kidonda lazma watu tuchuchumae
emoji38.png
huu ndio ukweli mchungu kusema ukweli.. vijana ambao ndio nguvu kazi ya Taifa siku hizi tumehamia kwenye betting, dah lazima tujiulize tatizo hasa ni nn??? Lkn Serikali inafurahia kwakuwa inaingiza Pato kubwa sana sekta hiyo hali ya kuwa inawaacha vijana wakiwa hohe hahe yaani mchochole fukara na masikini wa kutupwa. Let's think on this fellaz.
 
Hayo yote ni CCM usijumuishe watu wengine.

CCM ni mzawa ambaye kila jambo limemshinda unatambua tabia ya mzawa .

Nenda hizo sehemu ndio utaelewa kuwa mzawa yupo hivi
 
Back
Top Bottom