Kwa nini wakati wa Utawala wa Magufuli umeme haukuwa wa tabu kama awamu ya Samia?!

Shida ni kwamba matatizo yapo siku zote, Ila Mambo yalianza kuharibika Mwezi January huko tanesco na magu kafariki Mwezi wa tatu, ni Kama coincident imetokea shida zimekuwa kubwa wakati yeye anafariki na hazihusiani chochote na kifo chake hata angekuwepo matatizo ya mitambo yangetokea tu,Kuna shida tanesco sema imekuwa zahir mwaka huu na haihusiani na kufa kwa magu
 
M

Mwaka huu na miaka inayokuja tutaona Mengi, kikubwa tumuombee mama asimame kama raisi
Kweli tayari tumeshaanza kuona,eti wizara nyeti anapewa mtu Kama Makamba! Kwa uwezo up?
Anachochote anachoweza kueleza wizara alizopita alifanya Nini?
Huku jimboni kwake Bumbuli alifanya chochote Cha maana?
Au Lile pozi la Kama mtu mwenye hekima ndo criteria?
 
Tanzania yangu siasa imetutawala,siasa imeharibu direction ya nchi, siasa imeharibu elimu, siasa imezidi kufanya wananchi wanakua wajinga zaidi, siasa imefanya tufikirie kama watu wa karne ya 19,siasa inatufanya tuwe wajinga kifikra na tunakuwa vivuli wa watu Fulani,Tanzania yangu haita simama, hadi kizazi hiki kipite,Nanukuu na huu ni ukweli
 
Vipi wakati wa Richmond, SYMBION, na IPTL. TANESCO ilikua inaingiza hasara kiasi gani? Acha propaganda za kipuuzi kwasbb ya chuki, yule jamaa alipiga kazi na ndiyo maana akaamua kuchimba lile bwawa la Stieglers ili kuepukana na hizi hasara zote pamoja na upigaji.

Tusipoangalia sasa hivi, tutakuja kuambiwa bwawa tumekula hasara haliwezi kuzalisha umeme au hakuna fedha za kumalizia mradi ili watu waanze kufufua symbion na IPTL zao.
 
Umekubaliana na mwenzio?amekukumbusha bado unakataa?
 
Tusubirie kama kwa hili bado atakataa au atakubaliana naye umempa facts tuone atasemaje
 
Umekubaliana na mwenzio?amekukumbusha bado unakataa?
Kweli ulikua unakatika, lakin sio kama ulivyozidi ivi sawa,Issue mi nazungumzia frequently pasipo na logic, #tuwe wa kweli tusiishi kama vyawa,ipo siku tutaulizwa tuliifanyia nini Tanzania, tusimamie ukwel
 
Ukweli ni kwamba pamoja na kukatika umeme kwa nyakati fulani wakati wa uongozi wa Magufuli lakini kero hiyo imezidi na kushamiri mno kipindi hiki cha miezi 6 baada ya kifo cha JPM.

Sielewi tatizo ni nini!
Wakati wa Jiwe ulikuwa unakatika sana lakini ilikuwa marufuku kutangaza kuitangaza unauwawa. Halafu alivyokuwa na roho mbaya akamtumbua Mhandisi Mramba kwa aibu akila krismas nyumbani kwao kisa kabila lake.

Mchizi awekwe tu anapostahili huko kuzimu.
 
Ukweli ni kwamba pamoja na kukatika umeme kwa nyakati fulani wakati wa uongozi wa Magufuli lakini kero hiyo imezidi na kushamiri mno kipindi hiki cha miezi 6 baada ya kifo cha JPM.

Sielewi tatizo ni nini!
Akina kigogo wameingia serikalini lazima hayo yatokee.
 
Kuna watu wakisikia jina la Magufuli wanajaa sumu. 😁

Magufuli was the best hata ukimchukia. Amefanya kazi kubwa sana ndani ya muda mchache.

Kama hautaki kusikia mema yake pole sana, utakufa na shinikizo la damu!
 
Ukweli ni kwamba pamoja na kukatika umeme kwa nyakati fulani wakati wa uongozi wa Magufuli lakini kero hiyo imezidi na kushamiri mno kipindi hiki cha miezi 6 baada ya kifo cha JPM.

Sielewi tatizo ni nini!
Aiseeeh yaan huku kibamba mloganzila daaaaaaaah huyu mama hadi watu wameshamchukia hawampendi kabisa yaan mama anachukiwa ila yeye anajua anapendwa,umeme kila kukicha tena bila taarifa wanakata,kumbe ni sehemu nyingi ila mama ye maskini anajua anapendwa, tatizo anaongea juu ila chuni hakuna utekelezaji
 

Dalili za mimba changa.
 
Sisi kwetu haujawahi kukatika au una ugomvi binafsi na makamba
 
Kweli ulikua unakatika, lakin sio kama ulivyozidi ivi sawa,Issue mi nazungumzia frequently pasipo na logic, #tuwe wa kweli tusiishi kama vyawa,ipo siku tutaulizwa tuliifanyia nini Tanzania, tusimamie ukwel
Usha badilisha gia angani tena? Maana mie nilipo huku umeme naupata sana tu na ukikatika unakatika ama ambavyo tulizoeshwa tangu uhuru
 
Wacha kutuchosha na Maneno Mingi..

During Magufuli era umeme nani alisema ulikua haukatiki??

Utawala wa Rais yupi kutoka CCM sasa na uhuru wa miaka 60 umeme haukukatika au kupata electricity rationing?

Muhimu tu ni siku TANESCO wakipata competitive and autonomous company ndio itakua suluhu ya yote ila kwakua sasa wako na backup na ndio wafuaji pekee wa umeme you can tell them nothing...
 
Afadhali mgao wa kimyakimya kuliko ukatikaji holela
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…