Kwa mujibu wa Standing Orders, DAS ni mtumishi wa Umma

Kwa mujibu wa Standing Orders, DAS ni mtumishi wa Umma

Hapana kiongozi HAUPO SAHIHI. Katiba inamruhusu Rais kumteua mtanzania yeyote katika cheo ambacho Rais anateua, mfano mnenguaji wa bendi, Dj , Hawala, au mchezaji wa mchezo wowote anaweza kumteua kuwa mkuu wa wilaya au katibu tawala ili mradi tu AONE INAFAA
 
Hapana kiongozi HAUPO SAHIHI. Katiba inamruhusu Rais kumteua mtanzania yeyote katika cheo ambacho Rais anateua, mfano mnenguaji wa bendi, Dj , Hawala, au mchezaji wa mchezo wowote anaweza kumteua kuwa mkuu wa wilaya au katibu tawala ili mradi tu AONE INAFAA
umesema mwenyewe katika cheo ambao rais anateua!mimi nimeleta miongozo,wewe umeleta nini?
 
Mkuu Sunzu shukran sana kwa kuweka nondo penyewe. Lakini ujue hali halisi ya nchi ni kuwa kauli na uamuzi wa rais ndio sheria kuu ya nchi. Yeye ndiyo anajua kilicho bora kwa nchi. Bila shaka huwa unasikia wengi wakijieleza wanatekeleza matakwa ya rais - sio sera, sheria wala katiba. Si kuhusu madawati, elimu bure, kulipa kodi, kuanzisha viwanda, n.k.

Hivyo, usipoteze sana muda na vilivyo katika makaratasi labda kwa kutaka kutuelimisha kama ulivyofanya hapa. Tuna safari ndefu sana kufikia mfumo wa utawala unaoenda kwa sheria na kanuni maalum badala ya kutegemea utashi wa mtu binafsi.
 
Hivi mmesahau kuwa wakati wa kampeni mahali fulani mkuuu wa kaya aliwaomba wana CCM wasigombane kwenye kura ya maoni kwani akishinda urais kazi zipo nyingi tu kwani yeye ndie atakuwa mkuu wa kaya?
 
Mkuu Sunzu shukran sana kwa kuweka nondo penyewe. Lakini ujue hali halisi ya nchi ni kuwa kauli na uamuzi wa rais ndio sheria kuu ya nchi. Yeye ndiyo anajua kilicho bora kwa nchi. Bila shaka huwa unasikia wengi wakijieleza wanatekeleza matakwa ya rais - sio sera, sheria wala katiba. Si kuhusu madawati, elimu bure, kulipa kodi, kuanzisha viwanda, n.k.

Hivyo, usipoteze sana muda na vilivyo katika makaratasi labda kwa kutaka kutuelimisha kama ulivyofanya hapa. Tuna safari ndefu sana kufikia mfumo wa utawala unaoenda kwa sheria na kanuni maalum badala ya kutegemea utashi wa mtu binafsi.
umenipatia ushauri mzuri,i admit
 
Sijawahi kuona nafasi ya DAS ikitangazwa magazetini. Hao waliokuwepo walipatikanaje? Kama waliteuliwa, basi uteuzi ni uteuzi tu. Mtu anaweza kuteuliwa kutoka nje akaingia kwenye utumishi wa umma. Sidhani kama sheria inamzuia mteuaji kuwa lazima ateua miongoni mwa watumishi wa umma. Labda hilo ndo ulitakiwa kuliweka wazi. Hata hivyo sikuwahi kuona nafasi ya DAS au RAS ikitangazwa kwa ajili ya kupata watu wa kuajiriwa ngazi hiyo!!
 
hata hivyo hongera sana mkuu kwa kupata uDAS,muombe Mungu jamaa wasijishtukie,wazibe masikio la sivyo watakutengua.Makosa yaliyofanywa kwa Amoni hajawezi kuhalalisha makosa ktk uteuzi wako.Usitulaumu sisi,laumu kanuni na sheria
Umeishiwa hoja sasa unaanza kuhisi hisi watu hovyo. Maswala ya huyu ni fulani hayaruhusiwi hapa JF. Rudi kasome kanuni ambazo tumejiwekea hapa jukwaani.
 
Ukiachilia standing order Kuna muundo wa utumishi (scheme of service) ambao unaainisha sifa na vigezo vya kushika nafasi husika. To the best of my knowlede uteuzi wa baadhi ya Ma DAS akiwemo: Siyantemi, Casilida, Mtera, Asenga na wengine wenye kufanana na hao kama wapo ni batili kwa mjibu wa muundo wa utumishi


Ingeleta Maana sana wale wakurugenzi wa halmashauri walioteuliwa U-DC Hivi karibuni wakashika nafasi za U-DAS alafu hawa Vijana wakapewa U-DC

Tukiwaruhusu wanasiasa wakaharibu taratibu za utumishi wa umma tutakwama tu kama nchi.
 
Sijawahi kuona nafasi ya DAS ikitangazwa magazetini. Hao waliokuwepo walipatikanaje? Kama waliteuliwa, basi uteuzi ni uteuzi tu. Mtu anaweza kuteuliwa kutoka nje akaingia kwenye utumishi wa umma. Sidhani kama sheria inamzuia mteuaji kuwa lazima ateua miongoni mwa watumishi wa umma. Labda hilo ndo ulitakiwa kuliweka wazi. Hata hivyo sikuwahi kuona nafasi ya DAS au RAS ikitangazwa kwa ajili ya kupata watu wa kuajiriwa ngazi hiyo!!
nafasi ya DAS haitangazwi ni nafasi ya uteuzi. Ila mpaka ufikie kuteuliwa Kuna vigezo ambavyo Lazima uwe navyo kwanza ikiwa ni pamoja na kuwa mtumishi wa umma. Usiliangalie hili kwa mtazamo wa kisiasa hapa Kuna kosa la kikanuni limefanyika
 
Baadhi yetu tumekuelewa sana...pongezi kwa ufafanuzi uliotoa hapa...Hapa mimi nimeshangazwa mno...lakini mimi naishia kushangaa tu...kilichotokea ni HATARI...Nadhani wamedhamiria kumhujumu Rais...Ni kitu cha ajabu kimefanyika...
Muelimishe na " lizaboni' naona bado kalala
 
nafasi ya DAS haitangazwi ni nafasi ya uteuzi. Ila mpaka ufikie kuteuliwa Kuna vigezo ambavyo Lazima uwe navyo kwanza ikiwa ni pamoja na kuwa mtumishi wa umma. Usiliangalie hili kwa mtazamo wa kisiasa hapa Kuna kosa la kikanuni limefanyika

Siasa mbali na mimi. Hiyo kanuni inayosema kuwa mtu kabla ya kuteuliwa kuwa DAS ni lazima awe mtumishi wa umma kwanza ndo hujaiweka hapa. Ukiangalia pale penye qualifications ulizoziweka hapo juu hakuna mahali pamesemwa kuwa lazima huyo mtu awe ameshakuwa mtumishi wa umma kwa kipindi kadhaa au at all.
 
Hivi Amon Mpanju amewahi kuwa mtumishi wa umma!? Mbona uteuzi wake kuwa naibu katibu mkuu wa wizara ya sheria na katiba haukupigiwa kelele namna hii!? Ni nani asiyejua kuwa Mpanju ni mwanaCCM mtiifu na alishiriki kwenye mchakato wa kura za maoni katika kuusaka ubunge jimbo la Kawe kupitia tiketi ya CCM. Tuache double standards.
Mkuu kote ni mchemsho tu hata kwa huyo mpanju. rais anavunja sheria , kanuni kwenda mbele.
 
nafasi ya DAS haitangazwi ni nafasi ya uteuzi. Ila mpaka ufikie kuteuliwa Kuna vigezo ambavyo Lazima uwe navyo kwanza ikiwa ni pamoja na kuwa mtumishi wa umma. Usiliangalie hili kwa mtazamo wa kisiasa hapa Kuna kosa la kikanuni limefanyika

Madaraka ya rais wa Jamhuri kwa mujibu wa katiba iliyopo hayana mipaka. Anao uwezo wa kumfanya mtu yeyote ambaye hakuwahi kuwa mtumishi wa umma - kuwa mtumishi wa umma. Kisha akamteua kwenye nafasi yoyote anayoitaka. Angalia kuna precedence kibao tu huko nyuma ambako watu wametokea nje ya kazi za umma wakateuliwa kuchukua nafasi ambazo wengi tulitarajia watu wapande kuzifikia. Hilo sioni kama ni jipya! Aliowateua wote wana qualifications? Sidhani kama unaweza kutumia sheria kupinga uteuzi wa rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania na ukashinda; iwe mahakamani au kwenye vyombo vya habari!!
 
Hv ni nani hata hivyo anaweza kuthibitisha kuwa huyo mteule hakuwa mtumishi wa umma?Mtu aweza kuutumikia umma kwa namna nyingi.Unaweza kumwona n mvuvı, mkulima,mchuuzı,mzururuji n.k lakn akawa bado n mtumishi wa umma.
Teh teh the mkuu naona umebanwa kila upande unatafuta pa kutokea. Kubali wamechemsha hapa.
 
Naomba kunukuu Para A1 (21) ya Standing Orders ya 2009 kama kanuni za kudumu za Utumishi wa Umma........inasema "District Administrative Secretary" means a public servant in-charge of administration in a district; Ikimaanisha kuwa ni mtumishi wa umma atakayewajibika na shughuli za kiutawala ofisi ya Mkuu wa Wilaya.....Kwa kifupi kabisa huyu ni mtumishi wa umma ambaye upatikanaji wa upo wazi kabisa.

Mtumishi wa umma hateuliwi, mtumishi wa umma anapatikana katika namna ya ushindani ambapo mamlaka ya serikali iwe ni utumishi au mamlaka nyingine, hutangaza nafasi na zifa za mwombaji huanishwa. Usaili hufanyika na uchambuzi wa majina kwa mujibu wa vigezo hufanyika na hatimaye washindi huitwa kazini na kuwa watumishi wa umma ajira ya kudumu ''Permanent and Pensionable''.........

Sasa kati ya watumishi hao wa umma kulingana na sifa huteuliwa kuwa ma-DAS ambao ni Makatibu Tawala wa Wilaya ambao kimsingi majukumu yake ni kufanya shughuli za kiutawala katika ofisi ya mkuu wa wilaya.DAS huwa chini ya ofisi ya RAS-Katibu Tawala wa Mkoa.
Hivyo basi uteuzi wa DAS ni kama ulivyo uteuzi wa DED/MD/TEC Mkurugenzi wa Halmashauri, ni lazima awe mtumishi wa umma kwanza. Hii sio nafasi ya kisiasa.
Nimeonelea nitoe ufafanuzi huu baaada ya kuona jambo la ajabu sana kutokea jioni ya leo. Hatimae siasa zinanajisi utumishi wa umma. Tunaona Mwanasiasa Mtela Mwambamba na wenzake ghafla wameteuliwa kuwa ma-DAS. Sina hakika sana na wengine lakini ni dhahiri shahiri Mtela Mwampamba sio mtumishi wa umma.
Tunajua haja yenu ya kulipa fadhila makada, tunajua mnawarundika pale Ubungo ili kuikomoa UKAWA na Saidi Kubenea lakini kwa namna mnayofanya ni wazi mnaleta aibu kubwa sana. Tafadhalini fuateni utaratibu.

Naitaka mamlaka iliyomteua Mtela na wengine ambao hawakuwa watumishi wa umma itengue mara moja au itoe ufafanuzi ni kwa mazingira gani uteuzi umezingatia taratibu za kupatikana kwa watumishi wa umma

Nachosisitiza hapa ni kwamba KATIBU TAWALA WA WILAYA HUTEULIWA LAKINI NI LAZIMA AWE MIONGONI MWA WATUMISHI WA UMMA

KWA MUJIBU WA MUONGOZO-JOB DESCRIPTIONS FOR THE REGIONAL ADMINISTRATION YA 2011/2012 ILIYOTOLEWA NA TAMISEMI

EXPERIENCE

Preferably 10 years of working experience

PURPOSE OF THE JOB
The purpose is to coordinate and provide overall administration of District Commissioner’s Office necessary for assisting the District Commissioner in performing all administrative support services to LGAs and other institutions within the District.

MAIN ACTIVITIES

1. To advise the DC in performing statutory, delegated and other official functions.
2. To head the district administration and act as the warrant holder and collector of revenue in the District Commissioner’s office.
3. To supervise the implementation of administration and human resources management policy and other Acts pertaining to administration and human resources management in the District Commissioner’s office.
4. To facilitate the actual provision of employee benefits and welfare services.
5. To prepare expenditure and revenue estimates for the District Commissioner’s office.
6. To serve as assistant registrar for birth and death.
7. To assist the DC in conduct marriage ceremonies.
8. To coordinate implementation of ethics and value promotion activities including corruption prevention education.
9. To coordinate implementation of open performance review and appraisal system (OPRAS) in the District Commissioner’s office.
10. To coordinate disciplinary matters in the District Commissioner’s office.
11. To coordinate and actually assist in administering relief and disaster management activities including but not limited to rescue services, restoration and keeping of relevant records.
12. To oversee complaints and grievance handling; to assist the DC in disputes arbitration.
13. Responsible for matters pertaining to protocol affairs.
14. Any other relevant duty assigned to him or her from higher authorities.

QUALIFICATION
Preferably Degree of Masters or equivalent qualification from a recognized academic institution

KNOWLEDGE

The incumbent must have proficient knowledge in the doctrine of rule of law, good governance and principles of natural justice; human resources management; performance review methods and techniques; staff training, development and recognition; delegation; mentoring and coaching; and an understanding of relevant legislations, policies and procedures.

SKILLS

The incumbent must demonstrate the leadership and supervisory skills; team building skills; problem solving skills; basic counseling skills; negotiations skills; computer skills including the ability to operate spreadsheets and word processing programs; effective verbal, listening and written communications skills including the ability to prepare reports, proposals, policies and procedures; effective public relations and public speaking skills; research and program development skills; stress management skills; interviewing skills and; time management skills.

mkuu nilipoisoma hii post yako, nikamkumbuka Rev Mtikila (rip). yule bwana alikuwa sometimes ni nuisance kwenye opposition camp lakini nilipenda alivyokuwa anautumia mhimili wa mahakama in a very effective way.

I think it's time opposition waunde jopo la kudumu la wanasheria ambao jukumu lao liwe consistently kuzi-challenge all these illegal and illegitimate actions za serikali kupitia mhimili wa mahakama. some of those cases will be lost but am sure a sizeable number are likely to be won.
 
Madaraka ya rais wa Jamhuri kwa mujibu wa katiba iliyopo hayana mipaka. Anao uwezo wa kumfanya mtu yeyote ambaye hakuwahi kuwa mtumishi wa umma - kuwa mtumishi wa umma. Kisha akamteua kwenye nafasi yoyote anayoitaka. Angalia kuna precedence kibao tu huko nyuma ambako watu wametokea nje ya kazi za umma wakateuliwa kuchukua nafasi ambazo wengi tulitarajia watu wapande kuzifikia. Hilo sioni kama ni jipya! Aliowateua wote wana qualifications? Sidhani kama unaweza kutumia sheria kupinga uteuzi wa rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania na ukashinda; iwe mahakamani au kwenye vyombo vya habari!!
Basi ni hatari sheikh wangu manake rais anaweza kulala akaamka na kumtangaza rafiki yake kuwa jaji mtu ambaye hana utaalamu wa sheria huoni kwamba hiyo ni hatari? Tufuate miongozo jamani kuendesha nchi kwa akili zako tutakuja kujuta.haya
 
Umeishiwa hoja sasa unaanza kuhisi hisi watu hovyo. Maswala ya huyu ni fulani hayaruhusiwi hapa JF. Rudi kasome kanuni ambazo tumejiwekea hapa jukwaani.
kanuni zimezingatiwa,sijakutaja jina na pia sijakuhisi!ID yako sio fake ID,teh teh,nakuona umeanza kuwa smart,ktk maandalizi ya uDAS
 
Back
Top Bottom