Kwa muktadha huu "URAIS" ni wa CCM 2015...

Kwa muktadha huu "URAIS" ni wa CCM 2015...

Ni kweli CCM itashinda Uchaguzi Mkuu wa mwaka 2015. ushindi wake utatokana na sababu mbalimbali ikiwemo the fact kwamba chama kikuu cha upinzania, chadema, kinaendeshwa kwa misingi ya ulaghai...
 
Kuna popote ulishaandika lolote kuhusu madhaifu ya ccm? Na ni kwa nini ccm ishinde wakati unajua fika (au hujui?) kuwa hawana tena uhalali wa kuongoza hii nchi?

Kuna kitu watu wengi wanashindwa kunipata.... HASA ambao hawataki hata kidogo kusikia kuwa CCM inaweza endelea kubaki madarakani. Mie maoni yangu yanaelemea mtazamo wangu na si Mapenzi. Siwezi thou nikaongopa na kusema nina mahaba na CHADEMA... Kama nisivyo na mahaba na Wanasiasa wengi kwa kiasi kikubwa sana sababu ukweli unabaki kuwa ni wabinafsi! Na tunaposema wanasiasa waongo kwa hapa nchini wanaongoza ni CCM mana wao ndio wanashika nchi... Kwa hilo utaamua mwenyewe uniweke kwa kundi lipi.

Pamoja na kuwa sina mahaba na CHADEMA, Natambua umuhimu wa CCM kuachia nchi na sikwepi kuona ukweli kuwa kwa sasa tukitaka Uongozi mpya uje kuwatoa wana CCM tegemezi pekee ni CHADEMA kwa sasa (Thou anything can happen in the remaining time hadi Uchaguzi Mkuu).

Sina haja ya kuongea madhaifu ya CCM - Yapo wazi kila mahala! Kuna asiye jua masakata ya EPA/Buzwagi/Melemeta (to mention but a few); Regardless kuwa CCM wana madhaifu makubwa ambayo ni janga kwa taifa, iwe nchi na wanajamii sikwepi kuona ukweli kuwa wana CCM wanatumia kila namna kuweza ku maintain nafasi ya Uongozi waliyo nayo na juu ya hayo wana vingi vinavyozidi kuwabeba kama vile vipengele vingi vya katiba ya sasa inavyokumbatia Uongozi ulipo madarakani.

Kuweza kuwashinda CHADEMA ama chama chochote ile cha Upinzani WAJIPANGE! Wajitazame na wakubali madhaifu yao ili kuweza yarekebisha! Najua wengi maneno kama ya thread yangu (Hasa wa fuasi wa Chadema wasiotaka kusikia mapungufu aidha kwa kujiamini sana OR kwa kuona kuwa hawana kabisa mapungufu) hawapendi na wala hawataki kusikia habari hizi. Cha kusikitisha wao kama wadau wa Chama ndiyo wana nafasi na influence kubwa kwa vyama vyao kufanyia kazi yale yanayostahili kufanyiwa kazi.

Call me CCM or not.. Kwa kweli I don't really care. Ninachojali ni kuwa ujumbe umefikishwa kwa kuwakilsha 'Perspective' yangu on the matter. BTW naomba niongezee kuwa Kenya kama majirani zetu ni somo zuri sana kwa wao... Kuwa maneno ya wadau na wingi wa maoni hayo kwa uzuri juu ya chama siyo ambacho huweka Kiongozi kwenye kiti. Mwish wa siku 'Kura' ndiyo determinant ya mwisho... In other words katika Uchaguzi wa majirani zetu ilikuwa inaonekana kuwa Odinga ni kipenzi cha wengi na kuwa majority ndiyo wanamtaka na kuwa angeshinda kwa urahisi ukilinganisha na Kenyatta... Kazi bado ni kubwa sana! Uzuri tu tu kuwa bado ni mapema na inawezekana kwa kujipanga vema!
 
Ni kweli CCM itashinda Uchaguzi Mkuu wa mwaka 2015. ushindi wake utatokana na sababu mbalimbali ikiwemo the fact kwamba chama kikuu cha upinzania, chadema, kinaendeshwa kwa misingi ya ulaghai...

Mkuu ZeMarcopolo, naomba utolee ufafanuzi... Kusema kuwa CCM itashinda Uchaguzi Mkuu 2015 sababu tu CHADEMA kinaendeshwa kwa misingi ya 'Ulaghai' na hali 'Ulaghai' huo huo ni part and parcel ya CCM - Haitoshi.

Kama hutajali naomba ufafanuzi...
 
Last edited by a moderator:
Mkuu ZeMarcopolo, naomba utolee ufafanuzi... Kusema kuwa CCM itashinda Uchaguzi Mkuu 2015 sababu tu CHADEMA kinaendeshwa kwa misingi ya 'Ulaghai' na hali 'Ulaghai' huo huo ni part and parcel ya CCM - Haitoshi.

Kama hutajali naomba ufafanuzi...

Mkuu AshaDii,

Habari za Siku Nyingi?

Naomba kwanza nifanye marekebisho madogo kwenye swali lako.
Kwenye post yangu sijasema CCM itashinda kwa sababu TU chadema inaendeshwa kilaghai ila nimesema hiyo ni mojawapo ya sababu.

Wakati chadema inapata umaarufu, kilikuwa kiahubiri kupiga vita rushwa na ufisadi kila kukicha. Hii ilifanya watu wengi waamini chadema ina malengo ya dhati ya kupinga ufisadi. Hata hivyo tangu 2010 mpaka sasa chadema imehusishwa na ufisadi mwingi wa moja kwa moja ndani ya chama kuliko chama chochote cha siasa nchini. Hii imewaondoa chadema mioyoni mwa walioiamini na imesababisha chadema kubakia na makundi ya bendera fuata upepo na wapenda vyeo.

Ukipata fursa, tafadhali pitia kwenye thread iliyoelezea hali ya uungwaji mkono wa chadema ilivyo hivi sasa hapa
https://www.jamiiforums.com/jukwaa-la-siasa/415932-chama-cha-kilaghai-tanzania.html

Asante kwa swali lako na tuendelee kuwa pamoja katika mjadala huu...
 
Mkuu ZeMarcopolo, naomba utolee ufafanuzi... Kusema kuwa CCM itashinda Uchaguzi Mkuu 2015 sababu tu CHADEMA kinaendeshwa kwa misingi ya 'Ulaghai' na hali 'Ulaghai' huo huo ni part and parcel ya CCM - Haitoshi.

Kama hutajali naomba ufafanuzi...
Pamoja sana Asha....

Nimelipenda bandiko lako....

Nitarudi...

Bala.
 
Last edited by a moderator:
Mkuu ZeMarcopolo... Nimependa sana hilo bandiko lako. Naona kuna michango ya kutosha... Nitaisoma vema michango ya wadau wote kwa nafasi... Na kama hutajali nimeona niliweke hapa pia kwa manufaa ya wengine sababu inashabihiana sana na hoja niliyowakilisha hapa.

CC: EMT, Mkandara

CHADEMA ni chama kinachoendeshwa kwa misingi ya ulaghai. Chama kama hiki mtu yeyote atakayetaka kukiunga mkono kwa hoja anajikuta anakwazika.
Hii imesababisha CHADEMA kuungwa mkono zaidi na makundi mawili ya watanzania:

1. wale ambao ni bendera fuata upepo.
2. wale wenye malengo ya kupanda haraka na kwa urahisi kwenye arena za kisiasa za kitaifa.

Nitayachambua makundi haya mawili kama ifuatavyo:

1. Wale ambao ni bendera fuata upepo. Katika kundi hili kuna watu wa aina tatu:

i) Wale ambao wamedanganyika na propaganda kuwa chadema ni chama cha kikabila au cha kikanda na kwa vile wao wanatoka kwenye kanda hizo basi wanajisikia ukaribu zaidi na chadema. Hapa utaona kuwa propaganda za kukichafua chama kuwa ni cha kikabila au cha kikanda kimeweza kuwaongezea chadema nguvu katika maeneo inayoshutumiwa kuyapendelea.

ii)Wale ambao wamelaghaika na propaganda za kuwa chadema ni chama cha udini. Kuna waumini wengi wameviunga mkono vyama vya chadema na CUF kwa sababu tu wamekuwa wakisikia kuwa vyama hivyo vinashabiiana na dini zao. Hawa ni bendera fuata upepo ambao hawachuji ukweli wa taarifa na hawajiulizi chama kinaweza kuwanufaishi vipi kama waumini wa dini husika.

iii)Kundi la tatu katika bendera fuata upepo ni vijana ambao wanaona kuwa chadema ni kama fashion. Ukikaa nao chini vijana hawa kuwauliza kwanini wanaiunga mkono chadema hawana lolote la kuongea. Mfano wa watu waliomo kwenye kundi hili ni members wa jamiiforums ambao hurusha matusi kwa kila mtu anayehoji jambo juu ya chadema.

Makundi haya matatu ya bendera fuata upepo huwa ni rahisi sana kuvunjwa moyo na kukikimbia chama mara tu upepo utakapoelekea upande tofauti. Kwa mfano, iwapo chadema itafanya jitihada za kuhakikisha jamii inajua ukweli kuwa siyo chama cha ukanda wala ukabila, basi makundi haya mawili i) na ii) yatatoweka.

Vilevile iwapo chadema itasambaza elimu ya uraia na kuwawezesha wananchi kuchagua vyama vyama vya kuviunga mkono kwa hoja, basi makundi yote iii),ii) na i) itayapoteza.
Hizi ni changamoto zinazohitaji political calculations kudeal nazo.

2. Wale wenye malengo ya kupanda haraka na kwa urahisi kwenye arena za kisiasa za kitaifa:

Katika kundi hili wamo wanasiasa kama Dr. Wilbroad Slaa na Shibuda. Misingi ya wanasiasa wa aina hii kuhama kutoka kwenye chama kimoja mpaka kingine ni kuhakikisha tu kuwa wanaendelea kuwepo kwenye shughuli za kisiasa katika nafasi za uongozi. Hawana ugomvi wa kiitikadi na CCM.

Kimsingi hawa ni watu ambao iwapo leo hii CCM itawahakikishia kuwa watapata fursa ya kuwa viongozi wa juu, basi wako tayari kujiunga nayo. Wamejitoa CCM kwa sababu tu walinyimwa fursa ya kuwa viongozi katika ngazi walizogombea. Iwapo chadema itawanyima fursa ya kuwa viongozi, wataikimbia pia.
Mfano mzuri umeonekana hivi karibuni Lushoto ambaye kijana mpya katika siasa Deogratius Kisandu aliikimbia chadema kwa kukosa fursa za uongozi ambapo kimsingi alijiunga chadema kwa kuamini kuwa fursa hizo atazipata kwa urahisi zaidi ndani ya chama hicho.

CHADEMA imekosa uungwaji mkono katika misingi ya itikadi. Hii imesababishwa na ukweli kwamba cHADEMA imechukua itikadi zilezile za CCM, TANU na ASP na kushindwa kuwapa wananchi chaguo jipya. Zaidi ya hayo, hata kwenye ilani za uchaguzi za chadema hakuna offer tofauti na zile ambazo wananchi wanapewa na CCM. Kuthibitisha hili, chadema imepata wakati mgumu sana kupokelewa katika maeneo ambayo kuna chama kingine cha upinzani kilichojijenga kama Zanzibar. Iwapo chadema wangekuwa na itikadi au sera mpya ambazo utekelezaji wake unaelezeka, isingekuwa vigumu kupata wafuasi katika maeneo hayo.

Kwa vile CCM imeshapewa fursa ya kutawala, mapungufu yake yameonekana. Jukumu la chadema kwenye hili linatakiwa ni kuja na mkakati unaoelezea kwa undani ni vipi watafanya tofauti na CCM. Badala yake, kazi pekee inayofanywa na chadema ni kuainisha matatizo na kuyahubiri majukwaani bila kuelezea iwapo wana mkakati wowote mpya ili wananchi waupime. Hii inasababisha hata wasomi wanapovifananisha hivi vyama wanakosa zile tofauti za kuzijadili na mwishowe hujadili tabia za viongozi vya vyama na utendaji wao badala ya kujadili sera zake na itikadi.

Ulaghai wa CHADEMA ni sababu nyingine iliyofanya chama hiki kupoteza wafuasi makini. Mtu yeyote atakayejaribu kuichunguza chadema kidogo tu atagundua kuna mambo mengi yasiyofaa yanayofanywa na viongozi wake. Viongozi hawa hufanya hivi kujinufaisha wao wenyewe na familia zao. Kwa vile umaarufu wa chadema umetokana na uhubiri wa ufisadi, uwepo wa ufisadi ndani ya chadema umewavunja sana moyo wananchi walioamini kuwa wamepata tumaini jipya. Wale wanaoishabikia chadema kwa kufuata upepo wanapojua ulaghai huu, huvunjwa moyo na kuikimbia. Mfano wa hili ni kijana Mtela Mwampamba ambaye aliamini kuwa chadema ni tumaini jipya mpaka pale alipojionea mwenyewe kwa macho yake uhalisia wa mambo ndani ya chama hicho.

Hapa nitaainisha baadhi ya mambo yanayoiondoa CHADEMA usoni na moyoni mwa watanzania wanaotaka chama kinachopinga ufisadi.

1. Mmiliki wa jengo lililopangishwa na CHADEMA Kinondoni kama ofisi za makao makuu na bei ya pango kwa mwezi vimefanywa siri. Mara kadhaa swali hili limeibuliwa lakini hakuna jibu lililoweza kutolewa na uongozi wa CHADEMA.

2. Wanachama walioomba fursa ya kushiriki tenda ya kununua magari ya chama wamenyimwa fursa hiyo na hatimaye tenda hiyo imetolewa kwa usiri mkubwa. Chris Lukosi amekuwa akishutumiwa kuwa sababu ya kujitoa kwake CHADEMA ni kunyimwa tenda hii, lakini pale wadau walipohoji baada ya Lukosi kunyimwa tenda hiyo ni nani amepewa na kwa vigezo vipi?, kinaibuka kigugumizi.

3. Swala la Katibu Mkuu wa chama kujikopesha mamilioni ya shilingi zilizochangwa na walalahoi kwa ajili ya shughuli za chama. Ikumbukwe kuwa watu waliochangia M4C walifanya hivyo kwa vile waliamini kuwa michango yao itakiwezesha chama kujiimarisha. Taarifa kuwa pesa zimetumika kifisadi zimewavunja watu moyo.

4. Taarifa za Josephine Mushumbusi kulipwa mamilioni ya shilingi za chama kwa kazi anayoiita ya kujitolea. Wadau walihoji kuwa na wao wangependa kujitolea kwenye shughuli za chama ili walipwe hayo mamilioni. Ilidhihirika kuwa Josephine alipata fursa hiyo kwa upendeleo.

5. Pesa za ruzuku zimekuwa zikiishia Makao Makuu. Watendaji wa chama mawilayani wamekuwa wakifanya kazi bila nyenzo. Hii ilisababisha mpaka kukawa na mtafaruku huko Mpanda kwa kukosa ofisi ya wilaya ambayo kimsingi ni jukumu la chama makao makuu kuhakikisha chama kina ofisi za wilaya. Ikumbukwe pia kuwa matumizi haya mabaya ya fedha yalikuwa sababu ya mvutano wa kisiasa kati ya marehemu Chacha Wangwe na kiongozi Mkuu wa Chama.

6. Kumekuwa na taarifa za matumizi mabaya ya pesa za Sabodo jambo ambalo limeelezewa kuwa sababu ya kumfanya Sabado kuahirisha ahadi yake ya kuijengea CHADEMA ofisi za makao makuu na chuo cha siasa.

7. Katibu Mkuu wa CHADEMA ni miongoni mwa washutumiwa wa ufisadi wa mamilioni ya pesa za mradi wa maji wa Karatu.

8. Viti Maalum vya ubunge vimetolewa kwa upendeleo ambapo akinamama waliojitolea kukijenga chama wameachwa pembeni na nafasi hizo kupewa akinamama walio karibu na viongozi wa juu wa chama. Hapa ikumbukwe kuwa mwenyekiti wa Baraza la Wanawake la CHADEMA (BAWACHA) wa Taifa alishinda nafasi ya uchaguzi wa viti maalum, lakini akatolewa kwa kuambiwa kuwa hajakidhi vigezo vya kuwa mbunge ingawa amewaongoza wanawake wenzake kwa muda mrefu ndani ya chadema. Wakati huohuo mwanamama anayeishi Marekani, Leticia Nyerere amepewa Ubunge wa viti maalum kutokana na "kufahamiana" na mwenyekiti wa chama. Hili limewavunja moyo wengi walioanza kuiamini chadema.

9. Vijana kama Kafulila walioonekana kuwa na ari ya mabadiliko ndani ya chama wamekuwa wakinyimwa nafasi ya kugombea uongozi kinyume na katiba.

10. CHADEMA kukanusha kauli ya Nape kuwa wanapewa msaada na chama cha siasa cha Ujerumani, baadae ikadhihirika kuwa ni kweli wanapokea msaada huo. Hii imedhihirisha kuwa CHADEMA sio wawazi katika utendaji wao. Wadau wanajiuliza chama hicho cha siasa kinataka nini Tanzania mpaka kikipinge chama kilichoasisiwa na wapigania Uhuru na kutaka chadema iingie madarakani? Ikumbukwe kuwa muasisi wa CHADEMA Mzee Mtei, alikataa kushiriki harakati za kupigania uhuru na pia alikataa kujitolea kuijenga nchi baada ya Uhuru.

11. Hesabu za pesa zinazochangwa na walalahoi kwa ajili ya M4C imekuwa ni jambo la siri kubwa ndani ya CHADEMA.
 
  • Thanks
Reactions: EMT
Mkuu ZeMarcopolo... Nimependa sana hilo bandiko lako. Naona kuna michango ya kutosha... Nitaisoma vema michango ya wadau wote kwa nafasi... Na kama hutajali nimeona niliweke hapa pia kwa manufaa ya wengine sababu inashabihiana sana na hoja niliyowakilisha hapa.

CC: EMT, Mkandara

Sawasawa AshaDii, tuko pamoja.

Utakapokuwa unasoma michango ya wadau, usipitwe na jibu dhaifu la Mzee Mtei linalothibitisha jinsi alivyokataa kushiriki harakati za kupigania Uhuru na jinsi alivyokataa kujitolea kuijenga nchi baada ya uchumi wa nchi kuyumbishwa na vita vya Uganda mwaka 1979 - akajiuzulu.

Wikiendi njema ndugu yangu...
 
Mkuu AshaDii,

Habari za Siku Nyingi?

Naomba kwanza nifanye marekebisho madogo kwenye swali lako.
Kwenye post yangu sijasema CCM itashinda kwa sababu TU chadema inaendeshwa kilaghai ila nimesema hiyo ni mojawapo ya sababu.

Wakati chadema inapata umaarufu, kilikuwa kiahubiri kupiga vita rushwa na ufisadi kila kukicha. Hii ilifanya watu wengi waamini chadema ina malengo ya dhati ya kupinga ufisadi. Hata hivyo tangu 2010 mpaka sasa chadema imehusishwa na ufisadi mwingi wa moja kwa moja ndani ya chama kuliko chama chochote cha siasa nchini. Hii imewaondoa chadema mioyoni mwa walioiamini na imesababisha chadema kubakia na makundi ya bendera fuata upepo na wapenda vyeo.

Ukipata fursa, tafadhali pitia kwenye thread iliyoelezea hali ya uungwaji mkono wa chadema ilivyo hivi sasa hapa
https://www.jamiiforums.com/jukwaa-la-siasa/415932-chama-cha-kilaghai-tanzania.html

Asante kwa swali lako na tuendelee kuwa pamoja katika mjadala huu...

Habari ya siku ni nzuri Mkuu... Mambo yanaenda 50/50 hivyo Inshaallah namshukuru Mungu ni mwema. Nilienda kwanza kwenye Link... Nashukuru kwa kuiwasilisha hapa... Naamini kuwa nikiisoma nitapata mengi sana juu ya mada hii na zaidi ya hapo.

Nimekusoma kuhusu Chadema... Na ndiyo maana nikagusia kuwa pengine ilikuwa na nafasi kubwa zaidi ya kushinda Uchaguzi ulio pita kuliko hata uchaguzi huu. Hata hivyo 'Time' pekee ndio dawa ya yoote haya... Lets wait and see.

Sawasawa AshaDii, tuko pamoja.

Utakapokuwa unasoma michango ya wadau, usipitwe na jibu dhaifu la Mzee Mtei linalothibitisha jinsi alivyokataa kushiriki harakati za kupigania Uhuru na jinsi alivyokataa kujitolea kuijenga nchi baada ya uchumi wa nchi kuyumbishwa na vita vya Uganda mwaka 1979 - akajiuzulu.

Wikiendi njema ndugu yangu...

Huyo member uliye mtaja kwa "Mtei" naamini kuwa unamaanisha Mzee Edwin Mtei... Akiwa kama mzee mmoja wapo wa zamani, siamini kuwa hoja zake zinaweza kuwa dhaifu kiasi hicho... Yes; pengine mmepishana mitazamo na level za uelewa katika mada yako, but siyo kwenye udhaifu. Nitasoma, na kuangalia pande zote kwa kuamini kabisa kuwa nitajifunza toka kila upande wa member aliye changia.

Nakushukuru sana mkuu wangu... Nikutakie weekend njema na wewe pia. Pamoja Saana.
 
Pamoja sana Asha....

Nimelipenda bandiko lako....

Nitarudi...

Bala.

Balantanda... Genuinely huwa unapotea sana. Upo kama haupo. Nimefurahi kukuona na nafurahi zaidi juu ya acknowledgement zako juu ya bandiko. Hivyo nitasubiri kwa hamu input yako. Pamoja saana.
 
Last edited by a moderator:
Mkuu ZeMarcopolo... Nimependa sana hilo bandiko lako. Naona kuna michango ya kutosha... Nitaisoma vema michango ya wadau wote kwa nafasi... Na kama hutajali nimeona niliweke hapa pia kwa manufaa ya wengine sababu inashabihiana sana na hoja niliyowakilisha hapa.

CC: EMT, Mkandara

Unafikiri disaini ya watu ambao ZeMarcopolo amewataja hawapo CCM pia?

CCM hakuna watu wanaofuata upepo?

CCM hakuna wenye malengo ya kupanda haraka na kwa urahisi kwenye arena za kisiasa za kitaifa?

CCM haijafanya mambo ambayo yanakiondoa chama hicho usoni na moyoni mwa Watanzania wanaotaka chama kinachopinga ufisadi?

Kama hayo yanafanyika ndani ya Chadema, basi yatakuwa pia yanafanyika ndani ya vyama vingine kama CCM.

Vyote ni vyama vya siasa na wafuasi wa hivyo vyama ni Watanzania wale wale.

Kwa hiyo, suala linabaki pale pale kuwa tatizo siyo Chadema, CCM au CUF, bali ni Watanzania wenyewe.

Wachawi ni sisi wenyewe wala siyo CCM au Chadema.

Simple as that.
 
Unafikiri disaini ya watu ambao ZeMarcopolo amewataja hawapo CCM pia?

CCM hakuna watu wanaofuata upepo?

CCM hakuna wenye malengo ya kupanda haraka na kwa urahisi kwenye arena za kisiasa za kitaifa?

CCM haijafanya mambo ambayo yanakiondoa chama hicho usoni na moyoni mwa Watanzania wanaotaka chama kinachopinga ufisadi?

Kama hayo yanafanyika ndani ya Chadema, basi yatakuwa pia yanafanyika ndani ya vyama vingine kama CCM.

Vyote ni vyama vya siasa na wafuasi wa hivyo vyama ni Watanzania wale wale.

Kwa hiyo, suala linabaki pale pale kuwa tatizo siyo Chadema, CCM au CUF, bali ni Watanzania wenyewe.

Wachawi ni sisi wenyewe wala siyo CCM au Chadema.

Simple as that.

Uliyoandika yote ni sahihi, lakini umesahau kitu kimoja. In any state at any time t there can never be power vacuum. Hii inamaanisha kwamba ni lazima chama au watu fulani wawe incharge katika kuendesha nchi.

Watu hao kwa hivi sasa ni CCM. Chadema wanatafuta njia ya kuwatoa CCM ili wao waingie. Kwahiyo iwapo chadema watakuja cheaply na kutaka kuiga yanayofanywa na CCM, watawanyima wananchi sababu ya kutaka kuitoa CCM. Kadri Chadema inavyozidi kufanana na CCM ndio jinsi inavyozidi kupunguza uwezekano wa kuishinda CCM.

Angalia mfano wa footbal. Simba na Yanga. Azam ni timu nzuri na pengine hakuna kitu ambacho Simba au Yanga inafanya tofauti na Azam, lakini iwapo Azam inataka kupata washabiki wa aina ya Simba au Yanga itatakiwa kufanya kazi ya ziada.
Chadema imeshindwa kutambua hilo au kama imelitambua basi ubinafsi wa viongozi wake umetawala over jukumu walilo nalo.

Labda nitoe mfano mwingine wa mpangaji ambaye yuko kwenye nyumba inayovuja. Anataka kuhama kwa sababu hataki tena kunyeshewa na mvua. Kabla mkataba wake haujaisha na kabla hajasign mkataba wa kule anakotaka kuhamia anagundua kuwa nyumba anayotaka kuhamia nayo inavuja na mwenye nyumba awali alimwambia kuwa nyumba hiyo haina tatizo ni nzuri. Mpangaji huyu atakuwa na sababu kweli ya kubeba vitu vyake kwenda kwenye nyumba nyingine inayovuja?
 
Labda nitoe mfano mwingine wa mpangaji ambaye yuko kwenye nyumba inayovuja. Anataka kuhama kwa sababu hataki tena kunyeshewa na mvua. Kabla mkataba wake haujaisha na kabla hajasign mkataba wa kule anakotaka kuhamia anagundua kuwa nyumba anayotaka kuhamia nayo inavuja na mwenye nyumba awali alimwambia kuwa nyumba hiyo haina tatizo ni nzuri. Mpangaji huyu atakuwa na sababu kweli ya kubeba vitu vyake kwenda kwenye nyumba nyingine inayovuja?

Kwa hiyo kwako Watanzania ni wapangaji na wenye nyumba ni vyama?
 
Unafikiri disaini ya watu ambao ZeMarcopolo amewataja hawapo CCM pia?

CCM hakuna watu wanaofuata upepo?

CCM hakuna wenye malengo ya kupanda haraka na kwa urahisi kwenye arena za kisiasa za kitaifa?

CCM haijafanya mambo ambayo yanakiondoa chama hicho usoni na moyoni mwa Watanzania wanaotaka chama kinachopinga ufisadi?

Kama hayo yanafanyika ndani ya Chadema, basi yatakuwa pia yanafanyika ndani ya vyama vingine kama CCM.

Vyote ni vyama vya siasa na wafuasi wa hivyo vyama ni Watanzania wale wale.

Kwa hiyo, suala linabaki pale pale kuwa tatizo siyo Chadema, CCM au CUF, bali ni Watanzania wenyewe.

Wachawi ni sisi wenyewe wala siyo CCM au Chadema.

Simple as that.

Nakubaliana na hili... Na kwa mara nyingine nakubali kuwa tatizo ni sisi wa'Tanzania wenyewe... Poor attitudes ndiyo life style yetu.

Hata hivyo EMT it should be noted kuwa pamoja na kuwa Wananchi ndiyo tatizo kubwa, nje ya hapo vyama vya Siasa vina nafasi yake kubwa tu katika lawama; hasa katika kumchezeiya mwananchi.

From you point of opinion... Unadhani kuna hope ya kubadilika kwa attitudes za sie wa Tanzania? Unadhani ni akina nani wanatakiwa kutuamisha ili tutambue kama unavyotambua wewe kuwa tatizo kubwa ni sisi na siyo viongozi peke yake? What do you think should be done?
 
Kwa hiyo kwako Watanzania ni wapangaji na wenye nyumba ni vyama?

Hahahahahahahahahahahahahahaha mkuu huko siko kabisa.
Nimesema kuwa hakuwezi kuwa na power vacuum.
Watanzania hawawezi kuwa wapangaji ila wao ndio wanaamua chama gani cha kukiajiri.
Kama wameshakiajiri chama kimoja na kinakuja kingine kutaka kukitoa kile walichokiajiri, wanahitaji kuona added value kwenye hiki chama kipya. Wasipoiona tutaishia kwenye ile methali ya "zimwi likujualo,..."
 
Nakubaliana na hili... Na kwa mara nyingine nakubali kuwa tatizo ni sisi wa'Tanzania wenyewe... Poor attitudes ndiyo life style yetu.

Hata hivyo EMT it should be noted kuwa pamoja na kuwa Wananchi ndiyo tatizo kubwa, nje ya hapo vyama vya Siasa vina nafasi yake kubwa tu katika lawama; hasa katika kumchezeiya mwananchi.

From you point of opinion... Unadhani kuna hope ya kubadilika kwa attitudes za sie wa Tanzania? Unadhani ni akina nani wanatakiwa kutuamisha ili tutambue kama unavyotambua wewe kuwa tatizo kubwa ni sisi na siyo viongozi peke yake? What do you think should be done?

Kuhusu vyama kuchukua share ya lawama sawa, lakini hivyo vyama ni artificial persons wanaongozwa na real persons ambao ni Watanzania vile vile. Au unataka kuniambia viongozi wa vyama ni foreigners?

Kuhusu kubadilika kwa attitudes za Watanzania inawezekana kabisa kama wakiamua kufanya hivyo. Lakini itabidi kubadilisha attitudes za kila kitu. Tunatakiwa kuchange attitudes zetu siyo kisiasa tuu bali kwa kila kitu.

Kuhusu ni akina nani wanatakiwa kutuamsha ili tutambue kuwa tatizo kubwa ni sisi na siyo viongozi peke yake, ni sisi Watanzania wenyewe. Tusitegemee kabisa kuwa someone will come from somewhere to rescue us. Never.

Kama nilivyosema mwanzoni watu wengi wanaamini kabisa kuwa things have fallen apart and "It is no Longer at Ease". But either they're doing nothing because they strongly believe that "A Man of the People" will come and rescue them or that "The Beautiful Ones are not yet Born".

Lakini the majority of us are afraid of "The Petals of Bloods". We're still afraid to face "The Trial of Dedan Kimathi". Kwa hiyo hata akitokezea mtu kutoka sayari nyingine atakuta wengi tayari wameshaamka lakini wanaogopa kutoka nje kwa sababu kuna kiubaridi.
 
Hahahahahahahahahahahahahahaha mkuu huko siko kabisa.
Nimesema kuwa hakuwezi kuwa na power vacuum.
Watanzania hawawezi kuwa wapangaji ila wao ndio wanaamua chama gani cha kukiajiri.
Kama wameshakiajiri chama kimoja na kinakuja kingine kutaka kukitoa kile walichokiajiri, wanahitaji kuona added value kwenye hiki chama kipya. Wasipoiona tutaishia kwenye ile methali ya "zimwi likujualo,..."

Kwa hiyo ulikuwa na maana gani ulipotumia mfano wa mpangaji na mpangishaji.

Kisiasa unaweza kuwa sahihi kusema kuwa hakuwezi kuwa na power vacuum, and, in deed, some politicians become untouchable because of fear of any backlash occurring in a power vacuum situation. But who posses that power anyway? Politicians or the people?

Power vacuum is a myth. There is no such thing as a power vacuum that must be filled by political power. Social power, the kind made up of peaceful interactions and exchanges, is more than sufficient to create social order.

As philosopher Roderick Long wrote, "if by ‘politics' is meant the legalised oppression practiced by governments, then certainly libertarians are fighting for the abolition of politics."
 
Mkuu,

Hayo ni mawazo yangu... Nitaheshimu yeyote atakae sema sina hoja kwa hoja lakini si kwa hoja ya vioja kama uliyo acha hapa.

"Emancipate yourselves from Mental Slavery,
NON but Ourselves can Free our Minds"
- Bob Marley (Redemption Song)

 
Uchaguzi wa 2015 CHADEMA au Wapinzani hawawezi kuishinda CCM hata iweje, hata kama Uchaguzi uwe free & fair kuliko yote Duniani, bado hakuna Chama kinaweza kuishinda CCM kwa kura hapa Tanzania 2015 ni mapema mno, mimi kama kuna kitu ningeweza kuwashauri CHADEMA ni kuwekeza nguvu zote kwenye Udiwani na Ubunge, wahakikishe wanapata Madiwani wengi zaidi ili waweze kuongoza Halmashauri na Miji mingi zaidi, na hapo sasa ndio waonyeshe mfano kwa kuhakikisha Halmshauri na Miji wanayoiongoza inakuwa Mifano ya kuigwa ukilinganisha na Halmashauri za CCM, hapo ndipo sasa wanapoweza kuwapata Wananchi wengi sana na kuwahakikishia Ushindi 2020 au 2025, kwa maana watakuwa na cha kuongelea na kulinganisha!

Ila kwa hali ilivyo sasa wanaongea tu, mara Bw. Lowasa fisadi, mara sijui CCM Mafisadi, wananchi wengi wanasema hawa wanasema hivi kwa kuwa wako nje hata wao wakiingia watafanya hivyo hivyo, lkn kama wakiwa na Halmashauri labda zenye shule bora Tanzania, zinaongoza kwenye matokeo, au zinazosimamia mapato yetu vizuri, basi watakuwa na cha kutambia, bila hivyo hamna miujiza!

Kwenye Wabunge wahakikishe kwamba 2015 wana double idadi ya Wabunge wao, na hilo litawasaidia sana kuanzia 2015 kwenda 2020 kwa maana watakuwa na Sauti Bungeni na wanaweza kukwamisha mambo mengi sana yenye maslahi kwa umma Bungeni hata kuiangusha Serikali ikibidi!

Vinginevyo wakiwekeza sana kwenye kushinda Uraisi na wakaja kushindwa ndio utakuwa mwisho wa CHADEMA kama tuijuavyo, kitu ambacho sio kizuri kwa Demokrasia yetu!

Na ushahidi wa haya ninayosema utaonekana kwenye Chaguzi 2014, tutaona jinsi CCM itavyoshinda kwa kura nyingi yetu macho!
 
"Emancipate yourselves from Mental Slavery,
NON but Ourselves can Free our Minds"
- Bob Marley (Redemption Song)


Have No fear for a atomic energy, 'coz NONE OF THEM CAN STOP THE TIME! How long shall they kill our prophets, while we stay aside an' look..."

UKOMBOZI WA FIKRA. Komboa FIKRA ZA MTU na miguu yake itafuata automatically! Werevu walishaona hlo zamani... Nilitaraji leo MIJADALA MIKUBWA IWE NI KWA NAMNA GANI TUTAKOMBOA FIKRA ZETU, lakini ajabu bado tunahangaika na miguu yetu wakati FIKRA MFU. Hata kama miguu itakuwa imara kiasi gani, wapo wenye imani zao watakaoliwa na simba pasi kukimbia wakiamini Muujiza utatokea simba atageuka kuwa mwanakondoo. FIKRA MFU!

Tunahangaika na kubadili viongozi wakati FIKRA za raia wengi ni Kuchukua chao mapema? Tunahangaika na kuwekeza kwenye viwanda, wakati fikra za walio wengi ubora wa bidhaa yoyote ni lazima itengenezwe na mzungu (iwe imported). Tunahangaika na mikataba mizuri ya madini, wakati Fikra za wengi ni aje atajinufaisha binafsi? Kesho huyu wa mgodini, akihongwa Vx aseme madini yaliyopatikana ni gram 10 wakati ni zaidi g 50, akatae kwa fikra zipi wakati zilizopo ni za chukua chako mapema na thamani ya mtu ni KITU chake? Je, chini ya huo mkataba mzuri hatujaibiwa bado? Kwani wanaoruhusu twiga kusafirishwa nje si watanzania sisi wenyewe? Je, ni FIKRA za wangapi haziwezi kufanya hlo? Si labda 5% tu? Wanaowinda FARU na TEMBO wetu si sisi wenyewe?

Tofauti yetu ni huyu ataiba TEMBO huyu Sungura, kulingana na nafasi zetu. Lakini wote ni sawa tu, FIKRA ZETU MFU wote ni Wabomoa Taifa, HATUJENGI! TUKOMBOE FIKRA ZETU KWANZA. Tukiwekeza 50% ya jitihada zetu katika kupigani UKOMBOZI WA FIKRA, baada ya miaka 10 tutaona tulipofika.

Tukiendelea kuimba nyimbo za Wanasiasa, mara Maisha bora kwa kila mtanzania, Nguvu ya umma, Haki sawa kwa wote, Kilimo Kwanza, Serikali ya Majimbo, Muungano wa Mkataba, n.k tutakuwa TUNAWACHEKEA NYANI SHAMBANI, atakayeshangaa kuvuna mabua anastahili KUNYONGWA.

Huwezi kuishangaa CDM leo, pasi kuishangaa CCM, na huwezi kuishangaa CCM leo, pasi kuishangaa CDM. Kwangu wao si chanzo cha Utumwa wetu wa Fikra, ila ni miongoni mwa waendelezao utumwa huo.

UKOMBOZI U MIKONONI MWETU, MIMI NA WEWE. Ni SISI.
Mungu wetu yu tayari kutushindia vitani. Anaita sasa!
 
Back
Top Bottom