Kwa muktadha huu "URAIS" ni wa CCM 2015...

Kwa muktadha huu "URAIS" ni wa CCM 2015...

AshaDii frankly speaking I thought you were smart to post your thread here were partisanship is less pronounced................I am really beginning to smell the roses and it is sounding like X-MAS............CDM will not steal a victory because we are really tired by their lies and shoutings..................what they have refused 2 acknowledge is: we have sharp ears that can not stand nonsense............
 
Unaweza ukarudia kusoma ulichoandika hapo? Umeandika kwa sababu ya kuandika au unadata zake? Hata bila kuzunguka vijijini unaweza ukajiuliza kama kweli hao wananchi wa kijijini unaowazungumzia,tena bila ridhaa yao, kama kweli wanamaisha ya " kujitosheleza(pa kulala, chakula na nguo) " kwa nini kila siku wanakimbilia mijini hasa dsm wakati wamejitosheleza?

Kwenye kijani hapo - kwanza tukubaliane kwamba wananchiwa vijijini kwa ujumla wao wanajitosheleza katika mahitaji ya msingi i.e. vijijini, mfumo wao upo dominated na subsistence economy; Tukija kwenye suala la pili sasa kuhusu kwanini wengi wanakimbilia mijini, huo ni mjadala mwingine kwani hao sasa wanageuka kuwa wapiga kura wa mijini, hivyo hatuna haja tena ya kuwajadili in the equation per asha dii's argument kuhusu mwenendo wa wapiga kura vijijini ambapo hadi sasa as we speak, not less than 70% ya watanzania bado wanaishi huko;

Anyway sina imani katika demokrasia hasa hii ya kiafrika, warudi CCM au waje CHADEMA hakuna jipya watakaloleta hawa wanasiasa, Tanzania yetu hii ni kama jamii ya kwenye allegory of the cave ya Plato, watu wasiojua kusoma na kuandika (wajinga), nchi inayozalisha sifuri nyingi kwenye mitihani, wananchi wanaoshinda kusoma udaku na ushabiki wa vyama vya siasa wana uwezo wa kufanya maamuzi sahihi kweli?

Naunga mkono hoja, lakini muhimu zaidi ni kwamba kwa bahati mbaya haya hayawezi kubadilika ndani ya miaka mitatu, hence uzito wa hoja ya asha dii katika bandiko namba moja kule juu; je, kwa mtazamo wako, hali hii tunaweza kuibadilisha ili watanzania wafanye maamuzi ya maana ya kujileletea mabadiliko ya kweli, suala ambalo EMT hapo juu (tazama bandiko namba 14) amepinga kwamba haliwezi kutokea 2015? Binafsi naunga mkono hoja ya EMT, na naomba nieleweke kwamba haina maana kwamba naishabikia, bali naiunga mkono kwamba kwa mtazamo wangu, ipo sahihi;
 
Mkuu Mchambuzi, kumbuka ni mbinu ya CCM kufanya wapiga kura watokee wachache. Lakini lingine, ni vyombo hivyo hivyo vya CCM ndio vinakuambia wapiga kura walikuwa wachache hata kama walikuwa wengi.
 
Well....!
Sidhani kama nilitegemea uchambuzi wa tofauti sana toka kwako Bi. Asha hasa linapokuja suala la CDM.....

Ok sitaki kwenda sana huko ila baada ya kuwa nimewasoma sana wachambuzi wengi wa masuala ya kisiasa hapa JF na kwingine huko, nataka nianze na wewe kwa swali dogo tu. Wewe nafasi yako ni ipi katika "mabadiliko" au vyovyote itakavyokuwa hapo 2015??

Kwa kulifafanua zaidi swali, ngoja niliweke hvi katika ule usemi wa "changes ni mimi na wewe, Twaweza" nafasi yako ni ipi kuelekea hiyo 2015? Hichi ndio kitu cha maana zaidi kuliko vingi mtu anaweza kukujibu, kama we huamini katika mabadiliko hayo ni vipi utayaona kwa wewe kuwa sehemu ya mabadiliko? Au ukiwa umekata tamaa kama EMT, ni nini utaona?

Hizo ni pembe mbili zinazotosheleza kuwatoa kwenye uwanja wa mapambano. Sio haki kuyajadili mabadiliko ambayo wewe sio mpambanaji wake. Baada ya kuonja aina mpya ya uchambuzi wa masuala ya siasa za kwetu nimeona kitu cha tofauti sana,
nimesoma maandiko ya Samson Mwigamba na baadae nkasoma maandiko ya Anserbeth Ngulumo. Wote ni wanaharakati na viongozi wa CDM katika mikoa yao, nilichojifunza kwao ni kwamba hao ni watu wanaoueleza ulimwengu kile walichokuwa wanakisikia ila sasa wanakifanya, jinsi wanavyoshiriki kujenga mabadiliko ambayo wengine mnayatarajia kuyapima tu.

Kwenye andiko la majuzi Ngulumo alikuwa akiwapongeza makamanda wenzake wa huko kijijini kwake jinsi walivyofanikisha ushindi wa CHADEMA kwa vitongoji vya kwao huko, alieleza mengi na mpaka mwenzao mmoja aliuawa katika mapambano ila mwishoni CDM ilishinda karibu asilimia 80 au zaidi ya viti vya vitongoji huko Bukoba vijijini sijui wilaya gani hasa.

Na kuhusu Samson Mwigamba, ni mwenyekiti wa CDM mkoani Arusha, miongoni mwa hadithi yake ya kusisimua ni mjadala aliowahi kuwa nao na Mwanakijiji juu ya uchaguzi wa Arumeru Mashariki, masisimuo yanapatikana kwa majibu ya Mwigamba anavyoelezea mchezo wa siasa unavyochezwa na jinsi gharama wanazoziingia katika kugharamia hayo mabadiliko ambayo watu mnakuja kuyapima.

Kwanini nimewataja watu hao??

Hiyo ni mifano yangu binafsi (inayonivutia mimi) kujitosheleza kusema kuwa ufike wakati kila mtu kwa nafasi yake aziishi harakati halisi kuelekea mabadiliko tunayoyategemea. Leo wamejitwisha ufundi wa kuchambua na kukosoa masuala mbalimbali lakini mwishoni anajifanya neutral au ameficha gamba lake la CCM!

Sasa katika namna hyo tutajadili mabadiliko kweli?

Kwa kufupisha maneno mengi ninachotaka kusema ni kuwa Tanzania/Tanganyika ni yetu sote either uwe huna chama au hupendi siasa na wanasiasa, ni ukweli kuwa nchi yetu ina hali mbaya sana kama alivyosema EMT, hvyo suala la mabadiliko ni la lazima ili kuinusuru nchi yetu kuangamia kwenye mfumo ulioifikisha hapa na ni wazi mfumo huu unaipeleka nchi pabaya, hvyo sio sahihi kufikiri suala la kufanya mabadiriko linawahusu CDM peke yao tu, na kuwa kama 2015 CDM ikishindwa basi eti itakuwa imekomoka yenyewe tu (hizi ndio fikra za wengi),

kwa msingi huo tutakuwa tumepotoka sana kama jamii.....

Ni jukumu la kila mtu kucheza nafasi yake kwa vitendo katika kuwa sehemu ya mabadiliko tunayoyatamani wote. Hizi mbwembwe za kuja na chambuzi ndeefu kila kukicha kwenye hzi kurasa na kuta hazitatufaa sana, mabadiliko tunayoyatamani ni makubwa sana kuliko kile tunachofanya kila siku.

Tubadili aina ya uchambuzi tuleteane case study, naelewa sio lazima wote tuwe wanasiasa japo tunajukumu moja la kuleta mabadiliko ya kisiasa kupitia kwenye kada zetu, EMT tupe uzoefu wako unavyopambana na mabadiliko huko kwenye michakato yako sijui ni sheria sijui ni uandishi wa habari, Nguruvi3 tupe harakati zako halisi kutokea huko ulipo, Mchambuzi tueleze uzoefu wako na harakati zako za sasa, kama kuna watu unawajenga wanafanikiwa wapi wanashindwa wapi....

Kila mtu ana nafasi katika kujenga na kufikia hayo mabadiliko tunayoyataka wote, hayo sio mabadiliko ya CDM ila tu kwa baadhi yetu tunaamini tu CDM kama njia au msingi mpya wa kujenga tena kinachobomoka!

Ila narudia tena kushindwa kwa CDM haitakuwa aibu au kukomoka kwa CDM peke yao tu bali kwa kila anayeujua ukweli na aliyetamani mabadiliko fulani katika jamii yetu na hakuchukua na kucheza nafasi yake. Tuache na tupunguze mbwembwe za uchambuzi wa nadharia uliokithiri twende kwenye uwanja wa mapambano kila mtu achukue nafasi yake kujenga dhamira ya mabadiliko na watu wake kuelekea 2015.


CHANGES NI MIMI NA WEWE, TWAWEZA!
 
Last edited by a moderator:
Kwenye kijani hapo - kwanza tukubaliane kwamba wananchiwa vijijini kwa ujumla wao wanajitosheleza katika mahitaji ya msingi i.e. vijijini, mfumo wao upo dominated na subsistence economy; Tukija kwenye suala la pili sasa kuhusu kwanini wengi wanakimbilia mijini, huo ni mjadala mwingine kwani hao sasa wanageuka kuwa wapiga kura wa mijini, hivyo hatuna haja tena ya kuwajadili in the equation per asha dii's argument kuhusu mwenendo wa wapiga kura vijijini ambapo hadi sasa as we speak, not less than 70% ya watanzania bado wanaishi huko;



Habari ya kusema tukubaliane kwamba wananchi wa vijijini kwa ujumla wao wanajitosheleza kwa sababu ya subsistence economy naitilia shaka, ni theory iliyopitwa na wakati, tembelea huko vijijini uone kama hii subsistence economy inaexist.

Quote;
"Naunga mkono hoja, lakini muhimu zaidi ni kwamba kwa bahati mbaya haya hayawezi kubadilika ndani ya miaka mitatu, hence uzito wa hoja ya asha dii katika bandiko namba moja kule juu; je, kwa mtazamo wako, hali hii tunaweza kuibadilisha ili watanzania wafanye maamuzi ya maana ya kujileletea mabadiliko ya kweli, suala ambalo EMT hapo juu (tazama bandiko namba 14) amepinga kwamba haliwezi kutokea 2015? Binafsi naunga mkono hoja ya EMT, na naomba nieleweke kwamba haina maana kwamba naishabikia, bali naiunga mkono kwamba kwa mtazamo wangu, ipo sahihi;
"

Elimu ndio suluhisho la hili, uneducated angry mob wanaweza wakafanya mapinduzi makubwa tu,lakini wakipata madaraka huu utawala unaopigiwa kelele utakua na afadhali!
 
Elimu ndio suluhisho la hili, uneducated angry mob wanaweza wakafanya mapinduzi makubwa tu,lakini wakipata madaraka huu utawala unaopigiwa kelele utakua na afadhali!

Upo sahihi juu ya elimu lakini threat ni kwamba - hawa hawa wakifanikisha kuipa chadema ushindi watakuwa na matarajio beyond the ordinary kwamba maisha yao yatabadilika kwa kasi, na hii itatokana na upeo na elimu yao kuwa ndogo; so mtaji wa Chadema 2015 (iwapo itaenda ikulu) huo huo unaweza kugeuka kuwa mwiba wa chadema 2020, hasa kutokana na chadema kuendelea kuwa weak katika kuelezea umma juu ya mikakati yake ya muda mfupi, wa kati na ujao ili ikienda ikulu, wananchi wawe na subira kwamba matunda ya 'ukombozi' ynayo hubiriwa sio lazima wayafaidi wao bali ni ya watoto wao na wajukuu wao huko mbeleni; faida kwa generation ya sasa ihubiriwe kwamba itakuwa ni ujenzi wa misingi imara pamoja na kufanya reconstruction ya uharibifi uliojitokeza in the past 50 yrs; hivyo ndivyo chadema itakuwa salama baada ya kushinda 2015 (iwapo itashinda), otherwise CCM itakuwa kwenye fence waiting mapungufu haya yajitokeze then umma kuambiwa ' u see, kuongoza nchi sio lele mama, hakuna kitu chadema wanafanya, turidisheni ikulu tumalizie kazi tuliyoanza huko nyuma', na ccm ikirudi 2020 (iwapo itapoteza uongozi 2015), Chadema haitaweza kufufuka tena, chama kitakufa;
 
EMT tupe uzoefu wako unavyopambana na mabadiliko huko kwenye michakato yako sijui ni sheria sijui ni uandishi wa habari,
Nguruvi tupe harakati zako halisi kutokea huko ulipo,
Mchambuzi tueleze uzoefu wako na harakati zako za sasa, kama kuna watu unawajenga wanafanikiwa wapi wanashindwa wapi....

Mkuu jouneGwalu,

Umenena ya msingi sana kwenye bandiko lako namba 24 hapo juu, na umetoa mifano hai sana; Naomba ufahamu tu kwamba wigo wa mapambano unazidi kupanuka, na sote hatukuzaliwa wana ccm au wanachadema bali watanzania;sidhani kama kuna ubaya wa kupambana kwa hoja kwa maslahi ya watanzania nikiwa upande mwingine kwa mtazamo tofauti na upande huo mwingine hasa iwapo sote tunataka kufikia malengo yale yale, huku tukipishana tu njia; ndio maana katika mijadala imngi humu ndani, pamoja na umagamba wangu, huwa tunakubaliana katika hoja nyingi za msingi na upande wa magwanda;

Vinginevyo kwa ufahamu wangu na pia in practice, kutumikia wananchi sio lazima itokane na uongozi wako wa kisiasa, ukiwa na nia, kazi ya kuletea mabadiliko wananchi itafanikiwa tu, and trust me, kazi kubwa inafanyika katika hilo na matokeo yatajitokeza tu, kwani ni kwa wale wenye upeo mdogo tu ndio wanadhania kazi hiyo inaweza kufanikiwa pale tu mtu unapokuwa na madaraka; in actual sense, madaraka ni kikwazo kikubwa sana cha kuletea mabadiliko wananchi kwani ni wachache wanaotumikia wananchi, wengi hutumika na viongozi; kinachotakiwa ni nia na uzalendo, bila ya kujalisha wewe ni mwanachama wa chama cha siasa au ni raia tu mwenye uchungu na pia mapenzi na nchi yako;

Tupo Pamoja;
 
Naungana na AshaDii, kuwa CCM inaweza kushinda tena uchaguzi kwa sabubu zifuatazo-


  • Nguvu nyingi sana za makusudi za kutumia vyombo vya ulinzi na usalama ili kuhakikisha CCM inashinda na inaendelea kukaa madarakani.
  • Kutumia au kufuja fedha nyingi sana kuwapita wapinzani, rushwa, kununua vitambulisho vya kupigia, kutengeneza vitambulisho feki vya kupigia kura vya watu ambao hawa'exist n.k
  • Vyombo vya usalama kuingizwa katika siasa ya kuhakikisha ccm inashinda kwa mbinu yeyote....badala ya vyombo hivyo kulinda wanachi, kulinda mali zao....hivyo kutoa picha kuwa, hali ya umasikini iliopo, hali ya migogoro ya kidini inayo endelea, hali ya kuporwa rasilimali zetu, vyombo hivi vya ulinzi na usalama vinanufaika.
  • Kuwatishia wapiga kura kutojitokeza kwa wingi ya kuwa; siku ya uchaguzi kunategemewa kuwa na vurugu, hivyo kuweka askari wengi wenye uniform na silaa za kivita.
  • Vifaa vya kupigia kura kuchelewa kufika katika maeneo husika, kwa makusudi, hasa zile sehemu zenye ngome kubwa ya upinzani.
  • Kuwakatisha tamaa wapiga kura kwa kuwaambia kumbukumbu za daftari ya mpiga kura jina lake halipo, au zinaonyesha ameshakufa.
  • Tume ya uchaguzi kutokuwa huru, na inatia mashaka kuiamini inapotoa matokeo ya mshindi kama ni ya kweli au laa...tumeona zanbar, cuf walishinda...tume ilitangazaje...hadi leo kuna serikali ya uwk?! Kuna kipindi Zanzbr ilibidi nyerere aende ili yatangazwe tofauti na uhalisia.

Watawala wana kila kitu cha kuwafanya waendelee kutawala kupitia CCM, fedha zipo mikononi mwao, ulinzi na usalama upo mikononi mwao, tume za uchaguzi ni zao, bunge ni lao na wanam'remote tu spika na naibu wake watakavyo, vyombo vya habari wamevishika na vinavyoleta ubishi wanavifungia, mahakama zipo chini yao...nini kimebaki?

My take ni kuwa, until that day watawaliwa tutakapo amua (inaf is inaf) kwa kuandamana nchi nzima dhidi ya dhuluma za viongozi wetu wanaodhani nchi ni mali yao ya mfukoni. Lini sasa wananchi tutaamua kukiambia chama tawala kuwa inatosha, mimi nadhini itakuwa 2015 kama tume itaamua kutoa matokeo tofauti na maamuzi ya wananchi wote.

Mkuu K.Msese,hoja kuwa mabadiliko yatatokea pale tu tutakapo sema enough is enough na kuamua kufanya maandamano nchi nzima siikubali sana,kwani pamoja na rafu za CCM,haijafikia cruelty ya KANU ya Kenya ambayo iliondolewa kwa kura 2007!
Vi wapi vyama tawala vya Zambia,Malawi na Ghana?
Wananchi tukiamua,hakuna linalo shindikana!
 
Last edited by a moderator:
AshaDii;5734117]Maandalizi na mikakati ya kushika Uongozi wa juu wa Serikali huwa ni mzito na wakimahesabu na kwa maandalizi thabiti yaliyo jipanga vyema. Maandalizi hayo hayafanywi kwa siku moja, hayafanywi in Isolation na wala hayawezi fanikiwa kwa kubahatisha. Inahitaji nguvu ya Chama, nguvu ya uongozi wa Chama na kubwa zaidi nguvu ya wanachama ambao ndiyo Umma na ndiyo wana wajibu wa kumweka mtu katika kiti hicho kwa njia ya kura wakati wa Uchaguzi.
Nakubaliana nawe kabisa na kwa kuongezea tu ni pamoja na mikakati ya pamoja yenye lengo moja itakayofanywa kwa pamoja.
KUNDI LA WAPIGA KURA
Historia Kujirudia (hasa ya 2005)
Kuna kila dalili kwamba historia ya 2005 inaweza kujirudia i.e. watanzania wengi watakuwa wamejiandikisha kupiga kura ila wachache watakaopiga kura. Hata hivyo izingatiwe kuwa hili linaweza epushwa ama kupunguzwa kwa kiasi kikubwa kama: Kwanza iwapo Vyama pinzani, Vyombo Vya habari na Wanaharakai wa Demokrasia wataweza kuhamasisha wananchi juu ya umuhimu wa kujiandikisha kwa nguvu zaidi, na Pili ni kwa CHADEMA kuja na candidate mzuri, mashuhuri, mwenye experience ya kutosha ambaye ataweza himili na kushindana vyema na mgombea urais wa chama pinzani
AshaDii tatizo si kujiandikisha. Hebu tufikirie kuwa kama wamejiandikisha watu 100 wakapiga kura watu 30, tunasababu ya kuhamasisha wajiandikishe watu 500! Kinachotakiwa ni kufahamu kwanini hawa 70 hawakupiga kura. Kwa bahati mbaya serikali na CCM wanajua lakini wapinzani hawaonekani kuliona hili kama tatizo. Kunakitu kinaitwa voters suppression. Kule Marekani wakati Obama anaandikisha watu wanaoishi kwa hofu(walatino) Republican wakazuka na mkakati wa kusema Obama anataka kujua akina nani na wapo wapi ili baada ya uchaguzi warudishwe makwao. Hiyo ndiyo voters suppression kwamba waogope kupiga kura.

Kwa upande mwingine Obama alifahamu kuwa watakaoamua uchaguzi si Dmeocrat wala Republican ni hawa waliojificha na hivyo akafanya jitihada za kuwaondoa hofu. Hivyo ndivyo alivyowapiga Republican

Chaguzi chungu nzima zimepita na jambo la ajabu hakuna wapinzani na in fact hawataki kujishughulisha kujua kwanini wajiandikishe watu 100 wapige kura watu 30 na serikali haionekani kushtuka. Kwahiyo si suala la kuhamasisha au kuandikisha ni suala la kutafuta kwanini hawapigi kura
Kutokujifunga kwa wapiga kura
Watanzania wengi ambao ni wapiga kura na wanao kuwa na vitambulisho vya kupiga kura kwa nia hiyo ya kujiandikisha hawapo katika chama chochote
Ni kwasababu vyama vya upinzani havijawa na mkakati wa kuwa na daftari la wapiga kura wao ili kuwafuatilia siku ya kupiga kura.
Obama alikuwa na watu kwa kutumia postal code na siku ya uchaguzi ilipofika wale wazee walioonekana hawawezi mikiki ya usafiri waliandaliwa usafiri kwenda kupiga kura kwa kuwatafuta kwa postal code tu. Je, pamoja na ujima wetu hata daftari la kura wapinzani hawawezi? Nasema wapinzani kwasababu CCM wanayo yao tayari ingawa hayapo hadaharani.
Tunaona CHADEMA nguvu ya kuongeza wapiga kura ipo katika kubanana na hao ambao tayari ni wanachama wa CCM na wale wasio na chama ambao wanawapata pia. Tokana na furaha ipatikanapo pale wanapo faulu kuwavuta wana CCM wengi kuja Chadema inapelekea kuonekana kana kwamba Strategy yao ipo katika kuhakikisha wanachama wa CCM wanahamia CHADEMA badala ya nguvu katika kuhakikisha wanajenga ‘loyalties' kwa kuwavuta wale wasio na chama
Kama hakuna statistic na strategist uwezekano wa kufahamu wapi pa kwenda ni mdogo. Nitolee tena mfano wa Marekani. Obama alifahamu kuwa ili Romney ashinde ni lazima ashinde majimbo ya Ohio na Florida. Hata kama Obama angeyapoteza bado uwezekano wa kushinda ulikuwepo japo kwa ufinyu sana. Alichokifanya ni kwenda Ohio na Florida na kupiga kambi huko na Romney hakuondoka Ohio na Florida. Wakati hayo yakitokea Obama alikuwa na political capital maeneo mengine. As a result alimbana Romney asitoke Ohio na Florida na kumpiga huko huko ingawa alishashinda tena kabla ya Ohio na Florida kutangaza. Huu ndio mkakati wa kisiasa. Unasoma weakness za opponent unazigeuza kuwa mtaji.
Maana yangu hapa ni kuwa wapinzani bado hawana makakati na wanamkakati
Woga wa MabadilikoKura nyingi zipo vijijini, na wengi wao ni CCM ingawa inaenda inapungua na ni kwa sababu sio tu kwa sababu hawana upeo au elimu ya uraia bali by default, watu maeneo ya vijijini huwa ni ‘conservatives'. Hawapendi mabadiliko na ni waoga wa mabadiliko, wapo katika hali mbaya lakini bado wana amini kuwa uongozi mwingine unaweza waangamiza zaidi na kabisa
Kuna ushahidi mzuri tu wa kuonyesha kuwa Tanzania vijijini ya leo si ya jana. Haiwezekani mikoani wakaongoza kutoa wabunge wengi kuliko Dar es salaam. Hii maana yake ni kuwa kule vijijini sasa wanajitambua tena bila woga. Kilolo wanajenga ofisi ya CDM ambapo Ilala na Kindondoni hawawezi. Hali ipo hivyo kule Tarime na kwingineko. Wapinzani hawapaswi kudhani kuwa huko vijijini hakuna kura, ni kosa. Ni kosa hilo ndilo liliwafanya wasi kampeni Lindi na Mtwara leo tunaona kuwa kumbe huko ndiko kungekuwa salama kwao. Kama huna ujumbe mzuri hakuna atakayekuelewa awe mjini au kijijini
KUNDI LA CHAMA CHA MAPINDUZI Kwanza tujiulize ni kwa namna ipi CCM wame survive hadi hapo walipo?! Tuache yote hayo na tuanzie pale ambapo tulipata orodha ya "List of Shame" toka kwa Dr. Slaa, Orodha iliyotikisa na kusababisha viongozi hao wa juu kumaka kumfungulia kesi Dr. Slaa - suala ambalo halijafanikiwa hadi leo. Ile Orodha ilikuwa ni tosha kabisa kuwa hamasa kwa wananchi na wanaharakati kuing'oa CCM kwenye uchaguzi wa 2010. Lakini haikuwa hivyo...
Je, kulikuwa na ujumbe mahususi kwa wananchi? Kwa mwanasiasa makini siku zote huongea kutokana na mazingira. Leo mtu wa Mtwara ukimwambia kuhusu orodha ya mafisadi hatakuelewa kwasababu hiyo si shida yake. Shida yake ni chumvi, sukari na mafuta ya taa.Kama utaweza ku-connect with audience kwa kutumia ufisadi hilo ni jema lakini linahitaji charismatic and orator mzuri. Hivyo hoja hakiuwa orodha, hoja ni je walipokwenda Kigoma waliongelea reli, walipokuwa Songea waliongelea mbolea na walipokuwa sumbawanga waliongelea soko la mahindi?
Na pia inafanya Serikali kutoa maamuzi ambayo kimsingi na kimantiki hayaeleweki; kama vile kuvunjwa kwa POAC. Ukichukulia uzito na umuhimu wa Kamati yenyewe ikiwa ilikuwa inaangalia na kufuatilia asset zenye thamani ya trillion za shilingi, inafanya kuamini kuwa ni mtu asiye na akili tu ndiyo anaweza futa ama kukubali ifutwe LA SIVYO zinatakiwa sababu za Msing sana kuwakilishwa.
Hapa niseme kuwa wapinzani wanashindwa kutumia udhaifu wa serikali iliyopo madarakani na CCM kwa ujumla. Matahalani, wiki mbili zilizopita CDM walikuwa na mkutano kwa kile walichosema ni mahakama ya wananchi. Nilitaraji kuwa hoja ya James Mbatia kuhusu ufisadi wa hela za rada kuhusu elimu ingeelezwa vizuri sana. Kwa maneno mengine walitakiwa wailazimishe serikali ijiseme yenyewe mbele ya umma. Kwa vipi? Hapa wangembana mgombea mtarajiwa Bernad Membe ambaye si tu alishindwa kutaja waliohusika bali pia alipigia sana upatu pesa hizo. Kungetokea confusion kali kati ya Membe na serikali yake na hapo kesi ingekuwa wazi.

ulitaraji waeleze mkakati wao kuhusu tatizo la maji na suluhu. Walitakiwa waanishe vyanzo vya mapato ufuajaji na je wangefanya nini tofauti.
Kwa maneno mengine wajenge hoja zinazowagusa wananchi si kwa kelele bali kwa mpangilio na mantiki. walete mashitaka, waendeshe kesi na watoe hukumu katika mahakama hiyo. Sivyo, tumeshuhudia attacks kwa wana CCM kama kwamba hilo ndilo tatizo la wananchi! wrong!

Hata hivyo pamoja na matendo ya kidhaifu hayo yote, ukweli (kwa mtazamo wangu) unabaki kuwa kwa hali ilivyo sasa kisiasa ikiambatanishwa na matendo, attitude za wananchi na baadhi ya Viongozi pia na matukio infanya niamini kuwa 2015 CCM bado wana uwezo wa kuwa vinara wa Uraisi hata kama ni kwa asilimia ndogo kuliko siku zote za chaguzi kwa sababu hizi zifuatazo;

Wamejipanga VyemaKujipanga haijialishi ni njia ipi unatumia, kama ni chafu/safi, halali/si haliali, haki/siyo haki - inachojalisha ni mipango yako kuweza kufanikisha azma ya malengo ya mipango hiyo. Serikali ya CCM imekuwa hodari katika kuhakikisha inatengeneza mazingira wezeshi kwa wao kuweza kushinda uchaguzi mkuu ujao. Wamejitosheleza vyema katika Nyanja mbali mbali, tokana na vita baridi waliyo nayo dhidi ya wapinzani wao wakuu CHADEMA. Wamejikita katika kujizatiti kuwanyong'onyeza nguvu CHADEMA kwa kila namna inayowezekana hasa kwa kutumia madhaifu yao.

Viongozi wao wamekuwa wakijitahidi na kuweza kufanya kazi hiyo ya kwa bidii, Tumeona namna shutuma za CHADEMA kuingia mikataba na Wafadhili wa mabillioni ya shilingi (Sijui hii kesi iliishia wapi?); Tumeona suala la Kadi ya CCM ya Dr. Slaa vile ilisambaa katika vyombo vya habari ambayo mwanzo ilichukuliwa kwa wepesi na hatimaye kuweza ku ‘divert' attention ya baadhi ya viongozi wa CHADEMA kwa kulitatua tatizo badala ya kuangalia mambo mengine ya msingi na yalo na tija kwa shughuli za Chama
Hapa nadhani CCM wapo defensive na CDM offensive. Tatizo ni uzoefu, kwamba katika wakati mgumu CCM wanajua wajikwamue vipi. Bahati mbaya CDM wameshindwa kusoma mazingira. Lakini nakuhakikishia kuwa kwa kiasi fulani CCM wanajihani.

Hili la ku-divert attention ya CDM linatokana na udhaifu wa CDM.
Wao kama chama hawajaweza kuwa na strategists na pundits. Kwahiyo tuhuma inajibiwa baada ya kuleta uharifu. Hili tatizo ni la muda mrefu na haionekani kama wanaliona.
Wapo juu ya Taasisi; Kumekuwa na sarakasi nyingi Bungeni hadi kupelekea lawama zilizo kithiri dhidi ya Madame Anne Makinda na ndugu Job Ndugai – tokana na matendo yasiyowaridhisha wabunge wengi na wananchi kwa ujumla. Kubwa kuliko hapa karibuni kumefutwa na kuvunjwa kwa Kamati mbili (1) Kamati ya Ulinzi, Usalama na Mambo ya Nje iliyokua inaongozwa na Edward Lowassa na (2) Kamati ya Hesabu za Mashirika ya Umma (POAC) iliyokuwa inaongozwa na Zitto Zuberi Kabwe ambayo ilifutwa kabisa. Inaleta uwalakini sana ‘timing' ya events hizi hasa tokana na kuwa ripoti za kamati hizo zilikuwa zikae wiki chache baada ya tukio. Ikumbukwe ripoti ya mwisho ya Zitto ilipeleka kura ya kutokuwa na Imani kwa Waziri Mkuu Mheshimiwa Mizengo Pinda na hivo kusababisha kusimamishwa kwa mawaziri 8.
Narudi kule kule kuwa hawakutumia mahakama ya wananchi kikamilifu. Pengine ilionekana kama tatizo la mtu na si chama na hivyo kutopewa umuhimu wa kutosha. Hili tu wangejipanga vema na kuueleza umma kwa kina wananchi wangewaelewa nasikitika kusema hawakuweza kufanya hivyo.

Tuweke kiuto kwanza tutaendelea na sehemu iliyobaki.
 
Mkuu AshaDii mada ndefu kidogo najipanga kuchangia hoja kwa hoja si viroja.Pamoja sana.
 
Last edited by a moderator:
Kupokea kwa Oil Chafu toka CCM

Ni ajabu sana kuwa CHADEMA wapo haraka sana katika kupokea viongozi toka chama kingine (hasa cha wapinzani wao wakuu CCM) kwa mbwembwe na matangazo. Utata unakuja pale ambapo huyo aliyejitoa CCM ni Kiongozi na akifika CDM anapewa uongozi… Hiyo ni hatarishi kama huyo mtu ni pandikizi, pia kwa namna moja ama nyingine kuwanyima haki wale ambao wanaweza hiyo nafasi nje ya huyo mgeni. ; Hili litatokea na ni moja ya mambo ambayo yataigharimu CHADEMA urais 2015; CHADEMA wanaweza kuepuka kuwa chama chakupokea wale wote ambao wanaogopa kusimama kama wagombea wa CCM e 2015 kutokana na nguvu ya CHADEMA

Bahati mbaya siyo kutokana na Mapenzi juu ya CHADEMA na taifa, bali kwa nafsi na ubinafsi wao. Ni muhimu CHADEMA wakaliangalia upya hili; pengine CHADEMA waje na tamko kwamba mtu yeyote ambaye atahama kutoka CCM dadika ya mwisho hatopata nafasi ya kugombea kwani ni kuwanyima haki loyalists. Chama kije na kanuni kwamba ni lazima ujiunge na CHADEMA miaka miwili kwa mfano before uchaguzi ili uweze kupata experience na chama etc


Hata CCM nao wanapokea OIL CHAFU SANA kutoka CHADEMA mfano Juliana Shonza na Masalia wenzake.
 
Hapa tuko pamoja AshaDii, pamoja na mapungufu waliyonayo ccm, mie naona udhaifu mkubwa ni vyama vya upinzani kushindwa kusimama pamoja; angalau wakakubaliana kumwondoa ccm kwanza.

Badala yake tunaona wakipigana vita wao kwa wao wakiitana ccm-B n.k., hadi wanasiasa wetu watakapoazima ukurasa kutoka kwa jirani zetu Kenya, itachukua miaka mingi sana kuona mabadiliko ya kweli hapa nyumbani.
 
Last edited by a moderator:
Maadam bado wananchi bado wanaendelea kutafuta WATAWALA wa kuwaita WAHESHIMIWA basi itakuwa vigumu sana kuiondoa CCM madarakani. Yatizo sio Chadema, CUF wala NCCR bali watu wote nyuma ya vyama hivi na wananchi wenyewe tuna mtindio wa Ubongo unaoitwa kasumba ya mkoloni..

Mambo yoote yalokwisha tokea bado wananchi tumegawanyika na wengine wakiipigia debe CCM japo wanaumia ktk maisha. Ukiona nchi maskini ambayo inajengwa kutoka juu kwa kutumia mifumo inayokuza asilimia 1 kumiliki asilimia 90 ya Utajiri ilihali nchi hiyo watu wake ni maskini basi ujue hawa watu wana kasumba mbaya sana. je una sababu baina ya CUF na Chadema kuchukiana tena kisiasa vyama ambavyo havina hata nusu ya wabunge nchini? kuna sababu leo hii wananchi waislaam na wakristu kuchukiana hadi kufikia hatua tuliyopo?... na tujiulize mkoloni aliweza vipi kututawala?.. Sii kwa kupitia mambo kama haya?

Hivyo hadi siku wananchi wenyewe watakapo amka toka usingizi wa pono na kudai VIONGOZI badala ya WATAWALA na wakaijua tofauti baina na vitu hivyo ndipo tunapoweza kuona Upinzani wa kweli sio tu kwa vyama vya siasa bali hata wananchi wenyewe kujua tofauti baina ya UKWELI na MAMLAKA.

Binafsi yangu nimesha ondoa tumaini hasa baada ya kuona wananchi wenyewe tena hapa hapa JF wakikwaruzana kwa vitu walivyolengeshwa hata wasione ujinga ulotangulia nyuma yake.. Kwa mfano leo hii watu wanabishana na kuchukiana juu ya dini, na sii bure CCM wameondoa kabisa kasi ya watu kukichukia chama bali kuwagawa wao na waanze kuchukiana wenyewe...Leo watu wanazungumzia zaidi Uislaam na Ukristu na wapo tayari kuchukua hata silaha wauane, lakini wameshindwa kuelewa kwamba vitu hivi havitokei pasipo sababu na kuna mkono wa mtu..

Kanisa limechomwa Mbagala hadi leo hii hatuwajui walochoma isipokuwa watu wanashabikia kukamatwa kwa Sheikh Ponda ambaye ni bangusilo kuondoa hasira za wakristu lakini wahaini wenyewe are still at large, unsolved case watu wametulia. Yalipoanza kuiva bungeni tumeyaona ya Zanzivar, chuki inazidi baina ya watu wenyewe na sasa imefikia mahala ambapo tumegawanyika vibaya sana na hakika mwaka 2015 utakuwa kielelezo cha imani za watu, mshindi CCM...
 
Habari wana Jf,
.....
My General Take

Hadi hapa naamini kuwa Kuna kila dalili kuwa CCM itashinda, hata kama itakuwa kwa asilimia 51% za kura zote; Tofauti itakayokuwepo katika ushindi huo ni kuwa CCM itashinda kwa margine ndogo kuko zote katika historia za Chaguzi Tanzania. Mwenyekiti wa CHADEMA Mheshima Freeman Mbowe yeye kishajiapia kuwa ikishinda CCM 2015 atajiuzuru na naomba nimnukuu "Iwapo CCM itashinda uchaguzi mwaka 2015, basi nitajiuzulu Siasa". Ni kauli ya kutia moyo ya kuwa Chama kimejipanga vipi, kuwa kina uhakika wa Kazi na nguvu zake na kuwa Chama kitaikomboa nchi ifikipo 2015.

Vile vile iwapo kutakuwa na ushindi wa CHADEMA kama vile wengi wa Watanzania, Wanaharakati na Viongozi wa Chama hicho wanavyo dhania na kuamini; basi ni kuundwa kwa serikali ya umoja wa kitaifa hasa iwapo CHADEMA watapata kura nyingi ngazi ya Urais na wabunge wengi – ila nikiri kuwa tatizo ni kwamba suala la ndoa za vyama, CHADEMA walishajifunga na umma unajua fika na kwa kiasi kikubwa namna gani CHADEMA hawakubaliani a wazo la ‘Government of National Unity' kule ZNZ. Swali linabaki je ikitokea uwezekano wa GNU Tanzania bara na ikaonekana ndiyo suluhu pekee, CHADEMA watakula matapishi yao wenyewe? Hata hivyo naomba hili niliache hapa kwani ni mjadala mwingine mpya kabisa. Wanachadema... Hii nakala ni katika ku challengiana na kujitazama upya kuweza kufanikisha safari ya Ikulu.

Naomba nitumie hii nukuu ya vita from the Legendary Sun Wu. Naamini kuwa hii nukuu, inatumika vema na CCM katika tactics zake zake chafu za kisiasa hasa hizi za ‘Gutter Politics' ambazo ndio sababu pekee bado wapo hapo walipo. It is time Chadema start doing the same... (IMO).
"If your enemy is secure at all points, be prepared for him. If he is in superior strength, evade him. If your opponent is temperamental, seek to irritate him. Pretend to be weak, that he may grow arrogant. If he is taking his ease, give him no rest. If his forces are united, separate them. If sovereign and subject are in accord, put division between them. Attack him where he is unprepared, appear where you are not expected."


Pamoja Saana,

AshaDii.


AshaDii;

Je kuna uwezekano wa kupatikana kwa serikali ya mseto au umoja wa kitaifa mwaka 2015? Kwa maoni yangu naona kama ushindi wa 51% unaweza kuleta ubishi wa matokeo iwapo wapigaji kura wa miji mikubwa watapigia upinzani.

Kama vyama vya upinzani vinaweza kupata 60% DSM, 70% Arusha, Mwanza 70% n.k. Sidhani kama ushindi wa 51% unaweza kuisadia CCM.
 
Maadam bado wananchi bado wanaendelea kutafuta WATAWALA wa kuwaita WAHESHIMIWA basi itakuwa vigumu sana kuiondoa CCM madarakani. Yatizo sio Chadema, CUF wala NCCR bali watu wote nyuma ya vyama hivi na wananchi wenyewe tuna mtindio wa Ubongo unaoitwa kasumba ya mkoloni..

Mambo yoote yalokwisha tokea bado wananchi tumegawanyika na wengine wakiipigia debe CCM japo wanaumia ktk maisha. Ukiona nchi maskini ambayo inajengwa kutoka juu kwa kutumia mifumo inayokuza asilimia 1 kumiliki asilimia 90 ya Utajiri ilihali nchi hiyo watu wake ni maskini basi ujue hawa watu wana kasumba mbaya sana. je una sababu baina ya CUF na Chadema kuchukiana tena kisiasa vyama ambavyo havina hata nusu ya wabunge nchini? kuna sababu leo hii wananchi waislaam na wakristu kuchukiana hadi kufikia hatua tuliyopo?... na tujiulize mkoloni aliweza vipi kututawala?.. Sii kwa kupitia mambo kama haya?

Hivyo hadi siku wananchi wenyewe watakapo amka toka usingizi wa pono na kudai VIONGOZI badala ya WATAWALA na wakaijua tofauti baina na vitu hivyo ndipo tunapoweza kuona Upinzani wa kweli sio tu kwa vyama vya siasa bali hata wananchi wenyewe kujua tofauti baina ya UKWELI na MAMLAKA.

Binafsi yangu nimesha ondoa tumaini hasa baada ya kuona wananchi wenyewe tena hapa hapa JF wakikwaruzana kwa vitu walivyolengeshwa hata wasione ujinga ulotangulia nyuma yake.. Kwa mfano leo hii watu wanabishana na kuchukiana juu ya dini, na sii bure CCM wameondoa kabisa kasi ya watu kukichukia chama bali kuwagawa wao na waanze kuchukiana wenyewe...Leo watu wanazungumzia zaidi Uislaam na Ukristu na wapo tayari kuchukua hata silaha wauane, lakini wameshindwa kuelewa kwamba vitu hivi havitokei pasipo sababu na kuna mkono wa mtu..

Kanisa limechomwa Mbagala hadi leo hii hatuwajui walochoma isipokuwa watu wanashabikia kukamatwa kwa Sheikh Ponda ambaye ni bangusilo kuondoa hasira za wakristu lakini wahaini wenyewe are still at large, unsolved case watu wametulia. Yalipoanza kuiva bungeni tumeyaona ya Zanzivar, chuki inazidi baina ya watu wenyewe na sasa imefikia mahala ambapo tumegawanyika vibaya sana na hakika mwaka 2015 utakuwa kielelezo cha imani za watu, mshindi CCM...

Fikra sahihi za a true great thinker!
 
AshaDii,

But the other side of the coin is the people's willingness to change for themselves. This is the clincher. This is where it gets really tough because despite how good it could be people are very rarely willing to change for themselves.

I am in consent with almost all of your post… And I think this part I have quoted is one of the most problematic issue.

EMT… I have said it before like I will say it now. For an improved, better and developed Tanzania plus a better future for all Citizens of this generation and the next; Changes does not only rely on the Government alone, there has to be change in lot of entities, of the whole system itself… Most importantly the people's improvement of negative attitude of fear, insecurity and selfishness for the better. That is to say… It does not really matter if CCM is thrown out 2015, if we as the people of this nation will have the same attitude.

There are two things involved in expected Change by the majoriy; all these changes based on the Optimistic side rather than Pessimism.

1. That Chadema's victory come 2015 is inevitable – Which at this moment am not yet convinced.
2. The second one is dependent on the fact if indeed Chadema is the Victor of the Uchaguzi Mkuu. That peoples life will transform for the better… I am not convinced with this one either…

P.S – Please; apologies on the delay in response.
 
  • Thanks
Reactions: EMT
Sijasoma makala nzima ya AshaDii nataka kulala nitaisomna kesho, ila EMT acha mara moja ku under estimate Watanzania kiasi hicho, mimi na Familia yangu CCM haina kura hata moja, subilini tu lile bomu alilolisema Lowasa liotakavyofanya kazi yake vyema.

Wengi humu licha kuwa ni wachambuzi wazuri lakini mnashindwa kufanya calculation ya wapiga kura wa 2015 ni wa rika gani. hawa hawadanganywi kwa lugha ya amani na utulivu bali wanataka kuishi kama binadamu na siyo porojo za kwamba Chadema ni chama cha ukanda wa kaskazini wakati CCM ndio ina Wabunge wengi Kaskazini, this is ridiculous.

Naamka mapema kesho nitamsoma vizuri AshaDii ndio nitoe comment zangu.


Matola, nimefuatlia... So far naona hukupata nafasi ya kueleza mawazo yako kwa kina kuhusu hili. Nimependa hayo maelezo ya wapiga kura kutodanganywa kwa lugha ya 'Amani na Utulivu'.
 
Well....!
Sidhani kama nilitegemea uchambuzi wa tofauti sana toka kwako Bi. Asha hasa linapokuja suala la CDM.....

Kwa kulifafanua zaidi swali, ngoja niliweke hvi katika ule usemi wa "changes ni mimi na wewe, Twaweza" nafasi yako ni ipi kuelekea hiyo 2015? Hichi ndio kitu cha maana zaidi kuliko vingi mtu anaweza kukujibu, kama we huamini katika mabadiliko hayo ni vipi utayaona kwa wewe kuwa sehemu ya mabadiliko? Au ukiwa umekata tamaa kama EMT, ni nini utaona?

Nafasi yangu ipo Gwalu, this is one of them… Painting the picture as I see it whether kwa pen ama maneno. Ni watu wengi ambao wanacheza nafasi kubwa katika kuleta change waliogawanyika katika makundi ya wale ambao watajulikana kwa changes wanazochangia na wasiojulikana… Inaweza kuwa at a small scale but bado nafasi yake ipo.

Labda sasa wewe unipe mwanga… Unaposema kuwa siyo haki kuyajadili mabadiliko na hali siyo mpanganaji wake na hapo hapo ukiamini kuwa Change evolves kila mmoja kucheza nafasi yake inakuwaje hapo? Take note, kila mmoja na kila part ina umuhimu… Mtendaji, Mtendewaji, Mkosaji, Mkosolewa; na hakuna kinachoweza boreshwa bila kukosolewa… hayo yote yanafanya uwepo wa kitu ambacho kinaguswa kwa kila namna kuwapa nafasi wale ambao wapo interested kuelewa kwa kina zaidi bila kujali kama ina matokeo hasi ama chanya.

Nikutahadharishe thou... Ukiliangalia hili bandiko kwa jicho la kusema kuwa "Hutegemei uchambuzi tofauti na huu toka kwa mtoa mada sababu inahusu tu CDM" then kwangu naona unapotoka kiasi. Sababu kama you have read it accordingly utaona haihusu CDM peke yake, inahusu CCM, CDM na Wananchi.

Hiyo ni mifano yangu binafsi (inayonivutia mimi) kujitosheleza kusema kuwa ufike wakati kila mtu kwa nafasi yake aziishi harakati halisi kuelekea mabadiliko tunayoyategemea. Leo wamejitwisha ufundi wa kuchambua na kukosoa masuala mbalimbali lakini mwishoni anajifanya neutral au ameficha gamba lake la CCM!

Ni kitu gani ambacho kinampa mtu ruhusa ya kuchambua kitu kisiasa ndiyo maneno hayo yapewe uzito? Hivi mfano haya mawazo yangu hayatakiwi kwa mtu ambaye ni mwana CCM atoe hadi awe CDM? Hizi shutuma za mtu "Kujifanya" kunawiana vipi na topic at hand (regardless ya hii ama nyingine? - Labada iwe ya kizushi ama yakucheza dimba); Siamini na wala sidhani kuwa we are pressured ni kitu gani ama upande upi tunasimamia. Kupata ujumbe vema na kutambua kama ni wa msingi ama lah usiwe affected na aliyetowa yupo upande upi... Uwe affected na uongozwe na mantiki.

kwa msingi huo tutakuwa tumepotoka sana kama jamii.....

Ni jukumu la kila mtu kucheza nafasi yake kwa vitendo katika kuwa sehemu ya mabadiliko tunayoyatamani wote. Hizi mbwembwe za kuja na chambuzi ndeefu kila kukicha kwenye hzi kurasa na kuta hazitatufaa sana, mabadiliko tunayoyatamani ni makubwa sana kuliko kile tunachofanya kila siku.

Tubadili aina ya uchambuzi tuleteane case study, naelewa sio lazima wote tuwe wanasiasa japo tunajukumu moja la kuleta mabadiliko ya kisiasa kupitia kwenye kada zetu, EMT tupe uzoefu wako unavyopambana na mabadiliko huko kwenye michakato yako sijui ni sheria sijui ni uandishi wa habari, Nguruvi3 tupe harakati zako halisi kutokea huko ulipo, Mchambuzi tueleze uzoefu wako na harakati zako za sasa, kama kuna watu unawajenga wanafanikiwa wapi wanashindwa wapi....

Suala la kupotosha jamii… Kuna suala Matola kagusia hapo ambalo nimelipenda saana. Kuwa watu wanaelewa ni nini wanataka na huwezi kuwadanganya kwa kuwaambia kitu ambacho sicho kwa kufanya ndicho.

HATUWEZI na wala HAIWEZEKANI kutegemea mafanikio bila kujitafakari, kutafakariwa na wamazo wa watafakari hao kujulishwa bila kujali wame ku Criticise ama Lah. Suala la kuona mawazo yaliyowakilishwa ni mbwembwe sababu tu huyapendi ama kutoyakubali ni aina ya udhaifu wa kutotaka ona mabaya ya li/yale ambayo unataka yaonwe kwa uzuri tu. Kama uliweza kuyasoma mawazo ywa wanaharakati waliotowa uchambuzi kama huo wa Samson Mwigamba (as per your say) na ukavutiwa na kupenda, ni hivyo hivyo ambavyo inabidi utazame upande wa pili wa shilingi ikitokea hujapenda hayo mawazo.

JouneGwalu… Kuna mambo mengi sana nimegusia hapo. Naamini ningeelewa vema zaidi ungenijuza kabisa kua AshaDii, hapa sikubaliani napo kwa sababu hii…. But kwa kugeneralise kuwa there is no need of a long analysis…. Ni suala ambalo sikubaliani nawe. For kwa kweli ni suala ambali nitaendelea kufanya.

Katika masuala ya mabadiliko... Hapo nilipo bold... Hivi imagine JouneGwalu, hapa Jf huyo EMT, Nguruvi3, Mchambuzi na mimi mwenyewe pamoja na wengine wote wahusika tukifanya hiyo kazi ya kuleta threads za kila mmoja kutoa maelezo ya change anayofanya na mafanikio... Itakuwa interesting kweli? Sijui, but mie naona sidhani... Zaidi watu hawatachelewa kusema you are braggin na siyo kweli.

Ila narudia tena kushindwa kwa CDM haitakuwa aibu au kukomoka kwa CDM peke yao tu bali kwa kila anayeujua ukweli na aliyetamani mabadiliko fulani katika jamii yetu na hakuchukua na kucheza nafasi yake. Tuache na tupunguze mbwembwe za uchambuzi wa nadharia uliokithiri twende kwenye uwanja wa mapambano kila mtu achukue nafasi yake kujenga dhamira ya mabadiliko na watu wake kuelekea 2015.

CHANGES NI MIMI NA WEWE, TWAWEZA!

Hii paragraph ya mwisho sasa ndiyo nimekupata vema kwa hapa. Umesha fanya conclusion kuwa bandiko linahusu kuwa Chadema ishindwe na kuwa nataka hivyo. Sincerely... Naomba soma upya the whole article toka neno la kwanza to the final fulstop.

All in all nakubaliana na wewe... Change ni mimi na wewe. And this is my part in this... Nadhani umesikia kuwa hata Mwenyekiti wa Taifa Chadema -Mheshimiwa Mbowe katangaza kuwa sasa hawapokei tena wanachama wa CCM kwa muda huu uliobaki hasa wenye niya ya kwenda huko sababu tu wanaona kuwa CCM wanachemka. (Not the exact words but same meaning); Hivyo ina maana yawezekana kabisa mimi kama mmoja wa wengi walio wa 'Criticize' CDM katika hilo tayari tumecheza nafasi yetu kama wapambanaji. Asantw kwa mchango wako.
 
Hata CCM nao wanapokea OIL CHAFU SANA kutoka CHADEMA mfano Juliana Shonza na Masalia wenzake.

Mkuu... Haipaswi CDM kufanya suala ambalo ni dhaifu sababu tu CCM wanafanya. Inakuwa kama mchezo usiyo na tija na wala haina manufaa yeyote. Kikubwa ni kuboresha pale palipo pwaya baada ya utambuzi huo.

Mkuu ngogo, patiently waiting mchango wako... Mkuu Nguruvi3 nimekusoma. Karibu yote uliyowakilisha naunga mkono... Asanteni.
 
Last edited by a moderator:
Back
Top Bottom