Kwa sasa, mita nyingi za Luku zinaondolewa Tariff Zero

Kwa sasa, mita nyingi za Luku zinaondolewa Tariff Zero

Kwa wateja wote wa maeneo ya mijini wanapaswa kuwa Tarifa 1 ambayo ni matumizi ya nyumbani hadi unit 7500 kwa mwezi, wateja wa maeneo ya vijijini wanapaswa kuwa tarif 1 au tarif D1 kutokana na wastani wa matumizi yao wao wanaozidi wastani wa manunuzi ya unit 75 kwa miezi mitatu mfululizo wanakuwa T1 na wale ambao hawazidi na wapo vijijini wanakuwa D1.
Mimi nipo Goba, nimeunga umeme 2018. Tangia niungiwe umeme sikuwahi kutumia zaidi ya Units 50 kwa mwezi.
Lakini bado mmeniweka kwenye Tarrif kubwa ya T1 (75-7500) units.
Nataka kurudi ninapostahili D1 nifanyeje?
 
Kwa wateja wote wa maeneo ya mijini wanapaswa kuwa Tarifa 1 ambayo ni matumizi ya nyumbani hadi unit 7500 kwa mwezi, wateja wa maeneo ya vijijini wanapaswa kuwa tarif 1 au tarif D1 kutokana na wastani wa matumizi yao wao wanaozidi wastani wa manunuzi ya unit 75 kwa miezi mitatu mfululizo wanakuwa T1 na wale ambao hawazidi na wapo vijijini wanakuwa D1.
Wa mjini ambao hawazidi unit 75 kwa nini hawashuki automatically??

Tunanunua umeme bei ghali sana aisee, yaani unit 70 tunanunua kwa shilingi elfu 25, hali mbaya!
 
Ahaa nilikua sijui, kumbe kuondolewa zero tarif ni mpaka uzidishe matumizi miezi 3 mfululizo mi nilijua ni mara moja tuu na ni automatic.

Kwahio kumbe ni kweli tukiita tarif zero tunakosea..

Swali jingine, kwa mtumiaji wa hio tarif 1/D1 je ana limit ya kiwango cha juu cha MANUNUZI ya umeme?

Yaani kimfano yeye anatakiwa asizidishe matumizi ya unit 75 kwa mwezi ambapo lets say ni tsh 9000, Jee akinunua umeme lets say wa 30,000 lakini matumizi bado yakwa chini ya unit 75, Anaweza ondolewa kwenye taarif D1? Kuna mtu tulibishana sana.
Na kwa nyongeza, kipindi cha mwezi mmoja, kinasomeka kwa kalenda ya kawaida, yaani kuanzia tarehe 1 mpaka 30 (mwisho wa mwezi) au kinasomeka kama utaratibu wa bando za simu, yaani siku 30 toka ulipoweka umeme?
 
Ndugu wapendwa wateja wetu!

Wateja wetu wote wanawekwa kwenye makundi ya matumizi yanayoendana na matumizi yao kwa kuzingatia wastani wa matumizi na eneo alilopo.

Ifahamike kuwa hakuna mteja wa matumizi ya nyumbani anayeweza kuwekwa kwenyw kundi la matumizi ya viwanda.
Naombeni kuunganishwa Tarif 0
 
Mkuu kwanza hamnaga hiyonkitu unaita Tariff Zero. Tariffs zipo D1 , T1, T2 na T3.

Mteja utawekwa kwenye tariff husika kulingana na matumìizi yako ya umeme kwa mwezi. Sasa wewe kama unatumia zaidi ya unit 75 bado unataka ubakizwe kwenye D1 (ambayo ndio mnaita tariff zero)?

Nadhani ni kukosa uelewa au kushindwa kufuatilia terms and conditions. TANESCO toeni elimu kwa wateja wenu.

images.png
 
Hii wiki imekua Ni vilio kwa watu kila mahali,

Wengi wameondolewa tarrif zero, na Hakuna maelezo ya kueleweka.

Tumezoea ukizidisha matumizi ya unit 70 kwa mwezi, automatically system inakuondoa tariff zero (umeme wa 1,000= unit 8.4)
Kwa Sasa unaondolewa TU kwa lazima hata Kama ujazidisha.

Mtu Hana tv Wala redio, anatumia balbu 2 TU na simu kaondolewa tarrif zero. Akitaka kununua umeme UNAGOMA afu anaambiwa "unatakiwa upate key change".

Sijajua ndo ukusanyaji mpya wa mapato ya serikali kwa kulazimisha watu wengi watumie tarrif 4 (umeme wa 1000= unit 2.9) au Kuna kitu kingine pembeni kinaendelea TUFAHAMISHWE.

Kwa maana
Tangu huu mwezi uanze, vijana wa tanesco wamekua wakipita nyumba Hadi nyumba mara kwa mara, wakidai wanakusanya takwimu za mita za luku.
Why waondoe na mie nilitaka nikahamie huko Tarriff zero jamani.
Yaani Hawa jamaa sijui wanawaza Nini.
Saivi ni zamu ya masikini kuishi Kama mamshetani na wao wakamuliwe ama aanalipiza kisasi.
Jom alikamua mafisadi hela zikapatikana huyu kawachia.
 
Wa mjini ambao hawazidi unit 75 kwa nini hawashuki automatically??

Tunanunua umeme bei ghali sana aisee, yaani unit 70 tunanunua kwa shilingi elfu 25, hali mb

Mkuu kwanza hamnaga hiyonkitu unaita Tariff Zero. Tariffs zipo D1 , T1, T2 na T3.

Mteja utawekwa kwenye tariff husika kulingana na matumìizi yako ya umeme kwa mwezi. Sasa wewe kama unatumia zaidi ya unit 75 bado unataka ubakizwe kwenye D1 (ambayo ndio mnaita tariff zero)?

Nadhani ni kukosa uelewa au kushindwa kufuatilia terms and conditions. TANESCO toeni elimu kwa wateja wenu.

View attachment 1854399
Mimi sijawahi zidisha units 50 kwa mwezi tangia niunge umeme 2018 lakini hawajaniweka kwenye hiyo tarrif D1
 
Ahaa nilikua sijui, kumbe kuondolewa zero tarif ni mpaka uzidishe matumizi miezi 3 mfululizo mi nilijua ni mara moja tuu na ni automatic.

Kwahio kumbe ni kweli tukiita tarif zero tunakosea..

Swali jingine, kwa mtumiaji wa hio tarif 1/D1 je ana limit ya kiwango cha juu cha MANUNUZI ya umeme?

Yaani kimfano yeye anatakiwa asizidishe matumizi ya unit 75 kwa mwezi ambapo lets say ni tsh 9000, Jee akinunua umeme lets say wa 30,000 lakini matumizi bado yakwa chini ya unit 75, Anaweza ondolewa kwenye taarif D1? Kuna mtu tulibishana sana.
Ikishazidi mwezi mmoja, ukinunua umeme unaofuatia units zinakua chache
 
Jibu swali, acha kujibu kama roboti.

Umeulizwa, hizi taarifa ni za kweli?

Ulitakiwa kujibu NDIO au HAPANA!

Waswahili bana! Maneno meeengiii ujanja ujanja tu.

Narudia kukuuliza: HIZI TAARIFA NI ZA KWELI?
Mimi niko kwenye kiwango kidogo cha matumizi, nasubiri huu mwezi ninunue nione kama watakuwa wameondoa. Unaweza ukawapa mita namba na wakakuondoa maana hawa washezi
 
Jibu swali, acha kujibu kama roboti.

Umeulizwa, hizi taarifa ni za kweli?

Ulitakiwa kujibu NDIO au HAPANA!

Waswahili bana! Maneno meeengiii ujanja ujanja tu.

Narudia kukuuliza: HIZI TAARIFA NI ZA KWELI?
Tanasco ni kati ya mashirika yenye 'Poor customer care' mimi huwa nakereka nao sana hasa nikiwa na tatizo la umeme. Wana jibu lao kila unapowapigia wanakwambia 'Mafundi wetu watakuja hivi punde' unamaliza wiki wakati mwingine mwezi lakini ukiwapigia jibu lao ni hilo hilo tu.
 
Kile kipindi umeme unasumbua kuna watu wameondolewa kwenye tarif zero kutokana na kurudia rudia kununua umeme. Lakini Tanesco hayo malalamiko hata hawatilii manani
 
Elimu bure, flyovers, mishahara, barabara za lami, ndege, SGR, Bwawa la Nyerere, madawa, madaraja, mwendokasi, njia nane e.t.c. vinahitaji kulipiwa na sisi wenyewe.
KULIPA KODI NI WAJIBU WA KILA MWANANCHI.
Tatizo wala sio hilo, tatizo ni kuwa mzalendo wa nchi yako wakati kuna wachache wanaitafuna nchi kweli kweli. Hilo ni tatizo...tena kubwa tu!
 
Back
Top Bottom