Kwa sasa huenda 90% ya Degree hazina tena maana, hazikupi ajira wala maarifa ya kupata kipato

Kwa sasa huenda 90% ya Degree hazina tena maana, hazikupi ajira wala maarifa ya kupata kipato

Dah umeweka kozi ninayoisoma na juzi nimefanya last installment sidaiwi sijui nikadai hela yangu
 
Ngoja tusome tu hivyo hivyo, Saivi Hali Kila la sehemu ni ngumu haijalishi umesoma au hujasoma, tena Bora aliesoma kidogo ana mwanga wa Kupambana na maisha kuliko yule ambaye hajasoma.

So degree Bado ni Bora zaidi tena Zaidi.
 
Basi lala mkuu! Maana huwa tunasaidiana hivi kuamshana kifikra, hakuna wa kukushika mkono ila wewe mwenyewe.

As a matter of fact, kuna graduates walianza kubeba zege ili tu wafahamike na kupata connection, sio rahisi ila utalala ndani kusubiri Samia akupe kazi hadi lini?
Na kuna watu walianza Kama wagonjwa Sasa Ni wamiliki wa Hospital,wengine kama migambo Sasa Ni maboss wa usalama wa Taifa.

Either way you are doomed.
 
Mgesema hakuna ajira lakini siyo kusema degree hazina kazi. N akujiajiri siyo lele mama, hata waliosoma entrepreneur wanashindwa kujiajiri.
 
Ukweli usemwe na usemwe wazi ili kila mtu aujue. Wigo wa watanzania kusoma mpaka chuo kikuu ili kupata degree umekuwa mkubwa lakini huo mfumo umekuwa ni hasara na upotevu wa rasimali (muda, pesa na nguvu) kwa 90%.

Ajira mtaani kwa 90% hakuna kwa fani nyingi, ni sawa na kucheza kamili, na elimu ya vyeti vya chuo kikuu haina mchango wowote wa mhitimu wa level ya degree kuweza kujiajiri moja kwa moja. Hapa chini ni baadhi ya fani zinazoangukia kwenye kundi hilo.

1. Public administration
2. Political science
3. Business administration
4. Procurement and supply
5. Human resource
6. Sociology
7. Environment
8. Language
9. Mass communication
10. Tourism
11. Banking
12. Accounting
13. Economy
14. Finance
15. History
16. Insurance
17. Tax
18. Cooperative
19. Marketing
20.

Kama wewe ni mhitimu wa hizo fani kwa miaka ya karibuni utaelewa hicho nilichokiandika, na kama wewe ni mwanafunzi wa hizo fani anza kujiandaa kisaikolojia, hali ni mbaya mtaani. Wahitimu ni wengi na hawana ajira yoyote, wamechoka vibaya, wameshazunguka na mabahasha mpaka soli za viatu kuchakaa, wamejitolea mpaka basi, wameshikiza mpaka wamedondoka na wengi wamekata tamaa kabisa, vyeti vyao wamesahau hata vipo wapi, havina msaada. Bado wanakula, kulala na kutunzwa na wazazi wao, mashemeji au wajomba. Wengine wameamua kujiajiri katika fani zingine ambazo hazina uhusiano wowote wa fani walizosomea na zenye kuhitaji elimu ya darasa la nne tu.
Wajanja wengine wameamua kurudi chuo, hususani kwa ngazi ya Diploma kusoma fani za ualimu au afya ili kuingia kwenye mkondo wa kuja kupata ajira hapo baadaye.

Jamani hali ni mbaya na tete.
Ukweli usemwe!
Wewe huna mtu highly placed,ukiwa na mtu ajira ni immediate.Pole sana.
 
Mgesema hakuna ajira lakini siyo kusema degree hazina kazi. N akujiajiri siyo lele mama, hata waliosoma entrepreneur wanashindwa kujiajiri.
Kazi ya hizo degree ni ipi ikiwa tulizisoma kwa lengo la kutupatia ajira na kipato lakini zimeshindwa kutupa hizo vitu?
Zina faida gani sasa?
 
Wewe huna mtu highly placed,ukiwa na mtu ajira ni immediate.Pole sana.
Hao watu wenye high placed person wako wachache katika wengi tunaohitimu na degree zetu.
Hata kama wote tungekuwa na hizo connection bado balance ingekuwa pale pale, wengi (90%) tungekosa ajira na wachache (10%) wangepata ajira.
 
Hao watu wenye high placed person wako wachache katika wengi tunaohitimu na degree zetu.
Hata kama wote tungekuwa na hizo connection bado balance ingekuwa pale pale, wengi (90%) tungekosa ajira na wachache (10%) wangepata ajira.
Pole sana,I pity you so much.Ila kipo kitu ambacho sisi tumeshindwa kufanya:to change our mindset.Degree ilikuwa muhimu before the 1980s wakati ulikuwa unaajiriwa hata kabla ya matokeo na ulikuwa unatafutwa,sio sasa.Siku hizi ajira ni very hard to come by,kwa hiyo from early on tusi force kwenda vyuo vikuu,because it is useless.Tuji-engage in self employment activities mapema,in that case tutajiondolea stress na depression zisizo za lazima.

I would think it even better ku-opt for VETA courses na kuendelea na mfumo huo up to Diploma,degree au hata MSc kwenye mfumo wa VETA.I believe option hiyo ipo, kama haipo waanzishe.Tatizo letu ni tamaa zisizo za lazima,kwani bila kufika Chuo Kikuu huishi?
 
Ukweli usemwe na usemwe wazi ili kila mtu aujue. Wigo wa watanzania kusoma mpaka chuo kikuu ili kupata degree umekuwa mkubwa lakini huo mfumo umekuwa ni hasara na upotevu wa rasimali (muda, pesa na nguvu) kwa 90%.

Ajira mtaani kwa 90% hakuna kwa fani nyingi, ni sawa na kucheza kamili, na elimu ya vyeti vya chuo kikuu haina mchango wowote wa mhitimu wa level ya degree kuweza kujiajiri moja kwa moja. Hapa chini ni baadhi ya fani zinazoangukia kwenye kundi hilo.

1. Public administration
2. Political science
3. Business administration
4. Procurement and supply
5. Human resource
6. Sociology
7. Environment
8. Language
9. Mass communication
10. Tourism
11. Banking
12. Accounting
13. Economy
14. Finance
15. History
16. Insurance
17. Tax
18. Cooperative
19. Marketing
20.

Kama wewe ni mhitimu wa hizo fani kwa miaka ya karibuni utaelewa hicho nilichokiandika, na kama wewe ni mwanafunzi wa hizo fani anza kujiandaa kisaikolojia, hali ni mbaya mtaani. Wahitimu ni wengi na hawana ajira yoyote, wamechoka vibaya, wameshazunguka na mabahasha mpaka soli za viatu kuchakaa, wamejitolea mpaka basi, wameshikiza mpaka wamedondoka na wengi wamekata tamaa kabisa, vyeti vyao wamesahau hata vipo wapi, havina msaada. Bado wanakula, kulala na kutunzwa na wazazi wao, mashemeji au wajomba. Wengine wameamua kujiajiri katika fani zingine ambazo hazina uhusiano wowote wa fani walizosomea na zenye kuhitaji elimu ya darasa la nne tu.
Wajanja wengine wameamua kurudi chuo, hususani kwa ngazi ya Diploma kusoma fani za ualimu au afya ili kuingia kwenye mkondo wa kuja kupata ajira hapo baadaye.

Jamani hali ni mbaya na tete.
Ukweli usemwe!
ELIMU ni nyenzo ELIMU ni NGAO kitu pekee ambacho sijutii ELIMU imenipa confidence ambayo wale ambao hawajasoma wanakua na excuses nakujiona inferior....

Naziona fursa nyingi sana sanaaa huko nyumbani Tanzania tena bila ya kua na mtaji sema wengi wanapenda white collar job sema wahitimu wanaenda chuoni kukariri notes ila sio kujaza maarifa 😊☺️ yakuweza kuwasaidia kutawala maisha Yao.....

Watu waendelee kusoma kutanua mbongo zao

Wasalaam
Kwa Sasa +267
 
Back
Top Bottom