MsemajiUkweli
JF-Expert Member
- Jul 5, 2012
- 13,171
- 23,996
- Thread starter
-
- #201
Kama wanavyohangaika kina kinana na chogolo kutetea mkataba. Hii halijawahi kutokea.
Wanachotembeza Ni kibovu, hakinunuliki. Ni Kama pweza aliyechina.
Rais wa mpito ndivyo walivyo
Huo ndio ukweli ambao wana CCM wanapaswa kuujua
umeandika ukweli, nimethibitisha leo hapa mwanza. ccm inakufa kifo kibaya sana. wanaoisemea hawana uwezo wowote, wala ushawishi kabsa
Sukuma gang unahangaika sana. Vipi ule uzi wako kuhusu miga?Ilinichukua miezi mitano kufahamu kuwa Rais Samia hana maisha marefu ya kisiasa kwa sababu hana karama, kipaji na ujuzi wa uongozi.
Unaweza kuukataa ukweli lakini hata kama ukiukataa hakuwezi kuubadilisha kuwa uongo.
Mwl. Nyerere aliwahi kusema, “Ukweli una tabia moja nzuri sana, haujali mkubwa wala mdogo, hujali adui wala rafiki. Kwake watu wote ni sawa. Pia ukweli unayo tabia ya kujilipiza kisasi kama ukipuuzwa. Ukiniona nataka kupiga teke jiwe kwa kuwa unafikiri kuwa ni dongo au mpira, natumaini utanionya. Lakini nikilipuuza onyo lako kwa sababu eti wewe ni mdogo au kwa sababu sikupendi, nikalipiga teke, basi litanivunja dole japo ningekuwa nani. Ukweli haupendi kupuuzwapuuzwa”.
Rais Samia kwa sasa hakubaliki nchini lakini kibaya zaidi hakubaliki ndani ya kundi kubwa la watu wenye maisha ya chini ambao ni wengi nchini na hutumiwa kama “kete” ya CCM katika chaguzi.
Rais Samia amebandika mabango ya kujitangaza nchi nzima lakini kinyume chake watu wakiyaona wanaanza kuyatukana!
Sakata la kuwapa DP-World bandari zetu limekuwa ndio msumari wa mwisho katika kaburi lake la kisiasa baada ya kuwabambikia wananchi tozo mbalimbali.
Ndani ya CCM wameanza kukubali kuwa hali ni mbaya sana mpaka wameamua kuanza ziara za “kuwatongoza” wananchi hasa wa kupato cha chini huku wakisema eti Rais hawezi “kuiuza” nchi.
Katika hali ya kutapatapa wameanza kutumia mbinu ya udini ili kugusa hisia za imani ya dini angalau kundi la watu lenye mlengo wa dini yake lianze kumuunga mkono hasa kundi la watu wa kipato cha chini ambalo halitaki hata kumsikia.
Kinachowashitua zaidi ndani ya CCM ni kuona kuwa juhudi zote za kuwaleta ndani ya utawala wake wapinzani hasa CHADEMA katika “dhana ya kujenga umoja” haijazaa matunda endelevu na badala yake wananchi wa kipato cha chini hawataki hata kumsikiliza achilia mbali kumuona.
Ukiwauliza wananchi wengi kama wanakumbukumbu ya jambo lolote ambalo Rais Samia amelifanya na hawawezi kumsahau watakuambia ni tozo na kugawa bure raslimali zetu za Taifa.
Hotuba zake husahaulika pindi anapomaliza kutoa hotuba. Nadhani hata mawaziri wake ukiwauliza baada ya hotuba yake hawawezi kukumbuka alichokisema! Garbage in, garbage out.
Mikutano yake ya barabarani kwa sasa inakuwa na magari mengi zaidi ya wananchi ukiondoa wale wanaovalishwa nguo za CCM!
Historia nchini huonyesha kuwa Rais huanza kuchokwa na kuchukiwa katika kipindi cha pili cha utawala wake lakini Rais Samia imemchukua miaka miwili tu kuchukiwa na wananchi wengi.
Kwa jinsi hali ilivyo mbaya kuna uwezekano mkubwa Rais Samia akawa ni Rais wa kipindi kimoja katika historia ya Tanzania kwa sababu katika nchi yoyote wanaoleta mabadiliko ni watu wa kipato cha chini ambao kwa sasa hawataki hata kumsikia.
Ahaa, leo 30.07.2023 ndiyo nimeona hili la bandiko lako la jana. Ulipotea sana ila tunashukuru wewe ni mzima. Mkuu nadhani sasa unaanza kuona kitu tulichokuwa tunapiga kelele wakati mkiwa ''mnampelekesha'' Magufuli kipambe. Trust me, Samia ni matunda ya mche aliopanda Magufuli. Mimi hili nililiona linakuja japo sikuwa na uhakika. Samia sisi wengine tulishajua uwezo wake tangu akiwa makamu na ndiyo maana tulikuwa tunapigia kelele kuwe na mabadiliko ya mfumo ili tuwe na nchi isiyotegemea utashi wa rais. Haya sasa, it is too late. Kwa hii nchi yetu naona tukisubiri kudra za Mungu na tusiwe na cha kufanya. Unakumbuka Magufuli alishaweka blue print ya kushinda urais? Unajua watanzania walivyo waoga hata wakiibiwa kura? Hili la Samia kuchukiwa nakubaliana na wewe. Mwezi uliopita nilikuwa kijijini nikakuta kina mama waliokuwa CCM damu wanamtukana mno. Hawataki hata kumsikia. Tatizo ni kuwa hata akikataliwa kwa kura, si atafanya kama alivyofundishwa na Magufuli? Mimi naona pamoja na udhaifu wake, bado bado yuko sana.
Mama anakipeleka chama kubaya Kama JK 2010, namwangalia Kinana anavyoongea kama amekata tamaa Ila hana jinsi ndio ameachiwa jukumu hilo huku mwenyekiti wake akienda kubarizi Dubai na Saudia
Natamani jamii forum wangeruhusu kudownload uzi ili huu niupitie kila muda kuikumbusha akili yangu kuwa taifa limepata kiongozi wa hovyo kuwahi kutokea
Haujapungua, unaelekea kuisha hasa ukizingatia asilimia karibu 50 ya wananchi ni vijana na ndio hawaelewi kabisa kitu inaitwa uzalendo.
It’s a Liberal world.
Hao ni wapuuzi wanajifariji tuu ila wasisahau tunawakumbusha tuuAcha uongo wako hapa na upotoshaji wako hapa wa kijinga.
Rais samia anakubalika ,kupendwa na kuungwa mkono na watanzania wa makundi yote kutokana na kazi kubwa aliyoifanya ndani ya muda mfupi wa uongozi wake.
Katika kugusa maisha ya wananchi wa kipato cha chini ambao wengi wao ni wakulima ,Rais samia aliamua kuchukua hatua za makusudi na za kijasiri kwa kuhakikisha kuwa anawapatia mbolea za Ruzuku zinazogharimu Takribani Billion mia moja hamsini ,hali iliyopelekea mbolea kushuka bei sokoni,,mfano mbolea ya DAP iliyokuwa ikiuzwa laki na 40 ikaanza kupatikana kwa Elfu 70 tu,.sasa ni mkulima yupi au mwananchi yupi atakaye shindwa kumshukuru Rais samia hasa kwa kuzingatia asilimia kubwa ni wakulima? Alifanya hivi kwa kutambua ukweli kuwa uchumi mzuri ni ule unaowagusa watu wengi ,na hapa Tanzania ili uwaguse watu wengi nisharti uwekeze katika shughuli za kilimo kama alivyofanya rais samia ,ikiwepo kuongeza bajeti kufikia billion 970.
Ukija kwa vijana nako ni kicheko furaha na Tabasamu ,hasa baada ya kumwaga maelfu ya ajira mitaani katika ndani ya muda mfupi,lakini pia miradi mbalimbali ambayo imekuwa ikijengwa hapa nchini imechochea ajira nyingi sana kupatikana kwa vijana,lakini pia kwa vijana wanaomaliza kidato cha sita wanapewa mikopo bila shida ,na wawapo vyuoni ni raha tupu na Tabasamu hasa baada ya kuongeza fedha ya kujikimu kufikia elfu kumi kwa siku.
Ukienda kwa wafanyabishara nako ni matumaini kibao ,ambapo kwa sasa kila mfanyabiashara anajisikia fahari kufanyia biashara hapa nchini,kutokana na kuboreshwa kwa mazingira ya biashara hapa nchini,sasa wafanyabishara wanakadiriwa mapato kwa haki na palipo na dosari milango ipo wazi kwa mazungumzo,hali hii ndio imepelekea mapato kwa mwezi kupanda kufikia Trioni 2. Wafanyabishara kwa sasa wanajiona huru kuweka fedha zao benki bila wasiwasi wa kuchotewa fedha zao bila utaratibu wa kisheria au kibenki.
Ukija kwa watumishi wa umma unakuta nako ni shangwe ,nderemo na vifijo hasa baada ya mama wa shoka kuwapandishia mishahara kwa 23% hasa wa kima cha chini,kuwapandisha madaraja,kuwapa nyongeza ya mishahara ya kila mwaka,kuwalipa malimbikizo ya madeni yao na maboresho mengine mengi tu.
Sasa ukitaka kufungua hata biashara katika mwaka wako wa kwanza husumbuliwi na ulipaji wa mapato,kwa kuwa serikali imetoa nafasi ya kukuwa kimtaji na kupata uzoefu wa biashara na kusimama kibiashara.
Ukienda katika huduma za kijamii unakuta Rais samia amegusa kila eneo na kila mahali,iwe ni katika miradi ya maji au umeme au miundombinu una ona namna alivyowekeza vya kutosha ,ndio maana imefika hatua bwawa la nyerere linaanza mapema mwakani kuzalisha umeme.
Ni kundi lipi ambalo halijaguswa na utendaji wa Rais samia? Lipi ambalo halijafikiwa? Lipi ambalo halijatazamwa?
Masuala ya Tozo, je nchi gani ya ulaya au Marekani au zilizoendelea zilizopata maendeleo yake kwa kushushwa kutoka angani? Ni wapi ambako watu wake hawakujibana bana kulipa Tozo ili wajenge nchi zao? Ni wapi huko ambako mataifa yao na wananchi wao walikaa na kubweteka kusubiri wenzao kutoka mataifa mengine walipe Tozo na kodi ili wao wapewe maendeleo.
Watanzania hawajawahi kupinga Tozo na wakati wote wameunga mpango huo wa serikali,ndio maana walikuwa Tayari kuijenga nchi yetu kwa mikono yao ,maana waliona ni aibu kusubiri misaada kwa ajili ya kujengea matundu ya vyoo vya wanafunzi wetu mashuleni. Matokeo chanya ya Tozo hizo ni pamoja na ujenzi wa vyumba vya madarasa zaidi ya Elfu ishirini nchini kwote yaliyopelekea wanafunzi wote wanaofaulu kuanza masomo kwa wakati mmoja, utolewaji wa Elimu bure hadi kidato cha sita,Ujenzi wa vituo vya Afya kila kona ya nchi ikiwepo 234 miezi michache iliyopita ,utolewaji wa Ruzuku ya billion mia moja kila mwezi katika mafuta wakati wa mfumuko wa bei ya mafuta Duniani uliokuwa umesababishwa na vita vya ukrein, n.k.
Mambo aliyoyafanya Rais samia huwezi kumaliza kuandika hapa maana ni mengi sana ,hapo sijazungumzia namna alivyokuza uchumi wetu na kupelekea mzunguko mzuri wa fedha mitaani,kukuza na kuimarisha Demokrasia n.k
Hiyo gia haiwezi kuwavusha hamna ajenda mtaishia kuliwa vichwa na kula hasara kama kawaida yenuUlichokiandika ni ukweli.
Yaani wana CCM na wafanyakazi serikalini wanalazimishwa kwenda kupigia kampeni ugawaji wa maliasili za Taifa.
Haijawahi kutokea tangu kuzaliwa kwa Tanzania!
Aliyevujisha mkataba huu wa Kimangungo ahesabiwe shujaa wa Taifa, vinginevyo tungeujua wakati tayari utumwa wa Waarabu ulishajikita. Shujaa huyu abarikiwe sana.Ilinichukua miezi mitano kufahamu kuwa Rais Samia hana maisha marefu ya kisiasa kwa sababu hana karama, kipaji na ujuzi wa uongozi.
Unaweza kuukataa ukweli lakini hata kama ukiukataa hakuwezi kuubadilisha kuwa uongo.
Mwl. Nyerere aliwahi kusema, “Ukweli una tabia moja nzuri sana, haujali mkubwa wala mdogo, hujali adui wala rafiki. Kwake watu wote ni sawa. Pia ukweli unayo tabia ya kujilipiza kisasi kama ukipuuzwa. Ukiniona nataka kupiga teke jiwe kwa kuwa unafikiri kuwa ni dongo au mpira, natumaini utanionya. Lakini nikilipuuza onyo lako kwa sababu eti wewe ni mdogo au kwa sababu sikupendi, nikalipiga teke, basi litanivunja dole japo ningekuwa nani. Ukweli haupendi kupuuzwapuuzwa”.
Rais Samia kwa sasa hakubaliki nchini lakini kibaya zaidi hakubaliki ndani ya kundi kubwa la watu wenye maisha ya chini ambao ni wengi nchini na hutumiwa kama “kete” ya CCM katika chaguzi.
Rais Samia amebandika mabango ya kujitangaza nchi nzima lakini kinyume chake watu wakiyaona wanaanza kuyatukana!
Sakata la kuwapa DP-World bandari zetu limekuwa ndio msumari wa mwisho katika kaburi lake la kisiasa baada ya kuwabambikia wananchi tozo mbalimbali.
Ndani ya CCM wameanza kukubali kuwa hali ni mbaya sana mpaka wameamua kuanza ziara za “kuwatongoza” wananchi hasa wa kupato cha chini huku wakisema eti Rais hawezi “kuiuza” nchi.
Katika hali ya kutapatapa wameanza kutumia mbinu ya udini ili kugusa hisia za imani ya dini angalau kundi la watu lenye mlengo wa dini yake lianze kumuunga mkono hasa kundi la watu wa kipato cha chini ambalo halitaki hata kumsikia.
Kinachowashitua zaidi ndani ya CCM ni kuona kuwa juhudi zote za kuwaleta ndani ya utawala wake wapinzani hasa CHADEMA katika “dhana ya kujenga umoja” haijazaa matunda endelevu na badala yake wananchi wa kipato cha chini hawataki hata kumsikiliza achilia mbali kumuona.
Ukiwauliza wananchi wengi kama wanakumbukumbu ya jambo lolote ambalo Rais Samia amelifanya na hawawezi kumsahau watakuambia ni tozo na kugawa bure raslimali zetu za Taifa.
Hotuba zake husahaulika pindi anapomaliza kutoa hotuba. Nadhani hata mawaziri wake ukiwauliza baada ya hotuba yake hawawezi kukumbuka alichokisema! Garbage in, garbage out.
Mikutano yake ya barabarani kwa sasa inakuwa na magari mengi zaidi ya wananchi ukiondoa wale wanaovalishwa nguo za CCM!
Historia nchini huonyesha kuwa Rais huanza kuchokwa na kuchukiwa katika kipindi cha pili cha utawala wake lakini Rais Samia imemchukua miaka miwili tu kuchukiwa na wananchi wengi.
Kwa jinsi hali ilivyo mbaya kuna uwezekano mkubwa Rais Samia akawa ni Rais wa kipindi kimoja katika historia ya Tanzania kwa sababu katika nchi yoyote wanaoleta mabadiliko ni watu wa kipato cha chini ambao kwa sasa hawataki hata kumsikia.
CCM hawategemei sanduku la kura, sanduku lao la kura ni TISS na Polisi.Mimi ni CCM lakini siwezi kumpa Mama kura yangu! HATOSHI!
Wewe ni zero kabisa, maoni yako kila siku ni mashudu.Sasa kwanini kila siku kutwa kutukana mimatusi humu,ukubwa Jalala,kwanini wewe unashindwaga kutoa maoni yako kwa lugha za kiungwana,heshima na staha.? Kwani ni vipi matusi yako unayotoagaa yanaongeza uzito wa hoja zako?
CCM hawategemei sanduku la kura, sanduku lao la kura ni TISS na Polisi.
“Ukweli una tabia moja nzuri sana, haujali ukubwa wala udogo, hujali uadui wala urafiki. Kwake watu wote ni sawa. Pia ukweli unayo tabia ya kujilipiza kisasi kama ukipuuzwa" - Nukuu.Nukuu kutoka katika maandiko matakatifu pia hutuasa kuwa, ukiusikiliza na kuuzingatia, basi ukweli utakuacha huru.
Sukuma gang unahangaika sana. Vipi ule uzi wako kuhusu miga?