Kwa nini tuwaombee waliokufa?

Kwa nini tuwaombee waliokufa?

Mkuu hebu eleza kwa uzuri pale ambapo Petro alipomuona Musa na elia mpaka akamwambia Bwana na tujenge vibanda vitatu. Ikiwa waliokufa hawana uhusiano kabisa na walio hai je ni kwanini tena hawa walionekana. Nafikiri waweza eleza vizuri ili tuweze kuelewa nahisi lina uhusiano kidogo na mada hii. Please!!!!!!!!!!!!!!!
Mkuu, kwanza kabisa, Musa alivyokufa inadaiwa alizikwa na Mungu kama nimekosea unirekebishe... Ila Eliya inasemekana hakufa mara ya kwanza mara ya pili Yohana alikuja kwa roho ya eliya..
Pia bibilia haionyeshi lengo la wao kuja ama kuonekana kama linahusiana moja kwa moja na kutoa ujumbe kwa watu.
Nachoweza kusema, Sehemu kubwa bibilia ilikuwa haijadhihirisha kama kweli wafu waliokufa kwa ajili ya bwana, wapo mahali wanaishi pengine hapa (Mathayo17:1-13) palitosha kuthibitisha hilo kwa kuwaona Musa na Eliya, kupitia Petro, Yakobo na Yohane ukizingaita kwa mila za wayahudi ushahidi wa watu wa tatu ni kweli. kumbuka stori za wasadukayo na mafarisayo (matendo ya mitume 23:5, Mathayo 16:6, Mathayo 22:23, Marko 12:18-27), .

Vilevile Yesu kupitia mfano wa Lazaro: alisema Kuna Musa na MAnabii.. Ujumbe wa Yesu namna ufalme wa mbinguni unavyofanana, ni kwamba huwezi kutumia MAli ya Dunia kununua Uzima wa Milele kama ambavyotajiri hakuweza, pia hawezi mtu kutoka kuzimu akaja kukufundisha ukaamini injili, ikiwa huamini waliopo huwezi amini hata akitoka mtu kule akaja.

Pia tunapenda kuamini kuwa wafu wanaweza kurudi kwa lengo kuu ni ili tuwatumainie wao katika maisha yetu. Bibilia imesema amelaaniwa mtu yule amtegemeaye mwanadamu kuwa kinga yake, na huku moyoni amemwacha Mungu.

Kwa lugha nyingine wa kumtumaini sio mfu bali aliye hai ambaye amefufuka katika wafu(Yesu Kristo). KWani wafu hawana kumbukumbu yoyote tena...

Pia hapa kuna hili swala la "Bikira maria Mwombezi wetu" na stori ya watoto wa fatma: fransisca yasinta na lucia.. Binafsi napata shida kulitetea. Kwani MAria alionja mauti.

naweza tu kusema jambo moja: Mithali 16:25 Iko njia ionekanayo kuwa sawa machoni pa mtu; Lakini mwisho wake ni njia za mauti.

Kwani njia za Mungu si njia zetu na mawazo yetu si mawazo ya Mungu. KAma vile mbingu zilivyo juu sana ndivyo mawazo yake yalivyo dhidi ya mawazo yetu. Ila njia ya Munhu ni Njia ya Yesu kwani Yesu ni njia...
warumi 10:13


Ni heri ukichagua hard way usije ukapunguza NENO nawe ukajapunguziwa sehemu katika ule mti wa UZima.
matendo
11:4 Wala hakuna wokovu katika mwingine awaye yote, kwa maana hapana jina jingine chini ya mbingu walilopewa wanadamu litupasalo sisi kuokolewa kwalo.

mtumaini Mungu peke yake, kama ilivyoandikwa kifo ni mara moja na baada ya kifo ni hukumu (waebrania 9:25).......until further notice..
.
 
Hiyo ni biblia ya wakatoliki na ukatoliki si ukristo ni uislamu unaoamini katika mungu mke kabla ya version ya pili ya uislamu amabayo vatican walimpa muhamad ili kuwatoa waarabu kwa kristo yesu.
Mkuu Imani zote zilizo asi katoliki zimekuwa zikifanya blunder worldwide.. kuanzia kuruhusu divorce, utoaji mimba, mauaji ya huruma, u-gay na mambo mengine.. limebaki kanisa katoliki palepale..tena huwa halina tabia ya kujadili madhehebu mengine yoyote ama dini nyingine zozote katika mafundisho yao.. kama wafanyavyo evangelical christians ambao hawaachi kupondea katoliki na kujivuna lakini hatma zao sikuzote imekuwa aibu.... jaribu kufikiri tofauti.

Pia ningeomba uniambie nini maana ya pale yesu alipomwambia petro kwamba ni mwamba?
 
Hiyo ni biblia ya wakatoliki na ukatoliki si ukristo ni uislamu unaoamini katika mungu mke kabla ya version ya pili ya uislamu amabayo vatican walimpa muhamad ili kuwatoa waarabu kwa kristo yesu.

Nahisi wewe ni masalia halisi...

Masikini hujui hata historia ya Biblia..Hujui kuwa Vitabu vilipunguzwa na Martin Luther...

Daah....Ila wafuasi wa mama Hellena ni tabu ingine katika dunia..
 
Hiyo ni biblia ya wakatoliki na ukatoliki si ukristo ni uislamu unaoamini katika mungu mke kabla ya version ya pili ya uislamu amabayo vatican walimpa muhamad ili kuwatoa waarabu kwa kristo yesu.

ha ha ha!!!
 
Mkuu, kwanza kabisa, Musa alivyokufa inadaiwa alizikwa na Mungu kama nimekosea unirekebishe... Ila Eliya inasemekana hakufa mara ya kwanza mara ya pili Yohana alikuja kwa roho ya eliya..
Pia bibilia haionyeshi lengo la wao kuja ama kuonekana kama linahusiana moja kwa moja na kutoa ujumbe kwa watu.
Nachoweza kusema, Sehemu kubwa bibilia ilikuwa haijadhihirisha kama kweli wafu waliokufa kwa ajili ya bwana, wapo mahali wanaishi pengine hapa (Mathayo17:1-13) palitosha kuthibitisha hilo kwa kuwaona Musa na Eliya, kupitia Petro, Yakobo na Yohane ukizingaita kwa mila za wayahudi ushahidi wa watu wa tatu ni kweli. kumbuka stori za wasadukayo na mafarisayo (matendo ya mitume 23:5, Mathayo 16:6, Mathayo 22:23, Marko 12:18-27), .

Vilevile Yesu kupitia mfano wa Lazaro: alisema Kuna Musa na MAnabii.. Ujumbe wa Yesu namna ufalme wa mbinguni unavyofanana, ni kwamba huwezi kutumia MAli ya Dunia kununua Uzima wa Milele kama ambavyotajiri hakuweza, pia hawezi mtu kutoka kuzimu akaja kukufundisha ukaamini injili, ikiwa huamini waliopo huwezi amini hata akitoka mtu kule akaja.

Pia tunapenda kuamini kuwa wafu wanaweza kurudi kwa lengo kuu ni ili tuwatumainie wao katika maisha yetu. Bibilia imesema amelaaniwa mtu yule amtegemeaye mwanadamu kuwa kinga yake, na huku moyoni amemwacha Mungu.

Kwa lugha nyingine wa kumtumaini sio mfu bali aliye hai ambaye amefufuka katika wafu(Yesu Kristo). KWani wafu hawana kumbukumbu yoyote tena...

Pia hapa kuna hili swala la "Bikira maria Mwombezi wetu" na stori ya watoto wa fatma: fransisca yasinta na lucia.. Binafsi napata shida kulitetea. Kwani MAria alionja mauti.

naweza tu kusema jambo moja: Mithali 16:25 Iko njia ionekanayo kuwa sawa machoni pa mtu; Lakini mwisho wake ni njia za mauti.

Kwani njia za Mungu si njia zetu na mawazo yetu si mawazo ya Mungu. KAma vile mbingu zilivyo juu sana ndivyo mawazo yake yalivyo dhidi ya mawazo yetu. Ila njia ya Munhu ni Njia ya Yesu kwani Yesu ni njia...
warumi 10:13


Ni heri ukichagua hard way usije ukapunguza NENO nawe ukajapunguziwa sehemu katika ule mti wa UZima.
matendo
11:4 Wala hakuna wokovu katika mwingine awaye yote, kwa maana hapana jina jingine chini ya mbingu walilopewa wanadamu litupasalo sisi kuokolewa kwalo.

mtumaini Mungu peke yake, kama ilivyoandikwa kifo ni mara moja na baada ya kifo ni hukumu (waebrania 9:25).......until further notice..
.

Kuhusu Maria, soma Kumbukumbu 18:11-12.
 
Ndugu G'taxi kunamakosa nimeona katika maandishi yako, mwanzo nilidhani ni typing error lakini naona yanajirudia rudia, kwa kukusaidia tu hebu jaribu kujifunza matumizi sahihi ya R na L, hii ni kwa manufaa yako. kwaheri
 
Last edited by a moderator:
Ndugu G'taxi kunamakosa nimeona katika maandishi yako, mwanzo nilidhani ni typing error lakini naona yanajirudia rudia, kwa kukusaidia tu hebu jaribu kujifunza matumizi sahihi ya R na L, hii ni kwa manufaa yako. kwaheri

kunamakosa - kuna makosa
nimeona - nimeyaona.
 
Last edited by a moderator:
Ndugu G'taxi kunamakosa nimeona katika maandishi yako, mwanzo nilidhani ni typing error lakini naona yanajirudia rudia, kwa kukusaidia tu hebu jaribu kujifunza matumizi sahihi ya R na L, hii ni kwa manufaa yako. kwaheri

Hakuna mahala hujaelewa ndugu,hatupo hapa kufundisha kiswahili..si lazima sana uchangie tusichokihitaji,pita tu uendelee
 
Last edited by a moderator:
Unaijua Historia ya Biblia....Unajua kwann vitabu 73 na wengine 66....Fiatilia page tumetoa somo zuri...
Haya tena. Muhammad anasema uongo bila ya aibu. Hebu tumsome.

Kasema Mtume (S.a.w)
"Hakika maiti anajua nani anaembeba, na nani anaemuosha, na nani anaemtia kaburini mwake" (Mweli Mwaminifu, Juzuu ya 1-2, Hadithi Na. 422, Uk. 188)


MWAMDISHI SHEIKH SAID MOOSA MOHAMED AL-KINDY
Hivi jamani unaposema maiti kuna kujua tena? kuna uhai tena? yaani muislamu akifa, yule anaemosha, yaani anaemkamua mavi, anaemtia kidole matakoni kuhakiki kama mavi yote yameisha, anamjua, maana kuna siri hapo kwenye kukamua, wanaambiwa wasitoe siri hiyo nje, kwa ushahidi huu


Kasema Mtume (S.a.w) "Anaeosha Maiti basi aanze kwa kumkamua" (Mkweli Mwaminifu, Juzuu ya 1-2 Hadithi Na. 423, Uk. 188)


423 Na muradi wa kukamua, si kama inavyokamuliwa nguo, la: bali analazwa chali, kisha anakalishwa nkitako na huku anakandamizwa kidogo kidogo tumboni kisha unamrejesha tena chali kisha unamuinua kumkalisha na mkono wako uwe tumbono mwake, unafanya hivyo mara tatu, kisha unamosha tena. Na ikiwa umemtoka uchafu wote tumboni kwa njia ya haja utupu wa nyuma, Bai useme kitu wala msimwambie mtu, ukitoa siri yake maiti basi hupati thawabu, na badili yake unapata madhambi.


Hapo kwenye usitoe siri ndipo penye kutiana vidole makalioni kwa maiti maana huwezi jua kama uchafu umeisha mpaka umtie kidole kwa pamba au kitambaa cheupe,uone umetoka uchafu wa rangi gani, maana miti yule kwa mujibu wa Muhammad, anajua kabisa fulani kanitia kidole matakoni, kwa hivyo muislamu akitoa siri hiyo basi anapata dhambi, badala ya thawabau. SASA TUJIULIZE, JE Maiti anakuwa na ufahamu wowote? anaejua yote hayo ni marehemu aliye hai? Msikilize Mfalme Sulemani anavyosema.


Muhubiri 9:5 kwa sababu walio hai wanajua ya kwamba watakufa; lakini wafu hawajui neno lo lote, wala hawana ijara tena; maana kumbukumbu lao limesahauliwa


Kwa ushauri wangu, waislamu msitishike na hao maiti wenu, hawajui lolote, kwa hivyo hizo siri tupeni manzowafanyia hao marehemu wenu.



 
Nahisi wewe ni masalia halisi...Masikini hujui hata historia ya Biblia..Hujui kuwa Vitabu vilipunguzwa na Martin Luther...Daah....Ila wafuasi wa mama Hellena ni tabu ingine katika dunia..
safi mkuu, tena anatakiwa ajue yupo kwenye laana kwakuishi ndani ya sheria... na founder hellen white alikuwa freemanon by origin..
Seventh-day Adventist Cult Exposed

Truth about Seventh Day Adventist Church


ellen_g_white-freemasonry.jpg
 
Kuhusu Maria, soma Kumbukumbu 18:11-12.
Linasema hivi:
Kumbu 18:11 wala mtu alogaye kwa kupiga mafundo, wala mtu apandishaye pepo, wala mchawi, wala mtu awaombaye wafu.12 Kwa maana mtu atendaye hayo ni chukizo kwa Bwana; kisha ni kwa sababu ya hayo Bwana, Mungu wako, anawafukuza mbele yako.

asante
 
Mmmmh Matin luther simjui hata vitabu vy a Yakobo sijaviona kavitoa wapi na kapeleka wapi?
Hivi nyinyi muambiweje mjue kuwa vitabu hivyo viliondolewa na Martin Luther...? Na baada ya kuviondoa aliviwekka kama Index mpaka alipokuja kuviondoa moja kwa moja...

Kwataarifa yako hakuondoa vitabu hivyo tuu pia alitaka kuondoa kitabu cha Yakobo na Ufunuo...Tumshukuru Mungu Reformer mwenzake Calvin alimkataza...

Ngoja nikuulize...Hivi kama angefanikiwa kuviondoa vitabu vya Yakobo na Ufunuo na leo mngekuja kulalalma...?
 
Ila sio kama naikana dini yangu naipenda...ila kunamaswali najiuliza sana bila kupata jibu.
Je mbona hapo nyuma kabla ya dini kuenea sana watu walikuwa wakifanya matambiko, kuomba vilimani n.k mfano kuomba mvua, kuomba vitu mbali mbali na vilikuwa vinatokea mfano mvua inanyesha kubwa sana wakiomba.
Ila leo hii ulimwengu ulioacha matambiko ulozingatia dini mbona wakiomba havitokei kama enzi za babu zetu?

Me nakumbuka nilipokuwa mdogo huko arusha ukisikia wamasai wameenda kuomba mvua...na nikweli itanyeesha...

Na je kabla ya kuja Waingereza na Waarabu inamaana sisi sote Waafrica tulikuwa tunadhambi kwasababu hakukuwa na dini?




Nimekua najiuliza ni kwa nini mala nyingi hasa mwisho wa mwaka utasikia watu wengi wanakimbia majumbani mwao hasa vijijini na lengo ni kwenda kuwaombea ndugu walioishatangulia kwa maana ya kufa.

Wanaenda mbali na kupeleka maombi yao juu ya maisha yanayowazunguka kwa hao waliokufa,ni kweli kuna maana yoyote au kuna ulazima wa kufanya hili?kama ni kweli MUNGU tunaemuabudu na kuamini kua yupo na ndiyo alietuumba anapata nafasi ipi iwapo tutafikia kupeleka shida zetu kwa wafu?
 
like uuu

Linasema hivi:
Kumbu 18:11 wala mtu alogaye kwa kupiga mafundo, wala mtu apandishaye pepo, wala mchawi, wala mtu awaombaye wafu.12 Kwa maana mtu atendaye hayo ni chukizo kwa Bwana; kisha ni kwa sababu ya hayo Bwana, Mungu wako, anawafukuza mbele yako.

asante
 
Tatizo Biblia yenyewe haiko 'consistent' na inajipinga katika baadhi ya mambo na hivyo kuleta utata katika mambo hayo. Jambo moja linaweza kuonyeshwa kuwa linakubaliwa katika kitabu au mstari mmoja wa Biblia hali jambo hilo hilo linakataliwa katika kitabu au mstari mwingine wa Biblia. Kwa hiyo siyo vema kushikilia mstari mmoja wa Biblia au kusikiliza mchungaji mmoja anayesimamia baadhi tu ya mistari, bali ni muhimu kuangalia na kutathmini Biblia yote kwa undani kuhusu jambo unalotaka kulielewa lakini vilevile kuangalia muktadha (context) wa uandishi wa kitabu husika au mstari husika wa biblia.

Kuwepo kwa Biblia mbili au tuseme tatu, yaani moja yenye vitabu 66 ambayo inakubaliwa na kutumiwa na makanisa ya kiprotestanti na ya kipentekoste na ile yenye vitabu 73 inayokubaliwa na kutumiwa na katoliki ni tatizo mojawapo la msingi. Lakini vile vile biblia ya ziada iliyoandikwa kutokana na vitabu vilivyokusanywa na kuandikwa kutokana na maandiko mbalimbali ya wafuasi wa Yesu ambayo yaliachwa nje ya biblia za mwanzo inayotumiwa na kanisa la Yesu la watakatifu wa baadae (The Church of Jesus Christ of Later Saints) ni tatizo jingine. Ndani ya biblia yenyewe kuna mambo yenye utata mfano kuhusu kama kunywa pombe ni dhambi au la - sehemu moja ya biblia inaruhusu kunywa pombe (divai/mvinyo) hata yesu anatengeneza divai kwa muujiza; sehemu nyingine inakataza watu kunywa pombe. Vile vile biblia hiyo hiyo inaruhusu watu kuoa wake wengi huku sehemu nyingine inataka mtu kuoa mke mmoja n.k.

Jambo jingine lenye utata zaidi pia ni hoja ya kwamba baraza moja lililoandika biblia ya vitabu 66 lilivuviwa na Roho Mtakatifu, je kuna uhakika na ushahidi gani kuwa baraza jingine ambalo liliandika biblia ya vitabu 73 nalo halikuvuviwa na Roho Mtakatifu na hata hilo baraza jingine lililoandika biblia ya nyongeza ya Church of Jesus Christ of Later Saints kwamba nalo halikuvuviwa na huyo huyo Roho Mtakatifu?

Vile vile kuna utata kuhusu uzito wa dhambi kana kwamba dhambi zote zina uzito sawa au zina uzito tofauti. Mfano katika biblia tunaona ikiandikwa kuwa kuna dhambi za mauti na dhambi nyinginezo (Kitabu cha waraka wa Yakobo/Yohana). Lakini watumishi wengine huzungumzia kuwa dhambi zote ni sawa. Hivyo kuleta maswali mengi kuhusu hukumu anayostahili mtu mfano aliyeua binadamu mwenzake na aliyeiba kwa mfano sindano au kuku, je wapewe hukumu na adhabu sawa? Tunaona hata katika torati adhabu zinaendana na uzito wa kosa/dhambi. Ndipo falsafa ya hell(Jehanamu), purgatory (toharani), na paradise (Heaven) [Mbinguni] inakuja. Na kwa kuzingatia kuwa Mungu ni mtakatifu na mwenye haki lazima aonekane kutenda haki kuliko mwanadamu ambaye ni mwenye dhambi. N.K.

Safiii umeeleza vzr. Waliosoma sana dini/biblia kuna kitu kinaitwa 'law of gradation' unapaswa kuielewa nn lengo la biblia, Lengo kuu la biblia ni kueleza kwamba alakati za Mungu kumkomboa mwanadam ambalo linahitimishwa na kifo na ufufuko wa Yesu kristo!

Kama ilivyo mtoto mchanga anavyoanza kunywa maziwaya mama, anafata uji, vyakula vilaini mpaka anapokua kula ugali, vivyo hivyo katika harakati za mungu kumkomboa mwanadamu alimpitisha katika hatua hzo.

Kuna baadhi ya vitu katika vitabu fulani vilikatazwa lakin katika vitabu vingine vya baadae viliruhusiwa, na vingine viliruhusiwa badae vilikatazwa. Hapa ndo inaleta mkanganyiko wa vifungu, baadhi ya vifungu kupingana


Ishu ni kuelewa wakati na lengo la kitabu husika, kwa kutafsiri kifungu kimoja kimoja lazma baadhi vifungu vigongane.
 
naomba na mimi kuchangia japo kwa kifupi.

Mwanzo wa historia ya waisraeli marehemu walifikiriwa kuwa wamefungiwa katika shimo lenye giza nene, wamesahaulika, na hawezi kumsifu mungu...rejea zab. 6. 6:5; 30:9-10 pia zab 88:10-12)

baadaye iliingia imani kuwa roho za wenye haki zimo mikononi mwa mungu rejea (hek 3:1-7) na kwamba wafu watfufuka na baadhi yao watapata utukufu na wengine aibu rejea (dan: 12:2)

waliokufa wakiteteea imani yao waliamini mungu atawafufua wapate uzima wa milele rejea (2mak 7:9)
katika hatua hiyo ulijitokeza umuhimu wa kuwaombea wafu ili mungu aondoe zambi zao....mungu ni mkuu na anaweza yote tunaamini hivyo.. Rejea kitabu cha 2mak 12:38-46)

sasa msingi huu haupo katika vitabu ambavyo havijapokelewa na makanisa ya kiprotestanti ndiyo sababu ya mvutano kati yao na kanisa katoliki..

Ahsanta..

mkuu otorongongo.kwanza kabisa ondoa swala la dheebu lako ukitaka kusaidiwa kujua mambo. Kiukweli kimaandiko ibada ya kuwaombea wafu ni ibada za kishetani. Hai wezekani mtu hakiwa hai halimkataa yesu kwa matendo yake akaishi maisha ya dhambi.alafu ujifariji utamwombea kwa mungu amsamahe. Mungu ni mungu wa utaratibu na ndio maana alimtuma mwanawe aje akuhubirie wewe uliye hai.ili utengeneze kabla hujafa.na yesu ameongea wazi wazi na mnukuu:[tena kwa habari ya kiyama hamja soma neno hili.lililo nenwa na mungu akisema?mimi ni mungu wa ibrahimu.mungu wa isaka. Na mungu wa yakobo? Mungu sio mungu wa wafu,bali wa walio hai.na makutano waliposikia.walishangaa kwa mafundisho yake:[mayayo 22:31>33] sasa kwa nini hawa watu walishangaa hayo mafundisho ya yesu? Jibu hata wao waliaminishwa kuwaombea wafu.jambo ambalo yesu alilipinga wazi wazi.na hao wanao wafundisha watu kuwaombea marehemu hawatokani na mungu bali ni wajumbe wa shetani. Nitakupa sababu ambazo kama utatafakari kwa kina basi na wewe utaokoka kama sisi tulivyokua tumeaminishwa na kanisa katoliki. Ni hukweli usiopingika kutokana na kipengele hiki cha kuwaombea waliokufa.kimekua mlango mzuri wa shetani kuwafariji waamini kwamba wewe fanyatu dhambi hata ukifa siwatakuombea.na kupitia kipengele hichi watuwengi sana wameenda kuzimu kwa kufuata ushetani uhu.wa kuambiwa tutakuombea hata kama ukifa leo na mungu atakusamehe kabisa kabisa.mimi niseme wazi so mungu huyu ninayemjua mimi.anayesema baada ya kifo ni hukum.na anayetusisitiza kuishi maisha matakatifu.ukisoma [luka 16:] utakutana na story ya tajiri na lazaro ukiisoma hadithi ile utagundua yesu alikua anazungumzia maisha ya watu 2 tofauti yaani tajiri aliyeishi maisha ya anasa na dhambi na maskini lazaro aliyeishi maisha matakatifu sasa baada ya kufa maskini akawekwa mahali stahili na tajiri alipokufa vile vile akawekwa maali stahili.unaona huyu tajiri anamwomwomba mungu baada yakutafuta uruma za mungu kushindikana.anamwomba mungu atume mtu kutoka kule kuzimu akawaambie nduguzake watengeneze wangali hai wasije kwenda kule yeye alipo.mungu anamjibu naomba kunukuu:[akamwambia wasipo wasikia musa na manabii.hawata wasikia hata mtu akifufuka katika wafu] kwa maana hiyo basi mbinguni hatuingii kwa kutafuta lifti na uruma za kuombewa ukisha kufa.mbinguni tutaingia kwa kumwamini yesu yaani kuokoka na kuishi maisha matakatifu narudia tena [kuokoka] na [kuishi maisha matakatifu] nakushauri uachane na ibada za wafu zitakupoteza ndugu yangu na uhelimishe wengine waishi maisha matakatifu. Nakuacha na mstari uhu.[basi roho asema wazi wazi ya kwamba.nyakati za mwisho wengine watajitenga na imani wakisikiliza roho zidanganyazo,na mafundisho ya [mashetani]kwa unafiki wa watu wasemao uongo: 1thimotheo 4:1>2]
 
Back
Top Bottom