Kwa Mzozo huu wa Congo DR na Rwanda nani ananibishia kuwa EAC haiendi kufa na Wazungu kufurahia?

Kwa Mzozo huu wa Congo DR na Rwanda nani ananibishia kuwa EAC haiendi kufa na Wazungu kufurahia?

Tayari Tanzania, Burundi na Nusu ya Wakenya wanaisapoti Congo DR huku pia Uganda na Nusu ya Wakenya wakiisapoti Rwanda.

Wazungu ambao Siku zote hawataki Kuiona Jumuiya hii ya Afrika Mashariki ikistawi wamefanikiwa Kutugombanisha na kwa Uzuzu wa Wanaogombanishwa wamekubali Kuingia katika huu Mtego wa Kimkakati.

Hivi kwa Miradi mingi ya Kimaendeleo na Kimkakati Iiliyoko katika Jumuiya hii ya EAC mnadhani Congo DR na Rwanda (Wanachama wa EAC) zikiingia Vitani hawa Marafiki zao wakubwa Tanzania hatomsaidia Congo DR au Uganda haitomsaidia Rwanda?

Mnaacha kuwa Neutral katika huu Mzozo sasa Tanzania imeamua kuchukua upande kwa Kuisaidia Kisiri Congo DR kwa mategemeo ya kupata Tenda na Fursa nyingi za Kibiashara na hata Kumegewa kidogo Madini ya Congo DR Ili yawasaidie.

Na Uganda nayo vile vile (japo Kisiri) imeamua kuwasaidia Rwanda kwa ahadi ya Kufaidika na Madini ambayo kwa 60% yako upande wa Jirani na Taifa la Rwanda na chini ya Udhibiti mzuri wa Jeshi la Rwanda.

Saaa ni rasmi kuwa Vita ya Panzi huwa ni Furaha kwa Kunguru hivyo basi Mzozo huu wa Congo DR na Rwanda na kwa nchi za Tanzania na Uganda nao kuchukua upande wa Kuzisaidia ni Ushindi mkubwa kwa Wazungu ambao wametumia Akili Kubwa Kutugombanisha ili Jumuiya ya EAC isifanikiwe na waendelee Kutugawa ili tuendelee Kuwategemea huku Wao Wakitunyonya (hasa katika Rasilimali zetu) kutokana na Upan'gang'a (Upumbavu) tulionao.

Tulianza na Free Trade, kisha Customs Union, tupo njiani kwenda katika Monetary Union kisha tumalize na Political Federation ili EAC ikamilike kwa 100% ila kwa huu Upuuzi uliochanganyika na Unafiki wetu na Chuki zetu sioni Ukamilifu huu wa Kimalengo kwenda Kutimia na baadae kila nchi itaamua kuendelea na yake.

Wenye Akili tuliliona hili zamani mno.
wala usiseme wazungu kufurahia. speed ya kuingiza wanachama inatisha ni wazi itapasuka na kufa. kosa lilianza pale walipopitisha rwanda na burundi kuwa wanachama. Kosa kubwa wameingiza nchi ambazo bado si stable-DRC na South Sudan na tayari wanapika kosa lingine la kuiingiza somalia. EAC itakuja kuwa hopeless integration kama south asia ambayo members wake wamo india, pakistan, bangladesh na burmer(sina hakika kama burmer yumo)
 
Ni lini Uganda na Rwanda walisuluhisha migogoro yao, mpaka leo wawe marafiki!? hivi mpaka wa gatuna ulishafunguliwa?
Huna Akili na ndiyo maana huwa nawadharau baadhi ya Watanzania. Tokea Miezi kadhaa iliyopita mwaka huu Uganda kupitia Mtoto wa Rais Museveni Muhoozi Kainerugaba kwa Niaba ya Baba yake alienda Rwanda Kuzungumza na Rais Kagame na Kumaliza Mgogoro wao na huo mpaka Kufunguliwa rasmi na hata BBC walifanya Coverage yake na Walipongezwa mno.

Wiki Mbili baada Officially Rais Museveni alienda Rwanda na baada ya Mwezi Rais Kagame nae akaenda Uganda na mpaka hivi sasa naandika hivi ni kwamba Uhusiano wa Uganda na Rwanda umerejea na tena ndiyo umekuwa Imara kuliko hata ilivyokuwa awali.
 
Tayari Tanzania, Burundi na Nusu ya Wakenya wanaisapoti Congo DR huku pia Uganda na Nusu ya Wakenya wakiisapoti Rwanda.

Wazungu ambao Siku zote hawataki Kuiona Jumuiya hii ya Afrika Mashariki ikistawi wamefanikiwa Kutugombanisha na kwa Uzuzu wa Wanaogombanishwa wamekubali Kuingia katika huu Mtego wa Kimkakati.

Hivi kwa Miradi mingi ya Kimaendeleo na Kimkakati Iiliyoko katika Jumuiya hii ya EAC mnadhani Congo DR na Rwanda (Wanachama wa EAC) zikiingia Vitani hawa Marafiki zao wakubwa Tanzania hatomsaidia Congo DR au Uganda haitomsaidia Rwanda?

Mnaacha kuwa Neutral katika huu Mzozo sasa Tanzania imeamua kuchukua upande kwa Kuisaidia Kisiri Congo DR kwa mategemeo ya kupata Tenda na Fursa nyingi za Kibiashara na hata Kumegewa kidogo Madini ya Congo DR Ili yawasaidie.

Na Uganda nayo vile vile (japo Kisiri) imeamua kuwasaidia Rwanda kwa ahadi ya Kufaidika na Madini ambayo kwa 60% yako upande wa Jirani na Taifa la Rwanda na chini ya Udhibiti mzuri wa Jeshi la Rwanda.

Saaa ni rasmi kuwa Vita ya Panzi huwa ni Furaha kwa Kunguru hivyo basi Mzozo huu wa Congo DR na Rwanda na kwa nchi za Tanzania na Uganda nao kuchukua upande wa Kuzisaidia ni Ushindi mkubwa kwa Wazungu ambao wametumia Akili Kubwa Kutugombanisha ili Jumuiya ya EAC isifanikiwe na waendelee Kutugawa ili tuendelee Kuwategemea huku Wao Wakitunyonya (hasa katika Rasilimali zetu) kutokana na Upan'gang'a (Upumbavu) tulionao.

Tulianza na Free Trade, kisha Customs Union, tupo njiani kwenda katika Monetary Union kisha tumalize na Political Federation ili EAC ikamilike kwa 100% ila kwa huu Upuuzi uliochanganyika na Unafiki wetu na Chuki zetu sioni Ukamilifu huu wa Kimalengo kwenda Kutimia na baadae kila nchi itaamua kuendelea na yake.

Wenye Akili tuliliona hili zamani mno.
comrade....umenifanya nisikitike sana aisee!!!...inawezekana rais samia amekaribishwa china ili azinduliwe akili kuhusu upuuzi huu wa wazungu
 
Mleta mada akili fupi?
Wazungu wafurahije kwa maslahi gani ambayo wanayakosa kwa sasa?
 
Huenda uchumi wa Rwanda unategemea madini ya DRC. Ni mbinu za kuteka maeneo ili wazidi kupeta kiuchumi. Sasa tuache unafiki, EA iwe upande wa DRC.
 
Diplomasia toka 1999 lakini haikuzaa matunda hivo tsheked anachofanya ni sahihi ifikie mambo yawe wazi na dunia ijue Rwanda ni sababu kuu ya kuvuruga amani ya Congo maana kama ni waasi vipo vikundi zaidi 40 lakini M23 ndio yenye nguvu ya kufanya full attack, popote ndani ya DRC kwakua ni jeshi la nchi nyingine ndani ya nchi nyingine
Uwezo wa Fdlr kuwa tishio kubwa kwa Rwanda ni wa kutiliwa shaka, nakubaliana kwa sehemu na wewe huenda uwepo Fdlr unatumika kama sababu ya kudumisha uwepo wa Rwanda huko Kivu na kuzuia kujitanua kwa ushawishi wa hasimu zake Uganda na Burundi.

Ila kitendo cha Drc kuruhusu majeshi ya Uganda na Burundi kuendesha operation huko Drc huku Rwanda ikiwekwa kando huenda imechangia kwa Rwanda kuanzisha upya huu uasi wa M23.
Count Capone Bukyanagandi mtu chake zitto junior
 
Kama jumuuia ya Africa mashariki kabla ya Congo kujiunga, tulifanya makosa kuruhusu DR Congo yenye migogoro rukuki tangu ipate uhuru miaka ya 60 kujiunga na sisi. Ni kama tume nunua hiyo migogoro isiyo isha. Kwa akili hizo hizo tuliiruhusu South Sudan kujiunga na sisi. Na Sasa mzee wa migogoro mwingine Somalia naye ametuma maombi kujiunga na EAC. Popote duniani ukiwa na matatizo ktk nchi yako na unataka kujiunga ktk umoja fulani lazima uambiwe ' Clean up your mess first before you join us' Tulipaswa tuambie South Sudan, DR Congo na Sasa Somalia hivyo.
 
Uwezo wa Fdlr kuwa tishio kubwa kwa Rwanda ni wa kutiliwa shaka, nakubaliana kwa sehemu na wewe huenda uwepo Fdlr unatumika kama sababu ya kudumisha uwepo wa Rwanda huko Kivu na kuzuia kujitanua kwa ushawishi wa hasimu zake Uganda na Burundi.

Ila kitendo cha Drc kuruhusu majeshi ya Uganda na Burundi kuendesha operation huko Drc huku Rwanda ikiwekwa kando huenda imechangia kwa Rwanda kuanzisha upya huu uasi wa M23.
Count Capone Bukyanagandi mtu chake zitto junior

Fuatilia jinsi Kigali ilivokua ina operate kinshasa hadi kua na mkuu wa majeshi mnyarwanda ambae baadae alikua waziri wa ulinzi, lakini pia chief of intelligence wa DRC aliwahi kua mnyarwanda, visa pale ni vingi sana na kagame anajua nini afanye kuivuruga Congo na aendelee kuiba madini ya Congo, Kagame huyuhuyu alishakua mkurugenzi wa usalama wa Uganda kipindi wametoka porini na Museveni so kitu utakachojua wewe leo kwenye intelijensia PK anakijua vyema, sasa hoja kubwa kinshasa inajua kabisa Mfaransa, Mmarekani, na Mbeligiji anaiba pia Congo lakini wakulinda hayo maslahi ni Kagame ndio anatumika vyema kwa hoja hiyo huwezi kusikia west inamkemea PK hata itoke ripoti gani, lakini Kabila sr nae alijichanganya kusaini ile mikataba ya Rwamagana ambapo alikubali kuachia eneo ambalo walikuepo wacongoman wanaoongea kinyarwanda ambao ni watutsi ambapo huitwa Banyamulenge wanaokalia maeneo ya Gisenyi, Bunagana, Rutsuru, Goma, na maeneo mbalimbali ya Kivu province
 
Ina maana FARDC haina uwezo au imeshindwa kuilinda nchi yao..... viongozi wa Drc ni sehemu pia ya tatizo kwa kuwa na jeshi dhaifu

Uwezo wa kijeshi ni zaidi ya wingi wa askari kagame aliwekeza kwenye teknolojia sana huku akisaidiwa kusuka jeshi lake na marekani na Israel na kwa east Afrika ni Rwanda pekee hupokea msaada mkubwa wa kijeshi kutoka west, kagame na museveni hawachelewi kujifanya wanapigana vita ndani ya congo ili wakamilishe mission zao za wizi, sasa akipatikana kamanda wa jeshi la kongo mpambanaji kama Mamadou Ndala analiwa kichwa mapema sana atoe kiwingu, japo FARDC Wakikomaa huku wakisindikizwa na Tanzania na Burundi watamsumbua sana Kagame na ziara za Tshekedi majuzi ilikua ni pirposely upokezi wa silaha za DRC ilizonunua kuongeza nguvu huku akitafuta uungwaji mkono ili amtandike PK , na jana balozi wa Rwanda kafurushwa kinshasa hapo ujue FARDC wako standby muda wowote na hawataki kuiona M23 ikishamiri maana ukiwachekea M23 wakajiimarisha kuwatoa mbeleni itakua kazi sana kwanza wamekalia maeneo yenye Oral ( dhahabu,) na Diama ( Almasi) na madini mengine ya thamani
 
[emoji1][emoji1][emoji1]
Screenshot_20221030-151254.jpg
 
EAC ipi hii ya Rais Samia wa Tanzania na Rais Ndayishimiye wa Burundi kumsaidia kwa Siri Rais Tshisekedi na Congo DR yake huku Rais Museveni nae wa Uganda akimsaidia kwa ukaribu mno Mdogo wake na Nduguye Rais Kagame wa Rwanda?
Kesho Uganda ikikalia eneo la Tanzania kimabavu,kwa hiyo itasaidiwa na Rwanda kutupiga!!??
 
Uwezo wa kijeshi ni zaidi ya wingi wa askari kagame aliwekeza kwenye teknolojia sana huku akisaidiwa kusuka jeshi lake na marekani na Israel na kwa east Afrika ni Rwanda pekee hupokea msaada mkubwa wa kijeshi kutoka west,
Hizo silaha anazopokea lazima zinapitia Kenya, hivyo Kenya kama mwanachama wa EAC akishirikiana na wenzake ana nafasi kushinikiza suluhu kwa huu mzozo.
 
Hizo silaha anazopokea lazima zinapitia Kenya, hivyo Kenya kama mwanachama wa EAC akishirikiana na wenzake ana nafasi kushinikiza suluhu kwa huu mzozo.

Silaha atapitishia Bandari ya Dar na hua zinakua na escort ya JWTZ na wakifika Rwanda RDF hujulishwa nini kinapita ndio itifaki ya usafirishaji wa silaha na akipitia kenya atasindikizwa na KDF akifika Uganda UPDF hufahamishwa nini kinapita kwao hiyo ndio itifaki ili msafara usishambuliwe
 
 
Kesho Uganda ikikalia eneo la Tanzania kimabavu,kwa hiyo itasaidiwa na Rwanda kutupiga!!??

Fahamu kua udugu wa Rwanda na Uganda hua ni wakipekee ulianzia kwa RPG , rwegyema, kagame, mwasa na makamanda wengine kupigana msituni na kumweka museveni madarakani, na hawawezi kuachana, Baada ya pale museveni akawasaidia ndugu zake hao kushika madaraka Rwanda na ikawa hivo lakini Museveni mzee ana heshima ya kipekee kwa Tanzania licha ya kua trained Tanzania na undugu na familia ya mwalimu Nyerere na urafiki na wazee kama Butiku kamwe hawezi kuipiga Tanzania isipokua atajitahidi asuluhishe kama alivyokua akifanya mara zote inapotokea mzozo baina ya Dar na kigali, na historia ya maziwa makuu utaishangaa Rwanda na Burundi huongea Lugha moja na watu wa Ngara, kigoma lakini Baganda hushabihiana lugha na wahaya, lakini pia Nyankole na rwanda na kerewe na zinza huchangia baadhi ya maneno kwenye lugha zao kama ilivo masai Tanzania na kenya, jaluo Tanzania na kenya interection ni kubwa mno japo kagame anavuruga kwa wizi wake wa mali ya kongo
 
Back
Top Bottom