Kwa sasa imani, matumaini na mapendo ya watanzania wengi ni CCM pekee

Dogo unaota wewe!
 
among powerful, focused, committed and very strong institutions in the world 🐒
Mkuu nasikia wewe mtumishi,watumishi hawavutagi bangi,tafadhali mkuu kama umeanza kuvuta bangi acha bado tunakupenda na tunaihitaji akili yako ikiwa nzima.
Taasisi imara haiwezi kufanya yafuatayo kama ifanyavyo CCM;
1)Haiwezi kufuja pesa za umma kwa mambo yasiyo na maana.
2)Haiwezi kuingia mikataba nyonyefu kwa taifa.
3)Hawawezi kuwa na sera duni za kiuchumi na kisiasa.
4)Hawawezi kuendekeza ufisadi na rushwa.
Sasa hizi sifa zote ndizo za CCM,na tasisi imara haiwezi kuwa na hizi sifa.
 
Dogo unaota wewe!
kwan kuna ubaya gani kuota ndoto na hali ya kua si dhambi?

ndoto ni mawasiliano, maono, maonyo, na ishara kulingana na ulivyo ota

hata hivyo ukweli una tabia ya kuboa au kukera sana, na hata ikasemekana ukweli mchungu.
CCM inapendwa, inategemewa, ccm inaaminika, ccm ndio pekee tumaini la waTanzania wengi
 
Popoma at work
na sababu ya Imani hiyo kubwa ya waTanzania kwa CCM, ni ichapakazi wa viongozi wake wa kuu kwenye chama na serikali hasa Rais, comrade Dr.SAMIA SULUHU HASSAN na wasaidizi wake na mipango mikakati ya kuwakomboa waTanzabia kimaendeleo
 
napenda kukiri kwamba,
dosari, kasoro na changamoto mbalimbali kwenye taasisi yenye uzoefu na umakini mkubwa kama ccm, zipo na zitaebdelea kuepo tu, na tena sio kwenye ccm pekee bali taasisi nyingine zote unazozijua....

hayo ni mambo ya kawaida tupo nayo, yatakuepo na tunadeal nayo, tunarekebisha, tunasahihisha na tunasonga mbele....

CCM haiwezi kubabaika, kuzubaa wala kusita kuchukua hatua dhid ya dosari za kibinadamu au kisheria zinazotokea kwa kujua au kutokujua kwenye mikataba, miradi na programme mbalimbali za kimaendeleo. CCM hujirekebisha na kujisahihisha na inasonga mbele
 
Upuuzi Mtupu
inaweza kua hivyo miongono mwa uelewa mdogo kwa wachache miongoni mwenu, lakini kwa waTanzania walio wengi ndio wameshaamua hivyo tena kwamba imani, upendo na matumaini yao ni ccm
 
..hila na mabavu zinatumika dhidi ya vyama vya upinzani.

..Ccm imekata pumzi kuwatumikia wananchi.

..chama kimebakia kufanya ujanjaujanja, ulaghai, na hujuma, kubakia madarakani.
kuna upinzani wapi sasa TZ ndio hila na mabavu yatumike

CCM itabaki mdio pekee tumaini la waTanzania walio wengi sasa na daima
 
CDM mnatukana kilo MTU anayesifia au kupongeza jitihada za Serikali
nadhani ni vizuri ikafahamika bayana kwamba matusi na mihemko havisaidii kubadili hali halisi kua ccm chini ya kiongozi wake mahiri sana Dr Samia Suluhu Hassan ndio tumaini pekee la waTanzania walio wengi kwa sasa
 
Hakuna siku CCM ilijirekebisha.
Toka inaanzishwa mpaka sasa imekua ikifanya makosa yaleyale.
Na inachokipelekea CCM kufanya makosa yale yale ni sera mbovu za chama na ukiritimba wa wanachama.
 
Hakuna siku CCM ilijirekebisha.
Toka inaanzishwa mpaka sasa imekua ikifanya makosa yaleyale.
Na inachokipelekea CCM kufanya makosa yale yale ni sera mbovu za chama na ukiritimba wa wanachama.
si kweli kwamba haijirekebishi, na kwamba inafanya makosa yaleyale. huu ni upotoshaji....

kujisahihisha na kujirekebisha ni mila, desturi na utamaduni unaofanyika mara kwa mara ndani ya CCM ngazi zote.....

sera za CCM ni nzuri sana, zinaamsha matumaini na matarajio ya maendeleo ya waTanzania ndio maana inaaminika na kupendwa na wananchi na chaguzi zote inashinda kwa kishindo. HAKUNA MBADALA WA SERA ZA CCM HUMU NCHINI
 
Mkuu unataka niyataje makosa ambayo CCM inayarudia tokea kuumbwa kwake!?
CCM haijawahi kuwa nzuri isipokua ni kuwa raia wa Tanzania hatushuhulishwi na siasa kiundani.
Tunachoshukuru ni kula ugali kwa amani na kufanya kazi zetu kwa amani.
Hakuna serikali inayopendwa ilhali raia wake wako katika umasikini komavu wa kipato cha mtu mmoja mmoja.
Hao wanaojirekebisha na kuirekebisha CCM ndio hao kina ABDULRAHMAN KINANA!?
 
Uko sahihi kabisa,
 
kama haijawahi kua nzuri kwako, hiyo ni shida yako binafsi, yafaa udeal nayo kibinafsi, lakini sio uje hapa useme ati wananchi hawajishughulishi na siasa kiundani, huo ni upotoshaji wa waz kabisa.....

Ingekua ni hivyo CCM ingepata wap ushindi wa kishindo? na kama ingekua inarudia makosa haijisahihish nani angeichagua katika kila uchaguzi?

wanaorudia makosa ni wale wanao susisa, wanaozira, wanaogomea chaguzi na kubeba fikra akilini na mioyoni mwao kwamba wanaibiwa kura kumbe hawaeleweki na hawakubaliki na wananchi ....

amani na utulivu wa waTanzania ni matokeo ya jitihada na uwekezaji mkubwa unaofanywa na serikali ya ccm kuhakikisha ulinzi na usalama wa watu, mali na waTanzania wote ni kipaumbele namba moja cha nchi, na kwamba shughuli za siasa, biashara, kilimo n.k zinafanyika kwa uhuru, haki usawa na kwa amani
 
Unaongelea watanzania wapi? Watafuta vyeo au wananchi wa kawaida?
Hakuna raia mwema na mwenye moyo mweupe na nchi hii akawa CCM
hali halisi iko wazi wazi kabisa mchana kweupe,

kwamba imani, matumaini na mapendo ya waTanzania wengi kwa sasa yapo CCM, ndio chama pekee kinachobeba matarajio na matamanio ya makindi mbalimbali ya wananchi wengi humu nchini kutimiza ndoto zao za maisha
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…