Kwa sasa ni nadra sana kuwakuta hawa viongozi wapo Dodoma Makao Makuu, wote imekuwa ni njia moja Dar

Kwa sasa ni nadra sana kuwakuta hawa viongozi wapo Dodoma Makao Makuu, wote imekuwa ni njia moja Dar

Mwisho kabisaaa..kipi kianze kati ya mindset au katiba..
Jibu ni rahisi..ili uwe na katiba bora, lazima wanaoiandaa hiyo katiba wawe na mindset nzuri ambazo hazitakuwa na bias zozote au kufanya muhiml mmoja kuwa na nguvu zid ya mwingine..hivyo katiba bora huundwa na watu wenye mindset bora na sio katiba bora ilete watu wenye mindset bora..

..naheshimu maoni yako.

..lakini mimi nadhani tuanze na katiba mpya na bora.

..mindset tutaijenga kwa kutumia, rejea, dira, na muongozo wetu, ambao utakuwa ni katiba bora.

..hata MISAHAFU haikusubiri watu waache dhambi ndipo iteremshwe.

..Misahafu imeletwa ili iwarejeshe wanadamu ktk matendo mema.

..Katiba mpya na bora inatakiwa iletwe ili iwe muongozo wetu ktk kuenenda kwa kufuata taratibu na sheria.

..Na suala la mindset ni suala endelevu. Siyo suala ambalo linatokea mara moja, papo kwa papo, kama unavyowasha taa.

..Na kuongezea Tz tunao watu wa kutosha wenye maadili mema wanaoweza kubeba jukumu la kuandika katiba bora.
 
Dodoma vumbi

Dodoma hakuna beach

Dodoma maji ya chumvi

Ndio sababu zao[emoji1787]
 
Yaani kwa sasa ni nadra sana kuwakuta hawa viongozi wapo Dodoma makao makuu - wote imekuwa ni njia moko Dar - Magari yenye bendera za Mawaziri na Watendaji wengine wa Serikali wamerudi Dar kwa kasi kubwa mno. Yaani haipiti saa tatu ukiwa Morogoro kila siku unaona gari la kiongizo liko spidi kutoka au kwenda Dar na Dodoma. Matrafiki siku hizi hawana hata mpango wa kuyasimamisha tena. Wamechoka wanaangalia tu.

Gharama hizo za magari kukimbia njia ya Dar Dom ninaona ni kuwa mno kiasi kwamba angekuwepo Mwendazake isingekuwa hivi - wengine hadi juzi wamediriki kuamua kurudisha Ofisi zao Dar - Waziri yule kaitoa Ofisi Moro kuipeleka Dar badala ya Dodoma. Ninamkumbuka sana Mwendazake jamani!

Hivi leo hii tukiitisha roll call ya Viongozi Dodoma ni Mawaziri na Wanaibu Waziri na Makatibu Wakuu wangapi watakuwepo Dodoma leo?
Kumbuka juzi tu karibu wote walikuwa Dar kwa Sabasaba - leo Ijumaa tayari wanne wamepanga ndege na kuna magari zaidi ya 6 yanaelekea Dar now bila hata sababu yeyote. Pumzika kwa Amani Mwendazake! Tumekumiss sana sana!
Waliipemda Dodoma kinafiki, Mtesi hayupo amekwemda zake....thats why!!
 
Hapo sasa ndipo tunaingia kwenye mjadala wa kati ya kuku na yai kipi kinamtangulia mwenzake
Ni hivi nikisema mindset naamina utambuzi wa mtu binafsi kuelewa nini mana ya kuwa na katiba na jinsi ya kuiheshimh na kuilinda hiyo katiba.kama watu hawafika kwenye hiyo level ya kutambua umuhimu wa kuiheshimu na kuilinda katiba baas ujue hata hiyo mpyaa itasiginwaa mchana na usiku..
Mkuu, hapa hakuna cha kuku wala yai!
Huwezi kuacha kutunga katiba eti usubiri "utambuzi wa mtu", ingekuwa hivyo pasingeandikwa katiba popote duniani.

Nashangaa sana kwamba hata hili lililowazi kabisa unakaa na kulikomalia!
Jambo la pili nani wakuibadilisha hiyo kindset.? Jibu ni moja tu mindset haibadilishwi na mtu mwingine yyte yule isipokuwa na muhusika mwenyewe..leo ww ukiwa na mindset inayoheshimu uhuru wa mtu basi huyo mtu uliemuheshimu leo kesho na yeye ataheshimu wengine and it keeps on evolving..
Kwa hiyo wewe huoni umhimu wowote wa kuwepo na katiba yoyote, hata hii iliyopo hatuihitaji?
Mi nadhani huelewi unachoandika hapa kwa haya unayoeleza.
 
Dodoma ni pabaya.
Hongera mama Samia kwa kurudi Dar.
Usidanganyike.
Hana ubavu wa kurudi Dar huyo.

Atahangaika tu hivyo hivyo hadi atakapoondoka.

Kama kuna 'audacity' (nadhani neno ni 'uthubutu') ambao ungeweza kumletea sifa Magufuli, ni mambo kama haya.
Uamzi ulishafanyika siku nyingi, ulikosa mtekelezaji tu; yeye katekeleza.
 
Mwisho kabisaaa..kipi kianze kati ya mindset au katiba..
Jibu ni rahisi..ili uwe na katiba bora, lazima wanaoiandaa hiyo katiba wawe na mindset nzuri ambazo hazitakuwa na bias zozote au kufanya muhiml mmoja kuwa na nguvu zid ya mwingine..hivyo katiba bora huundwa na watu wenye mindset bora na sio katiba bora ilete watu wenye mindset bora..
Sioni jibu hapo aisee; ila mizunguko tu ya maneno!
"...wanaoiandaa hiyo katiba wawe na 'mindset' bora"; hiki ndio kitu gani?
Hawa watu tutawaagiza toka sayari ya Mars, kwa vile sasa hivi hawapo hapa?

Ni nani huyo "mpimaji" wa 'mindsets' zinazofaa ili wakae watutungie hiyo katiba?
 
..mimi hoja yangu ni kwamba uamuzi wetu haukuwa na tija, wala ulazima
Mkuu 'Jokaa Kuu', najua unafahamu vyema kabisa uamuzi ulipofanywa sababu zilizotolewa kwa uamzi huo, kwa wakati huo.

Lakini hata sasa, binafsi sioni ubaya wa makao makuu ya nchi yetu kuwa Dodoma.

Hata hayo mataifa mawili niliyoyatolea mfano na unakubaliana na mfano huo, wao pia walisukumwa na sababu maalum za kuhamisha makao makuu, wakijuwa kwamba uamzi huo unaambatana na gharama.
Maofisi ni 'asset' haziwezi kuwa ni hasara, kwani haziwezi kukosa matumizi mengine, au hata kuuzwa au kuwa vitega uchumi.
 
Mkuu, hapa hakuna cha kuku wala yai!
Huwezi kuacha kutunga katiba eti usubiri "utambuzi wa mtu", ingekuwa hivyo pasingeandikwa katiba popote duniani.

Nashangaa sana kwamba hata hili lililowazi kabisa unakaa na kulikomalia!

Kwa hiyo wewe huoni umhimu wowote wa kuwepo na katiba yoyote, hata hii iliyopo hatuihitaji?
Mi nadhani huelewi unachoandika hapa kwa haya unayoeleza.
Bwana kalamu! Kwa kuwa akili yako kwa sasa umeiseti kwenye katiba katiba katiba mpyaaa..baaas hata ninachokiandika hutaweza kukielewaaa wacha nikuachee tu na niendelee kujenga uchumi wa nchi kama rais alivyosisitizaa..
Ingekuwa watu wamepata utambuzi kwanza baas ile rasimu ya warioba ingeshapitishwaaa lakin kwa kuwa watu hawana utambuzi..tasimu imeishiwa hewaniii...kalagha bakhooo
 
Dawa ya mambo ya hovyo hovyo katiba mpya na sii mtu au mamlaka ndani ya Katiba ya sasa.Hivyo ikiwa unakereka na haya unga mkono juhudi za kizalendo,mwendo ni katiba mpya dawa ya mambo mbofumbofu.
Katiba nzuri ni kitu kimoja, usimamizi wa katiba hiyo ni kitu kingine. Iwapo tuna sheria inayosema kuwa makao makuu ya serikali ni Dodoma, kwa nini sheria hiyo haisimamiwi.
 
Bwana kalamu! Kwa kuwa akili yako kwa sasa umeiseti kwenye katiba katiba katiba mpyaaa..baaas hata ninachokiandika hutaweza kukielewaaa wacha nikuachee tu na niendelee kujenga uchumi wa nchi kama rais alivyosisitizaa..
Ingekuwa watu wamepata utambuzi kwanza baas ile rasimu ya warioba ingeshapitishwaaa lakin kwa kuwa watu hawana utambuzi..tasimu imeishiwa hewaniii...kalagha bakhooo
Hapana, usiondoke ukiwa na kinyongo na ninayoyaandika mimi, ukweli ni kwamba huna hoja ya kuitetea hapa.

Kuhusu "Rasmu ya Warioba", kwani hujui kilichotokea?

Ni wakati gani ilipelekwa kwa wananchi, na kwa sabau ya "upungufu wao wa utambuzi" wakashindwa kuipitisha?

Nakushauri vizuri tu hapa: fungua akili yako iwe huru. Acha kuilazimisha ikubali jambo ambalo halina mantiki kabisa kuling'ang'ania. Katiba tuliyo nayo sasa hivi inao upungufu mkubwa sana kwa nyakati zetu hizi. Hatuwezi kung'ang'ania katiba hiyo hiyo kwa sabau za uongo na kweli kama hizo unazozitoa wewe hapa.
 
Dawa ya mambo ya hovyo hovyo katiba mpya na sii mtu au mamlaka ndani ya Katiba ya sasa.Hivyo ikiwa unakereka na haya unga mkono juhudi za kizalendo,mwendo ni katiba mpya dawa ya mambo mbofumbofu.
Tatizo ni ujinga na ujuaji aisee hivi katiba ikibadilishwa inaweza kubadili maisha yako kivipi?

Vijijini sisikii kabisaaaaa habari ya katiba mpya na maisha yanaenda vizuri tu ila ujuaji wa watu wa mijini na kukosa kazi za kufanya waropoka tu KATIBA MPYA!!

Kuna watu wamefanikiwa chini ya katiba hii hii tuliyonayo pasipo kufungamana nayo na hata hawaijui na hawajawahi kuiona ila wewe upo unapiga domo tu.

Haya hao watu wa kale walikuwa na katiba ipi nzuri iliyowawezesha kuishi kwa amani na kindugu?

Swala hapa ni uwajibikaji,haki sawa kwa wote na kuheshimu sheria zilizopo kwa uwazi siyo kwa makundi ya watu.

Ningefurahi sana kusikia kusiwe na bunge kabisaaa kwani bunge ndiyo chanzo cha matatizo kwa wananchi kwa kutanguliza maslahi yao kwanza zaidi ya jamimi inayowazunguka.

Nani amewahi kupelekewa matatizo yake bungeni na akarejeshewa majibu kwa wakati na yenye tija na mbunge wake?
 
..uamuzi wa kuhamia Dodoma ulikuwa mbaya na wa kulazimisha.

..hatukupaswa kujenga makao makuu mengine wakati tulikuwa na makao makuu yanayojitosheleza hapa Dsm.

..sio kweli kwamba makao makuu ya nchi yanapaswa kuwa katikati ya nchi husika.

..Afrika Kusini kila mhimili una makao yake makuu.

..Executive wako Pretoria, bunge wako Cape Town, na mahakama wako Bloemfontein.

..Fedha tulizotumia kujenga Dodoma zingeweza kuelekezwa ktk sekta ambazo zinagusa maisha ya wananchi kama afya, elimu, maji, etc.
Uamuzi wa kujenda dodoma ulipitishwa mwaka na kuwa sheria 1972, yaani zamani sana. Haukuwa uamuzi wa kulazimisha kwani ulipita kjidemokrasia kabisa wawakilishi wa mikoa yote walipiga kura na kupitisha uamuzi huo isipokuwa mkoa wa Pwani ndio uliopinga (mwulize Kikwete kwa nini walipinga). Mwaka 1976 Nigeria nao waliamua kuhamisha makao kutoka lagos kwenda Abuja, na wao walishahama siku nyingi sana wakati sisi bado tunapiga maktaimu kila siku. Kutokuwa serious na sheria zetu ni sehemu ya uzembe wetu unaotufanya tushindwe kuendelea. Tulipopata mtu anayesimamia sheria sawasawa tukalalalamika sana kwa sababu hatukuzowea kutii sheria zetu.

Mwaka 1972 makao kuwa kjati kati lilikuwa ni jambo la muhimu sana kwa vile hakukuwa na miundo mbinu uionayo leo. hata hivyo, kuwa katikati ya nchi ni sababu mojawapo tu, lakini pia kutenganisha kitovu cha biashara na shughuli za serikali ni jambo la muhimu zaidi.

In the end, ni kuwa lazima tutii sheria zetu, kama hatuzitaki basi tuzifute siyo kuzikaidi. Sheria ya makao makuu kuwa Dodoma ipo na bado ni sheria halali, hivyo lazima tuitii.
 
Katiba nzuri ni kitu kimoja, usimamizi wa katiba hiyo ni kitu kingine. Iwapo tuna sheria inayosema kuwa makao makuu ya serikali ni Dodoma, kwa nini sheria hiyo haisimamiwi.
Katiba nzuri inajilinda na huwapa wananchi na wasimamizi uwezo wa kuisimamia isivunjwe ovyo ovyo. Ni katiba isiyompa mtu mmoja mamlaka makubwa, hata ya kumwezesha kuivunja katiba yenyewe bila kuhojiwa kwa mamlaka makubwa anayopewa na katiba mbovu.
 
Huwa nawashangaa sana watu wanaodai katiba mpyaa...mnashindwa kujua shida iko wap..hata ukiwa na katiba bora kama nn..bila kuwa na watu wanaoiheshimu ni kaz bure..katiba haijindeshi yenyewwwe..wapo watu wanaisimamia hiyo katiba..kama hao watu ni hovyoo baas wataikanyagaa tu hiyo katibaaa...hivyoo kinatakiwa ni mind set za hao watu zibadilike hapo ndipo katiba itasaidia..la sivyo ni kutwanga maji kwenye kinu..
Hii iliyopo tu inasiginwaa mchana kutwaa..
Kuna nchi ina kiwanda cha kuset mind? Katiba ni mwongozo mkuu wa do this, don't do this. Sasa hiyo mind unaiset ikatekeleze maagizo mabovu? Katiba imeachia madaraka kwa mtu mmoja kama Lori la mchanga lililokata breki, hata ukiset mind ya dereva itasaidia nini?
 
Katika mambo muhimu aliyofanya hayati Magufuli ni kutupeleka DODOMA, ni uamuzi utakaoheshimika vizazi na vizazi. Mnapozungumzia DSM kufaa zaidi ninashangaa, kumbuka kwamba DSM ilijengwa, haikuwa ilivyo Leo. Tatizo letu tunapenda vilivyojengwa, hatupendi kujenga.
Taifa la Israel liko jangwani, lakini miujiza inatendeka, wanafanya vitu vya ajabu, unaposikia Dubai ni miji ya ubunifu, watanzania tatizo hatupendi shida, tunapenda raha, tunataka tukae DSM ili kupiga dili bandalini, tumejaa wizi, uvivu na ubinafsi tu hamna lolote. Ni taifa la watu wa ajabuajabu waisopenda shida.
Tunapenda ngono, lakini hatupendi watoto, kwa sababu tunaogopa kulea, ila tunawapenda watoto wa kike walielewa na watu wengine, hatuko tayari kuleo watoto ila tunapenda uzinzi. Mwanaume was kweli ni yule aliyetayari kubeba wajibu hata ungekuwa mgumu kiasi gani. Wote CCM na wapinzani ni watoto wa mama mmoja. CCM wanataka katiba itakayowafanya waendelee kutawala, wapinzani wanataka katiba itakayowapa zamu ya kutawala, ukiangalia lengo LA wote ni kututawala basi, hakuna jipya.
Mnapoiona DSM kuna watu waliumiza vichwa ndo maana leo mnaiona nzuri, msifikiri kuna watu walikuwa wanaishi mahali fulani na kwenda kuijenga DSM. Waliojenga waliishi pale, walikuwa wanaume kweli kweli, leo mnasema tubaki DSM ili tuijenge Dodoma, ni nini hicho zaidi ya uoga, hofu na kutotaka kuwajibika kwa ajili vizazi vijavyo. Musione vyaelea vimeundwa. Kaeni Dodoma, jengeni Dodoma, acheni ujinga, mukistaafu, kaishini DSM ukiwa mtumishi wa serikali kaa Dodoma full stop mukienda kinyuma na hilo hatutawasamehe.
We want Dodoma our capital city and let it be. Katika hili hatutaki siasa.
 
Kama uko makini kwenye siasa za kimataifa unaweza fahamu nani mwenye nguvu kati ya katiba ya nchi na rais alieko madarakan..naomba urejelee utendaji kaz wa trump aliekuwa rais wa marekani..pamoja na kwamba wamarekani wengi wako vzur kichwani haswa kwenye masuala la nchi yao na katiba..lakin kichaa trump aliwatingisha kweli kweli had wakanyoosha mikono..sembuse haka ka nchi kalichojaa mazwazwaa kila kona..nakuhakikishia hata hiyo katiba iwejee rais kama hana heshima na ustaarabu kwenye ubongo wake ataikanyaga mchana kweupe na hatafanywa kitu
Dah! Umenikumbusha huyo mwendawazimu..ahahahah kuna siku alisema 'hivi mtu akinywa sanitizer hawezi pona Corona?'
 
Back
Top Bottom